Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə2/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   2   3   4   5   6   7   8   9   ...   25

Jiji la Dar es Salaam


Kusala ni mtoto wa Songea anayesoma shule ya Lilambo. Ana mjomba wake aliye karani wa bandari katika jiji la Dar es Salaam.

Wakati wa likizo, Kusala alikwenda Dar es Salaam kumsalimu mjomba wake. Alichukua sanduku lake la mbao na kifurushi cha chakula, akaenda mpaka mjini Songea. Kesho yake akaondoka kwa basi kwenda Dar es Salaam.

Basi hili lilipitia njia ya Njombe na jioni likafika Iringa. Hapo wakalala. Asubuhi yake wakaanza safari kwenda Morogoro kupitia Mikumi. Mikumi ni mbuga ya wanyama. Kusala aliona wanyama wengi. Kutoka hapo walikwenda moja kwa moja mpaka Morogoro ambako walifika kama saa kumi jioni. Baada ya kupumzika kidogo waliondoka kuelekea Dar es Salaam.

Walipokaribia Dar es Salaam, Kusala aliona majengo makubwa upande wa kushoto. Alimwuliza mwenzake aliyekuwa karibu naye, “Yale ni majumba gani?” Mwenzake akamjibu, “Yale ni majengo ya Chuo Kikuu. Ni mahali maarufu sana hapa nchini ambapo watu wanasomea shahada za elimu mbali mbali”.

Walipofika katikati ya mji, Kusala alishangaa sana kuona taa zenye rangi mbalimbali zilizotundikwa juu ya milingoti mirefu ya chuma. Aliona magari makubwa, mabasi mengi na motokaa ndogo nyingi. Alishangaa kuona magari mengi hivi.

Basi lilipofika kituoni Kusala alifurahi sana kumwona mjomba wake amekuja kumpokea. Usiku ule Kusala alilala sana kwa ajili ya uchovu wa safari.

Asubuhi yake Jumapili, mjomba wake aliwachukua yeye na binamu yake, Njoli, akawatembeza mjini. Kwanza walitembelea kiwanja cha ndege. Kusala alishangaa kuona jinsi kiwanja kilivyo kikubwa. Aliona ndege kubwa zikitua, akauliza, “Mbona Songea hakuna ndege kubwa kama hizi?” Mjomba wake akamjibu, “Songea ni mji mdogo. Hauna kiwanja kikubwa cha kutua ndege kubwa kama hizi”.

Kutoka kiwanjani Kusala alipelekwa kutazama Jengo la Bunge. Baada ya hapo walikwenda kwenye kivuko cha bahari kupitia Ikulu. Hapo Ikulu, Kusala aliona askari walinzi. Pia aliona mbuni na tausi. Akauliza,”Askari hawa wanafanya nini?” Njoli akamjibu, “Wanalinda zamu, maana hapa ndipo Ikulu, makao rasmi ya Rais wetu.”

Walipofika kwenye kivuko walikata tikiti wakaingia katika pantoni na kuvuka mpaka ng’ambo. Huko walitembelea mtambo wa kusafishia mafuta. Mtambo huu husafisha na kutenganisha lami, dizeli, mafuta ya taa na petroli.

Waliporudi walikwenda bandarini. Mjomba wake akawaonyesha ghala kubwa na mashine za kuinulia mizigo. Pia waliona meli nyingi kubwa kwenye magudi. Zilikuwa zikipakua na kupakia bidhaa. Pia yalikuwapo madau pamoja na mitumbwi. Wavuvi hutumia madau na mitumbwi kuvulia samaki.

Kusala vile vile alikwenda kuona stesheni kubwa ya gari la moshi. Hii ilikuwa mara yake ya kwanza kuona gari la moshi, kwa hivyo alishtuka aliposikia makelele na kuona moshi mwingi. Watu wengi walikuwa wakingojea gari liondoke.

Siku nyingine Kusala alipelekwa kuona viwanda. Aliona watu wengi wakifanya kazi. Kusala na Njoli waliona viwanda vya kutengenezea nguo, mablanketi, sufuria na madebe.

Kutoka huko walipitia Kariakoo. Hili ni soko kubwa la Dar es Salaam. Vyakula, mboga na matunda mengi huuzwa hapo. Biashara nyingi huendeshwa katika maduka makubwa karibu na soko hilo.

Kwa kweli Kusala aliona mambo mengi mageni. Aliona watu wakikimbilia mabasi. Wengine wakienda mbio kwa miguu. Siku ya mwisho alitembelea kiwanda cha kutengenezea nyama za makopo. Alipoondoka alimshukuru sana mjomba na ndugu zake. Alipofika Songea aliwaandikia barua ya kuwashukuru na kusema kuwa alifurahi sana kuona jiji la Dar es Salaam.


11. Перескажите текст из упражнения 10, ответив на следующие вопросы:

1. Kwa nini mtoto Kusala aliamua kwenda Dar es Salaam? Alichukua nini safarini? 2. Wakati wa safari yake mpaka jijini Dar es Salaam Kusala alipitia miji gani? 3. Alibahatika kuona nini njiani mwake? 4. Ni mambo gani yaliyomfanya Kusala kushangaa mno alipofika katikati ya jiji la Dar es Salaam? 5. Kiwanja cha ndege cha jiiji hilo kikoje? 6. Kutoka kiwanja cha ndege Kusala alipelekwa wapi? 7. Baada ya kufika ng’ambo Kusala na binamu yake waliona nini? 8. Katika bandari walionyeshwa vitu gani? 9. Ni mambo gani ya ajabu waliyoyaona kwenye stesheni ya gari la moshi? 10. Kusala alipelekwa katika viwanda vya aina gani? 11. Eleza habari za Kariakoo, ni mahali pa nini? 12. Je, Kusala aliwashukuru vipi mjomba na ndugu zake baada ya kurudi nyumbani?


12. Перескажите на суахили следующие сюжеты, обратив внимание на перевод подчеркнутых выражений:


  • В Восточной Африке много озер, самыми крупными из которых являются озера Виктория, Танганьика, Ньяса и Туркана. Множество рек берут свое начало в горах и впадают в Индийский океан, Средиземное море (bahari ya Mediterania) или в озера. Среди рек, несущих свои воды в Индийский океан, такие реки, как Рувума, Руфиджи, Руву, Вами, Пангани и Тана. В Средиземное море впадает такая великая река, как Нил. Она вытекает из озера Виктория, проходит через озера Киога и Альберт в Уганде, течет на север. Река Малагараси впадает в озеро Танганьика, а река Кагера - в озеро Виктория.

  • Большинство рек, протекающих по материковой части Танзании, не пригодны для судоходства, за исключением реки Руфиджи. Много рек в жаркое время года пересыхают, однако после очередного периода дождей они бурно разливаются, затопляя окрестности.

  • Река Пангани, впадающая в Индийский океан, является одной из наиболее важных для Танзании. Она берет свое начало неподалеку от городов Аруша и Моши на северо-востоке, в окрестностях гор Меру и Килиманджаро, где находятся наиболее густо заселенные районы страны, и течет в юго-восточном направлении до океана.

  • Река Руву впадает в океан немного севернее Багамойо. Она является основным источником воды для крупных сизалевых плантаций в Танзании. А самая большая река Танзании - Руфиджи. Но, к сожалению, прекрасные природные условия и плодородные почвы бассейна этой реки мало используются для земледелия, главным образом из-за ее частых и неожиданных разливов. На Занзибаре и Пембе реки небольшие, в сухой сезон они пересыхают.

  • Важнейшую роль в экономике страны и жизни местного населения играют озера. Основная масса населения западной части Танзании сосредоточена вдоль побережья озер. Здесь же находятся главнейшие сельскохозяйственные районы западных областей страны. Все озера очень богаты рыбой. Достаточно сказать, что только в одном озере Танганьика, глубочайшем в мире после озера Байкал, насчитывется до 200 разнообразных видов рыб. Некоторые экземпляры этих рыб весят килограммов сорок и более. Рыба является одним из основных продуктов питания местного населения.


Msamiati

mstari (mi-) 1) линия 2) строка Mrima (mi-) полоса побережья

mstari wa Ikweta экватор Восточной Африки (~20 км)

-ungana объединяться mwinuko (mi-) подъем,

-unganisha соединять, связывать возвышение

muungano (mi-) объединение, союз mchanganyiko (mi-) смесь,

hati (-) 1) документ; официальная смешение

бумага 2) свидетельство awali (-) начало



chini ya 1) под руководством awali 1) сначала, вначале

(властью, контролем) 2)раньше, прежде

2) в соответствии с чем-л. ustaarabu (ед.) культура,

-tia saini подписывать цивилизация

mwujiza (mi-) чудо, диковинка mfu (wa-) умерший человек

umbile (ma-) образ, форма -fua chuma ковать железо

maumbile (мн.) природа -zika хоронить, закапывать

mraba (mi-) квадрат, прямоугольник rais (ma-) президент; глава;

kilomita ya mraba квадратный председатель

километр jamhuri (-) республика



tabia ya nchi климат siasa (-) политика

mkazi, mkaazi (-) житель, обитатель haja (-) потребность,

ufa (nyufa) трещина, расселина необходимость

Bonde la Ufa Восточноафриканский windo (ma-) охота, добыча

разлом enzi (-) эпоха, время



usawa (ед.) равенство; mila (-) обычай

справедливость katiba (-) конституция; устав



usawa wa bahari уровень моря mifugo (мн.) скот; стадо

kilindi (vi-) большая глубина, -tosheleza удовлетворять

фарватер kina (vi-) глубина



wastani (ед.) среднее число kiungo (vi-) часть тела;

(количество) конечность



kwa wastani в среднем lami (-) асфальт

-piga mtindi выпивать; хмелеть -linda zamu стоять на страже

zeze (-; ma-) музыкальный rasmi 1)официальный

инструмент (струнный) 2) официально; легально



rimba (ma-) музыкальный makao rasmi резиденция

инструмент (типа ксилофона) gudi (ma-) причал, пристань



-tumbuiza исполнять мелодию, петь dau (; ma-) парусная лодка

-tawala править, господствовать (как правило одномачтовая)

-fufua 1) оживлять, воскрешать -pakia грузить, нагружать

2) восстанавливать -pakua разгружать, выгружать



mlingoti (mi-) мачта; столб mnara (mi-) башня, вышка

shahada ya elimu диплом, kopo (ma-) металлическая банка

аттестат об образовании nyama ya makopo мясные



binamu (-) племянник, племянница консервы

(сын или дочь брата отца) mundu (miundu) садовый нож

mkoa (mi-) область; провинция (кривой формы); серп

Ikulu (-) резиденция, дворец debe (ma-) коробка или

президента или правительства ящик из жести



mtambo wa kusafishia mafuta -sitawisha развивать;

нефтеперерабатывающее улучшать

устройство -ingiza ввозить,

pantoni (-) понтон импортировать

* * *

Урок 2. Somo la pili
Грамматика

Спряжение недостаточного глагола -po/ -ko/ -mo.


Как известно, релятивные форманты локативных классов -po, -ko, -mo, выполняя функцию глаголов “находиться”, “существовать”, “располагаться” и т.п., в настоящем времени спрягаются без показателя времени. Они оформляются лишь субъектными приглагольными показателями: wako shambani “они находятся в поле”; jina hili liko tangu zamani “это название существует издавна”; kituo cha afya kimo ndani ya jengo lile “медпункт расположен внутри того здания”; yupo hapa “он здесь” и т.д. Напомним, что при образовании отрицательных конструкций настоящего времени к этим формантам присоединяются отрицательные формы субъектных приглагольных согласователей: hawako; haliko; hakimo; hayupo и т.д.

Что же касается прошедшего или будущего времени, то для спряжения глагола “находиться” необходимо использовать глагол -wa “быть”, который, присоединяя к себе форманты -po, -ko, -mo, спрягяется обычным образом: walikuwako/ watakuwako; lilikuwako/ litakuwako; kilikuwamo/ kitakuwamo; alikuwapo/ atakuwapo.

Также возможен аналитический способ употребления этого глагола в контексте прошедшего или будущего времени, когда форманты -po, -ko, -mo спрягаются по модели настоящего времени, а предшествующий им вспомогательный глагол -wa оформляется показателем прошедшего или будущего времени: walikuwa wako/ watakuwa wako; lilikuwa liko/ litakuwa liko; kilikuwa kimo/ kitakuwa kimo; alikuwa yupo/ atakuwa yupo.

Глагол -po/-ko/-mo может образовывать негативные формы прошедшего или будущего времени также двумя способами, либо синтетическим – hawakuwako; halitakuwamo; hatakuwapo и т.д., либо аналитическим путем – walikuwa hawako; litakuwa halimo; atakuwa hayupo.

Следует отметить, что глагол -wa, присоединяя к себе форманты -po, -ko, -mo, редко оформляется показателем настоящего времени -na-, поскольку в таком варианте он может передавать значение обычности, регулярности нахождения, например:

Anakuwako kazini kila siku “Он (обычно) бывает на работе каждый день”.

Kiongozi wetu anakuwepo ofisini mnamo saa za asubuhi tu “Наш начальник (как правило) находится в офисе только в утренние часы”.
Mazoezi

1. Переведите предложения и измените время на прошедшее и будущее:

1. Tumo ndani ya chumba cha giza siku kutwa. 2. Wazee wako kwenye mkutano rasmi wa chama chao. 3. Ikulu ya serikali iko ng’ambo. 4. Makao makuu ya rais yako mbali. 5. Sheria ambazo zimo ndani ya hati hii ni za kufaa sana. 6. Uhusiano mzuri upo miongoni mwa majirani hawa. 7. Viwanda vya kufua chuma viko nje ya mji. 8. Jumba la makumbusho lililo maarufu liko kule karibu na mnara. 9. Zahanati ya watoto iko ghorofa ya chini. 10. Mabaharia kutoka madau yale wako bandarini. 11. Ofisi ya forodha ipo hapa upande wa kulia. 12. Kivuko kipo si mbali na huko. 13. Siku zote nimo ndani ya maktaba nikijifunza mila na jadi za Waafrika. 14. Jamhuri mpya iliyo huru iko kwenye ramani ya kisiasa ya dunia.


2. Замените утвердительные конструкции отрицательными:

mlikuwako; tulikuwa tupo; utakuwamo; zilikuwapo; lilikuwa lipo; nitakuwako; zipo; ulikuwa upo; yako; atakuwako; ilikuwa imo; litakuwako; yalikuwamo; utakuwako; zilikuwa zimo; wapo; palikuwako.



3. Переведите предложения, употребив глагол -po/ -ko/ -mo:

1. Они так долго находились за границей, что начали забывать свой родной язык. 2. Гости из Кении пробудут в этом отеле целую неделю. 3. Мы были там ровно три дня и успели многое посмотреть. 4. Равенства между мужчинами и женщинами в этой стране не существует изначально. 5. Цивилизация существовала здесь издавна. 6. Резиденция правительства раньше располагалась в самом центре города. 7. До революции эта маленькая страна находилась в составе могущественного королевства. 8. Где вы были, когда мы пришли? – Мы находились за домом. 9. Куда уехали наши соседи? – Они сейчас у своих родственников в деревне. 10. Самые большие магазины располагались на главной площади.


HISTORIA YA MOROGORO

Katika mwaka 1840 jina la Morogoro lilikuwa halipo kabisa. Ambapo hivi sasa ni katikati ya mji, kati ya stesheni na hospitali palikuwa pakiitwa Bungo Dimwe hapo zamani.

Zamani mto wa Morogoro ulijulikana kwa jina la Mto Mwele. Palikuwa na wakuu wengi wadogo waliokuwa wakiishi ndani na pembeni* ya sehemu ambayo hivi sasa inaitwa Morogoro. Misafara mingi ilipitia Morogoro hasa ile ya Waarabu wa biashara, na mara kwa mara walitumia nguvu kwa kuzipita nchi za wakuu hao. Wakati misafara hii ilipokuwa ikirudi pwani kutoka bara, ilikuwa na mamia ya watumwa walionunuliwa na waliokamatwa, wanaume, wanawake, na watoto kwa kuwauza kwenye soko la watumwa huko Unguja. Katika misafara hii walipeleka pembe za ndovu pia. Ilikuwa ni** jambo la uchungu kwamba wakuu wengi kutoka Tanganyika waliuza wenyewe watu wao kwa Waarabu ili kupata nguo, chumvi n.k.

Kadhalika desturi ya kizamani ilikuwapo, kwani mara kwa mara wakuu walipigana na wakuu majirani zao, na washindi waliwateka watu wengi, mabibi na mabwana na kuwafanya watumwa.

Kisabengo lilikuwa jina la mtu aliyekuja katika mtaa wa Morogoro kutoka nchi ya Wazigua. Yeye alikuwa Mzigua wa kwanza ambaye jina lake hilo, Kisabengo, lilipata kujulikana na kuogopwa sana na watu wa Morogoro. Kisabengo lilikuwa si jina lake hasa, ila alipewa na watu wa Morogoro. Jina lake lilikuwa Muhina. Watu wa Morogoro wakampenda kwa ushujaa wake, lakini waliuona pia ukatili wake kwa sababu alikuwa mjeuri kweli kweli. Wakati Muhina alipompiga mtu mmoja na akaanguka aliacha bunduki yake na kuchukua upanga wake na kumkatakata vipande vipande. Watu walioona kitendo hiki wakaanza kumwita kwa jina la Kisabengo yaani kwa lugha yao ya kikabila maana yake ni “mtu anayekatakata wenzake”.

Kabla ya kufika mtaa wa Morogoro Muhina alikuwa ni mtumwa**, lakini alitafuta njia ya kupata uhuru wake. Alipokuwa huru tena Muhina aliwashauri watumwa wengi kuwakimbia mabwana zao na kujiunga naye. Aliwapata wengi, lakini muda huo alipata taabu kubwa na Sultani wa Unguja. Kwa wakati huo katika Uzigua walikuwapo wajumbe wa Sultani wa Unguja ambao walitawala na kupanga mambo****. Wajumbe hao waliitwa mawaziri. Waarabu na wakuu wa Uzigua walikasirishwa sana na kitendo cha Muhina cha kuwaita watumwa kukimbia mabwana zao. Hii ndiyo sababu iliyomfanya aondoke nchi yake ya Uzigua asikamatwe na Sultani wa Unguja na mawaziri wake.

Mji na ngome ya Muhina huko Bungo Dimwe yaani jina la zamani la Morogoro ilikuwa karibu na mto Mwele. Siku moja shina kubwa la mti lilianguka ndani ya mto huo. Wakati maji yalipopita huko yalitoa kelele kama “rogoro-rogoro”. Watu walipotaka kuvuka mto Mwele waliuliza “Tutapita chini au tupite penye rogoro-rogoro? Neno “rogoro” lilitumiwa mara kwa mara mpaka jina la Mwele lilisahauliwa na ule mto kuitwa “Mrogoro”. Vile vile watu walianza kuita Bungo Dimwe kama Mrogoro. Baadaye jina hilo likageuzwa kuwa Morogoro.

Mji wenyewe upo chini ya milima ya kupendeza ya Uluguru. Huko kunaota mimea ya kila aina. Sehemu za ardhi zilizolimwa vizuri sana zipo kaskazini na magharibi ya Morogoro. Kuna mashamba ya mahindi, mtama, miwa, migomba n.k. Hata wakati uliopita wenyeji waliwahi kuvuna mpunga mwingi, lakini mwaka mmoja simba wengi walikuja kutoka milimani, waliua ng’ombe na watu wengi walioishi katikati ya Morogoro na kwenye vitongoji vya mji huo.

Hivi sasa katika vijiji vyote pembeni* na hata ndani ya mji wa Morogoro wanaishi ndugu na jamaa kutokana na*** wale watawala wa kale walioishi tangu zamani sana mahali hapo.
Maelezo

* Слово pembe “угол” с локативным суффиксом -ni передает значение “на окраине”, “в стороне от чего-либо”. Возможно двоякое согласование: pembeni mwa, pembeni ya.
** Связка ni сохраняется в прошедшем (или будущем) времени для того, чтобы подчеркнуть актуальность того факта, о котором идет речь.
*** Предлог kutokana na здесь можно перевести как “которые происходят от …” или “из древних родов правителей”.
**** Глагол -panga помимо значения “планировать, намечать” имеет ряд других значений, в том числе “налаживать, устраивать, организовывать”. Выражение -panga mambo в данном контексте можно перевести как “ хозяйничать, всем заправлять ”.
Mazoezi

4. Исходя из содержания текста, подтвердите или опровергните следующие высказывания по модели: Ni barabara; nimekubali; wasema kweli; ni hivyo ndivyo. Или: Sivyo hivyo; hapana; hata kidogo; kinyume chake; sikubali kabisa:
1. Jina la mji wa Morogoro lilianza kujulikana hata kabla ya mwaka wa 1840. 2. Misafara ya Waarabu wa biashara ilipita kwa urahisi sehemu za ndani na pembeni mwa mahali panapoitwa Morogoro sasa. 3. Waarabu walinunua watumwa kutoka kwa wakuu wa Tanganyika na kuwalipa kwa chumvi, nguo na vitu vingine. 4. Watu wa Morogoro walimpenda na kumwogopa sana Kisabengo kwa sababu alikuwa mtu mwenye nguvu na mkali sana. 5. Kisabengo alikimbia nchi ya Uzigua kwa sababu alitaka kusafiri na kuziona sehemu nyingine za Tanganyika. 6. Mji wa Morogoro ulipata jina lake hilo kutokana na jina la mto Morogoro. 7. Wakulima wa Morogoro waliacha kulima mpunga kwa sababu hawakupenda kutumia zao hilo kama chakula chao.
5. Расскажите о городе Морогоро, используя следующие выражения:

-julikana; sehemu za pembeni; misafara ilipita; watu wa biashara; mamia ya watumwa; -tumia nguvu; pembe za ndovu; jambo la uchungu; -teka watu; desturi ya kizamani; -kata vipandevipande; -pata uhuru; -pata taabu; -panga mambo; -lima ardhi; watawala wa kale.


6. Подберите антонимы к следующим словосочетаниям:

-ona uchungu mwingi; -kaa pembeni mwa mji; -pakia bidhaa melini; -kimbia nchini; mfano wa kusisimua; -komesha utawala; -teka watumwa; -danganya watu; -ungana pamoja; ustaarabu wa kale.


7. Переведите письменно следующий текст:
Mwanza: mji muhimu katika pwani ya ziwa Victoria

Kusini mwa ziwa Victoria, kuna moja ya miji mikubwa na maarufu ya Tanzania. Huo ni Mwanza. Mji huo unaozidiwa na Dar es Salaam kwa ukubwa lakini unashindana na miji ya Tanga na Arusha kushika nafasi ya juu baada ya jiji la Dar es Salaam, kwa miaka ya karibuni umeanza kupigania kupewa hadhi ya jiji.

Mji wa Mwanza ulijengwa na mmoja wa wazungu wa kwanza kufika katika eneo hilo mwishoni mwa karne ya 19, Emil Pasha. Licha ya kwamba mji huo uko mita chache kutoka ziwani, bado maji ni tatizo kwa wakazi wake.

Ingawa Waingereza waliuletea maendeleo makubwa na ya haraka mji huu lakini bado hadi leo hii baadhi ya wakazi wa Mwanza wanaishi katika mazingira mabaya na hasa wale waliojenga nyumba zao bila mpango katika vilima vinavyouzunguka mji huu.

Ziwa Victoria lina umuhimu wa pekee kwa wakazi wa mji huu. Ziwa hili ni chanzo kikubwa cha vipato vya wakazi wake na hasa wachuuzi wa samaki na wafanyabiashara wazungukiao eneo hili la Tanzania, Uganda na Kenya. Si hivyo tu. Ziwa Victoria ni kiungo muhimu cha mawasiliano kati ya mji wa Mwanza na wilaya za Sengerema, Geita, Biharamulo na Ngara ambapo kuzifikia inakulazimu zaidi kulivuka ziwa.

Karibu kila kitongoji katika mji huu kina umuhimu wake. Eneo la katikati ya mji lina stendi ambayo ni kubwa zaidi Tanzania hata kuzizidi zile za Dar es Salaam, Moshi na Arusha. Pia ni eneo muhimu kwa biashara likiwa na maduka ya jumla ambapo wafanyabiashara kutoka wilaya za mkoa huu hufika hapo kununua bidhaa. Hapa pia kuna kiwanja kikubwa cha ndege, kituo cha treni iunganishayo na Dar es Salaam bandari ya ziwa. Zaidi kuna mahoteli makubwa sana.

Mwaloni ni eneo muhimu la biashara wakati Kirumba kuna kiwanja cha mpira kikubwa na kizuri Tanzania, hali inayodhihirisha mapenzi makubwa ya soka kwa wakazi wa mji huu ambao timu yao ya Pamba hutoa wachezaji nyota.

Kitongoji cha Igoma kina viwanda muhimu kama kile cha soda aina ya Coca Cola, wakati Nyakato kuna kiwanda cha nguo. Mji wa Mwanza una kituo chake cha redio pamoja na gazeti.

Wakazi wengi zaidi wa Mwanza ni Wasukuma, ingawa bado kuna mchanganyiko mkubwa wa makabila mkoani humo, mathalani, Wajita, Wakerewe, Wasumbwa na mengineyo.
8. Переведите:

1. Еще два века назад такого названия как Морогоро не существовало вовсе, и сам город и река, протекавшая в его окрестностях, назывались по-другому. 2. Место, расположенное между железнодорожной станцией и больницей, было изестно под названием Бунго Димве. 3. Сотни людей, как мужчин, так и женщин, переправлялись из глубины континента на побережье, а оттуда на Занзибар, где в то время находился крупнейший рынок рабов. 4. Продажа бивней слонов приносила огромные доходы арабским торговцам, хотя сами они приобретали их очень дешево или просто обменивали на разные бытовые мелочи. 5. Жители Морогоро уважали своего лидера за храбрость, но в то же время и боялись, так как по характеру он был очень жестокий человек. 6. Мухине удалось убежать от своих хозяев, после чего он стал призывать других рабов поступить таким же образом. 7. Скрываясь от представителей занзибарского султана, которые всем заправляли в этих краях, Мухина перебрался в Бунго Димве. 8. Форт, находившийся недалеко от реки, был самым популярным местом среди жителей окрестностей. 9. Город, расположенный у подножья горного хребта Улугуру, выглядит очень живописно. 10. Представители многих народностей живут сегодня в Восточной Африке, среди них есть и те, чьи предки бесстрашно боролись за свою независимость. 11. Дар эс Салам является важнейшим транспортным узлом, соединяющим Танзанию с другими странами, например с Кенией, Угандой, Замбией. 12. Владельцами многих магазинов оптовой торговли, располагавшихся недалеко от центральной стоянки транспорта, были индийцы.


1   2   3   4   5   6   7   8   9   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət