Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə13/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   9   10   11   12   13   14   15   16   ...   25

12. Найдите в тексте “Mkwawa shujaa” эквиваленты следующих выражений:

придерживаться единого мнения; защищать свободу; давать последние наставления; нападать; мужественно сражаться; они были очень жестокими; убивали ни за что; ради своей выгоды; люди второго сорта; терпеть жестокость; оказывать сопротивление; укреплять свое войско; записываться в армию; ослабевать; казнить прелюдно; убегать в лес; давать клятву; быть захваченным в плен; застрелиться из винтовки.


13. Перескажите текст, используя выражения из предыдущего задания.
14. Переведите:

  1. Иностранцы начали посещать Восточную Африку, особенно ее прибрежные районы, еще в давние времена.

  2. Арабские колонизаторы пришли на побережье Восточной Африки в восьмом веке, так как их привлекала возможность выгодно вести там торговлю.

  3. На протяжении почти двух веков арабы и португальцы вели между собой жестокую борьбу, желая прибрать к рукам земли Восточной Африки.

  4. Одержав победу, арабы превратили все побережье в подконтрольную территорию Оманской империи.

  5. До середины 19-го века никому из европейцев не довелось увидеть своими собственными глазами те чудеса в Африке, о которых они слышали раньше.

  6. Именно англичане были первыми, кто отправился в Африку в поисках истоков Нила.

  7. Европейские миссионеры, которые были посланы в Африку с целью распространения христианства, также помогли открыть много нового на этом континенте.

  8. Дэвид Ливингстон был свидетелем того, как велась торговля рабами, и сердце его наполнялось горечью.

  9. Вернувшись в Европу, Ливингстон попросил послать в африканские страны миссионеров с тем, чтобы они помогали коренным жителям и защищали их от работорговцев.

  10. Когда Стэнли приехал в Африку забрать Ливингстона в Англию, тот был очень болен, но отказался вернуться домой, так как был предан своей идее открытия новых земель.

  11. После второй мировой войны Англия в соответствии с решением ООН получила право владеть Танганьикой как своей подмандатной территорией.

  12. Конституционное собрание Танганьики постановило, что стране будет предоставлена полная независимость в декабре 1961 года.


Msamiati

Arabia (-) Аравия mjumbe (wa-) 1) делегат,

Uajemi (ед.) Персия представитель 2) член

Bara Hindi Индия kauli (-) мнение, взгляд

himaya (-) 1) опека; опекунство kwa kauli moja

2) протекторат, управляемая единодушно; единогласно

территория mtemi (wa-) вождь

rasi (-) мыс -hifadhi беречь,

-vumbua открывать, защищать, охранять

обнаруживать; изобретать hifadhi (-) охраняемая



mvumbuzi (wa-) изобретатель, зона, заповедник

первооткрыватель usia (ma-) наставление,



marufuku (мн.) запрещение, отказ последняя воля

-piga marufuku запрещать, -usia давать последние

отказывать наставления; завещать



-eneza распространять misheni (-) миссия

-agiza 1) давать указания, mmisheni (wa-) миссионер

инструктировать 2) заказывать matanga (мн.) траур,



-funua открывать, раскрывать траурная церемония

mdhamini (wa-) 1) попечитель, marehemu (-) покойник,

опекун 2) поручитель умерший



-dhamini гарантировать, maiti (-) мертвое тело, труп

обеспечивать -pasha habari передавать



-kaza 1) закреплять, усиливать (сообщать) информацию

2) упорствовать, настаивать mwanajeshi (wa-) солдат,



waziri mkuu премьер-министр военнослужащий

-kabili 1) стоять перед (кем-л., чем-л.) jeshi (ma-) армия, войско

2) противостоять; оказывать Umoja wa Mataifa ООН

сопротивление uchaguzi (ед.) выборы

bakora (- ; ma-) палка, трость -vamia нападать,

-huzunika печалиться, горевать атаковать; вторгаться

adabu (-) вежливость, учтивость kiapo (vi-) клятва, присяга

-shika adabu быть вежливым, -nyonga вешать, казнить

воспитанным hadharani публично, на



mkataba (mi-) договор, контракт людях

fujo (-; ma-) 1) беспорядок, суматоха huzuni (-) печаль, скорбь

2) беспорядки, волнения -pigana kiume сражаться



Baraza la kutunga sheria мужественно

законодательное собрание -la kiapo, -apa давать



idhini (-) разрешение, одобрение клятву, присягать

mamlaka (-; ma-) власть, господство mateka (-) пленный,

-jiandikisha записываться, пленник; заложник

регистрироваться -funga mkataba заключать



bunduki (ma-) ружье, винтовка договор

-toroka убегать (от кого-л., чего-л.)

* * *

Урок 18. Somo la kumi na nane
Грамматика

  1. Номинативные конструкции с переходным глаголом.

  2. Приглагольные согласователи при самостоятельном употреблении

В языке суахили существуют словосочетания, состоящие из двух существительных. Первое из них является отглагольным именем существительным, образованным от основы переходного глагола с помощью префикса одного из именных классов, чаще всего класса одушевленных лиц или класса ki-/vi-. Вторым компонентом служит прямое дополнение к этому существительному. Такие словосочетания часто становятся устойчивыми, многие из них на русский язык переводятся одним словом: mfanya kazi “рабочий”; mpita njia “пешеход”, “прохожий”; kifungua kinywa “завтрак”; mrina asali “пчеловод”; mkana Mungu “атеист”.

Обратите внимание на то, что глаголы, участвующие в образовании таких словосочетаний, не оформляются словообразовательными именными суффиксами. Как правило, компоненты словосочетаний не сливаются в одно слово, а пишутся раздельно, хотя могут встречаться оба варианта.

Подобные словосочетания часто встречаются в пословицах:



Mchelea bahari si msafiri “Тот, кто боится моря, не путешественник”; Mchovya asali hachovyi mara moja “Тот, кто пробует мед, делает это неоднократно”.

Такие словосочетания продуктивно используются в образовании терминов: kiuavijidudu “антисептик”; kitoa madoa “пятновыводитель”; mpinga maendeleo “реакционер”; kipima hewa “барометр”.



Приглагольные согласователи могут употребляться самостоятельно, то есть без глагола, выполняя функцию предикативной связки ni. Их часто можно встретить со словами, выражающими качественную характеристику лица или предмета, его состояние. Например:

Yu nani? (Yeye ni nani?) “Кто он?”; Tu wazima (Sisi ni wazima) “Мы здоровы”; Mu hai (Nyinyi ni hai) “Вы живы”; U hali gani? (Wewe hali yako ni gani? “Как вы себя чувствуете?” Jibu hili li sahihi (Jibu hili ni sahihi) “Этот ответ правильный”.
Mazoezi

1. Найдите суахилийские эквиваленты сочетаниям из группы А в группе В. Проанализируйте образование новых словосочетаний и запомните их:

А/ фармацевт; продавец; дровосек; громкоговоритель; нефртяник; маляр; бульдозерист; казначей; депонент; десерт; пищевой контейнер.

В/ mchimba mafuta; mwuza duka; kihifadhia chakula; mwendesha katapila; mweka akiba; kitindamlo; mtoa dawa; mtia rangi; kikuza sauti; mweka fedha; mtema kuni.
2. Дайте русские эквиваленты:

mpiga mbizi; mshika zamu; kizima moto; msema ukweli; mwendesha trekta; mweka hesabu; kibadili hewa; kikamua machungwa; kisaga nyama; kivuta vumbi; kimenya mboga; kipangusia mdomo.


3. Образуйте словосочетания с отглагольными существительными, передав следующие значения:

музыкант; пожарный; землекоп; альпинист; дровосек; прохожий; бизнесмен; наездник; книголюб; велосипедист; мечтатель; микрофон; градостроитель; гурман; барабанщик; фотограф; сапожник; донор; сейсмограф.



4. Переведите:

1. Daktari alinithibitishia kwamba babangu yu mgonjwa sana na lazima alazwe hospitalini mapema iwezekanavyo. 2. Inasemekana kuwa mchezo huu wa kuigiza u mbaya sana wala sitaki kwenda kuutazama hata kidogo. 3. Pesa hizi zi kidogo sana hata hazitoshi kujinunulia mkate. 4. Naona wewe u mtoto hodari kwa jinsi ulivyosafisha viatu vyako vilivyokuwa vichafu mno. 5. Ijapokuwa tulikuwa tumechoka kupita kiasi wakati wa kufanya mitihani, sote tu wazima. 6. Yu nani yule anayeongea na binti yangu pembeni huko? 7. Viatu vyako vi vichafu kabisa, ulitembea wapi? 8. Kiongozi yule yu thabiti, ataikabili hatari yo yote.


UJASIRI WA JULIUS NYERERE

Watenda wema ni wengi bali mashujaa ni wachache. Mashujaa wenye kusimamia kweli na haki siku zote ni wachache zaidi. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere amethibitisha ushujaa wake kati ya mashujaa wachache wanaojulikana, kwani ni nani hapa Tanzania asiyejua kuwa yeye ndiye aliyekuwa baba wa taifa letu?

Julius Nyerere alizaliwa huko Butiama, Musoma mwaka 1922. Enzi hizo za ukoloni, mnamo mwaka 1945 alipofuzu masomo yake na kupata shahada ya ualimu huko Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki – Makerere. Ingetosha kwake kuitwa mwalimu wa Makerere kwani lilikuwa jina lenye sifa na hadhi kubwa.

Baada ya kumaliza masomo ya kupata shahada yake hiyo ya elimu, alianza kukiendesha chama cha waafrika ambacho kiliitwa “Tanganyika African Association” kwa Kiingereza na TAA kwa ufupi. Chama hiki ndio asili ya chama cha TANU na kilianzishwa mwaka 1929. Julius Nyerere alikitumia kama chombo cha kutuunganisha Watanganyika ili tupiganie uhuru wetu. Alijitolea kufanya kazi hizo zote mbili kwa moyo mkunjufu. Hapa ndipo ujasiri wote ulipoanza kuonekana.

Mwalimu Nyerere hakutosheka na kiwango kile cha elimu aliyoipata huko Makerere. Ni wazi kwamba alikuwa na lengo lake la kutaka kupata silaha zifaazo ili aweze kupigana na mkoloni.* Mwaka 1948 alifuzu mtihani wa chuo kikuu cha London na mwezi Aprili mwaka uliofuata aliwasili Uingereza kuchukua masomo ya juu zaidi. Oktoba 1949 alijiandikisha katika chuo kikuu cha Edinburgh kusomea shahada ya M.A.** katika masomo ya historia ya Uingereza, lugha ya Kiingereza, elimu ya mambo ya kale, sheria za katiba na elimu ya uchumi. Baada ya kujifunza huko Edinburgh kwa miaka mitatu alijipatia shahada yake ya M.A. hapo Julai 1952 akiwa Mtanzania wa kwanza kupata shahada hiyo. Huko Edinburg alionyesha ujasiri wake kwa mara ya pili kwani hotuba zake alizozitoa huko zilionyesha wazi nia ya kupigana na ukoloni. Hii ilithibitika katika insha aliyoiandika juu ya ‘Matatizo ya Rangi katika Afrika ya Mashariki’.

Mwaka 1952 Julius Nyerere alirudi Tanganyika na aliendelea kuwa mwanachama wa TAA huku akiwa mwalimu wa shule kubwa ya huko Pugu karibu na Dar es Salaam. Mara nyingi Julius Nyerere alitembea kwa miguu toka Pugu kwenda Dar es Salaam kufanya mikutano ya siasa. Mwaka 1953 alichaguliwa kuwa rais wa TAA. Ilikuwa tarehe 7 Julai 1954, TAA ilipozikwa na TANU ilipoibadili na kuzaliwa mjini Dar es Salaam na Julius Nyerere akiendelea kuwa rais wa chama hicho kipya.

Mnamo Machi 1955 Julius Nyerere alijiuzulu katika kazi yake ya ualimu huko Pugu, na akajizamisha kabisa kwenye siasa. Huu ulikuwa ujasiri mkubwa maana matumaini ya mbele yalikuwa katika kiza kikuu.*** Aliombwa, bali alikataa kuwa mhariri wa gazeti la ‘Kiongozi’, alikataa pia kuajiriwa na kampuni ya Shell – kwa kuwa alipenda kuongoza chama. Mwezi Juni mwaka ule ule alimshambulia gavana wa kikoloni kwa barua kwa ajili ya kutapanya mali za adui walioshindwa katika vita kuu ya pili. Mali hizo ziliwekwa katika ulinzi wa serikali ya kikoloni kisha zikagawanywa kwa hila. Gavana huyo alimlaumu Nyerere na kumwita mchochezi, lakini ukweli haukuweza kufichama.****

Kumshambulia mtawala wa kikoloni wazi wazi hivi lilikuwa jambo la hatari. Ingawa maadui walimzunguka pande zote alichurupuka mikononi mwao. Mnamo Disemba 1956 alitoa hotuba mbele ya mkutano wa nne wa Kamati ya Umoja wa Mataifa, akashauri mengi mojawapo lile la kuipatia Tanganyika uhuru wake mwaka wa 1966, uhuru ambao ulipatikana 1961 – miaka mitano kabla ya mwaka uliofikiriwa.

Katika mkutano wa Tabora uliofanyika Januari 1958, wajumbe wa TANU walitaka kuususia uchaguzi mkuu kwa sababu ya mgawo wa wajumbe katika Baraza la kutunga sheria kutegemea mataifa matatu yaliyopo Tanganyika. Julius Nyerere aliwaelewesha wajumbe umuhimu wa kuingia katika uchaguzi huo, la sivyo***** wangepoteza viti vyote kabisa. TANU iligombea ikanyakua viti vyote. Uwamuzi huu ulikuwa wa ujasiri pia.

Uhuru ulipopatikana hapo Disemba 1961 Mwalimu Nyerere alifanywa kuwa waziri mkuu, lakini baada ya siku kama arobaini tu hapo Januari, 1962 alikiacha kwa hiari cheo cha waziri mkuu ili aende akaimarishe chama cha TANU. Jambo ambalo watu wengi wangesita kufanya jambo kama hili. Mwaka huo huo wa 1962 shauri lilikatwa kuwa Tanganyika iwe Jamhuri na Julius Nyerere baada ya kushinda uchaguzi kwa kura nyingi sana aliapishwa kama ndiye rais wa kwanza wa Jamhuri ya Tanganyika.

Aprili 1964 mkataba wa Tanganyika na Unguja ulikubaliwa rasmi baada ya kutiliwa sahihi na rais Nyerere na rais Karume. Mataifa makuu ya ng’ambo yamejaribu kuleta maneno mengi ya ufidhuli juu ya muungano huu, lakini muungano umesimama imara. Hili ni jambo jingine la ujasiri alilolifanya Rais Nyerere.

Rais Nyerere yu thabiti katika kauli zake. Akishatamka jambo harudi nyuma. Mnamo Disemba 1965 Umoja wa nchi za Afrika ulipitisha azimio la kuvunja uhusiano wa kiserikali na Uingereza iwapo Rhodesia itajinyakulia uhuru kwa nguvu. Tanzania ilikuwa moja katika zile nchi saba zilizovunja uhusiano na Uingereza. Kuvunja uhusiano huko kuliiletea Tanzania dhiki kidogo, maana Waingereza nao wakasusa kuleta misaada. Rais Nyerere kwa sababu ya ujasiri hakutikisika. Kuna wakati pia Tanzania ilivunja uhusiano wake wa kiserikali na Ujerumani ya Magharibi baada ya kubali Ujerumani ya Mashariki iweke balozi wake Dar es Salaam. Wajerumani hawa wa Magharibi walitishia kuondoa wanahewa wao waliokuwa wakilifundisha jeshi letu. Rais Nyerere aliwaambia waondoe, licha ya wanahewa hata kila kitu cha Ujerumani ya Magharibi kilichomo Tanzania. Wajerumani wakafahamu kwamba Rais Nyerere yu jasiri.

Si jambo lililo jepesi kuziandika sifa zote za ujasiri zilizomfanya Julius Nyerere kuwa kiongozi shujaa.
Maelezo

* В собирательном значении в суахили часто употребляется единственное число вместо множественного, хотя на русский язык такие существительные принято переводить во множественном числе. Например:

Tumshinde mnyonyaji! “Победим эксплуататоров!”

Walimwangamiza fashisti “Они уничтожили фашистов”.

Mwananchi, uwe macho! “Соотечественники, будьте бдительны!”


** Сокращение от Master of Arts “Магистр гуманитарных наук” (первая ученая степень в области гуманитарных наук).
*** kiza – фонетический вариант слова giza “темнота”. В суахили встречаются случаи согласования по формальному признаку принадлежности к именному классу, когда начальный слог совпадает с префиксом какого-нибудь другого класса. В данном случае слово kiza попало в класс ki-/vi- (kiza kikuu). Однако при варианте giza обязательной является форма giza kuu. Как правило, такие явления наблюдаются у заимствованных слов. Сравните: cherehani nzuri – vyerehani vingi; madini nyingi – madini mengi; vita kuu – vita vikuu; kilabu mbili – vilabu viwili.
**** Слово -fichama “быть скрытым” – производная форма глагола -ficha “прятать” с суфиксом -ma. Эта производная форма, называемая статичной, относится к редким, малоупотребительным глагольным формам. Она передает значение устойчивого, постоянного состояния и может быть сравнима по смыслу со стативной формой с суффиксом -ka. Например: -fungama “быть закрепленным” (от -funga “закрывать, завязывать”); -tuama “останавливаться в развитии, быть в состоянии застоя” (от -tua “садиться, опускаться”).
***** La sivyo имеет значение “иначе, в противном случае”. Сравните другой вариант с тем же значением – vinginevyo.
Mazoezi

5. Дайте русские эквиваленты:

mashujaa wenye kusimamia kweli; -thibitisha ushujaa wake; enzi za kikoloni; ingetosha kwake kuitwa mwalimu; -pata shahada ya ualimu; jina lenye sifa na hadhi kubwa; asili ya chama; chombo cha kuunganisha watu; moyo mkunjufu; -jiandikisha katika chuo kikuu; -toa hotuba; mali ziligawanywa kwa hila; -jiuzulu katika kazi; -jizamisha kwenye siasa; matumaini ya mbele; ukweli haukuweza kufichama; -kataa kuajiriwa; mgawo wa wajumbe; -churupuka mikononi mwa adui; -susia uchaguzi; la sivyo; -gombea uchaguzi; -acha kwa hiari; -sita kufanya jambo; mkataba ulikubaliwa rasmi; maneno ya ufidhuli; -weka balozi; -leta dhiki; -apishwa kuwa rais.


6. Дайте эквиваленты на суахили:

выступать за правду; выступать на собрании; выступать вперед; во времена колониального господства; во время каникул; приходить вовремя; преуспеть в учебе; добиться успеха; успешно сдать экзамен; достойное имя; популярное имя; известное имя; человеческое достоинство; средство объединения; орудие борьбы; рабочие инструменты; бороться за независимость; биться с врагом; вести борьбу; уходить в отставку; уходить с поста; уходить из дома; мрачные перспективы; хорошие перспективы; не иметь никаких перспектив; разжигать огонь; разжигать войну; сеять вражду; осуждать кого-либо; обвинять друг друга; обвиняемый; бойкотировать выборы; одержать победу большинством голосов; баллотироваться на выборах; разрывать официальные отношения; устанавливать добрые отношения; развивать отношения.


7. Составьте 10 вопросов на суахили по содержанию текста и дайте на них ответы.
8. Расскажите на суахили, что вы знаете о Дж. Ньерере.
9. Переведите, используя желательно-побудительное наклонение с показателем -ka-:

1. Преподаватель велел нам сходить в библиотеку и взять новые учебники. 2. Мы попросили водителя ехать прямо, затем свернуть налево и остановиться. 3. Исследователь поехал в Индию для того, чтобы изучить жизнь слонов и написать о них книгу. 4. Давайте зайдем в кафе и поедим, так как впереди у нас долгий путь. 5. Соседка попросила меня съездить на вокзал и встретить ее дочь, поскольку сама она заболела. 6. Позвони редактору и скажи ему, что он должен срочно приехать на работу. 7. Если ты не знаешь, как готовить эту рыбу, иди и спроси у повара. 8. Полицейский приказал грабителю бросить свой нож и поднять руки.


10. Переведите текст:

Rashidi M. Kawawa

Rashidi Mfaume Kawawa, ambaye alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Tanganyika tarehe 22 Januari 1962, alipojiuzulu Julius K. Nyerere, ndiye aliyeanzisha vyama vya wafanya kazi nchini Tanganyika. Alizaliwa mwaka 1930. Alipochaguliwa kushika usukani wa serikali, alikuwa amekwisha fanya kazi za siasa, utumishi wa serikali na kuwa mchezaji hodari katika picha za sinema.

Rashidi Kawawa alizaliwa Songea katika ukoo wa mfanya kazi serikalini na mwindaji mashuhuri. Ukoo mzima wa Kawawa ni wawindaji mashuhuri. Rashidi M. Kawawa alielemishwa katika shule ya sekondari ya serikali, Dar es Salaam, na baadaye katika shule ya sekondari ya serikali, Tabora, ambako alijulikana sana kwa uhodari wake katika michezo ya kuigiza. Rashidi Kawawa alipendelea sana kazi za maendeleo, lakini alipoomba kazi katika Idara hiyo mara ya kwanza, alikataliwa kwani eti alikuwa mdogo mno. Badala yake akaingia kazi ya ukarani katika wizara ya usafirishaji umeme na kazi na baadaye alipata uhamisho kwenda Idara ya maendeleo mwaka 1951.

Rashidi Kawawa alipokuwa mfanya kazi katika Idara ya maendeleo aliendesha sinema na kuangalia maktaba ya picha za sinema – hata baadaye akajulikana sana kama mchezaji maarufu katika picha za sinema za Kiswahili kadha wa kadha. Zaidi ya kazi hizo alikuwa mshauri juu ya jadi za Kiafrika kwa wataalamu wa kutengeneza picha za sinema.

Mwezi Februari 1956, Rashidi Kawawa alijiuzulu katika kazi za serikali na akawa katibu mkuu wa Shirikisho la vyama vya wafanya kazi Tanganyika. Wakati huo huo pia akaaingia TANU. Akiwa katika kazi ya vyama vya wafanya kazi, alitembelea nchi mbali mbali za nje kuhusiana na kazi yake. Katika uchaguzi mkuu mwaka 1960 Rashidi Kawawa aliingia katika Baraza la kutunga sheria bila kupingwa akiwa mjumbe wa Nachingwea.

Rashidi Kawawa aliposhika usukani wa kuendesha nchi, yaani katika kipindi alipokuwa waziri mkuu, mambo mengi yalirekebishwa na serikali ya wananchi: vyama vya ushirika vingi vilianzishwa; utaratibu wa kumiliki ardhi ulitengenezwa ili upatane na mila za wananchi juu ya umilikaji wa ardhi; migomo ilifanywa si njia halali ya wafanya kazi kudai haki zao mpaka idhini ya waziri imetolewa. Shauri la kuitaka Tanganyika iwe Jamhuri lilikatwa kwa vile wananchi wengi walikuwa wanakerwa kerwa na lile jambo la kuwa chini ya malkia wa Waingereza hata baada ya nchi yao kupata uhuru kamili. Kwa upande wa serikali, mwaka 1962 ulikuwa mwaka wa kufanya kazi kweli ili kuipa nchi yetu sura ya Utanganyika. Katika kazi za serikali wananchi wengi walipewa madaraka makubwa sana. Wananchi pia waliitikia kwa kujitolea katika kazi za kujenga taifa.


11. Переведите текст:

Джомо Кениата родился в 1891 году примерно в 50 километрах от Найроби в довольно известной семье. Его отец и дед считались мудрыми людьми, которые могли давать советы и предсказывать будущее. Мальчику дали имя Камау Нгенги. В 1907 году он поступил в миссионерскую школу. Спустя семь лет, Нгенги принял христианство, и ему дали имя Джонстон. Джонстон Камау успешно окончил школу, проявив прекрасные способности и большую любознательность. В 20-е годы он работал переводчиком в Верховном суде, затем поступил на работу в департамент водоснабжения муниципалитета Найроби. “Мои обязанности, – рассказывал Кениата, – заключались в сборе денег за воду. Я носил широкий пояс, который на моем языке называется “кениата”. За этот пояс я закладывал полученные деньги. Когда ехал на велосипеде, мальчишки бежали за мной и кричали: “Кениата! Кениата!” Это слово так привязалось ко мне, что для многих я стал изестен как Кениата. Имя Джонстон впоследствии я заменил на более близкое моему народу – Джомо”. Так появилось имя Джомо Кениата, которое уже в конце 20-х годов стало известно не только в Кении.


12. Переведите текст и перескажите его на суахили:

Sheikh Abeid Amani Karume

Sheikh Abeid alizaliwa Unguja, kijijini Mwera, Wilaya ya Kati, katika mwaka 1905. Alipofika umri wa miaka minane, alipelekwa skuli ya hapo hapo kijijini kwa kusoma. Yeye alikuwa katika wale wanafunzi wa kikundi cha awali kupelekwa hapo na ndio walioifungua shule hiyo iliyojengwa na serikali.

Baba yake alipokufa Abeid alikuwa ni mtoto wa miaka minane tu. Kwa hayo yaliyotokea, aliona skuli nzima ni kama kwamba iliyofunikwa na giza. Pamoja na hayo alijikaza hivyo hivyo kuhudhuria. Ilikuwa ni kawaida yake anaporejea nyumbani kumsaidia mama yake Bibi Amina katika machungaji ya ng’ombe. Pia humsaidia katika kazi nyingine ndogo ndogo za hapo nyumbani kwani yeye akapenda kujituma na kufanya kazi hii na ile.

Alipofika umri wa miaka 13, mama yake mpenzi alimpeleka mjini kuendelea na masomo. Yeye hakuwa mgeni hapo mjini, kwani Mwera ipo masafa ya maili 7 tu kutoka mji mkuu wa Unguja. Kwa vile alivyokuwa akija mjini baadhi ya nyakati, aliweza kujuana na watoto wengi wa makamo yake na kuchanganyika nao katika michezo.

Wakati huo, zilikuwa zikipitia Unguja meli za namna kwa namna, kwani hii ilikuwa ikihesabika kuwa ni moja katika bandari mashuhuri ya Afrika ya Mashariki. Pia zikiteremsha bidhaa za kila aina na kuchukua zile za pande hizi. Nyingi katika meli hizo mpaka hivi leo zinatia nanga bandari hii ya Unguja. Kwa hivyo, hapo pwani zilizuka kazi nyingi na vijana chungu nzima waliweza kujipatia kazi ya kufaa. Abeid naye pia alijitia humo pamoja na wananchi wenziwe. Kwa vile alivyopata fursa ya kuzipandia meli nyingi, kukutana na kuzungumza na wasafiri, mabaharia na wafanya kazi wa humo, ilimjia hapo na yeye hamu kubwa ya kutaka kusafiri, kuona nchi za nje na kuweza kushuhudia kwa macho yake namna mataifa mbali mbali yanavyoishi katika dunia yetu hii.

Mawazo hayo yalimkaa sana moyoni mwake. Hapo alimkabili mama yake mpenzi na kumweleza fikra na maazimio yake na alimtaka ampe ruhusa kwa kuingia katika kazi za bahari. Bibi Amina alimkubalia mwanawe kuwa mwana wa bahari kwa kusikia kuwa safari zake zitakuwa za zile nchi za jirani na ataweza kumwona mwanawe kila mara meli yake itakapofika Unguja.

Katika 1920, Sheikh Abeid alitimia miaka 15 na hapo alipokelewa na kampuni kufanya kazi katika merikebu zao zile zinazosafiria pwanipwani ya Afrika ya Mashariki kwa kuipitia bandari kama zile za Dar es Salaam, Mikindani, Mafia, Tanga, Mombasa na kadhalika. Sheikh Abeid hufurahi sana meli yake inapofika Unguja, kwani hupata fursa ya kumzuru mama yake mpenzi, wazee wengine na kuonana pia na marafiki zake.

Baada ya miaka miwili, Sheikh Abeid katika 1922 aliingia kufanya kazi katika meli za nje na zile zilizosafiria nchi za mbali. Humu ndimo alimopata maarifa mengi na kuziona mwenyewe zile faida nyingi za safari. Katika miaka 17 aliyoipitisha humo merikebuni kwa kufanya kazi za namna mbali mbali, aliweza kuzitembelea nchi nyingi.

Katika mwaka 1938 fikra ilimjia ya kurejea kwao. Aliona wakati umefika kuyatumia yale maarifa aliyoyapata kwa masilaha ya wananchi wenzake. Zama hizo hizo ndipo alipowakusanya mabaharia na wafanya kazi wote wa mashua na motaboti za pwani na kuunda jumuiya yao ya ushirika. Kabla ya kusimamishwa jumuiya hii, wafanya kazi wa hapo wote walikuwa wakilipwa ujira mdogo tu. Mapato yote na mipango yote ya kazi ilikuwa ikidhibitiwa na matajiri wenye kumiliki mashua hizo. Kuwekwa kwa jumuiya hii kuliondosha ubepari huo na badala yake kumeleta faida nyingi. Umeondoka ule mgogoro na chuki; na badala yake yamepatikana masikilizano mazuri baina ya wafanya kazi na matajiri.

Huo ndio ushirika wa kikweli ulioletwa na kiongozi huyo. Msingi huu madhubuti wa ushirika alioujenga hapo pwani ulimpelekea kiongozi huyo kusifika na kupendwa si na wafanya kazi wa hapo tu, bali na wa sehemu nyingine za wananchi wote. Umashuhuri wake katika kujenga msingi wa kitaifa ukaanza kuzungumzwa, kujulikana na kuenea.

1   ...   9   10   11   12   13   14   15   16   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət