Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə23/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   17   18   19   20   21   22   23   24   25

mshikamano (mi-) солидарность, hayati покойный, умерший

сплоченность fani (-) область, сфера



-ghushi, -ghoshi подделывать idhaa (-) радиостанция

tunzo (-;ma-) награда, премия makala (мн.; -) статья

shairi (ma-) стихотворение, nishani (-) орден, медаль;

поэма; поэзия (во мн. ч.) награда



angalau, angalao хотя бы -adhimisha праздновать

rika (-) ровесник, сверстник -ona fahari гордиться

-tunuku, -tunukia награждать, -teua 1) выбирать

присуждать (премию и т.п.) 2) назначать (на пост и т.п.)



-fuatilia прослеживать (что-л.) kigezo (vi-) образец;

bayana ясно, очевидно критерий

-weka bayana разъяснить, -chapisha, -piga chapa

отчетливо показать печатать, издавать



-fufua 1) оживлять, воскрешать chapisho (ma-) публикация

возрождать (перен.) hisia (-) 1) чувство; эмоция



mwamko (mi-) 1) пробуждение 2) интуиция

2) отклик mtendaji (wa-) исполнитель


* * *

Урок 30. Somo la thelathini
Грамматика

Вспомогательная функция глаголов -ja, -enda, -tokea.


Глаголы -ja, -enda, -tokea могут использоваться как вспомогательные, дополняя, уточняя или конкретизируя основное действие, выражаемое смысловым глаголом. В переводе на русский язык основное значение таких вспомогательных глаголов не передается.

Глагол -ja “приходить” подчеркивает начало осуществления действия или целевой характер действия:



Alikuja kufahamu kwamba alifanya kosa kubwa “Он начал осознавать, что совершил большую ошибку”;

Pato litokanalo na wageni wanaokuja nchini mwetu kuja kutazama vitu mbali mbali ni kubwa “Доход от иностранцев, приезжающих в нашу страну, чтобы все посмотреть, огромен”.

Напомним, что глагол -ja выступает в роли вспомогательного в конструкции, где он стоит в отрицательной форме желательно-побудительного наклонения, а за ним следует основной глагол с показателем -ka-:

Angalia usije ukatumbukia ndani ya Pango la Pepo “Смотри, не упади в пещеру духов”.

Инфинитивная форма глагола -enda “идти” в качестве вспомогательного глагола обращает внимание на намеренность, направленность действия. На русский язык этот оттенок значения можно передавать с помощью союзных слов “с тем, чтобы”, “для того, чтобы”. Например:

Tuliamua kusafiri Afrika kwenda kutazama wanyama wa porini “Мы решили поехать в Африку, чтобы посмотреть диких животных”.

Глагол -tokeaпроисходить, случаться” помогает передать результативность действия и на русский язык может переводиться словами типа “оказался”, “стал” и т.п. Например:

Kitabu kimetokea kuwa cha kusisimua “Книга оказалась захватывающей”;

Tamasha hilo limetokea kuwachekesha wote “Вышло так, что это представление развеселило всех”.
Mazoezi

1. Переведите:

1. Wapenzi wa Kiswahili huwasili Dar es Salaam kila mwaka kuja kupeana mawazo kuhusu jinsi ya kukuza, kuendeleza na kuisambaza lugha hii. 2. Watafiti wa mambo ya kale wakaelekea Kilwa kwenda kuchunguza magofu ya makaburi ya Waarabu. 3. Wananchi wote hatimaye walikuja kufahamu umuhimu wa kutunza mazingira kwa ajili ya masilahi ya vizazi vya leo na vijavyo. 4. Ugonjwa wa babu ukatokea kuwa wa hatari mno hata madaktari walisisitiza dharura ya kumlaza hospitalini. 5. Akina mama wa kijijini waliamua kuwatembelea majirani zao kwenda kuwauliza habari za kujenga boma la maji ili kuimaliza shida ya ukosefu wa maji. 6. Saa ya dhahabu niliyomnunulia babangu kuadhimisha siku yake ya kustaafu ilitokea kuwa ya kughushiwa kinyume na vile alivyodai mfanyabiashara wa sokoni.


SHAABAN ROBERT: MAISHA YAKE

Imekuwa jambo la kawaida katika familia za Kiafrika kuwa na malezi ya pande mbili za baba na mama. Hivyo basi mtoto anastahili malezi ya kiumeni na kikeni*.

Shaaban Robert kiumeni kwake ni Dar es Salaam, licha ya kwamba babu yake alitokea Tunduru. Hivyo Tunduru ni asili yake.

Shaaban Robert alikuwa kalelewa** sana kwa wajomba zake ambako alipewa malezi ya kimila na desturi. Pia Shaaban Robert alikuwa jirani sana na Mwalimu Kihera ambaye pia alikuwa kama mzee wake, babu na mlezi maalumu. Mwalimu Kihera alikuwa na sifa ya ziada, malezi yake yalifuata mila na desturi ya Kimrima na Kiswahili.

Shaaban Robert alipotimia miaka minane mwaka 1917 hivi alipelekwa chuoni. Alijifunza abjadi za Kiarabu na masomo ya dini ya Kiislamu. Pia alitayarishiwa masomo ya shule ya Kizungu kwa wakati ule, hasa ikizingatiwa kuwa wajomba zake walikuwa wasomi katika shule za kikoloni za Kidachi.

Ikumbukwe kwamba nyakati hizo haikuwa jambo rahisi sana kwa watoto kupelekwa shule hasa za Kizungu, ukiachilia*** zile za dini.

Hali hiyo pia ilimkumba Shaaban, ndiyo maana Shaaban alikuja Dar es Salaam mapema mwaka 1920****, akaingizwa shule ya Kizungu. Akasoma Kizungu mpaka kumaliza darasa la nne la Kiingereza, na hilo ndilo lilikuwa darasa la mwisho la mtihani. Baada ya shule kufungwa na ikizingatiwa kwamba alikuwa keshafanya** mtihani wake, yaani kidato cha mwisho, aliomba ruhusa kwa baba zake wadogo na shangazi zake aende Tanga kwa mama yake, lakini pia baba yake alikuwa bado yuko Tanga wakati huo.

Kwa hiyo alipofika Tanga alikaa kiasi cha wiki moja hivi huko Machui. Aliamua aende akaonane na Mwalimu Mkuu ambaye alikuwa Mzungu, ili aombe nafasi ya kusoma pindi shule zitakapofunguliwa.

Alifanya hivyo kwa sababu mbili. Kwanza kama angelishindwa mtihani ule alioufanya, basi iwe anaendelea na masomo hayo, itakuwa hakupata hasara. Pili na kama itakuwa kafaulu basi itakuwa kapata** zaidi.

Tendo hilo mbali ya mwalimu mkuu kuona la maana na kumruhusu, alilichukulia kuwa ni moja kati ya mambo bora kabisa.

Mwezi Agosti mwaka huo huo majibu yalitoka na Shaaban Robert alifaulu vizuri sana. Alikuwa ni mwanafunzi wa pili katika shule zote za nchini Tanganyika kwa wakati huo.

Mwalimu Mkuu alifanya mkutano na kuzungumza kwa hamu kubwa ya kumsifu Shaaban Robert kuwa alifanya jambo la pekee ambalo halikuwahi kufanywa na mwanafunzi yeyote.

Pamoja na mambo hayo yote, malezi yake Shaaban yalimpamba kwa upole, heshima, utii, tabia njema, ukweli na mapenzi ya elimu. Tabia hii iliwavutia watu wengi waliokuwa wakimpenda.

Shaaban hakuishia hapo kielimu, DC***** wa Pangani wakati ule ndiye aliyemfungulia pazia Shaaban la masomo ya nje kwa njia ya posta. Inakisiwa kati ya mwaka 1932 na 1934, Shaaban alikuwa ni mwanafunzi wa kwanza kujiendeleza****** kwa masomo ya juu nje ya Tanganyika na ndivyo alivyoanza kupata masomo ya fasihi ya Kiingereza na mantiki. Alifaulu vizuri sana na mambo yake ni kama yalivyo ‘mwenye macho haambiwi tazama’.

Alistaajabisha sana watu, sababu kila aliyekutana naye akiwa mdogo wake, yeye humwita ‘kaka’ daima, hiyo ndiyo iliyokuwa tabia yake. Kwa mtu ye yote aliyekuwa makamo yake alimwita ‘bwana mkubwa’ au ‘babu’. Zaidi alikuwa yeye tayari kila wakati kukidhi haja kwa yeyote aliyekuwa na haja ya lake.

Inasemekana kuwa ilikuwa Septemba alipoingia ofisini kwa Mwalimu wa Kizungu, Tanga. Alipewa barua ili akapimwe katika hospitali. Aliporudisha majibu yalionekana kuwa safi, mganga alitumia maneno, “fit for service”*******.

Hivyo alipelekwa forodhani Tanga, na huko kwa mara ya kwanza Shaaban Robert aliyaaga maisha aliyokuwa akiyapenda ya ‘utoto na mwanafunzi’ na kuanza kuonja kuwa mtu mzima, mfanyakazi na mwenye kujitegemea.

Mwaka 1926 hadi 1944 alikuwa karani wa Idara ya Forodha. Halafu alihamishiwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga mpaka mwaka 1952. Pia akapelekwa katika Idara ya Upimaji Ardhi mpaka mwaka 1960 alipostaafu.

Katika kipindi hicho cha kazi, alionyesha utendaji wake wa kazi wa hali ya juu. Mara nyingi kilichodhaniwa kinaweza kufanywa na Mzungu tu, marehemu Shaaban alikifanya kwa ufanisi mkubwa. Kwa hali hiyo alipandishwa vyeo au daraja kadha wa kadha kwa umahiri wake na juhudi zake katika kazi.

Hakuelemea katika mapenzi ya kazi tu, bali alikuwa akizama katika falsafa ya lugha na fani zake. Sheikh Shaaban Robert hapana shaka ni bingwa wa fani mbali mbali; ni msanii na mtaalam aliyeiva katika taaluma mbalimbali.


Maelezo

* В словосочетаниях malezi ya kiumeni “воспитание в мужской среде” и malezi ya kikeni “воспитание в женской среде” локативная форма обусловлена необходимостью отличить их от несколько других по смыслу выражений. Сравните: malezi ya kiume “мужское воспитание” и malezi ya kike “женское воспитание”.


** Префикс субъекта в глаголах, оформленных показателем -ka-, может опускаться, но это относится только к существительным одушевленного класса в 3-ем лице ед. числа (kalelewa; kafaulu; kapata). Форма keshafanya образована в результате слияния показателей -ka- и -isha-.
*** ukiachilia/ukiacha “не считая”, “не принимая во внимание”.
**** mapema mwaka 1920 “в начале 1920 года”.
***** DC (District Commissar) “районный комиссар” (заимствование из английского языка).
****** Alikuwa wa kwanza kujiendeleza kwa masomo ya juu nje ya Tanganyika Он был первым, кто получил (получившим) высшее образование за пределами Танганьики”. После порядковых числительных или таких слов как “первый”, “последний”, в суахили обычно употребляется глагол в инфинитивной форме. На руский язык такой оборот переводится придаточным предложением или причастием.
******* fit for service “годен“ (из английского языка).
Mazoezi

2. Дайте русские эквиваленты:

malezi ya pande mbili; malezi ya kimila na desturi; mwalimu alikuwa kama mzee wake, babu na mlezi maalum; hali hii ilimkumba pia; -omba nafasi ya kusoma; majibu yalitoka; -zungumza kwa hamu kubwa; alifanya jambo la pekee; malezi yalimpamba kwa upole, utii na ukweli; hakuishia hapo kielimu; alimfungulia pazia la masomo ya nje; -jiendeleza kwa masomo ya juu; mtu aliyekuwa makamo yake; alikuwa tayari kukidhi haja kwa ye yote; majibu yalionekana kuwa safi; aliyaaga maisha ya 'utoto na mwanafunzi’; -onja kuwa mtu mzima; utendaji wa kazi wa hali ya juu; bingwa wa fani mbali mbali; msanii aliyeiva katika taaluma mbali mbali.


3. Переведите следующие выражения и составьте с ними предложения:

традиционное воспитание; арабский алфавит; интеллигентный человек; учиться заочно; совершенствовать свои знания; законы логики; удовлетворять потребности; уходить в отставку; производительность труда; высокое мастерство; деятель искусств; специалист высокого класса.


4. Ответьте на вопросы к тексту:

1. Nini asili yake Shaaban Robert? 2. Malezi ya kimila na desturi alipata wapi? 3. Elimu gani alijifunza shuleni? 4. Kwa nini baba yake akamleta Dar es Salaam? 5. Ni kitu gani kilichomleta Tanga tena? 6. Alipokuwa shuleni alisoma vipi? 7. Shaaban Robert alikuwa na sifa gani? 8. Masomo ya fasihi ya Kiingereza na mantiki aliyapata kwa njia gani? 9. Alionyesha dalili gani za malezi bora alipokutana na watu? 10. Baada ya kuacha maisha ya ‘utoto na mwanafunzi’ alikuwa akishughulika na kazi gani? 11. Katika kipindi cha kazi alionyesha tabia gani? 12. Shaaban Robert ametoa mchango gani katika ukuzwaji wa lugha na fasihi ya Kiswahili?


5. Дайте эквиваленты на суахили, обратив внимание на локативную форму существительных:

горькая жизнь на чужбине; маленький сельский домик; настольные часы моего дяди; чистый горный воздух; далекие детские годы; вкусная морская рыба; новая космическая станция; скудные растения пустыни; обычные школьные занятия; промышленность страны; дикие охраняемые животные; звонкие церковные колокола; большой настенный календарь; много книжных иллюстраций; красный шейный платочек; древние обитатели лесов; тяжелые полевые работы; веселые походные песни; разнообразные уличные фонари.


6. Переведите:

1. Российские спортсмены были первыми, кто поднялся на эту вершину. 2. Кениец был вторым, победившим в беге на 100 метров. 3. Тату была последним свидетелем, кого заслушали в суде. 4. Ему сказали, что он будет пятым при получении награды в Кремле. 5. Маленькая девочка была последней из спасенных в океане после кораблекрушения. 6. Я обещаю, что ты будешь первым, кому я раскрою свой секрет. 7. Мы были последними, кто пришел на станцию проводить деятелей искусств из США. 8. Ваш дом будет четвертым по счету в этом районе, где будут производиться ремонтные работы.




7. Переведите письменно текст:

Wahenga wetu

Watunzi mbali mbali wa mashairi na waandishi wa vitabu walijitahidi sana kuijenga na kuipanua lugha yetu ya Kiswahili. Watunzi hao waliudhihirishia ulimwengu kwamba lugha ya Kiswahili si duni. Ni lugha yenye fasihi yake ambayo huweza kupangwa kisanaa ikavutia watu. Si hivyo tu, bali lugha hii yaweza kuueleza utamaduni wetu, mila na jadi tulizozirithi kizazi baada ya kizazi.

Mmoja wa wahenga wetu maarufu alikuwa Shaaban Robert. Bingwa huyu alikuwa na karama ya utungaji wa mashairi na utenzi, pamoja na vitabu vya ufafanuzi na insha. Yeye alikuwa mmoja wa Waafrika wa kwanza kutunukiwa vyeo mbali mbali katika idara za serikali ya mkoloni, bali popote alipopelekwa, ubingwa wake wa utunzi ulivuma. Habari zake nyingi hupatikana katika kitabu chake "Maisha yangu na baada ya miaka hamsini”. Pia ameandika “Kusadikika”, na “Marudi Mema”, “Pambo la Lugha”, “Kielelezo cha Insha”, “Diwani ya Shaaban Robert” na vinginevyo. Kitabu chake cha “Wasifu wa Siti binti Saad” humweka Shaaban katika daraja la wahenga wasio na choyo. Kwa kufanya hivyo ametufunulia maisha adili ya mwimbaji huyu mwanamke ambaye pengine tusingejua habari zake.

Ubingwa wa Shaaban waweza kutambulika kwa jinsi alivyoweza kuyatumia maneno ya Kiswahili kwa ufasaha. Ingawa lugha atumiayo ni ngumu kidogo, alikuwa na karama ya kutumia maneno ya Kibantu akijaribu sana kuepa utumiaji wa maneno ya kutoka ughaibuni.

Marehemu huyo alisimama imara katika kutoa mafundisho juu ya unyenyekevu, kuheshimiana, pamoja na kuthamini kazi. Amesema katika maandishi yake kuwa mtu avunaye kazi za mikono yake huvuna furaha ya moyo wake, hivyo furaha yake ni timilifu. Aliwadharau matajiri na mabepari waliolima kwa nguvu za wenzao.

Mhenga mkuu mwingine alikuwa Mathias Mnyampala. Wakati wa kifo chake vitabu vyake viwili vilikuwa mikononi mwa wahariri. Yeye pamoja na kikundi cha wenzake walianzisha Chama cha UKUTA ambacho madhumuni yake yalikuwa ni kukikuza Kiswahili. Mhenga Mnyampala alifanywa mwenyekiti wa Chama hicho. Tena alikuwa mwanachama mashuhuri wa Kamati ya Kiswahili ya Taifa. Kitabu chake cha “Ngonjera* za UKUTA” kilichopigwa chapa baada ya kufa kwake ni johari thabiti miongoni mwa vitabu vya lugha.

Licha ya kazi hizo Bwana Mnyampala, ametunga kitabu kitokeacho katika mfululizo wa Johari za Kiswahili. Kitabu hicho ni “Diwani ya Mnyampala”. Mashairi ya Mnyampala ni ya mitindo mbalimbali. Husimulia matukio kama vile sikukuu za Taifa, mambo ya dini, ukuaji wa nchi yetu na ustawi wake, upanukaji na umaarufu wa lugha ya Kiswahili. Pia yamo mashairi mawili ya wasifu wa Shaaban Robert.
Maelezo

** Ngonjera – особый жанр стихотворного произведения в форме беседы, спора или дебатов, исполняемого в сопровождении музыки. Этот жанр очень распространен в Танзании и заключает в себе назидательный, поучающий смысл. Исполняется обычно самодеятельными коллективами. В русском языке нет точного эквивалента.
8. Перескажите текст “Wahenga wetu”, используя следующие выражения:

watunzi wa mashairi; lugha yenye fasihi yake; -pangwa kisanaa; -rithi kizazi baada ya kizazi; karama ya utungaji wa mashairi na utenzi; vitabu vya ufafanuzi; ubingwa wake wa utunzi ulivuma; wasifu wa mwimbaji mashuhuri; -funua maisha adili; -tumia maneno kwa ufasaha; -epa utumiaji wa maneno ya ughaibuni; -toa mafundisho juu ya unyenyekevu; furaha yake ni timilifu; -wa mikononi mwa wahariri; -pigwa chapa; mfululizo wa johari za Kiswahili; mashairi ya mitindo mbalimbali.


9. Переведите, обратив внимание на перевод русских причастных оборотов и условных предложений:

1. Он рассказывал мне об этом, улыбаясь. 2. Гуляя по лесу, надо быть внимательным. 3. Они ушли, забрав свои словари. 4. Читая газету, мой брат все время кашлял. 5. Они сидели молча, не глядя друг на друга. 6. Еще будучи ребенком, он часто плавал в том озере. 7. Будучи суровым человеком, она с трудом находила себе друзей. 8. Находясь на работе, не стоит долго разговаривать по телефону с друзьями. 9. Если ты его увидишь, отдай ему ключи от гаража. 10. Если сестра дома, я попрошу ее помочь мне. 11. Если мы не выедем из дома рано утром, то опоздаем на поезд. 12. Если мамы нет на кухне, поищите ее в саду.


10. Сделайте письменный перевод отрывка из произведения Шаабана Роберта “Insha na mashairi ”:
Wanyama wengi sana huweza kuogelea vema mara wakiingia katika maji. Mbwa, farasi, simba, ng’ombe na wengine hawana lazima ya kufundishwa kuogelea. Bali mtu hawezi kuogelea mpaka amejifundisha. Mtu ajuaye hana budi kumfundisha asiyejua kuogelea.

Baadhi ya mambo husahaulika baada ya kuyajua, lakini kuogelea hakusahauliki. Kuogelea hakuhitaji akili nyingi na mazoezi ya mfululizo. Akili ya wastani na mazoezi ya kitambo huweza kumfanya mtu kuwa mwogelea hodari.

Kila mtu hana budi kujua kuogelea. Tena ni bora kujifundisha wakati wa kuwa vijana. Mvulana au msichana huweza kujifundisha upesi kuliko mtu mzima. Walakini watu wengi hawajui kuogelea hata kidogo. Husemwa kwamba hata baadhi ya mabaharia, ambao huishi maisha yao yote katika bahari, hawajui kuogelea!

Kwa nini watu hawana budi kujifundisha kuogelea? Kwanza, kwa sababu ni namna nzuri sana ya taaluma au mazoezi. Hasa waganga husema kwamba ni taaluma bora, kwa sababu katika kuogelea musuli zote za mwili hutumika.

Pili, kuogelea huleta furaha kubwa. Katika siku za hari wakati wa kaskazi mtu huona furaha iliyoje kuvua nguo zake akajitosa katika maji baridi ya mto, au bahari, na kupiga mbizi na kuogelea na kuelea mpaka akachoka!

Tatu, kuogelea huweza kuwa kitu kingine kabisa kati ya maisha na mauti pengine. Huweza kuleta salama au wokovu wa maisha yetu. Hatujui siku ya kuwa katika hatari ya maji. Twaabiri tukasafiri, merikebu ikavunjika; twenda tukajifurahisha kwa kutweka katika ziwa, mashua ikapinduka; twateleza wakati wa kwenda juu ya ukingo wa mto, tukaanguka katika maji. Kama twaweza kuogelea, tuna nafasi ya kuokoa maisha yetu; bali kama hatuwezi, tuna hakika kubwa ya kufa maji. Basi kwa ajili ya salama yetu wenyewe, hatuna budi kujifundisha kuogelea.

Zaidi, kama twaweza kuogelea, tutaweza kuokoa watu wengine wasife maji. Ni vizuri vilioje kuweza kuokoa maisha ya mtu mwingine! Huwa huzuni kubwa kuona rafiki anakufa maji mbele ya macho yetu, wakati hatuwezi kumsaidia, kwa sababu hatuwezi kuogelea.
11. Переведите:


  1. Шаабан Роберт был интеллигентным и благородным человеком, готовым выполнять просьбы простых людей, обращавшихся к нему за помощью.

  2. Талант, которым он обладал, позволил ему заявить о себе как о великом писателе, чье творчество вошло в сокровищницу африканской литературы.

  3. Шаабан Роберт не ограничился знаниями, которые он приобрел в школе, и решил продолжить свое образование, изучая заочно английскую литературу и логику.

  4. Любую работу, которую ему поручали, он выполнял с большим мастерством и знанием дела, так что его неоднократно повышали в должности.

  5. Этот писатель был одним из тех, кто раскрыл огромные возможности суахили и показал всему миру, что это далеко не примитивный язык, и, что на нем можно создавать художественную литературу.

  6. Матиас Мньямпала, который также внес большой вклад в развитие суахили, создавал стихотворные произведения, описывал важнейшие события в жизни нации, восхвалял родной язык. Два его поэтических произведения посвящены описанию жизни Ш. Роберта.


Msamiati

malezi (мн.) воспитание, abjadi (-) алфавит

обучение (ребенка) adili, adilifu порядочный,



ufasaha (ед.) красноречие, благородный

хороший стиль (речи, письма) ughaibuni очень далеко,



ziada (-) дополнение, добавление на краю света

msomi (wa-) образованный pazia (ma-) ширма,

человек; интеллигент занавес



musuli (-), msuli (mi-) мускул timilifu завершенный;

wastani (ед.) средняя величина цельный

kidato (vi-) образовательный mhariri (wa-) редактор

класс (в средней школе) mantiki (-) логика



unyenyekevu (ед.) почтительность, johari (-;ma-) драгоценность,

снисходительность сокровище



-onja пробовать; испытывать -sadiki верить

umahiri (ед.) мастерство, -jitosa погружаться

квалификация kitambo (vi-) 1) короткий



mahiri умелый, искусный промежуток времени

-kidhi удовлетворять, 2) небольшое расстояние

исполнять hari (-) теплота, жар, зной



-elemea давить, придавливать; falsafa (-) философия

быть грузом (на чем-л.) mauti (-) смерть



msanii (wa-) деятель искусств -abiri ехать, путешествовать

(артист, художник, певец и т.д.) (на корабле, поезде и т.д.)



ufafanuzi (ед.) объяснение, -tweka водружать,

толкование устанавливать



-fafanua разъяснять, толовать mtunzi (wa-) сочинитель,

wokovu (ед.) освобождение; автор

спасение utenzi (tenzi) поэма,



-vuma славиться сказание в стихах

diwani (ma-) сборник стихов karama (-) дар (божий),

mhenga (wa-) 1) предок, талант

прародитель 2) мудрец wasifu (ед.) биография

3) предшественник жизнеописание;

-teleza скользить; быть -dhihirisha пояснять,

скользким обосновывать; раскрывать


* * *

Урок 31. Somo la thelathini na moja
Повторение грамматики:
1. Распределите следующие слова и словосочетания по группам в зависимости от грамматических моделей, по которым они образованы. Дополните списки своими примерами:

nani/nini: mchoraji; ujenzi; kivutio; maulizo; kuwasilishwa; upelekaji; somo; mhukumiwa; uandishi; mzima moto; kuendelezwa; uboreshaji; maendeleo; uongozi; mwanzilishi; mpenzi; uvutaji; kipato; mwendeshaji; utabiri; matumizi; kupatikana; mwandikiwa; kitendo; vyombo vya kulimia; mwokozi; mpanda baisikeli; maoni; mpishi; msema kweli; mpatanishi; mpendwa; msomi; kivuko; silaha za kuwindia; uhariri.
gani: shauri la kirafiki; mtumishi mtiifu; sura ya kupendeza; ndizi za kupikika; hadithi yenye kusisimua; mwanafunzi mwangalifu; apendaye kuimba; siku za karibuni; darasa la kwanza; kitabu cha kutafsiriwa; nchi ya mbali; msitu usiopitika; matunda ya sokoni; mtunzi mahiri; kisa chenye kuhuzunisha; njia ya kimaendeleo; mwandishi anayesimuliwa.
vipi: kujeruhiwa vibaya; kujenga kitaalamu; kusoma kwa makini; kukimbia haraka haraka; kujadili kwa kituo; kutazama kwa uangalifu; kusherehekea kitaifa; kuchoka sana sana; kuua kinyama; kusema kwa ufasaha.
2. Перечислите все известные вам производные формы от следующих глаголов:

-staafu; -pita; -fumba; -piga; -ruhusu; -kimbia; -zindua; -la; -furahi.


MAKEBA – MWANAMUZIKI NYOTA

WA AFRIKA

Mwanamuziki mashuhuri barani Afrika, Miriam Makeba wa Afrika Kusini alianza kuvuma katika ulimwengu wa muziki miaka ya 50 na 60. Katika mwaka 1972 alianza kujulikana kama mwanamuziki nyota wa kimataifa na kujipatia sifa kemkem sehemu mbalimbali duniani baada ya kutoa albam yake ijulikanayo kama “Kokoliko”.

Hata hivyo katika mwanzo wa kujulikana katika fani hiyo, Makeba alitunga nyimbo kadhaa na kutembelea sehemu nyingi duniani kwa kufanya ziara za maonyesho ya muziki ambapo katika ziara zake hizo aliwaburudisha na kuwasisimua watu kwa vibao vyake murua.

Mwaka 1977, Makeba kwa kushirikiana na mwanamuziki Miata Fahnubelleh, walionyesha kuanzisha ushirikiano mzuri ambao ungekuwa kielelezo kwa wanamuziki wengine kuwa na uhusiano mwema katika maisha na maendeleo ya fani yao.

Mwaka 1988, Makeba alitumbuiza kwenye uwanja wa Wembley, London wakati wa kusherehekea rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela kutimiza miaka 70 alipokuwa bado amefungwa gerezani. Katika onyesho hilo, watu waliohudhuria walijikuta wakitokwa machozi na onyesho hilo limeelezwa kuwa ni la aina yake* na kubwa kuliko yote yaliyowahi kufanywa na wanamuziki wote wa Afrika, hususan wanawake.

Makeba pia aliwahi kuimba ama kufanya maonyesho pamoja na wanamuziki maarufu duniani wakiwemo Madonna, mwanamuziki nyota wa muziki wa reggae** wa Afrika Kusini, Lucky Dube, Harry Belafonte na Dorothy Masuka.

Mwaka 1988, mwanamama huyo alitangazwa kuwa balozi wa Afrika katika muziki, hasa kutokana na kazi kubwa aliyoifanya wakati wa vita dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini.

Makeba ambaye alizaliwa mwaka 1932 katika familia yenye uwezo,*** aliingia katika ulimwengu wa muziki na kuwa mwanamuziki maarufu kutokana na nyimbo zake zinazogusa hisia na hali halisi ya maisha ya watu. Hiyo iliambatana na kipaji chake katika kuimba ambapo sauti yake ilionekana na utamu wa aina yake.*

Alimtegemea sana baba yake ambaye alifariki wakati mwanamuziki huyo alipokuwa na umri wa miaka minane. Baada ya kufa baba yake ambaye alikuwa ndiye mtafutaji wa chakula, Makeba alilazimika kwenda kufanya kazi kwa ajili ya kujipatia mahitaji muhimu kwa maisha yake na pia kuweza kuwasaidia kaka zake wawili na mdogo wake wa kike.

Wakati huo ndipo alipogundua kwamba muziki ndiyo kazi ambayo ingemwezesha kuepukana na kazi aliyokuwa akiifanya wakati huo ya utumishi wa nyumbani. Hata hivyo, kabla hajaamua kujiingiza katika fani ya muziki, Makeba alikuwa akifurahia kuimba kwaya kanisani pamoja na kwamba alikuwa hajapata uzoefu wa kumwezesha kupiga muziki wa kujiamini.

Wakati ubaguzi wa rangi ulipoanzishwa chini ya utawala wa makaburu, Makeba alikuwa amefikia umri wa miaka 15 na tayari alikuwa ameanza kujulikana katika masuala ya muziki.

Kadiri miaka ilivyokuwa ikienda mbele, ubaguzi ndiyo ulikuwa ukizidi kujichimbia mizizi**** na ulionekana kuwa ni kikwazo kwa wanamuziki wanaochipukia kupata mafanikio. Hivyo, Makeba alianza kuimba nyimbo za kukemea siasa za ubaguzi wa rangi na vitendo vilivyokwenda kinyume na ubinadamu na ndipo watu walipoanza kumsikiliza na kuvutiwa na nyimbo zake.

Nyota yake ya kutaka kujulikana katika ulimwengu wa muziki ilikuja kuanza kutoa mwanga mwaka 1959 wakati alipopata sehemu ndogo katika filamu ya “Come Back Africa” ambayo ilimwonyesha sehemu mbalimbali duniani na kumwezesha kutembelea sehemu kadhaa ikiwemo New York.

Baada ya kutembelea New York, Marekani, alipata mialiko mingine mbalimbali ya kuimba kwenye televisheni na kufanya maonyesho ya muziki kwenye klabu kadhaa. Pia aliwahi kualikwa kwenda kutumbuiza kwenye tafrija ya kuzaliwa rais wa zamani wa Marekani, John F. Kennedy.

Rafiki zake na waimbaji wenzake walimsaidia kutunga nyimbo kama “Pata pata” na kuimba wimbo uliotungwa kwa mara ya kwanza na mwanamuziki Fadhili William “Malaika” ambao hadi sasa umeleta mkanganyiko miongoni mwa wapenzi wa muziki juu ya nani mtunzi hasa na mwenye haki ya wimbo huo.

Makeba alizuiliwa na serikali ya Afrika Kusini ya wakati huo kuingia nchini humo na alilazimika aendelee kuishi New York, Marekani kama mkimbizi wa kisiasa. Mwaka 1960 alipata misukosuko baada ya kuzuiliwa kuingia Afrika Kusini kwenda kumzika mama yake.

Mwanamuziki huyo, ambaye vibao vyake vingi vimetokea kupendwa sehemu mbalimbali duniani, alibaki nje ya nchi kwa miaka 30 na alirudi nyumbani baada ya kutokomezwa kwa ubaguzi wa rangi.
Maelezo

* -a aina yake “своеобразный”, “бесподобный”. Сравните: -a aina ya pekee “специфический”, “единственный в своем роде”.
** muziki wa ‘reggae’ “музыка в стиле ‘рэгги’”.
*** familia yenye uwezo – “обеспеченная семья”.
**** -jichimbia mizizi “зарываться, окапываться”.
Mazoezi

3. Дайте эквиваленты на суахили:

alianza kuvuma; mwanamuziki nyota wa kimataifa; alijipatia sifa kemkem; ziara za maonyesho ya muziki; aliwaburudisha watu kwa vibao murua; kielelezo kwa wanamuziki wengine; watu walijikuta wakitokwa machozi; alitangazwa kuwa balozi wa Afrika katika muziki; vita dhidi ya ubaguzi wa rangi; familia yenye uwezo; nyimbo zinazogusa hisia na hali halisi ya maisha ya watu; sauti ya utamu wa aina yake; hii iliambatana na kipaji chake; mtafutaji wa chakula; kazi ya utumishi wa nyumbani; -piga muziki wa kujiamini; alikuwa hajapata uzoefu; -jichimbia mizizi; utawala wa makaburu; -onekana kuwa ni kikwazo; nyimbo za kukemea siasa za ubaguzi wa rangi; vitendo vilivyokwenda kinyume na ubinadamu; wimbo umeleta mkanganyiko miongoni mwa wapenzi wa muziki; alipata misukosuko; aliishi kama mkimbizi wa kisiasa; ubaguzi wa rangi ulitokomezwa.


4. Переведите:

1. Она прославилась в мире музыки. 2. Эта певица стала звездой мирового класса. 3. Она завоевала огромную популярность. 4. Мы посетили фестиваль музыки. 5. Она гастролировала во многих странах. 6. Эта замечательная мелодия очень бодрит. 7. Известный музыкант выступит сегодня по телевидению. 8. Она родилась в обеспеченной семье. 9. Ее песни затрагивают чувства людей. 10. Ее талант сочетался с огромным трудолюбием. 11. Я верю в свои силы и способности. 12. Мы накопили большой опыт в этих вопросах. 13. Его песни обличали политику расовой дискриминации. 14. Народы мира выступили против режима апартеида. 15. Это идет вразрез с нашими интересами. 16. Он стал политическим беженцем. 17. С неравенством было покончено.


5. Выпишите из текста предложения, в которых глаголы -ja, -enda, -tokea употреблены в своем вспомогательном значении.
6. Переведите письменно следующие заметки:
Tamasha la sanaa kufunguliwa leo

Tamasha la mwaka huu la sanaa la chuo cha sanaa cha Bagamoyo litafunguliwa rasmi leo na balozi wa Norway nchini.

Kabla ya ufunguzi rasmi kutakuwa na maandamano ya wasanii na wakazi wa mji wa Bagamoyo kabla ya kumalizikia kwenye chuo hicho litakakofanyika tamasha hilo.

Kwa mujibu wa ratiba ya maonyesho iliyotolewa jana, chuo kitafanya maonyesho manne: siku ya ufunguzi, Jumanne, Jumatano, Ijumaa na siku ya ufungaji Septemba 28.

Bendi mbili zinatarajiwa kutoa burudani wakati wa tamasha hilo. Maonyesho yote ya vikundi vya sanaa yatafanyika kwenye ukumbi mpya wa maonyesho ambao ulikabidhiwa kwa serikali ya Tanzania kutoka kwa serikali za Sweden, Norway na Denmark kwenye sherehe za mwaka jana za tamasha la tisa la sanaa.
Nataka kuwa mwanamuziki wa kimataifa

Mwanamuziki Fresh Jumbe amesema lengo kubwa alilo nalo kwa sasa ni kujitangaza ili akubalike kimataifa.

Jumbe ambaye anaishi na kupiga muziki Japan, alisema hayo jana alipohojiwa katika kipindi cha Radio Uhuru.

Alisema ijapokuwa amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuutangaza muziki wa Tanzania nchini Japan na yeye binafsi kujulikana huko, lakini dhamira kuu aliyo nayo ni kuwa mwanamuziki wa kimataifa.

“Lengo langu ni kuwa mwanamuziki wa kimataifa, baada ya hapo nitafanya juhudi za kuwanyanyua wanamuziki wengine wa Tanzania ili nao waweze kufanikiwa,” alisema.

Jumbe ambaye anamiliki bendi mbili nchini Japan, alisema hivi sasa ana wanamuziki watatu katika moja ya bendi zake iitwayo ‘African Express’ ambapo alimtaja mmoja kuwa ni Abuu Omari anayepiga gitaa la solo.

Mwanamuziki huyo alirejea nchini wiki iliyopita kwa ajili ya kuhani msiba wa baba yake aliyefariki dunia mwezi uliopita. Alisema baada ya kuhani msiba huo, atafanya mipango ya kushiriki katika maonyesho ya bendi za Tanzania alizozipigia kabla ya kuondoka nchini mwaka.

7. Дайте синонимы или объясните на суахили значение следующих слов и выражений:

bingwa; umahiri; -kidhi haja; ufanisi wa kazi; mtu wa makamo; msomi; msanii; mhenga; -fafanua; wasifu; ughaibuni; kitambo; hari; -vuma; sifa kemkem; -burudisha; murua; -tumbuiza; -ambatana; kipaji; -pata uzoefu wa kazi; kikwazo; -pata misukosuko; -nyanyua.


8. Переведите:

  • Имя Мириам Макебы хорошо известно среди любителей африканской музыки, так как это одна из звезд мировой эстрады, которая гастролировала во многих странах и завоевала огромную популярность благодаря своему уникальному голосу и таланту.

  • Во время ее концертов, когда она исполняла песни, посвященные простому народу и осуждающие политику расовой сегрегации, многие зрители с трудом сдерживали слезы.

  • Звезда Мириам Макебы вспыхнула по-настоящему на музыкальном небосклоне после 1959 года, когда она исполнила небольшую роль в художественном фильме “Возвращение в Африку” и стала получать много приглашений.

  • Танзанийский музыкант Фреш Джумбе, проживающий в Японии, заявил о своем намерении прославиться на весь мир и обещал, что сделает все возможное, чтобы помочь исполнителям из других музыкальных групп Танзании также добиться успеха.


Msamiati

ulimwengu (ед.) мир, свет; albam (-) альбом

вселенная kwaya (-) хор



kemkem много; во множестве gereza (ma-) тюрьма

-burudisha 1) охлаждать; бодрить kaburu (ma-) 1) бур, белый

2) развлекать, веселить поселенец 2) расист



kibao (vi-) песня, мелодия, utawala wa makaburu

музыкальное произведение режим апартеида



murua прекрасный, sifa (-) 1) положительное

замечательный; важный качество, достоинство



mkanganyiko (mi-) недоумение, 2) слава, известность

замешательство kipaji (vi-) 1) лоб



-sisimua 1) вызывать трепет, 2) талант, дарование

возбуждать 2) потрясать tafrija (-) 1) праздник,



kielelezo (vi-) 1) модель, образец торжество 2) развлечение

2) объяснение, описание ratiba (-) расписание,



-tumbuiza петь, напевать, график

исполнять песню malaika (-) ангел,



tamasha (;ma-) 1) зрелище, добрый дух

представление 2) фестиваль mkimbizi (wa-) беженец,



-ambatana сопровождаться беглец

msukosuko (mi-) 1)волнение, ubaguzi wa rangi расовая

беспокойство 2) беспорядки (мн.) дискриминация



-hani оплакивать, горевать; -tokomeza 1) уничтожать,

участвовать в траурной убивать 2) устранять

церемонии -dhamiria намереваться

beni, bendi (-) оркестр, dhamira (-) цель,

музыкальный ансамбль намерение



* * *

Урок 32. Somo la thelathini na mbili
Повторение грамматики:
1. Составьте предложения с глаголами -kumba; -vuma; -staafu; -goma; -songamana; -itisha; -karabati в аналитических конструкциях. Воспользуйтесь приведенной ниже таблицей наиболее характерных сочетаний глагола -wa со смысловыми глаголами в таких конструкциях:

-li-/-ta- … -ki- -me- … -ki-

-li-/-ta- … -na- -ki- … -na-

-ngali- … -na- -ki- … -me-
2. Составьте предложения с глаголами -chapisha; -pachika; -zindua; -rekebisha; -adhimisha в аналитических конструкциях по образцу:

-chimba: Kisima cha maji kiwe kimechimbwa kabla ya kuanza msimu wa masika.

-lipa: Mishahara ya wafanya kazi iwe inalipwa kila mwezi bila ya kucheleweshwa.
3. Используйте существительные wakimbizi; utawala wa makaburu; mantiki; karama в предложениях, составленных по модели -li-/-ta- … -po/-ko/-mo, например:

watembezi:Tokea vita vilipoanza watembezi walikuwa hawapo tena kwenye maonyesho haya.
4. Составьте предложения со следующими глаголами, употребив все возможные варианты выражения модальности:

-fafanua; -wasili; -fuatilia; -sadiki; -onja; -kidhi.



5. Переведите текст:

Shafi Adam Shafi gwiji wa fasihi

Adam Shafi alizaliwa mjini Zanzibar mwaka 1940. Baada ya elimu yake ya shule ya msingi alijiunga na chuo cha ualimu cha Seyyid Khalifa (sasa chuo cha ualimu cha Nkrumah) mwaka 1957 hadi mwaka 1960. Alipata diploma ya juu katika fani ya siasa ya uchumi katika iliyokuwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Ujerumani mwaka 1963. Alipata mafunzo ya uandishi wa habari mjini Prague nchini Czechoslovakia (sasa Jamhuri ya Czech) mwaka 1964 hadi mwaka 1965, nchini Sweden mwaka 1982 na nchini Marekani mwaka 1983.

Waandishi ni watazamaji na wasikilizaji wakubwa wa jamii. Waandishi ndiyo hutukumbusha yaliyotokea. Kusingekuwepo waandishi tusingefahamu yaliyopita. Kila mmojawetu kila siku anahangaika na maisha. Tunaamka, tunakula, tunakwenda kazini au masomoni. Tunarudi, tunalala, kesho yake hayo hayo: kila kukicha na kuchwa tunaona mengi, tunayapita, tunayasahau. Ila waandishi? Wasanii? Kazi yao kuweka kumbukumbu ya haya mambo. Kuyahadithia.

Wapo waandishi wa aina nyingi. Wanahabari. Waandishi wa elimu na historia. Washairi. Watunzi wa muziki na nyimbo. Sinema. Tamthiliya. Wapo waandishi wa fasihi kama Adam Shafi.

Shafi alianza na kitabu cha “Kuli”, kinachoelezea mgomo maarufu wa wafanyakazi maskini, Unguja mwaka 1948. Mwenyewe anasema alikuwa na miaka minane tu. Na ingawa anakumbuka juu ya tukio hilo utotoni, alikuja kuhadithiwa na mtu akaweka kumbukumbu na baadaye maandishini. “Kuli” kilichapishwa Tanzania miaka ya sabini.

Baadaye kikafuata “Kasri ya Mwinyi Fuad”. Na miaka karibuni Shafi kaibuka na “Vuta N’kuvute”, kitabu kilichopata tuzo kwenye tamasha la vitabu, Dar es Salaam, mwaka 1998. Ni kisa cha mapenzi, tena mapenzi makali na mazito kati ya mtoto wa Kihindi na Mwafrika. Humo mna siasa na harakati za uhuru na mengi mengine. Mseto wa mapenzi na siasa, ambao si waandishi wengi wa Kiswahili wamemudu kuufanya.

Mwaka 2003 mwanafasihi huyu akatoka na “Haini” ambacho kama anavyosema mwenyewe kiliogopwa na wachapishaji wengi nchini. “Haini” si mchezo. Kitabu cha joto, cha moto, cha kuchachafya.

Kama kawaida visa vyote vya Shafi hujaa mateso, shida, majonzi, taabu za Mwafrika; lakini haviishii na hisia hizi za kukata tamaa na kutokwa machozi. Wahusika wake huteseka lakini mara wakaibuka, wakaamka na kupamba na matatizo yao. Matumaini ndiyo rangi ya suluhisho lake.

Maandishi yake gwiji huyu wa fasihi huchanganya kila kitu: furaha, simanzi, vita, amani, mapenzi, karaha, starehe, maonyo, elimu na mengine tele. Mwenyewe Shafi ni mtu wa kawaida kabisa, inawezekana kuiita hulka, tabia na namna yake “mfurahia maisha”: kachangamkia uhai, hasa. Kaishi, anaishi… hamalizi. Kila mara, atasema, ana mikakati ya kufanya jambo fulani, kuandika kitabu kingine kipya, kuendeleza fasihi na Kiswahili…

Anasema huchukua wastani wa miaka mitano kumaliza kitabu kimoja. “Huwa sina haraka hata kidogo…” Huandika kwanza kwa mkono halafu ndiyo akachapa katika tarakilishi.

Vitabu vyake vyote Shafi vinaonyesha maisha ya sasa na yale yaliyopita. Anapenda kuhusisha historia ya jamii. Kwa hivyo mbali na kustareheshwa unafahamishwa mambo yaliyopita ya zamani.
6. Дайте русские эквиваленты:

-jiunga na chuo cha uandishi wa habari; -pata diploma ya juu; fani ya siasa na uchumi; watazamaji na wasikilizaji wa jamii; -hangaika na maisha; jihanagaisha na maandalizi ya mkutano; -hangaikia mitihani; kila kukicha na kuchwa, -weka kumbukumbu ya matukio; mwanahabari; mwandishi wa habari; mtunzi wa nyimbo na muziki; -weka maandishini; -ibuka na maandishi mapya; harakati za uhuru; mseto wa mapenzi na siasa; kitabu cha kuchachafya; hisia za kukata tamaa; si mchezo huo!; suluhu ya amani; -suluhisha ugomvi wa majirani; -jaa tele; maliasili tele; hulka ya binadamu; -husisha historia ya jamii.



7. Дайте эквиваленты на суахили:

поступать в вуз; вступить в общество литераторов; стать членом профсоюза; пройти курс ускоренного обучения; факультет журналистики; институт языкознания; суетиться по поводу работы; заботиться о хлебе насущном; каждый божий день; создавать себе множество проблем; брать на заметку слова выдающегося писателя; печальные события; быть охваченным горем; волнующая история; мирное урегулирование конфликта; улаживать ссору; наполнять бочку до краев; быть в изобилии; иметь многочисленных сторонников; радиожурналист; корреспондент газеты; спортивный комментатор; писатель; поэт; композитор; музыкант; драматург; телеведущий.


8. Переведите отрывки из романа Шафи А. Шафи Vuta Nkuvute”:

…Denge na Yasmin walibakia peke yao chumbani na kwa muda kidogo walikaa kimya kila mmoja akimtazama mwenzake. Kila mmoja alikuwa na maneno ya kutaka kumwambia mwenzake, lakini yalikwama yakawa hayatoki vinywani mwao. Denge aliondoka pale alipokuwa amekaa na kwenda kukaa na Yasmin juu ya kitanda. Aliushika mkono wake na kuupapasa, akimwambia, “Nilikusubiri sana siku ile.”

“Ilikuwa bahati mbaya.”

“Nilikuwa na hamu ya kukutana na wewe.”…


…Ilikuwa kiasi cha saa moja na nusu za usiku, Denge yumo chumbani mwake. Meza ndogo iliyokuwemo chumbani humo ilikuwa imezungukwa na makaratasi, Denge ameshughulika anaandika. Mlango uligongwa na bila ya kuinuka au kuangalia mlangoni Denge aliitika, “pita”.

Mlango ulifunguliwa taratibu na alipogeuka na kalamu yake mkononi Denge alimwona Yasmin amesimama mlangoni, uso wake umejaa tabasamu.

Denge alimwangalia Yasmin kama kwamba anamwona kwa mara ya kwanza kwa jinsi alivyozidi kupendeza. Nywele zake alizifunga vizuri kwa misokoto iliyokuwa kama matuta yaliyokaribiana. Uso wake ulizidi kunawiri na kanzu ya rangi ya zambarau aliyoivaa ilimkaa vizuri mwilini … Denge alimtazama akamwona kama bi.harusi aliyetayarishwa vizuri tayari kwa sherehe ya kuingia nyumbani.

“Mbona unan’tazama sana?” Yasmin aliuliza.

“Nani atakayekabiliwa na uzuri kama huo akaufumbia macho!”

Yasmin alicheka sana akakumbuka siku ile mazungumzo yao juu ya mapenzi yalivyoanza chumbani mwa Mwajuma. Aliingia ndani na kuusindika mlango. Alisogea karibu na ile meza na kuyaangalia makaratasi yaliyotawanyika mezani pale. “Unaandika nini?” aliuliza.

“Habari.”

“Habari gani?”

“Habari za kuwakashifu wakoloni wa Kiingereza na vibaraka wao jinsi wanavyowatesa wananchi, siyo Zanzibar tu bali Afrika nzima.”

“Sasa unamwandikia nani habari hizo?”

“Habari hizi nazipeleka katika gazeti moja nchi za nje.”

Yasmin aliyaangalia yale maandishi na kujaribu kuyasoma. Yaliandikwa kwa lugha ya Kiingereza na kwa elimu yake iliyoishia darasa la sita, Yasmin hakuweza kuelewa kiliandikwa nini ndani ya makaratasi yale. Alisogea karibu zaidi na kumpapasa nywele Denge akimwuliza, “Na kazi hii umeianza lini?”

“Zamani.”…
…Yasmin alipigwa na mshangao akabaki kumtazama Denge. “Huogopi hayo mambo unayoyafanya?” aliuliza.

“Niogope nini?”

“Huogopi kukamatwa? Kwanza unajua kwamba polisi wanakutafuta?”

“Najua sana kama polisi wananitafuta, wananifuata kila n’napokwenda lakini nimewashinda ujanja. Hata wakinikamata wakanifunga kazi hii itaendelea kwani siko peke yangu, tupo wengi, Zanzibar, Darsalama, Ulaya, kila pahala duniani.”

“Wanasema wewe koministi.”

“Nani?”


“Hao polisi.”

“Kwao wao kila mpinzani wao ni koministi, ndiyo silaha yao kubwa ya kutaka kuwapumbaza watu, siyo hapa tu, kila pahala ambapo kuna mapambano ya kupinga ukoloni. Sisi ugomvi wetu siyo makoministi wala siyo ukoministi, makoministi siyo wanaotutawala, ni wakoloni, wakoloni wa Kiingereza. Unajua hayo?” Denge aliyaeleza hayo akiwa sasa amebadilika kwani aliyokuwa akiyasema yalitoka ndani ya moyo wake, hakuna utani wala masihara.”

“Mimi siyaelewi hayo, lakini Denge jihadhari maisha yako, mimi najua kwamba polisi wanakutafuta, wanakutafutia sababu ndogo tu wakukamate,” kwa sauti ya unyonge huku uso ameuinama chini Yasmin alisema.

Darling! Hapana cha kuogopa, haya ni mapambano, mapambano ya vuta n’kuvute, ni vita, tena vita vikubwa kila mmoja anamuwinda mwenzake. Wao au sisi, lakini ushindi ni wetu, tutashinda tu.”


9. Переведите:

• Организация издателей Танзании (ПАТА) соорудила 50 павильонов в одном из выставочных залов Дар эс Салама для предстоящей недели книги, которая начинается в ближайшую пятницу. Павильоны предназначены для участников книжного фестиваля, который проводится в Танзании ежегодно.

Председатель организации ПАТА, выступая перед журналистами сказал, что среди участников фестиваля будут также представители Кении и Уганды.

Он также добавил, что в этом году планируется уделить особое внимание книжной продукции, предназначенной для учебного процесса в начальной и средней школах. Кроме того, будут демонстрироваться книги, имеющие важное значение для подготовки к выпускным экзаменам.

Авторы этих учебников, как пояснил председатель ПАТА, прошли специальную подготовку на курсах, проводившихся его организацией. Все они имеют большой опыт работы в соответствующих учебных заведениях и департаментах министерства образования и культуры Танзании.
• Правительство Занзибара намерено основать новый ежедневный печатный орган на языке суахили, задачей которого будет шире информировать население о тех положительных процессах, которые происходят в сельской местности.

Об этом было заявлено главой занзибарского правительства во время его беседы с корреспондентами по окончании семинедельных курсов совершенствования журналистского мастерства, проходивших в телевизионном центре Занзибара.

Он выступил с критикой в адрес двух правительственных газет, которые не удовлетворяют должным образом потребности населения в получении информации о внутренней жизни островной части Танзании.

Большинство существующих сейчас газет, а также сами журналисты, подчеркнул глава занзибарского правительства, в основном нацелены на освещение политических проблем и разногласий на Занзибаре, игнорируя усилия простого населения в своих регионах и его вклад в развитие всей страны.


10. Поставьте 10 вопросов к следующему тексту и расскажите на суахили о том, что такое канга:

Kanga

Kanga ni nguo ya desturi ya watu wengi wa Afrika ya Mashariki. Kanga ni kitambaa chenye umbo la mstatili (прямоугольник) na hiki kitambaa kina mabombwe (узоры) ya rangi nyingi mbalimbali. Kati kati ya mstatili kuna picha za wanyama, mimea, watu au maumbo mbalimbali.

Ukubwa wa kanga ni kutoka mkono wako mmoja mpaka mkono mwingine. Urefu ni kipimio baina ya shingo lako mpaka gotini. Au kipimio cha kanga ni inchi arobaini na nne upana wake na inchi sitini urefu wake.

Kitambaa cha aina hiyo kililetwa katika Afrika ya Mashariki kabla ya mwaka wa 1900, yaani wakati wa kuanzishwa biashara ya nje. Nguo hizi zilitoka Ulaya, Uhindini na nchi nyingine za mashariki. Wareno walileta kitambaa chenye mabombwe kukiuza kama leso.Wanawake walikata leso nusu nusu na halafu kuvishona vitambaa viwili tofauti kuitengeneza nguo mpya. Kitambaa kile kipya kilifanana na mnyama au ndege aitwaye kanga. Basi jina la nguo za kanga limetokana na ndege huyo mwenye madoa doa.

Kanga huvalika kwa njia tofauti, kama nguo, juu ya kichwa, kuwabeba watoto, hutumika kama kitandiko cha meza, cha kutanda kitanda na kadhalika. Watu huvaa kanga kusherehekea uzazi, arusi, au kuomboleza. Watu wengi hupeana kanga kama zawadi. Mara nyingi kanga hununuliwa kama jozi.

Kanga zinatumiwa kwa mawasiliano pia. Kila kanga ina methali au ujumbe, inaweza kuelezea vitu vingine bila ya usemi. Hii hapa ni mifano ya misemo kadhaa inayoweza kuonekana kwenye kanga: “Fimbo la mnyonge halina nguvu”, “Lia na tabia yako usilaumu wenzako”, “Naogopa simba na meno yake, siogopi mtu kwa maneno yake”, “Kheri nyuki kuliko chuki”, “Mke ni tunda ni wajibu kumtunza”, “Tusisahau kwetu’.



11. Переведите на суахили:

Танзанийская кухня1

К основным продуктам питания танзанийца относятся бататы, маниока, кукуруза, рис, бананы. Это именно те продукты, которые встречаются повсеместно.

Способ их приготовления довольно прост. Бататы или маниоку запекают на углях и едят как самостоятельное блюдо, как сладкий хлеб на завтрак. Можно из них приготовить и гарнир к основному блюду, сварив их в кокосовом молоке (maji ya dafu). Из кукурузной муки готовят кашу угали (-songa ugali). Ее варят без сахара, соли или молока. Молоко, кстати, используется только для забеливания чая, а других молочных продуктов традиционная кухня танзанийцев не знает. Рис обычно отваривают на воде или кокосовом молоке, предварительно поджарив рис на растительном масле. Бананы, большие зеленые, также можно тушить (-tokosa) в кокосовом молоке, поджаривать или запекать в банановых листьях. Блюда из бананов особенно популярны на севере Танзании.

Все эти перечисленные выше блюда – своего рода гарнир, к которому подаются разнообразные соусы (mchuzi). Это вкусная и ароматная овощная приправа с небольшим количеством мяса или рыбы. Основа такого соуса – поджаренный лук и свежие томаты. А дальше по вкусу хозяйки можно добавить другие овощи и специи (viungo). Соус мчузи может быть и чисто овощным. Например, вместо мяса в него можно добавить фасоль.

Из всех видов мяса танзанийцы предпочитают баранину, курятину или козлятину. Свинину практически не едят и не только мусульмане, но и христиане. Возможно, это объясняется религиозной и межэтнической терпимостью танзанийцев. Тем не менее, при желании свинину можно купить.

Что касается рыбы, то на рынке она довольно дорогая, поэтому крупную рыбу обычно ловят на продажу, а в повседневную еду идет мелкая рыбешка дагаа, которую добавляют в соус мчузи как в свежем виде, так и сушеную.

Естественно, что на танзанийскую кухню оказали влияние две крупных неафриканских общности – арабы и индийцы, издавна проживающие в Восточной Африке.

Танзанийцы, как правило, едят два раза в день. Обычное меню не отличается разнообразием: утром – чай с хлебом или остатками ужина, вечером – рис или угали с мясным, рыбным или фасолевым мчузи. Едят обычно на циновке, которая является важным предметом обихода. На ней не только едят, но и спят, размалывают муку, натирают кокос (-kunia nazi kwa mbuzi), беседуют, выясняют отношения и т.д.


12. Выучите наизусть слова песни “Malaika”.

MALAIKA

Malaika, nakupenda Malaika,

Malaika, nakupenda Malaika,

Nami nifanyeje, kijana mwenzio,

Nashindwa na mali sina, we,

Ningekuoa Malaika.


Kidege, hukuwaza kidege,

Kidege, hukuwaza kidege,

Nami nifanyeje, kijana mwenzio,

Nashindwa na mali sina, we,

Ningekuoa Malaika.
13. Запомните суахилийские пословицы. Если возможно, подыщите им эквиваленты в русском языке:

Mpanda ngazi hushuka. Apandaye ngazi mwishowe hana budi kuteremka.

Mgeni aje mwenyeji apone. Akitokea mgeni kwenye nyumba watu wote hunufaika kwa kula chakula kingi na kizuri.

Mchele mmoja mapishi mengi. Mchele ni namna moja lakini huweza kupikwa kila aina ya upishi kama pilau n.k. Kila mmoja ana uhodari wake mbali katika kukitengeneza kitu kimoja chicho hicho.

Rahisi haihalisi. Kitu rahisi yaani cha bei ya chini, huwa hakina manufaa sana au hakina maisha marefu.

Wema hauozi. Kumfanyia mtu wema ni kama kuweka akiba isiyooza, kwani wema wako haupotei bure. Kuna siku yule mtu atakufanyia nawe wema vile vile.

Vita vya panzi (кузнечик) ni furaha ya kunguru (ворона). Panzi wanapopigana faida huwa ni ya kunguru, kwa sababu hupata nyama ya bure. Marafiki au jamaa wakigombana huwa ni furaha kwa adui yao.

Upatilize udongo uli maji. Uwahi udongo, kwa mfano kwa kujengea, ungali u maji, kwani ukikauka utakushinda.

Usisahau ubaharia kwa kupata unahodha. Kwa sababu ya kupata unahodha, yaani cheo cha juu, usisahau ubaharia, cheo cha chini, kwani usipotahadhari unaweza kukosa hata huo ubaharia.

Ujana ni moshi, ukenda haurudi. Ujana ni mfano wa moshi, kwani moshi ukienda zake haurudi tena mahali ulikotoka. Ya zamani hayarudi tena.
12. Сделайте на суахили сообщения на темы:

А/ Значение языка суахили для народов Восточной Африки;

B/ Литература и искусство Танзании.


Msamiati

gwiji (-) знаток, специалист hulka (-) 1) естество

mwinyi (mamwinyi) феодал; 2) натура, нрав; характер

помещик; ; буржуа tarakilishi (-) компьютер



masihara (-) шутка; насмешка -nawiri светиться, сиять

maandishi (мн.) 1) сочинение, kitivo (-vi-) факультет

произведение 2) письменность leso (-; ma-) 1) косынка,



karaha (-) 1) антипатия, платок 2) шаль, накидка

неприязнь 2) отвращение jozi (-; ma-) пара



-chachafya беспокоить, ujumbe (ед.) послание;

надоедать весть; сообщение



majonzi (мн.) печаль, скорбь; tabasamu (-) улыбка

горе tuta (ma-) 1) гряда, грядка;



suluhisho (ma-), suluhu (-) клумба 2) насыпь

урегулирование; разрешение zambarau пурпурный

(проблемы, конфликта и т.п.) malaika (-) ангел, добрый дух

-suluhisha регулировать, -kashifu 1) разоблачать

улаживать (ссору, разноглаия) 2) оскорблять, обижать



tamthiliya (-) пьеса; драма kanzu (-) национальная

tele 1) множество, большое одежда типа рубахи

количество, [из]обилие (белая мужская,



2) много, обильно, в изобилии цветная женская)

1   ...   17   18   19   20   21   22   23   24   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət