Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə20/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   17   18   19   20   21   22   23   24   25

4. Закончите фразы, опираясь на содержание текста:

1. Takriban nchi kutoka mabara yote matano zilishiriki katika maonyesho ya utalii ya kimataifa ambayo … 2. Nchi hizo zilitembeza utalii wao, kuanzia … 3. Mwaka uliopita kwa mujibu wa Shirika la Dunia la Utalii, … 4. Katika mwaka huo kiasi cha safari za kitalii … zilifanyika kwenye pembe mbali mbali za dunia na kiasi hicho ni … kuliko mwaka uliotangulia. 5. Nchi zinazoongoza katika biashara ya utalii ni … 6. Nchi ambazo biashara zao za utalii zilizorota ni … 7. Nchi za Afrika zilizofika kwenye maonyesho ya Berlin ni … isipokuwa … 8. Kenya ilifika katika maonyesho na mashirika yake …, huku Tanzania na … 9. Uganda nayo pia haitaki … 10. Nchi hiyo iliitwa “Lulu ya Afrika” na … ambaye …


5. Перескажите текст, используя словосочетания:

-tembeza utalii; -enda sambamba na; biramu la karne ya 21; matokeo ya kukumbuka mileniam mpya; kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi; katika pembe mbali mbali za dunia; nchi za usoni; -tupwa nyuma; kipimo kidogo; biashara ilizorota; -rekebisha dosari; anwani mashuhuri za watalii; -wakilishwa kwa wingi wa mashirika; machafuko ya kisiasa; juhudi zimezaa matunda; daftari la safari.


6. Переделайте предложения, употребив желательно-побудительное наклонени и переведите их:

1. Siku moja mwalimu alimtuma Juma nyumbani kwake kutazama saa na kurudi darasani upesi iwezekanavyo. 2. Baada ya kumaliza elimu yake ya miaka minane Juma alikata shauri la kwenda mjini kujitafutia kazi. 3. Shabaha na lengo lake lilikuwa kwamba lazima kufika mjini Nairobi haraka iwezekanavyo. 4. Kisha yule polisi akamgeukia Juma na kumwamrisha kusimama ili kumpeleka jela. 5. Sultani akasema, “Lakini kwanza hatuna budi kukumbuka vyema jinsi ya kutenda ili kuweza kurudia umbo letu la kibinadamu”. 6. Tena haiwezekani kucheka kabisa wakati wo wote, tukicheka tutaendelea kukaa katika hali hiyo mpaka kufa. 7. Yule msimulizi akamjibu mfalme akamwambia, “Naomba kukatwa kichwa kwa upanga”. Mfalme akamwita askari akamwamuru kumkata kichwa yule mtu pale pale. 8. Sultani akamwambia Muki, “Nitakuachia huru, lakini kwanza naomba kunieleza siri ya nguvu ya mbio zako za ajabu”. 9. Baba yake akampa shauri, “Mwambie kukupa ng’ombe kumi, na ng’ombe watano kukupa kwanza kabla hujaingia pangoni”. 10. Askari wetu watakutana Ngulu, kisha watakwenda tambarare ili kuwa tayari kuwashambulia Wakamba kutoka upande wa mashariki. 11. Mzee mmojawapo aliwaambia askari kukusanya kuni na kuzitia moto ili kufanya moshi wake kuonekana toka mbali.


7. Переведите тексты и перескажите их на суахили:

Paa kuwindwa miezi sita tu Zanzibar

Serikali ya Zanzibar imeamua kuchukua hatua kadhaa za kudhibiti uwindaji wa paa ambao idadi yao imekuwa ikipungua sana ili kuwanusuru wasitoweke visiwani hapa.

Taarifa ya serikali iliyotolewa na waziri wa kilimo, maendeleo ya mifugo na mali asili, Adam Mwakanjuki ilisema, kuanzia sasa uwindaji wa wanyama hao visiwani utakuwa kwa kipindi cha miezi sita tu kwa mwaka na muda uliobaki utatumika kuwapa nafasi kuzaliana na kulea watoto wao.

Hata hivyo taarifa hiyo ilisema kuwa uwindaji wa paa aina ya ‘Nundu’ ambao ni adimu duniani umepigwa marufuku. Katika nchi za Afrika ya Mashariki paa hao hupatikana Kenya na idadi yake imepungua sana.



Tembo waleta athari Sikonge

Kundi kubwa la tembo limeharibu zaidi ya ekari 120 za mazao mbalimbali ya chakula na biashara katika wilaya ya Sikonge, mkoani Tabora, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Kwa mujibu wa maelezo ya mkuu wa wilaya hiyo, Beatrice Mkina, tembo hao walivamia vijiji vingi mbali mbali. Alisema, wanyama hao wamekuwa wakila zaidi viazi, mtama, mahindi na karanga, ambapo pia wamekuwa wakipita kwenye mashamba ya tumbaku na kuyaharibu. Tembo hao wanakula pia tumbaku.

Mkuu wa wilaya alisema kwamba amejaribu kutoa taarifa mara kadhaa kwa maofisa wa wanyamapori waliopo kwenye kituo cha Ipole wilayani humo, lakini mpaka sasa hajapata taarifa iwapo maofisa hao watakwenda kuwapiga tembo hao.

Alisema tembo hao wamekuwa wakivamia mashamba kila baada ya muda, na kama hatua za haraka hazitachukuliwa, kuna uwezekano wa tembo hao kuharibu mazao zaidi, na kuwaathiri wananchi.

Tembo hao inasemekana wametokea kwenye hifadhi ya Ugala na pori la Kitunda ambako ukame umeathiri malisho yao. Wananchi wamekuwa wakikabiliana na tembo hao kwa kuwapiga mawe na kuwakimbiza, lakini Bi. Beatrice alisema kwamba wanaendelea kuingia kwenye shamba moja hadi jingine. Hata hivyo maisha ya wananchi hayako hatarini.


8. Найдите в текстах из предыдущего задания предложения с аналитическими глагольными формами и проанализируйте их.
9. Подберите синонимы к подчеркнутым словам и выражениям:

-jumuika; -hamasisha watu; mbinu za kizamani; sherehe zimetia fora; dosari; -nusuru; kwa mujibu wa; -dhibiti; chini ya biramu; takriban; kiingilio -faidika; nchi za usoni; kipimo kidogo; -tupwa nyuma; dosari; mwakilishi; machafuko ya kisiasa; utulivu; -jiweka kando; -pora; mhudumu; msimamizi; mtembezi; -boresha; uzoefu; msingi wa maisha; motisha; uzio; matunda mabovu; -kata tamaa.



10. Переведите письменно следующий текст:

Tanzania yanunua faru Afrika Kusini

Faru kumi weusi wataingizwa nchini kutoka Afrika ya Kusini baadaye mwaka huu zikiwa ni juhudi za kuongeza idadi ya wanyama hao ambao wapo hatarini kutoweka.

Msimamizi mkuu wa hifadhi ya Mkomazi iliyopo mkoani Kilimanjaro Bw. Tonny Fitzjohn alimwambia mwandishi wetu wa habari kuwa faru hao watarushwa kwa ndege kubwa za mizigo aina ya Hercules za Jeshi la Anga la Afrika Kusini Agosti mwaka huu.

Bw. Fitzjohn alisema mradi wa kuhamishia faru kutoka Afrika Kusini una lengo la kuboresha mbuga ya Mkomazi na unafadhiliwa na mfuko wa hifadhi ya wanyamapori wa George Adamson.

Alisema faru hao wamemgharimu dola za Kimarekani 45,000 kila mmoja na kwamba Jeshi la Anga la Afrika Kusini limejitolea kumsaidia kuwasafirisha bure faru hao wakati kampuni ya kimataifa ya British Petroleum (BP) imejitolea kutoa mafuta ya ndege bure kwa ndege zitakazotumika.

Meneja mwendeshaji wa mbuga ya Mkomazi, Bw. Arisaria Nnko alisema matayarisho yote kuhusiana na zoezi hilo yamekamilika. Bw. Nnko alitaja mambo yaliyofanyika katika matayarisho hayo kuwa upanuzi wa kiwanja kidogo cha ndege kiweze kutua ndege aina ya Hercules na ujenzi wa uzio maalum wa umeme kuwazuia faru hao kutangatanga wasije kukutwa na majangili.

Alisema matayarisho mengi kuwa pamoja na kujenga maboma maalum sita yatakayotumika kuwapokelea na kuwalishia kwa mikono hadi wazoee kidogo binadamu na utayarishaji wa kompyuta maalum ndogo sana zitakazowekwa kwenye pembe za faru hao ili kuwajua wakati wote wapo wapi.

“Hata kama jangili atavuka nyaya za umeme tulizoweka na akafanikiwa kumuua faru akatoroka na pembe yake, bado tutaweza kufuatilia kompyuta hiyo hadi alipoificha pembe yake,” alisema Bw. Nnko kwa kujiamini.

Akijibu swali, Bw. Fitzjon alisema faru hao kutoka Afrika Kusini ni aina ile ile na kizazi cha faru waliopelekwa huko kutoka Afrika Mashariki. Faru hao walitolewa eneo hilo hilo la Mkomazi lakini upande wa pili wa Kenya ambako kuna mbuga ya wanyama ya Tsavo mwaka 1962.
11. Переведите:


  1. Почти все страны участвовали в Международной выставке, рекламируя свой туристический бизнес, в том числе свои заповедники, роскошные пляжи, достопримечательности, современные отели.

  2. В наши дни развитие туризма неразрывно связано с проблемами охраны окружающей среды, стоящими перед всем миром. Проблема борьбы с браконьерством особенно актуальна на африканском континенте.

  3. За одно только десятилетие показатели этой отрасли экономики возросли на 20 процентов, что почти вдвое выше, чем за предыдущий отрезок времени.

  4. К сожалению, африканский континент сильно отстает в развитии туризма в своих странах, и рост в полтора процента является самым низким за все время.

  5. В то время как большинство стран Африки видят реально результаты своих усилий в развитии этой сферы, такие страны как ЮАР и Зимбабве оказались в числе отстающих. Поэтому им пришлось рекламировать себя особенно активно.

  6. Одним из самых посещаемых туристами регионов Африки является Восточная Африка, которая особенно популярна среди гостей из Германии и Швейцарии.

  7. Танзания была представлена на выставке 27 туристическими компаниями, в то время как Кения превзошла ее и прислала своих представителей от 37 организаций.

  8. Министры, участвовавшие в торжествах по случаю официального открытия выставки, воспользовались этой возможностью и встретились, чтобы обсудить пути и методы развития сотрудничества между своими странами.


Msamiati

-tembeza 1) водить, возить -kiri признаваться,

2) демонстрировать, сознаваться

рекламировать asilimia (-) процент

mtembezi (wa-) турист; -amuru приказывать,

посетитель (выставки и т.п.) предписывать



biramu, beramu (ma-) 1) флаг, -nusuru 1) спасать,

знамя 2) символ; лозунг освобождать, 2) защищать



mwakilishi (wa-) представитель mwongo (mi-) 1) десяток

-wakilisha представлять; 2) декада; десятидневка

уполномачивать dosari (-) дефект, изъян,



kipimo (vi-) 1) единица недостаток

измерения 2) величина jeshi la anga военно-



msimamizi (wa-) 1) надзиратель воздушный флот

2) управляющий -tangatanga ходить взад и



jangili, jangiri (ma-) браконьер вперед; слоняться

-rekodi записывать, фиксировать -faidika получать выгоду,

mradi (mi-) 1) план, проект извлекать пользу

2) объект (строительный и т.п.) -kanusha 1) отвергать,



milenia (-) тысячелетие отклонять 2) опровергать

* * *

Урок 27. Somo la ishirini na saba
Грамматика

Конструкции с глаголами чувственного восприятия.


В суахили можно встретить целый ряд глаголов, передающих различные формы чувственного восприятия. Например: -ona “видеть, чувствовать”, -sikia “слышать, чувствовать”, -angalia “смотреть внимательно, наблюдать”, -hisi “чувствовать, ощущать”, -fuatilia “следить”, -kuta “встретить, обнаружить”, -kumbuka “помнить” и др. За подобными глаголами при этом часто следует глагол, оформленный показателем -ki-, отображая действие, процесс или состояние, наблюдаемые или ощущаемые в момент действия. На русский язык такие глагольные конструкции можно переводить причастными оборотами или с помощью придаточного предложения:

Tulimwona mtoto akianguka mtini “Мы видели падающего с дерева ребенка”;

Nilipoingia ukumbini nilimsikia akiimba “Войдя в зал, я услышал, как он поет”.

После глагола -kuta также может употребляться глагол с показателем -me-, передающим результат или завершенность действия:

Wakakuta nyumba zimechomwa moto na mji umeangamizwa kabisa “Они обнаружили, что дома сгорели, а город уничтожен до основания”.

За такими глаголами как -ona, -sikia, -hisi нередко следует глагол с показателем -na-, отражающим незавершенность, продолжительность действия во времени, о котором идет речь. В этом случае смысл конструкции очень близок к тому, что передается с помощью показателя -ki-. Например:

Usiku ule walisafiri sana jua lisiwaone wanakuja, na mchana walipumzika “В ту ночь они долго шли, чтобы солнце не видело, как они подходят, а днем отдыхали”.

Говоря о глаголах чувственного восприятия, следует иметь ввиду и их производные формы, например -onekana “быть видимым”, -sikika “быть слышимым”, -jikuta “оказаться (в какой-л. ситуации)” и другие. Они также встречаются в контекстах, перечисленных выше, и требуют употребления соответствующих глагольных конструкций.


Mazoezi

1. Раскройте скобки, употребив глагол в требуемой по смыслу форме. Переведите полученные предложения:

1. Alipokaribia nyumba ya baba yake alisikia sauti ya mti (-chongwa). 2. Watoto walionekana (-cheza) kwenye sehemu zilizokuwa wazi, na moshi ulionekana (-panda) kutoka kwenye nyumba fulani fulani. 3. Kulikuwa na ua mkubwa kuizunguka nyumba ya chifu na aliweza kumwona mlinzi (-simama) mlangoni akiangalia kijia kinachotoka bondeni. 4. Tegu alimwona jirani yake (-kimbia mbio) kwenye kijia kilichokuwapo kando ya mto. 5. Alikuwa amechoka kumwona baba yake (-shughulika) na uchongaji tu daima. 6. Wasiwasi wa Juma ulimtoweka wakati alipokutana na jamaa mmoja wa kwao (-rudi) Nairobi baada ya likizo ya mwezi mmoja. 7. Chifu alionekana (-toka) kwa mbali, na alikuwa anatembea mbio mbio. 8. Goja akajibu: “Sikutaka kumkuta Mfupa (-kalia) kiti cha Ufalme. 9. Watu walionekana (-songa mbele) na kushika mikuki yao juu, na waliitelemsha wakati ule walipokutana na rafiki uso kwa uso tu. 10. Tegu alimwangalia Mkamba mmoja (-endea) Mchaga kwa nyuma na kumpiga kichwani.


2. Переведите предложения, употребив глаголы чувственного восприятия и оформив последующие глаголы соответствующим образом:

1. Из окна моего дома я каждое утро наблюдал, как рабочие шли в сторону завода быстрым шагом. 2. И вдруг он почувствовал, как кто-то внимательно смотрит на него. 3. Когда ты увидишь, что сестра возвращается домой, попроси ее сходить в магазин за молоком. 4. Мы встретили отца, направлявшегося в поле и несущего огромную корзину для сбора кукурузы. 5. Я помню, как по праздникам мама готовила вкусные блинчики с джемом. 6. Ты слышал, как кричали гиены прошлой ночью? 7. Если вы увидите, что дедушка отдыхает, играйте тихо, чтобы не беспокоить его. 8. Облака на небе рассеялись, и было видно, как солнце медленно исчезает за горизонтом. 9. Было слышно, как вода с грохотом обрушивалась со скалы вниз. 10. Войдя в сад, они застали детей прыгающими с деревьев. 11. Гуляя по лесу и фотографируя редко встречающиеся растения, туристы вдруг обнаружили, что заблудились. 12. Вернувшись из длительной поездки, родители застали своего сына сильно похудевшим и изможденным. 13. Мы услышали, как зазвонил звонок, и пошли на занятия.


UHARIBIFU WA MAZINGIRA TANZANIA

Suala la mazingira limekuwa likijadiliwa kwa kina ulimwenguni kote ikizingatia kuwa mazingira ni uhai. Hata hivyo hatua zinazochukuliwa kuyahifadhi zina kazi ndogo kuliko ile ya uharibifu.

Baada ya mkutano wa kimataifa ulioitishwa na Umoja wa Mataifa Rio de Janeiro, Brazil takriban miaka minne iliyopita, uharibifu wa mazingira umekuwa ukiongezeka na hivyo kuzidisha hatari ya umaskini utakaoendelea kuzikumba nchi zinazoendelea. Hii inatokana na ukweli kwamba mazingira mazuri yana nafasi kubwa sana kwa maendeleo ya nchi na hasa pale mali asili zinapotumiwa kwa utaratibu wa kisasa lakini usio na madhara kwa mazingira.

Tanzania ni moja ya nchi zilizoshiriki kikamilifu kwenye Mkutano wa Mazingira wa Brazil, na ni nchi ambayo imo vitani dhidi ya waharibifu wa mazingira. Lakini vita hivi vimekuwa ni vigumu sana kwani kwanza, wapiganaji kwa njia moja au nyingine ni miongoni mwa wasababishaji wa uharibifu wa mazingira bila ya wenyewe kujitambua. Pili, ni hali ya kupigana vita na matokeo ya uharibifu badala ya kwanza kutambua na kudhibiti chanzo cha uharibifu na hii inakuwa ngumu zaidi kutokana na umaskini wa wananchi wake lakini si nchi.

Kwa ujumla umaskini wa Tanzania ndio sababu kubwa ya uharibifu wa mazingira. Umaskini huo ndio hasa unaomfanya mtu wa kijijini asipate elimu ya umuhimu wa utunzaji mazingira, kwa vile hajui madhara ya uharibifu wa mazingira, asilimia kubwa ya maisha yake, na utamaduni wake, yamo katika uharibifu wa mazingira.

Mazingira ambayo yanasababisha kuenea kwa magonjwa ni yale yaliyo machafu mathalani yasiyo na vyoo, na maji safi ya kunywa, kutokuwa na mashimo ya taka, kutoyachemsha na kutoyatunza hasa maji ya kunywa na misongamano ya watu katika eneo dogo, ni vyanzo vikuu vya maradhi.

Tatizo la mazingira haliishii hapo tu, hukua na kuelekea katika hewa ambayo huchafuliwa mara nyingi na viwanda. Kwa jamii maskini, ni nadra sana kuwa na ufahamu kwamba nyumba zilizopo karibu na maeneo ya viwanda zinahatarisha maisha hasa kwa kuvuta hewa yenye mchanganyiko wa kemikali ambazo zitadhuru maisha yetu ya baadaye.

Uharibifu wa ardhi nao umekuwa ni tatizo kubwa sana katika suala la mazingira. Hii imechangiwa sana na kutotumiwa kwa njia za kitaalamu katika kulima, kuwepo mifugo mingi katika eneo moja dogo na ujenzi wa nyumba usiofuata taratibu za kitaalamu.

Watu bado hawana uchungu wa maisha yao hasa kwa miaka ijayo inayoelekea kukabiliwa na jangwa, ukame, njaa na umaskini uliokithiri. Wapo watu ambao bado wanafyeka misitu kwa madhumuni ya kupata mbao, kuni na mkaa. Baadhi ya watu bado mitizamo yao ipo kwa maisha ya leo bila ya kuangalia maisha yajayo vizazi vijavyo vitaishi vipi? Wapo baadhi ya watu ambao bado wanachoma misitu kama moja ya mbinu za uwindaji bila ya kuelewa madhara yake.

Utumiaji wa kemikali na baruti kuvulia samaki kwa kiasi kikubwa unaharibu mazingira hasa kwa wanyama waishio baharini.

Baadhi ya watu wanakata miti ovyo huku wakielewa madhara yake, lakini kutokana na umaskini, hudiriki kufanya hivyo ili waweze kupata mbao, kuni au mkaa kwa ajili ya biashara. Vile vile watu wanaelewa sana madhara ya uvuvi wa baruti kwani hayapo kwa samaki tu, bali hata kwa mtumiaji mwenyewe.

Haya ndiyo mazingira ambamo vita dhidi ya waharibifu wa mazingira inapiganwa. Je, Tanzania itaweza kushinda wakati umaskini ndio kwanza unakithiri?*

Pamoja na hayo, zipo silaha ambazo zinaweza kutumika kushinda vita hivi dhidi ya uharibifu mkubwa wa mazingira nchini. Moja na muhimu ni suala la usafi kuwekwa katika utamaduni kwa lazima ili usafi wa mazingira ndani na nje ya nyumba iwe ni desturi ya kila siku kwa familia. Kutofanya hivyo huhesabika kuwa ni sawa na kuvunja sheria za nchi. Pili, kuwepo na adhabu ya kisheria kwa waharibifu wote wa mali asili zetu ambazo ndizo zinazolinda mazingira. Na mwisho, serikali kugharimia katika kupeleka wataalamu sehemu zote zenye mali asili ambazo ndizo zinaharibiwa. Wataalamu hawa, watawasaidia wananchi jinsi ya kuzinyonya kitaaluma maliasili zetu bila ya kuzidhuru na hivyo kunufaika nazo sasa na hata kuendelea kuwepo kwa vizazi vyetu vijavyo. Kwa hali hii hata suala la umaskini kwa kiasi kikubwa litaweza kupunguzwa makali.

La sivyo, uharibifu wa mazingira utaendelea kuwepo kizazi hadi kizazi. Shime Watanzania, kwani vita hivi si vya kiserikali tu, bali hapana budi wote kuelewa uchungu utakaotokea pindi nchi itakapogeuka jangwa kama jinsi dalili zinavyoanza kujitokeza na kujionyesha.


Maelezo

* …wakati umaskini ndio kwanza unakithiri “в то время, как обеднение (населения) только увеличивается”. Оборот ndio kwanza часто встречается в значении “только, только что”. В предложении он, как правило, занимает начальную позицию или после субъекта, но никогда после предиката: Somo ndio kwanza limeanza “Урок только начался”; Ndio kwanza wamekuja “Они только что пришли”.
Mazoezi

3. Дайте русские эквиваленты:

-jadiliwa kwa kina; -itisha mkutano; uharibifu wa mazingira; -zidisha hatari ya umaskini; -tumia mali asili kwa utaratibu wa kisasa; -leta madhara kwa mazingira; -shiriki kikamilifu; -dhibiti chanzo cha uharibifu; asilimia kubwa ya maisha ya wananchi; msongamano wa watu; vyanzo vikuu vya maradhi; mchanganyiko wa kemikali; -kabiliwa na umaskini uliokithiri; mbinu za uwindaji; -kata miti ovyo; uvuvi wa baruti; suala la umaskini litapunguzwa makali; dalili zinaanza kujionyesha.


4. Дайте эквиваленты на суахили:

оказывать вредное воздействие; широко обсуждать проблему; созывать международный форум; развивающиеся страны; развитые страны; наносить ущерб окружающей среде; повысить опасность обнищания масс; делать что-либо в полную силу; тем или иным способом; контролировать источники загрязнения; большое скопление людей; промышленные отходы; использование химикатов; решиться что-то сделать; это равносильно нарушению закона; снизить остроту проблемы; из поколения в поколение; признаки этого уже появились; превратиться в пустыню.


5. Переведите, используя отрицательную форму инфинитива:

1. Незнание правил дорожного движения помешало ему получить водительские права. 2. Их взаимное недоверие продолжало расти и привело к полному разрыву отношений. 3. Неучастие наших спортсменов в крупных международных соревнованиях огорчило очень многих. 4. Руководство больницы критиковали за несоблюдение санитарных норм медперсоналом. 5. Из-за невыполнения производственного плана рабочим сильно сократили зарплату. 6. Неприменение военной силы – один из важнейших принципов нашей новой стратегии. 7. Концерт не состоялся из-за неприбытия целой группы артистов. 8. Дети бедняков не могут учиться в школе из-за неуплаты их родителями денежного взноса.


6. Переведите следующий текст и преобразуйте его в диалог. Инсценируйте диалог в лицах:

Uwekezaji sekta ya utalii huangalia

pia mazingira

Wizara ya maliasili na utalii imesema baadhi ya maombi ya wawekezaji katika sekta ya utalii huchelewa kutokana na kuchelewa kupata tathmini ya athari zake kwa mazingira.

Waziri wa maliasili na utalii, aliliambia bunge jana kwamba inabidi maombi ya wawekezaji yaangaliwe kwa kina ili kukwepa athari za mazingira kwa sehemu zinazohusika.

Alikuwa akijibu swali la nyongeza la Henry Shekifu aliyetaka kujua sababu za kuchelewa kwa baadhi ya maombi ya wawekezaji katika sekta ya utalii.

Waziri alisema, “Kimsingi maamuzi mengi hayachukui muda mrefu isipokuwa mambo ya kuangalia ni uharibifu wa mazingira.”

Bw.Shekifu alidai kuwa yupo mwekezaji aliyecheleweshwa kwa zaidi ya miezi sita katika eneo la Magamba, bila kupatiwa maelezo yoyote ya ucheleweshaji huo.

Swali la msingi liliulizwa na William Shelukindo, aliyetaka kujua mpango wa serikali wa kuyaendeleza maeneo yenye mandhari za kitalii wilayani Lushoto.

Waziri alisema eneo lote la milima ya Usambara limewekwa katika mpango kamambe wa utalii, wenye lengo la kuendeleza ukanda wa kaskazini wa utalii.

Hata hivyo, waziri alisema serikali haitatangaza utalii katika maeneo ya milima, mito na mabonde ya asili kwa sababu hayajaendelezwa kwa utalii.

Alisema serikali inahakikisha wanyamapori wanahifadhiwa na kutunzwa kwa uangalifu kwa ajili ya kuinua pato la taifa na kutunza kwa ajili ya vizazi vijavyo.


7. Переведите письменно следующий текст:

Makamu wa rais aafiki kuhusu sheria

kudhibiti mazingira

Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameafiki pendekezo la baraza jipya la hifadhi na usimamizi wa mazingira kuwa zitungwe sheria kali na iundwe mahakama maalum ili kudhibiti wachafuzi wa mazingira nchini.

Pendekezo hilo lilitolewa kwa makamu wa rais na mwenyekiti wa baraza hilo jipya, alipokuwa akimkaribisha makamu wa rais kutoa hotuba ya uzinduzi wa baraza hilo. Katika hotuba ya uzinduzi huo wa baraza la hifadhi na usimamizi wa mazingira, makamu wa rais alisema kuwa serikali iko mstari wa mbele katika kutilia mkazo suala zima la mazingira na ndiyo sababu baraza hilo limewekwa chini ya ofisi yake.

Alisema sheria zilizopo kwa kiasi fulani zinatoa nafasi kwa watu kutokuwa makini lakini wakati umefika ambao zinahitajika sheria kali ili kuokoa mazingira yetu. Amelishauri baraza hilo kubuni mikakati madhubuti ya kuielemisha jamii pamoja na kubuni mbinu mbali mbali kama vile kubuni nishati nyingine badala ya ile inayotokana na miti.

Baraza hilo halina budi kutilia mkazo mikoa mingine katika utaratibu mzima wa kuielemisha jamii kuhusiana na athari zinazotokana na uchafuzi wa mazingira badala ya kutazama Dar es Salaam tu. Alizitaka taasisi zote zinazohusika na utoaji vibali kwa wawekezaji kuwa makini, kwani wawekezaji wengine wanaweza kuchangia katika kuharibu mazingira yetu hasa wale wanaowekeza katika viwanda.

“Ili kuweza kufanikisha hilo bila ya kuwabughudhi wawekezaji, ni lazima tuwe na viwango vya kimataifa vya uhifadhi na usimamizi wa mazingira”, alisema.

Makamu wa rais alilionya baraza hilo jipya kuepukana na malumbano na idara ya kuhifadhi mazingira kama ilivyokuwa katika mabaraza yaliyopita.

1   ...   17   18   19   20   21   22   23   24   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət