Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə15/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   11   12   13   14   15   16   17   18   ...   25

2. Найдите в тексте эквиваленты следующих выражений:

достопримечательность, представляющая интерес для туристов и изыскателей древностей; от построек остались руины; ознакомиться с образом жизни других людей; старейшины; в чьих руках он (город) находился; подконтрольная экономическая зона; прибрежная полоса Восточной Африки; вкладывать деньги в торговую деятельность; арабское господство закончилось на какое-то время; когда эта тактика удалась; города, возникавшие на юге Африки; их власть продержалась недолго; арабы вернули свои позиции; шире развернуть торговую деятельность; новый порядок уплаты налогов и пошлин; построить военизированную крепость; оберегать военные секреты; находиться под контролем Германии; одновременно с другими территориями; для острастки захватчиков; день ото дня.


3. Дайте русские эквиваленты:

-tafiti mambo ya kale; mtafiti wa lugha za nadra; -geuka magofu; gofu la mtu; -jionea kwa macho yako mwenyewe; himaya ya kiuchumi; -enda sambamba; -endelea sambamba; -funga ukanda; ukanda wa pwani; kanda za kaskazini; -wekeza katika maendeleo ya sayansi; shughuli zimekoma; -komesha utawala wa kikatili; -vumbua mkakati mpya; mkakati wa kuendesha vita; kuchipuka kwa miji mipya; majira ya machipuko; -tanua eneo la miliki; -tanua kinywa; -kumbana na upinzani mkali; -kumbana na shida za maisha; chama cha upinzani.


4. Переведите вопросы и дайте на них ответы на суахили:

1. Каков примерно возраст города Килва? 2. Что сейчас представляет собой этот город? 3. Благодаря чему Килва Кисивани получил свою первоначальную известность? Когда это было? 4. Какая экономическая деятельность велась вдоль побережья Восточной Африки во времена, когда она находилась под контролем торговцев с арабского востока? 5. Как развивалась история Килва Кисивани в 13-14 веках? 6. Каким образом этот город оказался в руках европейцев? 7. Как долго португальцы хозяйничали на острове Килва? 8. Какие порядки установил правитель Омана на островах Килва и Занзибар и с какой целью? Когда это было? 9. Кто ему помогал в попытках закрепить свое господство? 10. Под чьим контролем оказалась континентальная часть Танзании в конце 19 начале 20 веков? 11. Что происходило на Занзибаре в это время? 12. Каков был вклад англичан в развитие острова Килва?


5. Переведите следующий текст письменно:

Kuhusu asili ya utamaduni wa Pemba

Vijiji ambavyo vinafaa vijadiliwe kwa undani zaidi na watafiti wa historia ya Pemba, ni Kiuyu na Micheweni. Sababu kuu iliyojitokeza ni kuwa vijiji hivyo vinakaribiana sana. Pamoja na hayo Kiuyu kinaelekea kuwa ndicho kijiji au ndio lango lililowapokea wageni wa mwanzo na kuwakaribisha ndani ya kisiwa cha Pemba.

Uchunguzi uliofanywa na watafiti katika Kiuyu na Micheweni ulionyesha kuwa vijiji hivi viwili vina utamaduni mchanganyiko. Upo utamaduni ambao unaweza kufananishwa na ule unaoweza kupatikana Tanzania bara na pia upo utamaduni wa Kiarabu. Dini ya Kiislamu ndiyo dini inayotawala. Watu wa maeneo hayo ya Pemba hawakuchanganyika sana damu na kisura na kiumbile, wanaelekea kuwa Wabantu zaidi kuliko Waarabu. Hata hivyo, tabia zao, mavazi na desturi zao nyingi zimeelekea katika utamaduni wa Kiarabu. Ngoma na nyimbo zao zimekuwa katika hali ya mchanganyiko wa Ubantu na Uarabu.

Kwa jumla, upo ushahidi wa kuonekana kwa macho, kama watu, vitu nakadhalika, ambao unadhihirisha kuwa maeneo hayo yana uhusiano wa muda mrefu sana na Uarabuni. Kutokana na ushahidi wa kihistoria uhusiano au aina hiyo ya utamaduni mseto ulikuwepo kwa muda mrefu. Taarifa hizo za kihistoria zilizoandikwa zinaonyesha kuwa baina ya miaka 700-850 tayari utamaduni wa Waswahili ulikuwepo na ulikuwa umekwishaathiriwa na Waarabu.

Ushahidi mwingine unaeleza kwamba yalikuwepo maingiliano ya kibiashara na ya ndoa baina ya watu wa asili mbalimbali waliokuwa wakiishi pwani. Miongoni mwa Waswahili wenyewe inawezekana kuwakuta watu wenye asili ya Kishirazi itokayo Uajemi.

Jambo ambalo bado linabakia kuwa na utata kwenye utafiti ni kwamba hakuna maelezo thabiti kuhusu watu hao walivyoishi pamoja na ni nani aliishi hapo kwanza.

Kutokana na taarifa za mapokeo kutoka kwa wazee wa Micheweni, wanavyofahamu wao, ni kuwa wakati walipofika watu kutoka Mrima, watu ambao walidai kuwa ni Washirazi, Pemba ilikuwa haina watu. Taarifa za wazee hao zinadai kuwa Washirazi ndio watu wa kwanza kufika Pemba.

Lakini kufuatana na taarifa za historia zilizoandikwa, kabla ya kuja Washirazi mnamo mwaka 1100 tayari misikiti ya mwanzo ya mawe ilikuwa imekwishajengwa na kuwa Pembe ilikuwa ni mojawapo ya makao ya mwanzo ya Kiislamu Afrika ya Mashariki.Washirazi walifika Pemba kwa kutumia jahazi wakitokea Uajemi.


6. Подберите синонимы к подчеркнутым словам:

-karibiana sana; sababu iliyojitokeza; utamaduni mchanganyiko; dini inayotawala; -changanyika damu, kisura na kiumbile; ushahidi unaodhihirisha; maingiliano ya kibiashara; jambo lenye utata; -fanya utafiti.
7. Переведите:

  • Танганьика получила свою независимость 9 декабря 1961 года почти после векового господства германских и английских колонизаторов. Это стало результатом сложной, длительной и самоотверженной борьбы народа, желавшего добиться свободы и права на уважение.

  • В историю борьбы за независимость вошло имя героя Мквава, который на протяжении десяти лет конца 19 века мужественно противостоял германским колонизаторам вместе со своими соплеменниками. Но, поскольку силы были неравные, Мквава потерпел поражение и предпочел смерть унижению от врага.

  • Еще одну героическую страницу в историю антиколониальной борьбы в Восточной Африке вписали участники восстания Маджи Маджи (vita vya Maji Maji) в период 1905-1907 годов. В этом движении как никогда ранее проявился дух единения народа Танганьики. Около 20 народностей южных районов страны, объединившись, выступили против германских колонизаторов. К сожалению, им не хватило четкого руководства и хорошей организации, и восстание было жестоко подавлено.

  • После второй мировой войны народу Танганьики пришлось добиваться своего права на независимость у англичан, которые правили в этой стране с 1917 года. Политическая партия ТАНУ под руководством Дж. К. Ньерере довела эту борьбу до победного конца.

  • Ньерере, умерший в 1999 году, был не только выдающимся лидером своего народа, но и мудрым политиком, признанным во всем мире за его огромный вклад в дело прогресса и независимости в Африке.


8. Переведите и озаглавьте следующий текст. Перескажите его на суахили:

Baada ya waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika Julius Kambarage Nyerere kujiuzulu wadhifa huo, kazi kubwa aliyoifanya ni kuzunguka nchi nzima. Katika kazi hiyo hakuacha kijiji kikubwa wala kidogo, alifika kila pembe ya Tanganyika ambako alikuwa na jukumu kubwa la kuwaelemisha wananchi faida na jinsi ya kujiletea maendeleo yao wenyewe.

Alikuwa akitoa elimu kubwa juu ya kujitegemea ikiwa Watanganyika wanataka maendeleo ya haraka. Aliwaeleza wananchi, katika kila kijiji alichotembelea kwamba maendeleo yao yataletwa na wao wenyewe.

Mwalimu Nyerere alisema kuwa baada ya uhuru kupatikana, Tanganyika haikuwa tena na wajomba wala shangazi ambao wangeweza kuleta maendeleo.

Alieleza kuwa wakati wakoloni wakitawala kwa ufidhuli ardhi ya Tanganyika na watu wake, waliweza kuleta maendeleo kidogo, hasa sehemu ambazo waliona wana maslahi makubwa kwa ajili ya maendeleo ya nchi zao.

Ni kutokana na sababu hizo, maendeleo katika eneo moja hadi jingine yalikuwa yakitofautiana mno kufuatana na umuhimu wake kwa wakoloni. Katika mazingira hayo, maeneo ambayo yalikuwa yakitumika kwa uzalishaji wa mali kwa wakoloni yalikuwa na huduma za jamii kuliko maeneo mengine.

Maeneo yaliyokuwa yakiwazalishia mali wakoloni yalikuwa na barabara nzuri, hospitali nzuri kwa ajili yao na nyingine za hali ya chini kwa ajili ya wafanyakazi wao wanapougua. Baadhi ya maeneo ya namna hiyo pia yalikuwa na umeme, maji na nyumba nzuri walizokuwa wakiishi.

Katika maeneo ya vijijini aliyotembelea, Mwalimu Nyerere alitumia kila aina ya usafiri uliokuwepo na uliowezekana kulingana na mazingira kwa wakati huo. Alipanda punda, aliendeshwa katika baisikeli na pia alitembea kwa muda mrefu hadi anamaliza mizunguko hiyo ambayo inaelezwa ilimchukua zaidi ya miezi mitano.

Kila kijiji alichokuwa akipita, Mwalimu Nyerere alishirikiana na wenyeji katika kilimo, aliwaonyesha na kuwaelekeza namna kilimo bora kinavyoweza kuwaongezea mapato na pia alishiriki katika ujenzi wa barabara na majosho.

Kiongozi huyo wa TANU katika kuonyesha mfano, alishika jembe, alipanda mbegu, alivuna na alishiriki katika kuanza ujenzi wa majengo ya shule ama zahanati.



Katika kazi hiyo ya kuzunguka nchi nzima, Nyerere pia alijaribu kutoa ushawishi kwa wanavijiji kuishi jirani jirani ili serikali iweze kutoa huduma zinazowezekana kwa urahisi zaidi. Hili baadaye lilikuja kuwezekana na kuonyesha mafanikio makubwa.
9. Закончите следующие предложения, выбрав подходящий вариант из скобок:

  1. Utawala wa kikoloni ulianzishwa pwani ya Afrika ya Mashariki na (Waarabu; Waingereza; Wareno).

  2. Wazungu wa kwanza walifika Afrika ya Mashariki ili kuyashuhudia kwa macho mambo yake ya ajabu (karne 4 hivi nyuma; kati kati ya karne ya 19; mwanzoni mwa karne ya 20).

  3. Watu wa misheni walikuja Afrika kwa madhumuni ya (kufanya uchunguzi wa bara hili; kueneza dini ya Ukristo; kufanya biashara ya watumwa ipigwe marufuku).

  4. Mzungu aliyependwa na kuheshimiwa kuliko wote na wenyeji ni (Richard Burton; Speke; David Livingstone; Stanley).

  5. Mwaka 1890 sehemu ya pwani ya Afrika ya Mashariki ilinunuliwa na Wadachi kutoka kwa (mtawala wa Unguja; Waarabu wa Oman; wakoloni wa Uingereza).

  6. Waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika huru alikuwa (Julius Nyerere; Rashidi Kawawa; Sheikh Abeid Amani Karume).

  7. Shujaa maarufu wa Afrika aliyejulikana kwa jina la Mkwawa (alinyongwa na wanajeshi wa Kijerumani; alifungwa jela kisha akatoroka; alijiua mwenyewe asije akakamatwa).

  8. J. Nyerere aliiacha kazi ya ualimu kwa sababu alitaka (kuwa mfanya biashara; kujizamisha katika mambo ya siasa; kufanya kazi ya uhariri gazetini).

  9. Sheikh Amani Abeid Karume amepata umaarufu kati ya wananchi wote wa Unguja kwa vile (alivyokuwa baharia jasiri; alivyofundisha watu elimu mbali mbali; alivyoanzisha ushirika halisi wa wafanya kazi).

  10. Pongezi nyingi za kukomesha uovu wa biashara ya watumwa ziwaendee (Waingereza; Waarabu; Wadachi) ambao walipitisha sheria ya kuzuia biashara hiyo mnamo mwaka (1910; 1860; 1807).

  11. Watu wa kwanza wanaodhaniwa kuingia kisiwani Pemba walikuwa (Waarabu; Washirazi, Wahindi).

  12. Dini inayotawala kisiwani Pemba ni (Uislamu; Ukristo).


10. Переведите:

  1. Багамойо, бывшая столица Восточной Африки немецкого периода, находится в 75 км к северу от Дар эс Салама, на противоположном Занзибару берегу.

  2. Когда-то город Багамойо был известным центром работорговли благодаря своей хорошей природной гавани, идеальной для судоходства и мореплавания.

  3. Первым каменным зданием в Багамойо была старая тюрьма у берега океана, где под землей толпы рабов ожидали прихода арабских судов.

  4. Город Багамойо также был отправным пунктом для первых европейских исследователей на их пути к поискам истоков Нила. Такие известные исследоватили Африки, как Ливингстон, Стэнли, Бартон, Спик побывали в Багамойо.

  5. Туристов привлекает музей с замечательной коллекцией фотографий и сувениров, относящихся к Ливингстону и немецкому колониальному периоду.

  6. Башня первой католической церкви в Восточной Африке также расположена в Багамойо. Это башня носит имя Ливингстона, поскольку здесь одну ночь находилось его тело перед отправкой в Лондон.

  7. Одной из достопримечательностей Багамойо являются руины Каоле, которые состоят из развалин двух мечетей и около 30 могил.

  8. Таможня и склад также были построены немцами в конце 19 века. На развалинах склада сохранились чаши, которые когда-то были заполнены керосином для того, чтобы крысы не проникали в складские помещения.


11. Познакомьтесь с суахилийскими пословицами и переведите их. Обратите внимание на модель словообразования существительных:

  • Mchezea moto humteketeza

  • Mtaka yote hukosa yote

  • Mchimba kisima hakosi maji

  • Mchomwa mwiba haendi tena

  • Mchunga farasi usipande punda

  • Mpanda ngazi hushuka

  • Msema kweli hakosi

  • Mzoea punda hapandi farasi


12. Подготовьте сообщения на темы:

А/ Исторические этапы развития Танзании;

B/ Выдающиеся лидеры Танзании;

С/ Исторические места Восточной Африки.


Msamiati

-tafiti изучать, исследовать -kumbana na сталкиваться,

mtafiti (wa-) исследователь, наталкиваться

изыскатель upinzani (ед.) 1) оппозиция,



gofu (ma-) развалины, руины противодействие

-jionea увидеть воочию; 2) протест, сопротивление

убеждаться в чем-л. tende (-) финик



silaha (-) 1) оружие 2) орудие -wekeza инвестировать,

sambamba 1) параллельно вкладывать деньги

2) одновременно, вместе mseto (mi-) смесь,



ukanda (kanda) пояс, район, зона смешение

maingiliano (мн.) 1) связи, Ushirazi (ед.) г. Шираз

взаимоотношения Mshirazi (wa-) потомок

2) взаимопроникновение перса из Шираза

-tanua расширять, раздвигать utata (ед.) 1) неясность,

-chipuka 1) распускаться, неопределенность

прорастать (о растениях) 2) путаница, сложность

2) появляться, возникать (перен.) mapokeo (мн.) предание,

dhana (-) 1) мысль, идея; устное народное творчество

точка зрения 2) концепция mkakati (mi-) тактика



-nyanyasa глумиться, wadhifa (nyadhifa) пост,

издеваться, унижать должность



unyanyasaji (ед.) угнетение, josho (ma-) место для

притеснение умывания, стирки, мытья



* * *

VI. UTIBABU, ELIMU NA MAMBO YA DINI

Здравоохранение, образование, религия
Урок 21. Somo la ishirini na moja

Грамматика

  1. Аналитические глагольные конструкции с показателем -ki- во вспомогательном глаголе -wa.

  2. Глагол -wa в глагольных конструкциях, передающих значение “в том числе, включая” и т.п.

Вспомогательный глагол -wa в аналитических конструкциях, оформляясь показателем условного наклонения -ki-, указывает на одновременность протекания действия, выраженного смысловым глаголом придаточного предложения, с другим действием, передаваемым глаголом главного предложения. При этом смысловой глагол придаточного предложения может быть оформлен показателем -na- (многократность, регулярность действия на момент речи) или -me- (завершенность действия к моменту речи или состояние в тот момент). На русский язык такие сложные глагольные конструкции можно переводить причастиями или деепричастным оборотом. Например:

Utaweza kuona magari mengi barabarani yakiwa yanachukua abiria “Ты сможешь увидеть на улице много машин, перевозящих пассажиров”;

Yakiwa yamepandwa kwa wakati wa kufaa, maua haya hayatakosa kusitawi majira yote “Посаженные вовремя, эти цветы непременно будут цвести весь сезон”;

Akiwa amejawa na hofu Tegu alijibu “Почувствовав страх, Тегу ответил”.

Отрицание в таких конструкциях осуществляется во втором компоненте, т. е. смысловом глаголе:

Tegu, akiwa bado hawezi kusema kwa kuduwaa alimfuata baba yake “Будучи все еще не в состоянии говорить от удивления, Тегу последовал за своим отцом”.
В суахили существует несколько глагольных форм, с помощью которых можно выразить такие значения как “в том числе, в их числе, включая, среди них” и т.п. Например, конструкция глагола -wa в сочетании с показателем условного наклонения -ki- и конечным локативным релятивом -po/-mo – -kiwapo/-kiwamo (и их фонетические варианты -kiwepo/-kiwemo), где согласование осуществляется по класу существительного, о котором идет речь, и которое следует за этой глагольной формой. Например:

Safarini nimenunua vitu kadhaa ikiwamo ramani ya Kenya “Во время путешествия я купил несколько вещей, в том числе карту Кении”;

Amepata rafiki wengi akiwapo Mwafrika mmoja “У него появилось много друзей, среди них один африканец”.

В другой конструкци с тем же значением, ikiwa ni pamoja na, глагол -wa, как правило, стоит в неопределенно-личной форме. Но могут встречаться и личные формы, где согласование осуществляется по классу существительного, которое занимает препозицию по отношению к этому союзному слову. Сравните:

Amepata rafiki wengi ikiwa ni pamoja (wakiwa ni pamoja) na Mwafrika.

Надо заметить, что в обеих этих конструкциях согласование возможно по одному из локативных классов, обычно ku- или mu-. Приведем для сравнения предложение – “В его столе много разнообразных предметов, в том числе и острый нож”, которое имеет несколько возможных вариантов перевода:

Mezani mwake mna vitu mbali mbali kikiwemo (mkiwemo) kisu kikali;vikiwa ni pamoja na kisu kikali;ikiwa ni pamoja na kisu kikali; … kukiwa ni pamoja na kisu kikali.
Mazoezi

1. Переведите:

1. Nilipofika kwa mjomba wangu wakati wa likizo nilimkuta akiwa anashughulika na ujenzi wa boma la maji. 2. Katika bandari tuliwaona wapagazi chungu nzima wakiwa wanabeba mizigo na vitu vingine. 3. Walipokuwa wakiishi pwani ya bahari walizoea kuona meli za kigeni zikiwa zinapakua na kupakia bidhaa mbali mbali. 4. Nikiwa nimejaa furaha tele kwa ajili ya zawadi niliyonunuliwa nikamkimbilia mamangu na kumbusu. 5. Ukiwa umepotea njia uwaulize wenyeji au usipowakuta, tumia simu ya mkono niliyokupa ukaniulize mimi. 6. Alifanya hatua nyingine kadhaa akasimama akiwa hajui la kufanya kwa jinsi alivyoshtuka kumwona joka mkubwa ajabu akiwa anamsogelea pole pole. 7. Usimsumbue kaka yako kwa maswali ya kipumbavu akiwa anajiandaa kwa kupasi mitihani ya chuo kikuu. 8. Afadhali wajifunze namna ya kutumia kompyuta wakiwa wanajifunza bado na wenye uwezo wa kufahamu mambo upesi upesi. 9. Tutashindwa kuukamilisha ujenzi wa daraja hili tukiwa tumeishiwa na pesa zote.


2. Переведите предложения, используя формы -kiwamo/ -kiwapo или -kiwa ni pamoja na:

1. Каждое утро я читаю все газеты, которые мне приносят домой, включая и газету “Ухуру”. 2. Рабочие, объявившие забастовку, требовали предоставить им больше прав, в том числе право на бесплатное лечение. 3. В своем выступлении главный врач подчеркнул некоторые актуальные вопросы, в том числе и проблему отсутствия средств на строительство родильного дома. 4. Принимая присягу, новый президент обещал сделать важные шаги, включая меры по предотвращению экономического кризиса. 5. В этой маленькой стране есть много полезных ископаемых, включая медь и золото. 6. Он объявил о своей добровольной отставке, называя много причин, среди них несогласие с политикой, проводимой правящей партией.


USITAWI WA MAMBO YA UTIBABU

Uganga ni kitu ambacho watu wa kila sehemu ulimwenguni walikuwa nacho tangu awali. Babu zetu walishambuliwa na magonjwa pia. Toka hapo kale babu zetu walitumia dawa za miti shamba kuponya maradhi au kupunguza maumivu. Kwa vile maisha yao yalikuwa ya taabu taabu iliwabidi wajue dawa nyingi. Walijua dawa za kuponya mtu akiumwa na nyoka, tandu au nge. Walijua dawa za kuponyesha maumivu ya tumbo au kichwa. Inasemekana pia kuwa walijua dawa za magonjwa kama kichaa au kurukwa akili.

Hapo kale uganga ulikuwa ni kazi iliyorithiwa. Mtoto mkubwa wa mganga alirithi uganga wa baba yake na akiwa yungali hai*, baba huyo aliambatana sana na mtoto wake mkubwa, mara nyingi wa kiume, ili amwonyeshe jinsi sayansi ya kuponya maradhi ilivyokuwa inaendeshwa na miti shamba ambayo ilitumiwa kuponya maradhi mbali mbali. Bila ya shaka wataalamu wa siku hizi wangelipenda kudadisi kama kweli miti shamba hiyo ilikuwa ni dawa ya maradhi fulani.

Jitihada kubwa ilifanywa na serikali ya Wadachi kuanzisha na kusitawisha mambo ya utibabu wa kisasa nchini. Idara ya utibabu ilianzishwa kwa mara ya kwanza na Wadachi tarehe 1 Aprili, 1891 wakiwapo madaktari watano na watumishi wa hospitali kumi na wanne wa Kidachi. Hospitali ndogo ndogo kadha wa kadha zilianzishwa katika sehemu kubwa ya Tanganyika. Kusudi kubwa la Idara hiyo wakati huo lilikuwa kutibu watumishi wa serikali, lakini pia ilitambulikana kwamba mipango ya kuweka kinga kwa magonjwa ni ya muhimu sana katika maendeleo ya uchumi wa nchi.

Kazi iliyoikabili Idara ya utibabu ilikuwa kubwa sana lakini ukosefu wa fedha ulizuia upanuaji wa kazi hizo. Hali ya usafi na kanuni za afya zilikuwa mbaya sana hasa katika miji mikubwa ya Tanga na Dar es Salaam. Lakini kwa ajili ya ukosefu wa fedha, mifereji ya maji na kazi za kuondoa uchafu na kuua mbu hazikuweza kuongezwa.

Vita kuu ya pili pia ilizuia maendeleo ya Idara ya utibabu. Madaktari kumi na mmoja walichukuliwa vitani na kazi zote za dawa zilipunguzwa. Lakini wagonjwa walizidi sana kwenda hospitali kupata matibabu. Ingawa hivyo yalikuwapo mafanikio mema fulani. Kazi iliyokuwa ya maana sana ilikuwa ni kutiliwa mkazo kwa ubora wa chakula kizuri kwa mwili na magonjwa yanayotokana na kutokula chakula cha kutosha na cha kufaa.

Baada ya vita, Idara ya utibabu ilifanya maendeleo mazuri ingawa mambo mengine mabaya, kwa mfano kuwa na hospitali mbali kwa Wazungu, yalikuwa bado yapo. Kazi za dawa hazikutosheleza mahitaji ya watu kwa vile ambavyo watu wengi walikwenda hospitali kutibiwa na kuacha miti shamba. Fedha iliyoongezwa haikutosha kununua vifaa vya hospitali na pia haikutosha kupanua shule za kufundishia waganga. Licha ya fedha, hawakuwapo watu wa kutosha wenye elimu iliyotakiwa ili wachukue mafunzo mbali mbali ya uganga. Kazi za utibabu hazikuweza kuendelea pasipo Waafrika wenyewe kupewa ujuzi na madaraka katika kila daraja la wauguzi. Manesi na madaktari Waafrika wengi walitakiwa.

Katika mwaka 1951 halmashauri ya mafunzo ya waganga ilianzishwa. Mafunzo ya miaka mitatu ya wasaidizi wa madaktari yaliendelea Dar es Salaam wakiwa wanachukuliwa wanafunzi waliohitimu darasa la kumi. Mafunzo ya miaka miwili kwa wasaidizi wa madaktari katika hospitali za shamba, yaliendelea Mwanza. Kwa shule ya Mwanza walichukuliwa wanafunzi waliohitimu darasa la nane.

Lakini kwa upande wa kuzuia magonjwa maendeleo hayakuwa makubwa. Mahitaji ya kuwapo** kwa vituo vya kutolea dawa na kuzuia magonjwa katika sehemu za shamba na pia kwa ajili ya kutolea elimu ya mambo ya usafi na afya nzuri yalikuwa makubwa sana. Vituo hivyo vingalikuwa vinatoa dawa na kuwa na vyumba vidogo vya kulaza wagonjwa, vyumba vya kuzalishia na sehemu za kuangalia afya ya watoto wachanga, na pia vyumba vya kutolea mafunzo ya elimu ya usafi na afya. Ilitazamiwa kuwa hatimaye vituo hivyo vingelikuwa badala ya hospitali ndogo.

Katika mwaka 1960 hospitali kubwa ilifunguliwa mjini Dar es Salaam, yaani hospitali iitwayo Muhimbili sasa. Palikuwa pia na hospitali arobaini na nane nyingine za serikali, hospitali kwa matibabu maalumu sita na hospitali ndogo ishirini.

Toka wananchi waanze kushika madaraka ya serikali mwaka 1960 jambo la ubaguzi kwa wagonjwa lilianza kuondolewa pole pole. Hata uhuru ulipofika hapakuwa na hospitali za Wazungu tena. Hospitali zilianza kutibu watu wa rangi yo yote kama ilivyotaka sheria ya serikali. Kwa mfano, hospitali ya ‘Ocean Road’ mjini Dar es Salaam ilianza kuitwa hivyo baada ya kukomesha ubaguzi huo. Zamani ilikuwa inaitwa hospitali ya Wazungu.

Wananchi wengi watumishi wa serikali walipata vyeo vya madaraka makubwa katika Idara ya utibabu toka juu mpaka chini na toka Dar es Salaam mpaka katika miji midogo mingine iliyoko bara. Mipango ya baadaye iliendelea kutegemea kuwapo** kwa fedha na wataalamu, wananchi wengi walizidi kwenda nchi za ng’ambo kujifunza mambo ya utabibu wa aina mbali mbali. Na misheni zilizidi kushirikiana na serikali bega kwa bega katika kuyapiga vita maradhi. Wananchi pia walizidi kutambua faida ya hospitali na walianza kujitolea kujenga majumba ambayo walitaka yatumike kama hospitali katika vita ya kupigana na maradhi.

Wakati huo ulikuwa muda wa jitihada nyingi za kufanya jambo lo lote la kuinufaisha nchi yetu kwa kadiri inavyowezekana. Tanganyika mpya ilihitaji kila raia aone kuwa ana wajibu na yu sehemu ya wajenzi wa taifa jipya.

1   ...   11   12   13   14   15   16   17   18   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət