Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə17/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   13   14   15   16   17   18   19   20   ...   25

5. Ответьте на вопросы по содержанию текста:

1. Kwa nini watu hawawezi kutosheka na elimu waliyo nayo sasa? 2. Mtoto inambidi kusoma mpaka umri gani aweze kufanya kazi vizuri? 3. Kwa nini watoto wa leo wahimizwe kusoma? 4. Watoto walioacha skuli katika umri mdogo wamefanyiwa mpango gani na serikali? 5. Kwa nini wakati wa ukoloni mwisho wa elimu ya watoto wa kimaskini ulikuwa ni darasa la nane? 6. Waalimu nao wana wajibu gani? 7. Watoto wa kimaskini walianguka mitihani ya mwaka 1963 kwa sababu gani? 8. Uwamuzi gani ulipasishwa na Baraza la Mapinduzi? 9. Je, mipango ya kuleta waalimu kutoka nje inawafaa Watanzania au sivyo? 10. Ufunguo wa kuleta maendeleo katika mambo ya elimu ni kitu gani?


6. Выучите диалог наизусть:

Amina: Ndugu, wafanya kazi wapi?

Hermas: Nafanya kazi Chuo Kikuu.

Amina: Tafadhali nifahamishe mfumo wenu wa elimu.

Hermas: Kwa ujumla, mtoto hapa Tanzania huanza shule akiwa na umri wa miaka kama nane.

Amina: Husoma shule ya msingi kwa miaka mingapi?

Hermas: Saba. Akimaliza anaweza kuchaguliwa kuingia sekondari ambako atasoma kwa miaka minne. Akifaulu mtihani wake vizuri, huchaguliwa kwa miaka mingine miwili.

Amina: Baada ya hapů!ÿfanya nini?

Hermas: Akifaulu anaweza kuingia Chuo Kikuu kusomea shahada ya kwanza, ambayo kwa kawaida huchukua miaka mitatu.

Amina: Ni lazima kuufuata utaratibu huu?

Hermas: Hapana. Baadhi ya wale wamalizao darasa la saba, hurudi vijijini na wengine huingia vyuo vya ualimu, au hujifunza kazi za ufundi.

Amina: Je, yaweza kuwa hivyo kwa wale wamalizao miaka minne sekondari?

Hermas: Ndiyo. Baadhi yao hujitafutia kazi mijini na vijijini na wengine hujifunza ufundi.

Amina: Katika shule za sekondari kunafundishwa masomo gani?

Hermas: Masomo ya kawaida tu, kama vile lugha, hasa Kiswahili, Kiingereza na Kifaransa; hesabu; jiografia; historia; elimu ya siasa; biolojia, kemia na fizikia. Uchumi na fasihi pia hufunzwa.

Amina: Na huko Chuo Kikuu?

Hermas: Kwa kawaida Chuo Kikuu huwatayarisha wanafunzi kufanya kazi za kitaalamu katika serikali na mashirika ya uzalishaji na ya huduma. Hivyo hutoa waalimu, wanasheria, mameneja, wahasibu na madaktari. Pia huendeleza taaluma kwa kufanya uchunguzi.
7. Переведите письменно следующий текст и озаглавьте его:

Kuna kundi la watoto wetu ambao wamefikia umri wa kwenda shule lakini wamekataliwa kupokelewa katika shule hizo kwa sababu ya kushindwa kulipa michango inayowekwa na shule. Ingawa serikali na viongozi wetu mara kadhaa wametoa maelekezo kwamba michango hiyo isizuie wanafunzi kupokelewa, tatizo hili linaendelea katika baadhi ya shule nchini. Kwa hiyo, tamko la waziri wa elimu na utamaduni mwishoni mwa wiki la kutilia mkazo msimamo wa serikali juu ya jambo hili, linapaswa kukaribishwa.

Ingawa waziri katika matamshi yake amezielekeza zaidi shule za msingi, tamko lake linapaswa kuzingatiwa na hata shule za sekondari za serikali na za binafsi.

Tatizo hili la wanafunzi kukataliwa kupokelewa kwa sababu ya kushindwa kulipa baadhi ya michango, huko nyuma lilijitokeza sana katika baadhi ya shule zetu za msingi.

Mtindo huu wa kuwakataa wanafunzi umekuwa hauendi sambamba na sera ya taifa inayotaka kila mtoto aliyefikia umri wa kwenda shule aende shule. Matokeo ya mtindo huo ni kwamba baadhi ya watoto wetu wameshindwa kupata elimu hii muhimu ya msingi katika wakati wake kwa sababu tu ya uwezo mdogo wa wazazi wao wa kulipa baadhi ya michango.

Mbali na shule hizi za msingi, tatizo hili pia limekuwa likijitokeza katika baadhi ya shule zetu za sekondari. Shule hizi hujiwekea michango, ambayo mara nyingi ina nia nzuri ya kuendeleza shule, lakini hugeuka kuwa kipingamizi cha kuwazuia wasiokuwa na uwezo wa kuilipia.

Hatusemi kwamba michango mbalimbali inayowekwa katika shule zetu ifutwe. Kwa sababu, mara nyingi michango hii ni ya kusaidia maendeleo ya shule zenyewe. Lakini ni vizuri upatikane utaratibu mzuri wa kulipa michango hii.

Kwa hiyo, ni matumaini yetu kwamba msisitizo uliowekwa na waziri katika jambo hili utazingatiwa na shule zote na wizara itafuatilia kuona kwamba watoto wetu hawakataliwi kupokelewa shuleni kwa sababu ya kushindwa kulipa michango ikiwa uwezo wa kufanya hivyo hawana.


8. Найдите в тексте из предыдущего задания суахилийские эквиваленты следующих выражений и составьте с ними предложения:

школьный возраст; быть лишенным возможности поступить в школу; давать указания; это стоит обдумать; быть не в состоянии заплатить взнос; проблема обнаружилась со всей остротой; это идет вразрез с; курс правительства; становиться серьезной преградой.


9. Перескажите на суахили:

  • Wizara ya elimu na utamaduni ya Tanzania imefuta michango yote ya fedha taslimu wanazochanga wanafunzi pamoja na wazazi wao katika shule za msingi. Taarifa ya wizara hiyo imeeleza kuwa michango hiyo imefutwa ili kuboresha viwango vya elimu katika hatua ya msingi. Taarifa pia imefahamisha kwamba imegundulikana kuwa michango mbalimbali wanayotozwa wanafunzi na wazazi wao imeathiri maendeleo ya elimu ya msingi kutokana na baadhi ya wazazi kushindwa kulipia fedha za kuandikishwa. Hata wale walioandikishwa wanashindwa kuendelea na masomo baada ya kushindwa kulipiwa michango mbalimbali.

  • Wanafunzi wa darasa la saba nchini Tanzania leo wanafanya mitihani yao ya kumaliza elimu ya msingi. Meya wa manispaa ya Ilala Hamis Juma, katika salamu zake kwa wanafunzi wanaofanya mitihani hiyo, amewataka kuwa watulivu na makini wakati wote wanapofanya mitihani. Kwa upande wa manispaa yake, alisema wanafunzi watakaofanya mitihani hiyo ni 8,952 ambapo wavulana ni 4,400 wakati wasichana ni 4,552.

  • Mkutano wa kimataifa wa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo, utaanza rasmi Septemba 1 hadi 9 katika chuo kikuu cha Dar es Salaam. Mwenyekiti wa maandalizi ya mkutano huo Fidelis Benedict aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa wanazuoni 250 kutoka mabara yote duniani wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo. Alisema kauli mbiu ya mwaka huu kwa mkutano huo ni “Tuifanye dunia mahali pema pa kuishi”, ambapo mada zitakazojadiliwa ni kuhusu ukimwi na athari zake kwa vijana, uongozi na maendeleo.

10. Переведите:

  1. Каждый человек должен стремиться достичь определенного уровня образования и получить максимум знаний для того, чтобы идти в ногу со временем.

  2. В колониальные времена дети бедняков были лишены возможности учиться, так как их родители не имели средств к существованию, не говоря уж о возможности заплатить наличными за обучение своих детей.

  3. В наше время все дети школьного возраста, в том числе и дети неимущих родителей, имеют возможность получать начальное образование, не испытывая на себе никакой дискриминации.

  4. Система образования в этой стране позволяет принимать в высшие учебные заведения детей всех слоев общества без каких-либо ограничений или предпочтений.

  5. В своем выступлении министр подчеркнул, что долг всех преподавателей побуждать учащихся к учебе и всячески помогать овладевать знаниями, которые пригодятся им в их дальнейшей работе на благо народа.

  6. Помимо начальных школ, проблема нехватки учебных пособий обнаруживается и в средних школах, и это является огромным тормозом в развитии образования.

  7. Курс правительства этой страны не соответствует реальным интересам народа и идет вразрез с теми обещаниями руководителей, которые они давали во время предвыборной кампании.

  8. Университет – это центр образования, который вносит весомый вклад в дело подготовки высококвалифицированных специалистов во всех областях знаний, включая инженеров, менеджеров, математиков, бухгалтеров и других.

  9. Знатоки и любители суахили соберутся вместе, чтобы обсудить вопросы развития языка, литературы и, вместе с тем, высказать свое мнение на тему об использовании суахили в программах обучения в высшей школе.

Msamiati

-lingana соответствовать, совпадать -salia оставаться

-linganisha сопоставлять, сравнивать muhali трудно; невозможно

mnyonge (wa-) притесненный человек maelekezo (мн.) указания,

mhasibu (wa-) бухгалтер; счетовод наставления

kima (vi-) 1) величина, размер tamko, tamshi (ma-) речь,

2) уровень 3) цена, стоимость выступление; заявление



kima cha chini минимум sera (-) 1) политика, курс

kima cha juu максимум 2) стратегия

hima (-) спешка, торопливость mada (-) тема

-himiza 1) торопить, ускорять mfumo (mi-) система, строй

2) побуждать, призывать seuze не говоря уже о…



-tia hima поторапливать kipingamizi (vi-) преграда,

taalimu, taaluma (-) препятствие

1) образование, ученость fii (-) плата; взнос

2) область знания; наука msisitizo (mi-) обращение

mapendeleo (мн.) предпочтение, внимания, подчеркивание

предвзятость fasihi (-) литература



kauli mbiu лозунг; призыв mbali na кроме; помимо того

azma (-) цель, намерение; решение -fuatilia прослеживать,

manispaa, munispaa (-) городской следить

совет; муниципалитет taslimu (-) наличными



-pasi сдать, выдержать (экзамен) -durusu изучать, учить

-pasisha принимать; пропускать mwanazuoni (wa-) ученый
* * *

Урок 23. Somo la ishirini na tatu

Грамматика

  1. Инфинитивная форма глагола и общее настоящее время -a- в заглавиях и газетных заголовках.

  2. Глагол -wa в желательно-побудительном наклонении в сочетании с конечными локативами -po, -ko, -mo.


Инфинитивная форма глагола часто встречается в заглавиях и газетных заголовках, заменяя личные формы глагола. В этом случае инфинитив, как правило, передает ожидаемое или планируемое действие, которое еще не совершилось, но совершится в ближайшее время. На русский язык такие заголовки чаще всего переводятся с помощью глагола будущего времени. Например:

Rais kumpokea mgeni mkubwa “Президент примет высокого гостя”;

Mkutano wa viongozi wa Afrika kufanyika Addis Ababa “Совещание африканских лидеров состоится в Аддис Абебе”.

Общее настоящее время с показателем -a- также употребляется в заглавиях, но в отличие от инфинитива, оно акцентирует действие, которое уже совершилось, либо совершаемое в данный момент. Точный перевод подскажет контекст. Сравните: Rais ampokea mgeni mkubwa “Президент принял (принимает) высокого гостя”; Mkutano wa viongozi wafanyika Addis Ababa “Совещание руководителей состоялось (проходит) в Аддис Абебе”.


Глагол в желательно-побудительном наклонении передает значение просьбы, пожелания или побуждения к выполнению действия. Особенностью глагола -wa в этом наклонении заключается в том, что в сочетании с локативными формантами -po, -ko, -mo он может еще указывать на желательность или необходимость совершения действия в определенном месте. В предложениях с такими формами всегда присутствуют обстоятельства места, либо существительные с локативным суффиксом -ni, которые могут выступать как подлежащее. Например:

Amani iwepo duniani! “Пусть будет мир на земле!”

Skuli mpya ziwepo mjini mwetu “Новые школы должны быть в нашем городе”;

Kituoni hapa lazima kuwepo ratiba ya usafiri wa mabasi “На этой остановке обязательно должно быть (вывешено) расписание автобусов”.

Отрицательная модель данной конструкции строится с помощью негативного форманта -si-:

Watu wasiwepo hapa! “Люди не должны находиться здесь!”


Mazoezi

1. Переведите следующие заголовки:

1. Madaktari kukutana Jumanne kujadili utumiaji wa dawa jipya la kinga. 2. Mazungumzo ya viongozi wa dini yafanyika mji mkuu. 3. Mchezo wa soka wafutwa kwa ajili ya mgogoro. 4. Maonyesho ya vitabu ya kimataifa kufunguliwa mwishoni mwa wiki hii. 5. Masharti mapya yawepo kuhusu utozwaji kodi. 6. Duniani kuwepo ushirikiano kupambana na ukimwi. 7. Jijini pasiwepo kiwanda cha saruji.


2. Переведите предложения на суахили, используя желательно-побудительное наклонение глагола -wa с соответствующим локативным релятивом:

1. Директор стремится к тому, чтобы в нашей школе были компьютеры в каждом классе. 2. Мы мечтаем о том, чтобы в нашем районе был современный спортивный центр. 3. Власти города решили, что на этом месте должен быть зоопарк. 4. В соответствии с планом развития нашего села здесь должна быть крупная птицеферма. 5. Эта территория очень опасная, люди не должны находиться здесь. 6. Президент призвал политические партии покончить с разногласиями с тем, чтобы в стране был устойчивый мир. 7. Пусть будет крепкая дружба между нашими народами! 8. Наша организация борется за то, чтобы между мужчинами и женщинами было полное равенство, и не было никакой дискриминации. 9. Умирая, отец завещал своим сыновьям, чтобы между ними не было никакой вражды, а было взаимопонимание и взаимовыручка. 10. Пусть в вашем доме будет мир да любовь!


SERIKALI KUPAMBANA NA DINI

YENYE VURUGU

Mkuu wa wilaya ya Lushoto Bw. Elia Mpesa amesema kuwa serikali itakuwa tayari kupambana na dini yoyote yenye lengo la kuvuruga amani nchini kwa kuleta mfarakano na dini nyingine.

Bw. Mpesa alisema hayo alipokuwa akitoa hotuba yake katika kikao cha viongozi wa dini ya Kiislamu na ya Kikristo pamoja na madiwani kilichofanyika Ijumaa iliyopita katika ukumbi wa ofisi yake.

Alisema serikali itaendelea kuwahudumia na kuwatendea haki wananchi wake kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za nchi chini ya msingi mkuu wa usawa wa binadamu bila kuingilia uhuru wa kuabudu, lakini itapambana na wenye kuvuruga uhuru huo.

Alisisitiza kuwa viongozi wote wa dini wahubiri upendo ili kulinda na kudumisha amani nchini pamoja na kuwasaidia viongozi wengine wa serikali bila kujali vyeo vyao.

Aliwaomba viongozi wa dini kuwaelemisha waumini kuwa viongozi mbalimbali wa serikali wana dini lakini hawaongozi kwa kutumia misingi ya dini ila kwa kufuata katiba ya nchi.

Bw. Mpesa alisema kuwa anatumaini viongozi hao watahubiri mambo mema na kuyakemea maovu bila aibu kwa ajili ya usitawi wa dini, taifa la Tanzania, Afrika na ulimwengu mzima.

Katika kikao hicho ambacho ni cha kwanza tangu apewe wadhifa huo, aliyapongeza madhehebu yote ya dini kwa mchango wao wa kuboresha huduma za jamii serikalini kwa kuanzisha vituo vya afya na shule wilayani hapo.


ASKOFU WALAANI MALUMBANO YA KIDINI

Askofu Basil Sambano wa kanisa la Anglikana la Dar es Salaam, amelaani vitendo vya malumbano ya kidini vinavyofanywa na baadhi ya waumini wa dini za Kikristo na Kiislamu kote nchini.

Katika waraka wake alioutoa kwa vyombo vya habari jana, askofu Sambano alisema sababu zinazopelekea uhusiano wa Wakristo na Waislamu kuzorota* kuanzia miaka ya 80 mpaka sasa hazijulikani waziwazi, na akataka kila upande kufikiria mikakati na mbinu za kukabiliana na hali hiyo.

Askofu Sambano alisema uenezaji dini kwa njia ya kushawishi watu, kuoana, au kwa njia ya biashara haviwezi kuleta athari katika jamii lakini dini zinapoenezwa kwa mabavu, dharau, chuki na kulazimisha ndipo matatizo yanapotokea.

Alionya kuwa mihadhara ya dini ya kukashifiana inayoendelea hivi sasa hapa nchini, hasa jijini inaweza kusababisha ghasia na kuvuruga amani.

“Vita zinazoanza kwa chanzo cha imani ni vigumu kumalizika na makovu au matokeo yake hudumu vizazi hadi vizazi,” alisema.

Askofu alisema dini zote huhubiri upendo wa Mungu na kuwa ni lazima watu wapendane bila kujali tofauti zao kiimani, jinsia, rangi, lugha, umri au tofauti yoyote ya kimaumbile ya mtu na akasema wasio na upendo hawana dini.
MAASKOFU WAHIMIZA IMANI

Maaskofu Katoliki wamewashauri Watanzania kuheshimu na kuthamini imani mbali mbali za wananchi wote, ili pawepo maelewano na amani ya kudumu nchini.

Rai hiyo ilitolewa na rais wa baraza la maaskofu katoliki askofu Justine Samba, wa jimbo la Musoma. Alisema waumini wa madhehebu yote wanapaswa kujenga moyo wa kuheshimu na kuthamini imani ya kila mwananchi, wakizingatia kanuni na katiba ya nchi inayosema “kila Mtanzania ana uhuru wa kuabudu dini anayotaka.”

Alisema ukweli huo pia unathibitishwa na matamko rasmi ya Umoja wa Mataifa katika ibara yake ya 19. Kiongozi huyo wa maaskofu kwa niaba ya maaskofu wenzake, alimpongeza na kumshukuru Rais wa Zanzibar kwa hotuba yake ya sikukuu ya Idd El Fitri,** kwa kuhimiza uelewano, upendo na heshima katika kuthamini imani mbali mbali baina ya waumini wa madhehebu yote nchini.


Maelezo

* Sababu zinazopelekea uhusiano … kuzorota. “Причины, которые приводят к ухудшению отношений”. Глагол -peleka “отправлять”, “посылать” в направительной форме в данном контексте можно переводить как “приводить к чему-либо”, “вызывать что-либо”.
** Idd El Fitri “Ид-аль-фитр” – мусульманский праздник подношения по случаю розговенья по окончании поста в месяце рамадан.
Mazoezi

3. Дайте русские эквиваленты:

lengo la kuvuruga amani; -leta mfarakano; -ingilia uhuru wa kuabudu; msingi mkuu wa usawa; uhuru wa kuabudu; bila kujali vyeo vya viongozi; watahubiri mambo mema na kuyakemea maovu; madhehebu ya dini; vitendo vya malumbano; uhusiano umezorota; sababu hazijulikani wazi wazi; -fikiria mikakati na mbinu za kukabiliana na hali mbaya; uenezaji dini kwa mabavu; -sababisha ghasia; bila ya kujali tofauti za kijinsia; -toa rai; -jenga moyo wa kuthamini imani zote; matamko rasmi ya Umoja wa Mataifa; kwa niaba ya maaskofu wenzake.



4. Дайте эквиваленты на суахили:

подрывать мир; нарушать спокойствие; подрывать доверие; расходиться во взглядах; расходиться друг с другом; разделяться; отделяться; основные принципы; основы знаний; фундаментальные законы; бороться с врагами; бороться за независимость; бороться против дискриминации; свобода совести; политическая свобода; свобода печати; верующие; вера; доверие; недоверие друг к другу; взаимные упреки; ссора; споры; ухудшаться; улучшаться; нормализоваться; стратегия и тактика; методы исследования; способы получения нового лекарства; оказывать влияние; влиять; оказывать помощь; принимать во внимание; подчеркивать; обдумывать.


5. Переведите письменно следующий текст:

Kiongozi wa Wahindu apongeza mshikamano

wa Watanzania

Kiongozi wa madhehebu ya Wahindu Shri Pandya, amezisifu juhudi zinazofanywa na serikali za kuwaunganisha Watanzania na kuwafanya wawe kitu kimoja bila ya kujali tofauti zao za kidini, kiitikadi, jinsia na rangi.

Shri Pandya amesema hayo jana wakati alipomtembelea rais wa nchi na kufanya naye mazungumzo mafupi Ikulu, Dar es Salaam.

Kiongozi huyo alisema juhudi hizo za kuwafanya Watanzania waiishi kama familia moja ni muhimu sana kwa usitawi wa wananchi wenyewe na taifa kwa ujumla.

Amesisitiza kuwa tofauti za kidini au rangi zisiwepo katika maisha ya Watanzania na hasa kwa kuzingatia kwamba wote wanamwamini Mungu yule yule, na kwamba wanafanana kiroho isipokuwa tofauti zao ziko katika maumbile tu.

Shri Pandya amewahimiza Watanzania kujali elimu kwani ndiyo inayomwezesha mtu kuyakabili mazingira anayoishi katika dunia ya leo na vile vile itamwezesha katika kuchangia maendeleo ya nchi yake.



6. Переведите:

  • Президент страны напомнил всем мусульманам, проживающим здесь, как важно уважать всех других граждан, не являющихся последователями ислама. Выступая по случаю праздника Ид-аль-фитр в главной мечети города Дар эс Салаама, президент сказал, что правительство Танзании предоставило абсолютно всем свободу выбирать себе любую религию. Поэтому мусульмане, как и остальные граждане, обязаны уважать религиозные убеждения других людей, а все, кто не являются мусульманами, должны проявлять уважение к людям этой религии. “Пусть будут добрые отношения, любовь и согласие между всеми нами,”- подчеркнул президент в своем выступлении.

  • Руководители всех религиозных конфессий Танзании призвали политические партии страны, а также всех граждан преодолеть существующие между ними противоречия, проявить мудрость и уважение к религиозным убеждениям каждого во имя мира и спокойствия. Надо признать, что политическая нестабильность в стране не может отвечать интересам граждан, будь то последователь ислама, христианства или какой-либо другой религии, подчеркнули религиозные деятели.

  • Имамы Занзибара поблагодарили президента страны за его вклад в укрепление мира и достижение прогресса на благо всего населения. Сейчас, подчеркнули они, когда страна стоит на пороге очередных выборов, очень важно сохранить мир и не допустить раскола в обществе на основе религиозных разногласий. Только в условиях мира и согласия можно достичь процветания и лучшей жизни.


7. Переведите следующий текст и выскажите свое мнение на суахили по поводу его содержания:
Dini ni imani

Sisi Waafrika tunajua kwamba dini ni imani, mtu akiwa hana dini sisi hatusemi mbaya, lakini tunasema huenda ikawa imani yake ndogo. Hatusemi kuwa yeye ni mbaya, hatuthubutu kusema hivyo, huwa na shaka tu kuwa imani yake ni fupi kwa sababu anaishi hana kitu anachokiamini. Dini zinatufunza kupendana wenyewe kwa wenyewe, kuheshimiana, na kusaidiana katika dhiki zaidi kuliko katika raha, kwani raha hazina msaada, lakini misaada iko katika dhiki.

Tukisikia mwenzetu katika sisi yumo katika dhiki tukusanyike tumsaidie mtu huyo. Basi dini ni kitu kizuri kinachotufunza mambo mazuri, hakuna dini inayofunza mabaya.
Msamiati

-vuruga вносить беспорядок; maovu (мн.) 1) зло; вред

нарушать; мешать 2) несправедливость



vurugu (-; ma-) беспорядок, kovu (ma-) шрам, рубец

путаница waraka (nyaraka) 1) письмо,



-farakana расходиться во послание 2) документ

взглядах, иметь разногласия -zorota ухудшаться,



mfarakano (mi-) разногласия, отставать (в развитии)

раскол; расхождения в взглядах mbinu (-) 1) метод; прием;



ghasia (-) беспорядок; способ 2) тактика

неразбериха mabavu (мн.) сила,



imani (-) 1) вера, верование насилие, принуждение

2) доверие 3) убеждение diwani (ma-) член



-abudu молиться; поклоняться городского совета

-hubiri проповедовать mhadhara (mi-) лекция

hubiri (ma-; -) проповедь -kashifu позорить,

mwumini (wa-) верующий человек оскорблять

ibara (-) раздел; абзац jinsia (-) 1) пол (физиол.)

Ikulu (-) резиденция 2) национальность

правительства; дворец президента malumbano (мн.) ссоры,


1   ...   13   14   15   16   17   18   19   20   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət