Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə18/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   14   15   16   17   18   19   20   21   ...   25

askofi (-; ma-) епископ взаимные оскорбления

imamu (ma; -) имам rai (-) мнение, суждение;

mshikamano (mi-) солидарность точка зрения

kwa niaba ya от имени (кого-л.) itikadi (-) идеология;

-thubutu посметь, отваживаться мировоззрение

chombo cha habari средство -kemea ругать; порицать;

массовой информации (СМИ) кричать на кого-л.



madhehebu (мн.) учение; roho (-) 1) душа; жизнь

вероучение 2) дух, сознание



* * *

Урок 24. Somo la ishirini na nne

(marudio)
1. Переведите текст:

IMANI ZA USHIRIKINA ZISIKWAMISHE

MAENDELEO

Uchawi na ushirikina ni mambo yasiyoaminika katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia, kwa sababu hayana ushahidi wa kisayansi. Katika dunia ya leo kila jambo linapaswa kuthibitishwa na kuungwa mkono na ushahidi wa kitaalamu. Lakini jamii nyingi maskini, bado zimejikita katika imani za kichawi na ushirikina.

Na watu wenye imani hizo wako wengi, wasomi na wasiokuwa wasomi, wanaoishi mijini na vijijini, baadhi yao wakiwa hawafanyi jambo bila kupata ushauri unaotokana na uchawi wa kila aina.

Imani hizi, hasa zinapoelemea wasomi zinakuwa na athari kubwa katika maendeleo ya jamii. Katika nchi ya Tanzania, kwa mfano, yapo maeneo ambako maendeleo hakuna, huku watu wakiishi* kama ilivyokuwa zama za mawe. Kuna watu wazaliwa wa maeneo hayo ambao wamepata elimu nzuri na kazi zenye madaraka, lakini wanashindwa kuendeleza au kujenga kwao kwa kuogopa kulogwa, na hivyo kuacha sehemu hizo kubaki nyuma bila ya maendeleo yo yote.

Kwa mfano Sumbawanga, mojawapo ya wilaya za mkoa wa Rukwa ni sehemu inayosifika sana kwa mambo ya uchawi na ushirikina, na watu wengi wanahofu kwenda huko maana wanakijiji wilayani huko hawataki kuachana na tabia ya kuamini ushirikina, jambo ambalo husababisha kuwepo kwa ugomvi miongoni mwao na hata mauaji.

Lakini zipo sehemu katika Tanzania hii hii, ambako baada ya watu kufutilia mbali** imani za kishirikina, maendeleo makubwa yamepatikana kwa maana ya watu kuwa na elimu, kujenga nyumba bora za kisasa na kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo.

Ukweli ni kwamba iwapo watu wanataka maendeleo ni lazima watupilie mbali** imani za kishirikina, kwani bila hivyo watahofu kushiriki jambo lolote la maendeleo ya jamii.

Kwa sehemu kama mkoa wa Rukwa na kwingineko ambako imani hizo zimejikita inapaswa sasa wananchi waelemishwe kwamba uchawi na ushirikina ni mambo ya udhanifu na zenye kustahili kupigwa vita ili zisikwamishe maendeleo. Na viongozi wanastahili kuwa mstari wa mbele kutoa elimu hiyo kuwawezesha wananchi kuondokana na imani hizo.


Maelezo

* Местоимение huku “здесь” часто употребляется в роли союзного слова со значением “при этом, в то же время”. Как правило, последующий глагол оформляется показателем -ki-.
** Словосочетания -futilia mbali, -tupilia mbali в своей основе имеют глаголы -futa “стирать; вычеркивать” и -tupa “бросать, выбрасывать”. Двойная направительная форма и слово mbali “далеко” усиливают основное значение этих глаголов, придают особую категоричность действию, выражаемую таким образом. В данном контексте эти словосочетания можно перевести такими выражениями как “полностью отказаться, отмести напрочь, выбросить из головы” и т.п.

Можно привести и другие примеры образования подобных словосочетаний. Оформленные двойной направительной формой и сопровождаемые словом mbali, глаголы приобретают значение близкое к идиоматическому. Например, от глагола -acha “оставлять, покидать” – -achilia mbali “забыть напрочь, покинуть навеки, убрать с глаз долой”; -kataa “отказываться” – -katalia mbali “отказаться наотрез, отвергнуть категорически”; -potea “теряться” – -potelea mbali “сгинуть, исчезнуть навеки вечные”; -vunja “разбивать, ломать” – -vunjilia mbali “разбить вдребезги”. Перевод таких словосочетаний на русский язык зависит от контекста. Например, то же выражение -futilia mbali может переводиться как “аннулировать; ликвидировать на корню; стереть с лица земли.”


Mazoezi

2. Дайте русские эквиваленты:

-fanya uchawi; -athirika na uchawi; -wa chini ya ushawishi wa mchawi; -kosa ushahidi wa kisayansi; -pata ushahidi wa kutosha; -jikita katika imani za ushirikina; -ungwa mkono na wasomi wengi; -kataliwa mbali na wataalamu; -ishi kama zama za mawe; kazi zenye madaraka; -logwa mpaka kufa; -logwa kipumbavu; -sifiwa na mambo ya uchawi; -achana na tabia ya kuamini ushirikina; -futilia mbali imani za ushirikina; -shiriki shughuli za maendeleo; -elemea kama mzigo mzito; -kemea imani zenye kukwamisha maendeleo; mambo ya udhanifu mtupu; -stahili kupigwa vita; -wa mstari wa mbele.


3. Ответьте на вопросы:

1. Kwa nini uchawi na ushirikina hayaaminiki sana siku hizi? 2. Ni jamii za aina gani hasa zinazojikita katika imani za ushirikina na kwa sababu gani? 3. Je, watu wote hupendelea kupata ushauri kutoka kwa wachawi? 4. Kuna ubaya gani katika mambo ya uchawi na ushirikina? 5. Je, Tanzania kote kunafuatwa imani kama hizo? 6. Ni lazima hatua zipi zichukuliwe ili kuwafanya watu waondokane na imani za ushirikina na ulozi?


4. Переведите:

  • В Танзании не все дети, достигшие школьного возраста, имеют возможность учиться, потому что плата за обучение, устанавливаемая в некоторых школах, зачастую не по карману их родителям. Это касается не только начальных школ, но и средних, как частных, так и государственных. Порядок, обязывающий родителей платить за учебу их детей, не согласуется с главной стратегией государства, направленной на то, чтобы каждый ребенок, достигший школьного возраста, ходил в школу. Поэтому следует хорошо продумать такой порядок, чтобы учесть возможности бедного населения. Платное обучение в школах нельзя отменить совсем, так как деньги нужны на развитие системы образования. Но должны также соблюдаться интересы тех, чьи родители не в состоянии заплатить деньги.

  • Крупный медицинский центр был торжественно открыт вчера на востоке столицы. В этом центре будут лечить людей с заболеваниями сердечно-сосудистой системы, а также будет проводиться большая научно-исследовательская работа. Министр здравоохранения, выступая на открытии этого центра, сказал, что подобные медицинские учреждения будут создаваться в различных районах города. Например, в будущем году планируется открыть роддом в одном из новых районов, где наблюдается острая нехватка медицинских учреждений, в том числе и аптек. Министр обратил внимание всех медицинских работников на важность проведения профилактических мер, особенно в этот зимний сезон, когда сильно возрос уровень заболеваемости гриппом.

  • Вакцинация от желтой лихорадки уже не является обязательной для туристов, въезжающих в Танзанию. Для Африки типична малярия, однако ее можно предотвратить, используя средства против насекомых. Также рекомендуется после захода солнца надевать одежду с длинными рукавами, а ночью спать под москитной сеткой. Пить следует только кипяченую воду или бутилированную. От кубиков льда и овощных салатов лучше отказаться совсем.



5. Переведите следующий текст письменно:

Viongozi wa dini watoa mwito kuelewana

Viongozi wa dini nchini Tanzania wametoa mwito kwa serikali na viongozi wa vyama vya siasa na Watanzania wote kumaliza tofauti zilizojitokeza kati yao kwa amani na utulivu. Katika tamko la viongozi hao kuhusu hali ya kisiasa nchini walilotoa juzi mara baada ya kukutana mjini Dar es Salaam, wamesema katika shughuli za kisiasa hekima, busara, haki za binadamu na sheria za nchi vizingatiwe, viheshimiwe na kupewa umuhimu.

Tamko kamili lililotiwa saini na viongozi hao linasema: “Sisi viongozi wa dini kutoka Jumuiya ya Kikristo Tanzania, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania tuliokutana leo kuzungumzia hali ya kisiasa ilivyo nchini hivi sasa, tunapenda kutoa rai yetu kwa viongozi wa serikali na vyama vya siasa kuhusu hali hii. Tumesikitishwa na vifo vilivyotokea huko Unguja na Pemba na majeruhi walioumizwa Unguja, Pemba na Dar es Salaam kufuatia maandamano yaliyofanyika na vyama vya upinzani mnamo Januari.

Kutokana na hali hii sifa ya nchi yetu ya kujulikana kama kisiwa cha amani duniani imeingia doa na kwamba hali hii isipodhibitiwa itapelekea kuvunjika kwa amani na utulivu, jambo ambalo hakuna Mtanzania anayelitamani. Hapana budi kutambua kuwa gharama ya kuirudisha amani ikishapotea ni kubwa mno isiyoweza kulipika.

Ikumbukwe kuwa nchi hii ni yetu sisi sote yaani raia, serikali, viongozi wa dini na viongozi wa vyama vya siasa. Hivyo ni jukumu letu kuilinda kwa maslahi ya umma wote wa Watanzania kwa sababu amani na utulivu vitakapotoweka sisi sote tutaathirika na kulaumiwa.

Aidha tunatoa rai kwa serikali na viongozi wa vyama vya siasa kutumia njia ya kukaa na kufanya mazungumzo kwa pamoja mara kwa mara kwa lengo la kumaliza tofauti zao.”


6. Переведите:

1. Древние люди добывали себе все необходимое в лесах, где росло много фруктов, растений и кореньев, включая и те, из которых получали лекарства. 2. Древесина использовалась для изготовления разнообразных изделий, в том числе орудий для охоты, рыбной ловли и земледелия. 3. Племена банту селились по берегам рек и озер, в том числе и вокруг таких, как Виктория, Танганьика и Ньяса. 4. Различия между племенами, проживающими в Восточной Африке, заметны во многом, в том числе и в их традициях строить себе жилища. 5. Много рек Танзании несут свои воды в Индийский океан, в том числе и река Руфиджи, известная своим быстрым течением. 6. В медицинских учреждениях ОРТ работает много местных специалистов, включая и тех, кто получил высшее образование в России.


7. Перескажите на суахили следующий текст:

Serikali ya Marekani itawafadhili wanafunzi 50 wa kike watakaojiunga na masomo ya elimu ya juu katika vyuo mbalimbali nchini Tanzania katika mwaka huu wa masomo. Hatua hiyo inafuatia juhudi za mikakati mbalimbali iliyofanywa na serikali katika kuinua kiwango cha elimu kwa wanawake nchini.

Kulingana na ofisa anayeshughulikia masuala ya uhusiano wa ubalozi wa Marekani, wanafunzi hao watalipiwa gharama za masomo yao na nchi yake kwa kipindi chote cha masomo yao.

Alisema ufadhili huo utatolewa kwa miaka mitatu mfululizo ambapo jumla ya wanafunzi 150 watabahatika kupata ufadhili wa kusoma kwa kozi mbalimbali watakazojiunga katika vyuo vya elimu ya juu. Alisema dola za Marekani milioni moja zitatumika kugharimia mafunzo hayo.

Alisema wanafunzi watakaofadhiliwa ni wa kutoka vyuo mbalimbali vya elimu ya juu wanaochukua kazi za shahada ya kwanza. Hatua hiyo itapunguza kwa kiwango kikubwa pengo la elimu kati ya wanafunzi wa kiume na wa kike katika vyuo vya elimu ya juu nchini ikiwa ni pamoja na kumwendeleza mwanamke katika karne ya sayansi na teknolojia.

Hatua ya serikali ya Marekani imekuja wakati wa kufaa sana huku ikizingatiwa kwamba kuna mpango maalumu unaoendeshwa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wa kutoa upendeleo kwa wanafunzi wa kike. Hii ni sehemu ya mikakati ya kupunguza pengo kati ya wanafunzi wa kike na wa kiume wanaojiunga na masomo ya elimu ya juu.

Chini ya mpango huo wanafunzi wapatao 400 wamenufaika tokea uanzishwe miaka minane iliyopita. Hivi sasa mpango huo ni moja ya utaratibu unaotumika katika hatua za kujiunga na masomo ya elimu ya juu ambapo wanafunzi hutakiwa kuhudhuria masomo ya awali kabla ya kufanya mitihani ya mchujo.
8. Дайте аргументированные ответы на следующие вопросы:


  1. Je, wanawake wanastahili kupewa usawa katika mikakati ya kueneza elimu kati ya wananchi?

  2. Hali ilivyo nchini Urusi inatuwezesha kudai kwamba ubaguzi hakuna kamwe baina ya wanawake na wanaume ?


9. Переведите и подберите синонимы к подчеркнутым словам:

-ponya maradhi; -ambatana na masharti; -dadisi; mganga; mwuguzi; mpiga mbio; -onyesha busara; -fariki dunia; -peleka habari; -tarajia kupata kitu; ni dhahiri; aidha; kima cha elimu; -andaa mkakati; -toa rai; azma; -jikaza kiume; wadhifa wa juu; -pasisha waraka muhimu; kwa mabavu; -sababisha vurugu; -salia peke yako; -pewa maelekezo; -leta hali ya utulivu; -zingatia sera ya serikali; -farakana kiadui; maelewano kamili; uchumi wa kuzorota; -kemea itikadi ya ubepari; msomi; -achana na tabia; -jikita katika imani; -shawishika na mawazo ya udhanifu; mfululizo wa mitihani; -maliza kozi ya fasihi ya Afrika.
10. Переведите:

1. Этот врач хорошо знает нетрадиционные методы лечения. 2. Он вылечил больного, ужаленного скорпионом. 3. Важнее предотвратить болезнь, чем лечить ее. 4. Эта вакцина старая, ей нельзя пользоваться. 5. Основные нормы санитарии здесь строго соблюдаются. 6. Гость приехал в сопровождении охраны. 7. Он очень любопытен, любит все выведывать. 8. Медицинским работникам прибавили зарплату. 9. Мне дали мудрый совет. 10. Он сделал этот шаг преднамеренно. 11. Дискриминации достигла апогея. 12. Я получил эту должность недавно. 13. Хочу быть полезным своей партии. 14. В этом вопросе следует проявить благоразумие. 15. Главнокомандующий выступил с длинной речью. 16. Это не соответствует вашему положению в обществе. 17. Сравним два этих предложения. 18. Был установлен максимальный уровень взноса. 19. Необходимо ускорить развитие этой области науки. 20. Невозможно изменить эту систему. 21. Такой общественный строй не может существовать долго. 22. Администратор вызвал к себе главного бухгалтера и дал ему указания. 23. Было крайне трудно сдать этот экзамен. 24. Встреча состоится одновременно с лекцией. 25. Они разошлись во взглядах, и между ними начались ссоры и взаимные оскорбления. 26. Ему следует поменять свою тактику, которая отстает от стратегии. 27. Как ты посмел опозорить этого человека? 28. Политическая ситуация начала ухудшаться. 29. Прошу тебя, не кричи на меня и не вмешивайся в мои дела. 30. Сегодня сам епископ будет выступать с проповедью перед верующими. 31. Раскол в их организации обнаружился очень скоро.


11. Переведите сказку и перескажите ее в лицах:

Sababu ya gamba la kobe kuwa na nyufa

Kobe alikuwa ameoa bibi kobe, wakakaa pamoja kwa upendano siku nyingi. Baada ya miezi kupita, akaja mwewe akafanya urafiki na kobe, akazoea kuja kuongea naye kila mara. Lakini kobe aliona uchungu kwa sababu hakuweza kwenda anapokaa mwewe akaongee naye huko, maana hana mabawa ya kumwezesha aruke juu mpaka kitundu cha mwewe.

Siku moja alikaa akifikiri sana mpaka akapata akili, akamwita bibi yake akamwambia: “Mke wangu, huoni kuwa rafiki yetu mwewe ataanza kutuchukia siku hizi?” Mke wake akamwuliza, “Kwa nini?” Akajibu, “Kila siku huja kwetu kuongea, lakini mimi siwezi kuruka juu, na kwa hivi sijapata kumfikia kwake anapokaa.” Mke wake akamwambia, “Basi, kwa nini huoteshi mabawa upate kuruka juu mpaka kwake?” Kobe akajibu, “Wewe mpuuzi sana, nitawezaje kuotesha mabawa nami nilizaliwa hali hii niliyo nayo sasa?” Basi, bibi akamwuliza, “Utafanya nini basi upate kufika kwake?” Akajibu, “Nyamaza tu, mimi nitapata njia.”

Basi, baada ya muda kupita akamwita mke wake, akamwambia, “Mke wangu, njoo unifunge kama kwamba ni furushi la tumbako, na afikapo mwewe umwambie ya kuwa ni tumbako tu, nataka uichukue ili ukatununulie chakula.” Basi, bibi kobe alikwenda akatwaa makuti akamfunga kobe ndani, akamfunga humo kama kwamba ni furushi la tumbako. Akamweka upande akamwacha huko.

Baadaye mwewe akaja, akamwona bibi kobe, akamwuliza, “Jambo bibi, mumeo amekwenda wapi?” Bibi kobe akajibu, “Sijambo bwana, mume wangu amekwenda mbali kutazama ndugu zake. Harudi kwa siku nyingi, nami hapa nina njaa sana. Hakuniachia hata punje moja ya mtama.” Mwewe akajibu, “Pole bibi, nimesikitika kusikia habari zako, labda hakawii sana huko alikokwenda.” Yule bibi kobe akajibu, “Najua harudi upesi nami nitakufa kwa njaa. Je, bwana mwewe, huko unakokaa wewe hakuna watu wenye chakula?” Mwewe akajibu, “Wako watu wengi wenye chakula, lakini cha kuuza tu.”

Basi, hapo bibi kobe alikwenda pembeni akalileta lile furushi, akamwonyesha mwewe, akasema, “Mume wangu alipoondoka aliniachia furushi hili la tumbako, akaniambia ‘Akija bwana mwewe labda atalichukua furushi hili la tumbako akununulie chakula, ule usife kwa njaa’.” Basi, mwewe akakubali, na pale pale akalishika lile furushi kwa makucha yake, akaruka nalo juu sana. Alipokuwa akikaribia kitundu chake juu mlimani, mara alisikia sauti ikimwambia, “Nifungulie bwana, ni mimi rafiki yako kobe. Nilikuambia ya kuwa siku moja nitakuja kuongea nawe kwako.”

Lakini mwewe alishtuka mno kusikia sauti inatoka katika lile furushi, na mara ile makucha yake yalifumbuka. Maskini kobe alianguka chini kwa kishindo puu!

Basi hivyo urafiki wao ulivunjika, na tokea siku ile kobe alikuwa na nyufa katika gamba lake, na wote waliozaliwa tokea siku ile wanazo nyufa vile vile. Kama hamsadiki hadithi hii, basi, mwonapo kobe tena, mchungulie gamba lake, mtaona nyufa alizozirithi.


12. Познакомьтесь с некоторыми звукоподражательными словами (идеофонами), встречающимися в языке суахили, т.е. словами, помогающими выразить характеристику действия через восприятие его звука, образа, цвета и т.п. Чаще всего такие слова употребляются с глаголами:
-cheka kwe-kwe-kwe (kwa-kwa-kwa) громко хохотать

-bweka bwe-bwe-bwe громко лаять

-lia kwi-kwi-kwi плакать навзрыд

-chemka chem chem бить ключом

-didimia di-di-di исчезнуть совсем

-dunda du-du-du сильно биться, пульсировать

-anguka tifu упасть в песок

anguka puu (buu) упасть на жесткое

-anguka pwaa упасть в грязь

-anguka chubwi упасть в воду

-fyeka fye выкорчевывать с корнем

-kataa kata kata отказываться наотрез

-lala fo-fo-fo спать, как убитый

-katika ka-ka-ka надломиться с треском

-eupe pe-pe-pe белый-белый

-eusi ti-ti-ti черный-пречерный
13. Сделайте сообщения на суахили по темам:

А/ Проблемы здоровья в современном мире;

В/ Реформа образования в РФ.
Msamiati

uchawi (ед.) колдовство; магия -fadhili 1) делать добро

mchawi (wa-) колдун; знахарь 2) покровительствовать

ushahidi (ед.) свидетельство, -elemea 1) давить

доказательство 2) полагаться,



kozi (; ma-) курс (дисциплина) доверяться (перен.)

mfululizo (mi-) 1) непрерывность -kita стоять прочно;

2) последовательность опираться на что-л.



mfululizo подряд, без перерыва -tamani 1) страстно желать

msomi (wa-) 1) образованный 2) стремиться, устремляться

человек 2) интеллигент 3) ученый bawa (ma-) крыло



-loga 1) околдовывать 2) очаровывать utulivu (ед.) спокойствие;

3) дурманить; дурачить мир



mlozi (wa-) колдун, маг, mpuuzi (wa-) глупец; болван

волшебник punje (-) зерно, зернышко



udhanifu (ед.) предположение, mwewe (-) коршун

допущение kitundu (vi-) гнездо



maandamano (мн.) процессия, gamba (ma-) панцирь; чешуя

шествие; демонстрация



* * *

VII. SIKUKUU, UTALII NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

Праздники, туризм, проблемы экологии

Урок 25. Somo la ishirini na tano
Грамматика

Аналитические глагольные конструкции -me- + -ki-.


Аналитическая глагольная конструкция, где вспомогательный глагол -wa оформляется показателем -me-, а смысловой глагол показателем -ki-, довольно часто встречается в суахили. Как и в других вариантах сочетания показателей в сложных глагольных формах, общее значение конструкции складывается из значений каждого из компонентов: показатель -me- передает завершенность действия и сохранение его результата на момент речи, -ki- выражает повторяемость, длительность действия. В целом это может означать начало продолжительного регулярного действия в определенный момент речи. На русский язык такие конструкции следует переводить глаголом настоящего времени, либо с помощью дополнительных глаголов начать, “стать” и т.п. в зависимости от контекста:

Sikukuu hii imekuwa ikisherehekewa kila mwaka tangu 1964 “Этот памятный день отмечают ежегодно с 1964 года”;

Wenyeji wamekuwa wakiifuata desturi hii kwa kuwakumbuka mababu zao “Жители стали следовать этой традиции в память о своих предках”.

Обратите внимание на то, что отрицание в таких конструкциях стоит в смысловом глаголе настоящего времени:

…imekuwa haisherehekewi “перестал отмечаться”;

…wamekuwa hawafuati “не стали следовать”.



Mazoezi

1. Переведите предложения и проанализируйте употребление аналитических глагольных форм:

1. Kwa muda wa miaka mingi nimekuwa nikitamani sana kuuona mlima Kilimanjaro. 2. Goja akaitikia kwa kuinamisha kichwa akasema, “Kifo hiki kimekuwa kikitazamiwa kwa muda mrefu”. 3. Mama yake akauliza, “Sijui mtoto wetu ametuletea ndege au nyama gani ili kunisaidia kuwalisha wanaume wawili?” Tegu akamjibu, “Nimekuwa nikifanya mazoezi tu, mama”. 4. Akina baba wengine wamekuwa wakichukua watoto wao porini kuwinda siku zile. 5. Mpaka sasa fedha nyingi zimekuwa zikitumika katika kujenga mahospitali na kuponyesha watu. 6. Tutamchinja yule mbuzi ambaye mama amekuwa akimlisha kwa miaka miwili iliyopita. 7. Kila asubuhi amekuwa akifika kazini kwani anataka kutengeneza vitabu vyote vya ofisi. 8. Amekuwa akitembelea mji wa Nairobi mara mbili au tatu hivi kila siku. 9. Amekuwa akizurura zurura ovyo mjini na mara nyingi alichelewa matembezini bila kufika nyumbani kwake mpaka saa nane au tisa usiku. 10. Baada ya kupita muda kidogo amekuwa haitunzi kazi yake vizuri wala kujiwekea akiba yoyote.



2. Переведите предложения, используя аналитические глагольные конструкции с показателями -me- + -ki-:

1. Последние годы мои родители стали интересоваться политикой и ежедневно читают газеты. 2. Этот день стал отмечаться как общенародный праздник только с прошлого года. 3. Вопросы защиты окружающей среды от хозяйственной деятельности человека волнуют ученых уже давно. 4. В наши дни люди начали бороться за свои права, используя все возможные методы, включая и политические. 5. Стада обезьян стали совершать набеги на кукурузные поля и вредить крестьянам. 6. Он не ходит больше к врачу с тех пор, как его вылечили с помощью нетрадиционной медицины. 7. Теперь каждый год мы сажаем новые деревья и кустарники у нашей школы. 8. По выходным дням отец стал ходить на футбол и брать сына с собой.

1   ...   14   15   16   17   18   19   20   21   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət