Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə16/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   12   13   14   15   16   17   18   19   ...   25

Maelezo

*…akiwa yungali hai можно перевести как “…еще при жизни…” (буквально: “…будучи еще живым”). Это аналитическая глагольная форма, где -ki- во вспомогательном глаголе -wa показывает, что действие происходит одновременно с другим, основным действием в предложении (aliambatana). Место смыслового глагола в этой конструкции занимает недостаточный глагол -ngali со значением “еще/ все еще/ пока”. Форма yungali может иметь свой вариант angali (но только для 3-го лица ед. числа). Другие примеры:

Mtoto huyu afundishwe lugha yake ya jadi akiwa yungali mdogo “Этого ребенка следует обучать родному языку, пока он еще маленький”;

Afadhali ukile chakula hiki kikiwa kingali moto “Лучше съешь эту еду, пока она еще горячая”.
** В языке суахили нет самостоятельных глаголов со значением “находиться”, “пребывать”, “иметься”, их роль выполняет глагол -wa с локативными формантами. В тексте встретилась инфинитивная форма такой конструкции – kuwapo, выступающая в функции существительного со значением “нахождение”, “пребывание”, “наличие”, “присутствие”. Другие примеры:

Kuwapo kwake mkutanoni kuliwashangaza watu wengi “Его присутствие на собрании удивило многих”;

Waziri alisisitiza kuwako kwa matatizo makubwa “Министр подчеркнул наличие серьезных проблем”.

Противоположное значение (ненахождение, отсутствие) передается с помощью отрицательного инфикса инфинитива -to-: kutokuwapo/kutokuwako/kutokuwamo:

Kutokuwako kwa njia nzuri kulisababisha balaa kubwa “Отсутствие хороших дорог вызвало большую беду”.
Mazoezi

3. Дайте русские эквиваленты:

walishambuliwa na magonjwa; dawa za miti shamba; -punguza maumivu; -ponya maradhi; kazi iliyorithiwa; baba aliambatana na mtoto wake; wangependa kudadisi kama ni kweli; juhudi kubwa ilifanywa; walisitawisha mambo ya utibabu wa kisasa; watumishi wa hospitali; ilitambulikana; mipango ya kuweka kinga kwa magonjwa; idara ya utibabu; upanuaji wa kazi; hali ya usafi na kanuni za afya; kazi za kuondoa uchafu; kazi za dawa zilipunguzwa; kutokula chakula cha kutosha; hospitali mbali kwa Wazungu; -panua shule za kufundishia waganga; -pewa ujuzi na madaraka; kila daraja la wauguzi; kwa upande wa kuzuia magonjwa; vyumba vya kulaza wagonjwa; vyumba vya kuzalishia; -pata vyeo vya madaraka makubwa.


4. Дайте эквиваленты на суахили:

использовать средства народной медицины; излечивать опасные болезни; облегчить невыносимую боль; находиться в сопровождении коллег; средство от головной боли; выведывать чьи-либо секреты; делать огромные усилия; методы современной медицины; обучать медперсонал больницы; ставить заслон на пути болезням; применять вакцину; задачи, стоящие перед департаментом; проверять санитарные условия; соблюдать нормы защиты здоровья; работы по борьбе с загрязнением; фармацевтическая промышленность; проблемы недоедания среди бедного населения; полноценное питание; удовлетворять потребности в лекарствах; приобретать оборудование для больниц; учиться на врача; врачи всех категорий; профилактика болезней; покончить с расовой дискриминацией; получить ответственный пост; тесно сотрудничать; объявить войну болезням; приносить пользу народу.


5. Переведите и перескажите следующие тексты:

Hospitali ya Ocean Road

Hospitali maarufu sana iliyopo jijini Dar es Salaam katika barabara ijulikanayo kwa jina la Ocean Road, imetimiza miaka 100. Hospitali hii kwa sasa inahudumia wagonjwa wa kansa.

Sherehe za maadhimisho hayo zilifanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa utamaduni wa Ujerumani ambapo ilihudhuriwa na waziri wa afya.

Hospitali ya Ocean Road imegeuzwa kuwa hospitali ya kuhudumia wagonjwa wa kansa tangu mwaka 1987. Kabla ya hapo hospitali hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kuhudumia majeruhi wa kivita wakati wa ukoloni.

Baada ya Tanzania kupata uhuru, hospitali hiyo iligeuzwa kuwa ya serikali ambapo ilianza kutoa huduma za uzazi zilizohamishwa kutoka hospitali ya Muhimbili.
Chanjo ya homa ya manjano haina haja tena

Wizara ya afya ya Tanzania imefuta sharti la kuonyesha cheti cha chanjo dhidi ya ugonjwa wa homa ya manjano kwa wasafiri wanaoingia nchini.

Hapo kabla kumekuwako na utaratibu wa kuhakikisha kuwa kila mgeni anayeingia nchini awe amepata chanjo dhidi ya ugonjwa wa homa ya manjano, utaratibu uliokuwa unawahusu hata wageni wanaotoka katika nchi jirani za Kenya na Uganda.

Wizara ya afya imefanya uamuzi wa kuondoa sharti la kuwa na cheti cha chanjo dhidi ya ugonjwa huo kwa wasafiri wote wanaoingia nchini kwa kupitia katika viwanja vya ndege na vituo vya mipakani.

Hata hivyo taarifa ya wizara hiyo imewashauri wasafiri wote kuendelea kupata chanjo hiyo hasa wale ambao watakuwa wanasafiri kwenda au kupita katika nchi zenye ugonjwa wa homa ya manjano kama za Afrika ya Kati, Afrika ya Magharibi na Amerika ya Kusini.
6. Переведите, используя аналитическиее формы в подчеркнутых глаголах:

1. Пребывая в состоянии гнева, начальник уволил своего лучшего сотрудника. 2. Вдалеке я увидела свою подругу, ехавшую на велосипеде. 3. Путешествуя по Танзании, мы видели множество обезьян, пересекающих дорогу со своими детенышами на спине. 4. Войдя в спортивный зал, я увидел своих сокурсников, играющих в баскетбол. 5. Композитор сочинил свою самую популярную песню, будучи еще совсем молодым. 6. Будучи все еще маленьким ребенком, он каждый раз начинал плакать, когда его мама уходила на работу. 7. Они плохо разбирались в этом деле, которое было все еще новым для них. 8. Чувствуя себя все еще больным, он отказался поехать в командировку.


7. Закончите предложения:

1. Ningalikuwa baharia katika meli kubwa … 2. Ningalikuwa waziri wa sheria wa nchi hii … 3. Ningalikuwa inspekta mkuu wa polisi … 4. Laiti ningelikuwa simba katika hifadhi ya wanyama … 5. Kama ningalikuwa mfanya biashara tajiri sana … 6. Ningalikuwa na paka 20 nyumbani mwangu … 7. Kama ningalikuwa na ndege kubwa ya kibinafsi … 8. Ningalikuwa sultani mwenye watumishi wengi … 9. Kama ningalikuwa na watoto kumi … 10. Laiti ningaliishi katika enzi ya wafalme wa Urusi …


8. Сделайте письменный перевод следующих текстов:

Ukimwi

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi Dakta Peter Piot amesema kuwa, Umoja wa Mataifa umeamua kuwa, kuanzia sasa fedha za kutosha zitatengwa kwa ajili ya kupambana na kuenea kwa virusi vya ukimwi katika Bara la Afrika.

Dakta Piot ameyasema hayo, wakati akiwahutubia wanachama wa chama kisichokuwa cha kiserikali cha walio katika mapambano na ukimwi nchini, alipotembelea ofisi ya huduma ya chama hicho jijini Dar es Salaam. Amesema, pamoja na uhakika huo uliotolewa na Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake, bado kuna haja kubwa kwa kila taifa kuchukua hatua za makusudi katika kuhakikisha kuwa ukimwi unapigwa vita na kila mwananchi pale alipo.

Pia amesema ni jambo la kutia moyo kuona kuwa, kasi ya maambukizo ya virusi vya ukimwi, na ukimwi mkoani Mbeya, imepungua katika miaka mitano iliyopita, wakati ambapo Botswana inaongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi wa ukimwi duniani, ikifuatiwa na Afrika Kusini na Zimbabwe wakati dunia nzima ina mamilioni ya wagonjwa wa ukimwi hivi sasa.

Naye mwenyekiti wa chama hicho Profesa Kanywanyi amesema, inawezekana kujikinga kuambukizwa virusi vya ukimwi kwa kutoa elimu, ushauri pamoja na kuimarisha mawasiliano dhidi ya ukimwi na virusi vyake, kwa kupashana habari katika jamii kuhusu ugonjwa huo wa hatari.
Ugonjwa wa malaria

Imeelezwa kuwa watu karibu elfu tatu na nusu wamefariki dunia kutokana na kuugua ugonjwa hatari wa malaria wilayani Tunduru mkoani Ruvuma kwa miezi sita ya mwanzo ya mwaka huu.

Mganga mkuu wa wilaya ya Tunduru Dakta Ngoli amesema kipindi hicho jumla ya wagonjwa laki moja na 50 elfu walilazwa katika zahanati na hospitali ya wilaya hiyo ambapo kati ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano walikuwa 65 elfu, na elfu mbili na mia sita kati yao walifariki dunia.

Kufuatana na hali hiyo Dakta Ngoli aliwaita wakazi wa wilaya hiyo kutumia vyandarua vilivyotiwa dawa ya mbu pamoja na kupata ushauri wa kitaalam pindi wanapojisikia kuwa na dalili za malaria.


9. Переведите:

  1. Медицина существовала с древних пор, когда еще наши предки могли лечить разные болезни с помощью лекарственных растений.

  2. Специалисты современной медицины пытаются проверить, правда ли то, что некоторые рецепты древности исцеляли тяжелобольных.

  3. Министерство здравоохранения поставило себе задачу провести работу по профилактике заболеваний и предотвращению опасных инфекций.

  4. Ответственные посты в министерстве заняли специалисты высокого класса из числа местных жителей, в том числе и те, кто получил образование заграницей.

  5. Нехватка финансовых средств явилась основной причиной, которая препятствовала расширению работ по борьбе с загрязнением окружающей среды.

  6. Санитарные условия в пунктах по раздаче лекарств среди населения были на очень низком уровне. Директор отделения министерства здравоохранения этого района выступил с резкой критикой в адрес некоторых руководителей, отвечающих за соблюдение всех норм санитарии.

  7. Этот госпиталь обслуживает раненых, которые пострадали в борьбе за независимость и против расовой дискриминации.

  8. Национальное здравоохранение не смогло бы развиваться успешно без вовлечения самих африканцев в дело подготовки медицинских работников, в том числе высококвалифицированных врачей, ассистентов врачей и медсестер.

  9. В этой больнице есть много отделений, включая палаты для стационарных больных, родильное отделение, отделение по уходу за новорожденными. Кроме того, есть учебный центр по вопросам санитарии.

  10. Дальнейшие планы правительства зависели от наличия денег и специалистов, которые считали бы своим долгом служить на благо народа.


10. Переведите письменно следующий текст:

Marathon

Ni busara tuangalie matukio machache ya vifo vya ghafla ambayo yamewahi kutokea duniani, na kuandikwa katika vitabu maarufu vya historia, ili yawe kumbukumbu na funzo kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Tukio la kwanza lilitokea mwaka 490 B.C. (kabla ya kuzaliwa Kristo) ambapo mpiga mbio hodari wa Ugiriki aliyeitwa Pheidippides, alifariki ghafla baada ya kukimbia kutoka mji wa Marathon hadi mji mkuu wa nchi hiyo, Athens, kupeleka habari kwamba jeshi la nchi hiyo lilikuwa limepata ushindi mkubwa vitani dhidi ya Waajemi.

Historia inaonyesha kuwa ushindi huo ambao haukuwa umetarajiwa sana na Wagiriki kutokana na maadui wao kuwa dola yenye nguvu wakati huo, ulikuwa wa kufurahisha mno kwa upande wa Wagiriki na ndipo jemadari wao, Militiades, aliona asingeweza kulala bila habari hizo kufikishwa nyumbani haraka.

Katika mapambano hayo, jeshi la Waajemi lilikuwa likiongozwa na jemadari mkuu Darius ambaye alikuwa na historia ya umaarufu katika himaya ya Uajemi, na kwa maana hiyo haikutegemewa angeweza kushindwa katika vita hivyo.

Ingawa idadi ya majeruhi upande wa Waajemi haikutolewa, lakini inaelezewa kuwa jumla ya wapiganaji 192 wa Ugiriki waliuawa.

Hivyo, akiwa amepewa agizo kupeleka taarifa hizo muhimu, Pheidippedes alikimbia bila kusimama popote kutoka Marathon yapata maili 26 na yadi 385 (kilometa 42), hadi Athens ambapo anakaririwa kuwaambia viongozi wa Ugiriki kwamba “Furahini, Furahini, tumeshinda vita”.

Baada ya hapo alianguka chini na kufa papo hapo. Inaaminika kwamba huenda mjumbe huyo alifariki kutokana na baadhi ya sehemu za moyo wake au mishipa ya damu kushindwa kufanya kazi sawa sawa.

Ingawa hakuna kumbukumbu zozote zinazoonyesha sababu za kiafya zilizosababisha kifo cha mpiga mbio huyo (na hasa kwa vile uchunguzi wa kitiba wakati huo ulikuwa duni) ni dhahiri kuwa Pheidippedes alifariki kutokana na uchovu.

Aidha, kutokana na tukio hilo la kusikitisha, kwa heshima yake dola ya Ugiriki ilipendekeza kuanzishwa “mbio za Marathon” na kuwa moja ya michezo maarufu ya riadha ambao hushindaniwa na wakimbiaji mbalimbali duniani.

Mbio hizo zilishindaniwa kwa mara ya kwanza katika michezo ya kwanza ya Olimpiki ambayo ilifanyika mjini Athens mwaka 1896, na zimekuwemo katika Olimpiki zote zilizofuatia hadi wakati huu.
11. Перескажите текст “Marathon”, используя следующие выражения:

ni busara; kifo cha ghafla; mpiga mbio hodari; -peleka habari; -pata ushindi mkubwa; -tarajia ushindi; dola yenye nguvu; historia ya umaarufu; -pewa agizo; -fa papo hapo; sababu za kiafya; uchunguzi wa kitiba; ni dhahiri; kwa heshima yake; michezo ya riadha.


Msamiati

uganga (ед.) 1) медицина; -changa 1) молодой, юный

врачевание 2) магия; колдовство 2) недозрелый, недоспелый



mti shamba (mi-) лекарственное riadha (-) физкультура;

растение легкая атлетика



-ponya, -ponyesha исцелять, -nufaisha быть полезным,

вылечивать приносить пользу (выгоду)



cheo (vy-) 1) пост, должность tandu (-) многоножка

2) чин, ранг; положение в обществе nge, nge скорпион



ubaguzi (ед.) 1) дискриминация chandarua (vy-) москитная

2) расизм сетка



-bagua дискриминировать, wajibu (ед.) долг,

сигригировать обязанность



-dadisi 1) разузнавать, расспрашивать kansa (-) рак (болезнь)

2) любопытствовать homa ya manjano желтая



mdadisi (wa-) любопытный, лихорадка

любознательный человек usafi (ед.) 1) чистота



jemadari (ma-) командующий 2) санитария

-kinga 1) оберегать, предохранять mfereji wa maji водопровод

2) предотвращать (заболевание) mawasiliano (мн.) 1) связь,



-weka kinga (-) обеспечивать сообщение 2) общение

защиту; ставить заслон -fariki dunia умирать



dawa ya kinga вакцина mkurugenzi (wa-) директор

kanuni (-) правило, норма; kirusi (vi-) вирус

принцип dola (-; ma-) государство;



kumbukumbu (-) 1) память держава

2) воспоминание; хроника -ambatana сопровождаться



* * *

Урок 22. Somo la ishirini na mbili
Грамматика

Вспомогательные глаголы -isha, -pata, -wahi.


Помимо глагола -wa “быть”, в языке суахили есть ряд других слов, выступающих в роли вспомогательных глаголов, которые, примыкая к смысловому глаголу, теряют свое лексическое значение. Глагол -isha “кончать” передает значение завершенности, законченности действия. Обычно конструкции с этим глаголом переводятся на русский язык соответствующим глаголом с частицей “уже”. Часто глагол -isha употребляется в своей усеченной форме -sha- и сливается с основным глаголом: amekwisha kuisoma > amekwisha isoma > ameshaisoma.

Усеченная форма -sha- может употребляться в глаголе не только с показателем перфектности -me-, но и с показателем прошедшего времени -li-, сравните: Maduka yote mjini yameshafungwa “Все магазины в городе уже закрыты” (на данный момент) и Maduka yote mjini yalishafungwa “Все магазины в городе были уже закрыты” (контекст прошедшего времени).

Форма -sha- сочетается и с показателем условного наклонения -ki-, передавая значение, которое на русский язык можно перевести деепричастием совершенного вида, либо глаголом совершенного вида в условном придаточном предложениии: Ukishaamua kujiunga nasi fanya haraka kuyakamilisha mambo yako “Раз уж ты решил присоединиться к нам, поторопись закончить все свои дела”.

Глагол -pata “получать” также выполняет функцию вспомогательного глагола в модальных конструкциях со значением успешного осуществления действия, выраженного основным глаголом. На русский язык переводится как “удаваться”, “смочь”, либо просто глаголом совершенного вида:

Alipata kujua hayo “Ему удалось это узнать”; Tumepata kuupanda mlima huo “Мы смогли взобраться на эту гору”; Mgonjwa amepata kutibiwa maradhi ya hatari “Больного вылечили от опасного заболевания”.

Глагол -wahi “успевать” тоже может выполнять роль вспомогательного глагола, передавая такие значения как “доводиться”, “случаться”, “приходиться”:

Waliwahi kuliona ziwa Baikal “Им довелось увидеть озеро Байкал”; Ninakumbuka vizuri jinsi nilivyowahi kuongea na mwandishi huyo “Я хорошо помню, как мне случалось беседовать с этим писателем”.
Mazoezi

1. Переведите предложения и сделайте их отрицательными:

1. Mtafiti wa Kiingereza alipata kugundua jambo jipya lenye kuhusu historia ya binadamu wa kale. 2. Magofu haya yaliwahi kutembelewa na watalii wengi. 3. Chama cha upinzani kimekwisha kutangaza mpango wake wa kuiunda serikali ya mseto. 4. Kiongozi huyu alipata kugombea cheo cha urais kwenye uchaguzi uliopita. 5. Wafanya biashara wamekwisha kuwekeza mitaji mingi katika maendeleo ya sekta ya utibabu. 6. Mchezaji mashuhuri wa Urusi aliwahi kujinyakulia medali ya dhahabu katika mashindano ya kimataifa ya mchezo wa riadha. 7. Imepata kutambulikana kuwa uganga wa miti shamba unaweza kuleta madhara makubwa kwa afya ya mtu. 8. Watoto wachanga wamekwisha kupata chanjo za dawa ya kinga dhidi ya maradhi ya hatari.


2. Переведите предложения, используя вспомогательные глаголы -isha, -pata, -wahi:

1. Как только корреспонденты узнали эту новость, они поспешили сообщить о ней. 2. Закончив обедать, дети побежали к озеру. 3. Мы смогли отремонтировать машину только к вечеру, поэтому нам ничего не оставалось, кроме как продолжить наше путешествие утром. 4. Туристам удалось перебраться на противоположную сторону реки после того, как начала работать паромная переправа. 5. Как только тот красивый многоэтажный дом будет достроен, жильцы смогут переехать в новые квартиры. 6. Крестьяне еще не собрали весь урожай, а морозы уже наступили. 7. Моему внуку уже исполнилось 8 лет, а его родители еще не отправили его в школу. 8. Вам приходилось видеть, как растут ананасы? 9. Мне ни разу не довелось побывать в этом удивительном заповеднике. 10. Посадив кукурузу, мы начали пропалывать рисовое поле.


ELIMU NI KITU MUHIMU

(kutokana na hotuba ya Abeid A. Karume)

Elimu ni kitu bora sana na chenye thamani kubwa. Tulisema kwamba tunataka elimu ya kisasa na tusitosheke na elimu hii tuliyo nayo leo, kwa sababu tunataka tulingane na wanadamu wenzetu.

Kila mtoto anahitajiwa afikie kima maalumu katika masomo ya msingi ndipo afanye mtihani wa kuingia katika skuli za sekondari. Kwa hivyo panahitaji mpango wa kumtengeneza mtoto mpaka afike katika kiwango maalum. Serikali imekwisha weka mpango kuwa kila mtoto akisha maliza masomo ya msingi apate masomo zaidi ya elimu ya sekondari kwa muda wa miaka mitatu, ili mtoto huyo akiwacha skuli awe amekwisha fika umri wa miaka kumi na sita mpaka kumi na saba. Kwa sababu mtoto wa umri wa miaka kumi na sita mpaka kumi na saba anaweza kutumia akili yake na akifundishwa jambo akafahamu. Lakini akiwacha skuli katika umri wa miaka kumi na mbili mpaka kumi na nne huwa hana uwezo wa kufanya kazi yo yote vizuri. Ilivyokuwa* tunaamini kwamba ‘Mwana umleavyo ndivyo akuavyo’, basi lazima tuwahimize watoto wetu wakasome, kwa sababu watoto wa leo ndio wazee wa kesho, na kwa hivyo tuwaandae katika taalimu za kila namna.

Hivi sasa serikali imefanya mpango kwa watoto waliowacha skuli katika umri mdogo wajifunze kazi za kilimo, ufundi, viwanda na kadhalika.

Mtakumbuka kwamba wakati wa ukoloni shule zilikuwa zikilipiwa. Na wanyonge wengi walikuwa hawana uwezo wa kuvumbua hata chakula chao seuze kutafuta fii ya kumlipia mtoto shuleni; isitoshe** na mapendeleo yalikuwepo. Ingawa wazee wa kimaskini walijikaza kuwalipia watoto wao, lakini mwisho wa elimu ya watoto hao ni darasa la nane. Ilikuwa muhali kupata kuingia darasa la juu ambalo ataweza kujifunza elimu itakayomfaa kushika kazi za madaraka ya juu. Wakoloni walikuwa wakiwanyima watoto wa kimaskini elimu ya sekondari na kuwapa elimu hiyo watoto wa kibepari.

Tuna azma ya kujitahidi kama tuwezavyo kuwapatia elimu ya sekondari idadi kubwa ya watoto wa wanyonge. Kwa hivyo, tunataka kila mtoto adurusu masomo yake na afahamu. Isitoshe** waalimu nao vile vile wanao wajibu wao wa kuwatia hima watoto kila mara.

Katika mwaka 1963, ulifanywa mtihani katika skuli zetu zote za Unguja na Pemba ambao watoto wengi wa kimaskini walianguka.*** Kwa kweli hasa hawakuanguka lakini ilikuwa ni siasa tu. Hapo mwanzo watoto wa kimaskini hawakuwa wakipelekwa sekondari kwa sababu wazee wao walishindwa kuwalipia. Kwa hivyo walipasishwa watoto wa kibepari kwa sababu wazee wao ndio walioweza kuwalipia. Kwa bahati nzuri mwezi 12 Januari 1964, Mapinduzi yakatokea, na mara tu likaundwa Baraza la Mapinduzi, na fikra yake ya mwanzo ilikuwa ni kuwafikiria watoto wa wakulima na wafanya kazi kwa taabu zilizowapata kwa muda mrefu. Baraza la Mapinduzi likaamua kuwa watoto wote walioanguka katika mtihani wa 1963, warudishwe tena ili waingie katika sekondari, na wengi katika hao hivi sasa wamo serikalini na wana kazi nzuri sana. Vijana hao leo wanatufaa katika shughuli mbali mbali za maendeleo ya taifa. Sasa watoto wote wa wakulima na wafanyakazi maskini wanapata elimu bila ya kubaguliwa.

Lazima tuipindue elimu kwa kuleta waalimu kutoka nje, baadaye mkisha fahamu nyinyi wenyewe mtashika kila kitu katika nchi yenu na kuleta mafanikio. Sasa iliyosalia ni jitihada yenu na ufunguo wa jitihada hiyo ni masikilizano, na kuoneana huruma. Na mtambue kwamba nchi yetu imekusudia kupindua vitendo vyote vibaya katika mipango yote ya elimu.
Maelezo

*Ilivyokuwa tunaamini… “Так как мы верим…”. Глагол -wa с релятивом -vyo- имеет контекстуальное значение “так как”, “поскольку”, “раз уж”. Сравните синонимичные варианты – kwa vile tunaamini; kwa jinsi tunavyoamini.
**Глагол -tosha “быть достаточным” в неопределенно-личной конструкции желательно-побудительного наклонения с отрицанием – isitoshe переводится как “кроме того”, “мало того”, “более того”.
***walianguka “упали” здесь можно перевести как “провалились” (на экзамене).
Mazoezi

3. Дайте русские эквиваленты:

kitu chenye thamani kubwa; tusitosheke na elimu tuliyo nayo; tulingane na wanadamu wenzetu; -fikia kima maalum; uwezo wa kufanya kazi; taaluma za kila aina; tuwahimize watoto wetu wakasome; shule zilikuwa zikilipiwa; na mapendeleo yalikuwepo; ilikuwa muhali kuingia darasa la juu; -durusu masomo; -tia hima; wanatufaa katika shughuli za maendeleo; -pata elimu bila ya kubaguliwa; -oneana huruma; -pindua vitendo vibaya; kima cha chini; kima cha juu.



4. Переведите:

1. Образование – это бесценная вещь. 2. Это не соответствует истине. 3. Эти вещи несопоставимы. 4. Он достиг определенного уровня образования. 5. Это максимум, что я могу. 6. Нам установили минимальный размер зарплаты. 7. Их подготовили к вступительным экзаменам. 8. Нас призывают к активным действиям. 9. Платное образование лишает их возможности учиться. 10. Это сделать почти невозможно. 11. Вам следует постараться изо всех сил. 12. Студентов отбирали без каких-либо предпочтений. 13. Мы не подвергаемся ни малейшей дискриминации. 14. Тебе следует лишь немного поднапрячься. 15. Руководство школы нацелено устранить предвзятое отношение к детям малоимущих родителей.

1   ...   12   13   14   15   16   17   18   19   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət