Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə12/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   8   9   10   11   12   13   14   15   ...   25

4. Переведите:

  1. До независимости в Танганьике строилось очень мало предприятий обрабатывающей промышленности.

  2. В горнодобывающей промышленности добыча алмазов и золота занимает ведущее место. Один из самых известных алмазных рудников находится в Мвадуи.

  3. Танзания импортирует не только машины и оборудование, но также закупает потребительские товары и продовольствие.

  4. Особое место во внешней торговле Танзании занимают соседние африканские страны, особенно Кения и Уганда.

  5. На международной ярмарке, открывшейся на этой неделе в Дар эс Саламе, павильон министерства сельского хозяйства этой страны был отмечен как один из лучших.

  6. К участию в выставке были привлечены государственные компании и частные предприниматели, а также представители кооперативного движения из многих зарубежных стран.

  7. После подведения итогов победителям конкурсов в торжественной обстановке были вручены призы и различные памятные сувениры.

  8. В Танзании еще недостаточно асфальтированных или бетонных дорог, хотя в последнее время индустрия дорожного строительства заметно шагнула вперед.

  9. Это явилось результатом не только помощи извне, но и усилий центрального правительства и руководителей областного уровня, нацеленных на развитие этой важной отрасли национальной экономики.

5. Переведите и перескажите на суахили следующую притчу:

Pelelezeni mambo

Kwanza watu walifikiri dunia ni sawasawa kama meza ilivyo, kumbe, walipozidi kupata maarifa waliona kuwa ni mviringo! Kwanza watu walifikiri jua ndilo linalopanda na kushuka, kumbe, ni dunia inayozunguka! Basi, tusikae kimya tukikubali mambo tuliyofikiri kuwa ya kweli tulipokuwa hatujaanza kusoma, bali lazima tuendelee kila siku tukijaribu kupata maarifa zaidi. Tena, tukipata kujua elimu kidogo, tusifikiri ya kuwa tumekwisha hitimu na kujua elimu zote za dunia. Nakuambieni sasa ya kuwa hakuna mtu ye yote dunia nzima aliyekwisha hitimu na kupata elimu zote. Tunapata elimu kidogo tu, yaani ile tunayofundishwa na ile tunayoigundua sisi wenyewe, lakini ziko nyingi za namna nyingi sana. Kweli tumekuwa kama vipofu sita waliokuwa na hamu ya kujua tembo ni kama nini.

Walikuwapo vipofu sita, nao kila mara walikuwa hodari sana katika kupata habari za mambo yote. Siku moja walikwenda wapate kujua tembo ni kama nini.

Kipofu wa kwanza alimkaribia tembo, na kwa bahati alijikwaa, akaanguka mbavuni mwa tembo. Akampapasa mbavuni, akasema “Lo! Tembo amefanana na ukuta wa nyumba!” Wa pili akamkaribia tembo akaishika pembe yake, akaipapasa, akasema “Ah! Ni nini hiki? Naona kitu laini chenye ncha! Kumbe, tembo ni kama mkuki!” Wa tatu akaja akaushika mkonga wa tembo mkononi mwake, akaupapasa, akaukunja na kuukunjua, akasema “Ehe, sasa nimekwisha jua tembo ni kama nini. Hakika ni kama nyoka!” Sasa yule wa nne akaja, na kwa kuwa alikuwa mfupi, akamshika tembo gotini, akampapasa gotini, kisha akasema “Kumbe, huyu mnyama anayesifiwa kuwa wa ajabu sana ni kama mnazi tu!” Wa tano alikuwa mtu mrefu, akaja akamshika tembo sikio, akalichezea kidogo, kisha akasema “Mtu awe kipofu wa namna gani, lakini ataweza kujua mara ya kuwa tembo amefanana na upepeo!” Wa sita alikuja nyuma ya tembo, akamshika mkiani, akauchezea mkia, akasema “Ha! Ni hivyo, kumbe, tembo ni kama kipande cha kamba!”

Basi, wale vipofu sita walianza kubishana kwa muda mrefu, na kila mtu aliyashikilia maneno yake mwenyewe. Kumbe, aliyoyasema kila mtu yalikuwa kweli, lakini nusu ya kweli tu!

Basi, hayo ndiyo mafundisho ninayotaka mjifunze: Tukijua kidogo tusijivune tukatangaza kila mahali jinsi tulivyo watu wenye maarifa yote, ila tuzidi kupeleleza mambo. Labda tutaona kuwa yale tunayoyajua ni nusu ya kweli tu, kama walivyojua wale vipofu sita!


6. Выскажите свое мнение по поводу этой притчи.
7. Дайте эквиваленты на суахили:

находиться в руках белых поселенцев; добыча полезных ископаемых; золотые рудники; заниматься розничной торговлей арахиса; обнаружить запасы железной руды; вялая торговля; нехватка рабочей силы; намеренно сдерживать развитие местной промышленности; успешно выполнить поставленную задачу; быть круглой формы; получать разносторонние знания; достичь северного полюса; ровный асфальт; придерживаться своего мнения.


8. Отгадайте загадки, выбрав подходящий ответ из приведенных ниже подсказок:

  • Upande wo wote umjiao atakuona.

  • Utahesabu mchana na usiku na hutamaliza kuhesabu.

  • Yaenda mbali lakini haiondoki ilipo.

  • Twamsikia lakini hatumwoni.

  • Ni kitu gani kutoa ni kuongeza.

  • Ndugu wawili wafanana sana, lakini hawatembeleani.

  • Nikitembea yuko, nikikimbia yuko, nikiingia ndani hayupo.

  • Kuku wetu hutagia mayai mikiani.

  • Kina mikono na uso lakini hakina uhai.

  • Hachelewi wala hakosei safari zake.

[matunda; macho; jua; kinyonga; sauti, kivuli; saa; njia; nywele; shimo]
9. Подготовьте на суахили сообщения на темы:

А/ Экономика ОРТ; В/ Экономика РФ.


Msamiati

setla (ma-) поселенец almasi (-) алмаз; бриллиант

-jishughulisha заниматься (чем-л.) -jikwaa спотыкаться

uchimbaji (ед.) разработка, добыча laini гладкий; ровный

ncha (-) 1)острие; наконечник mkonga (mi-) хобот

2) оконечность machimbo (мн.) шахта;



upepeo (pepeo) веер; опахало карьер; рудник

kusudi, kusudio (ma-) цель, jaribio (ma-) 1) попытка

намерение 2) эксперимент



kusudi [для того] чтобы njugu (-) земляной орех,

makusudi [пред]намеренно, арахис

умышленно mviringo (mi-) круг,



-shikilia придерживаться (чего-л.) окружность

maarifa (мн.) 1) знания 2) опыт rejareja в розницу

* * *

V. KURASA ZA HISTORIA

Страницы истории
Урок 17. Somo la kumi na saba

Грамматика

  1. Инфинитивный оборот в начале предложения.

  2. Союз kwa jinsi в придаточных предложениях причины.

Глагол в инфинитивной форме может стоять в начале предложения, обозначая действие, выполненное субъектом непосредственно перед началом другого действия. На русский язык такой инфинитив с дополнением или обстоятельством чаще всего переводится деепричастным оборотом либо придаточным предложением времени:



Kusikia hayo akarudi “Услышав это, он вернулся”;

Kufika mjini alimpigia simu mwenzake “Как только он приехал в город, он позвонил своему другу”;

Kumwona polisi mwizi akajificha nyuma ya gari “Увидев полицейского, грабитель спрятался за машиной”.

Близкой по смыслу является конструкция инфинитива в сочетании с предлогом baada ya либо личная глагольная форма с релятивом времени -po- или с показателем условного наклонения -ki-:

Baada ya kusikia (aliposikia, akisikia) hayo akarudi nyuma;

Следует заметить, что употребление инфинитива в начале предложения всегда обусловлено контекстом прошедшего времени, в то время как названные выше синонимичные конструкции могут употребляться в более широком контексте. Сравните:

Kuja nyumbani nilianza kupika “Придя домой, я начала готовить”;

Baada ya kuja (nitakapokuja) nyumbani nitaanza kupika “Как только я приду домой, я начну готовить”;

Nikija nyumbani mara naanza kupika “Приходя домой, я сразу начинаю готовить”.
Как известно, придаточные предложения причины в языке суахили вводятся с помощью союзов kwa sababu, kwa vile, kwa kuwa, kwani, maana. Слово jinsi “способ, метод” с предлогом kwa (а иногда и без него) приобретает значение, синонимичное этим союзам. Однако особенностью союза kwa jinsi является то, что глагол придаточного предложения при этом обязательно оформляется релятивом образа действия -vyo-. Сравните:

Hakuenda kutembea kwa jinsi mvua ilivyoanza и Hakuenda kutembea kwa sababu (kwa vile, maana) mvua ilianza “Он не пошел на прогулку, так как начался дождь”;



Kwa jinsi safari ilivyokuwa ndefu tumechoka mno и Kwa kuwa safari ilikuwa ndefu tumechoka mno “Поскольку путешествие было долгим, мы очень устали”;

Mtoto hakuruhusiwa kuogelea mtoni kwa jinsi alivyo mdogo bado и Mtoto hakuruhusiwa kuogelea mtoni kwani ni mdogo bado “Ребенку не позволили купаться в реке, потому что он еще слишком мал”.

Глагол придаточного предложения с союзом kwa vile также может быть оформлен релятивом -vyo- (kwa vile mvua ilivyoanza, kwa vile safari ilivyokuwa ndefu).

Релятивный формант может быть вынесен и в союз amba-: kwa jinsi ambavyo mvua ilianza, kwa jinsi ambavyo safari ilikuwa ndefu, kwa jinsi ambavyo mtoto ni mdogo.

Негативные конструкции с союзом kwa jinsi строятся соответственно по правилам отрицания релятива:

Alikataa kushiriki mchezo kwa jinsi asivyopenda mpira wa miguu (или kwa jinsi ambavyo hapendi mpira wa miguu) “Он отказался участвовать в игре, поскольку не любит футбол”.



Mazoezi

1. Переведите:

1. Kufika klabuni alimkuta rafiki yake wa tangu zamani. 2. Kusikia maneno yake makali Mariamu alianza kutokwa na machozi. 3. Kuona mambo yameanza kuchafuka aliamua kuhamia kwingineko. 4. Kufungua tu mfuko wake Roza alifahamu kwamba ameibiwa fedha zote. 5. Kuambiwa hayo tulikata shauri kubaki mahali hapa hapa. 6. Kuwasili stesheni nikafanya haraka kujinunulia tiketi ili kuiwahi treni. 7. Kufika bandarini meli imefunga gati na imeanza kupakuliwa bidhaa.


2. Переделайте инфинитивный оборот предложений в предыдущем задании, не меняя смысла.
3. Переведите предложения, употребив инфинитивный оборот:

1. Когда мы приехали в саванну, нас встретил руководитель тургруппы. 2. По прибытии в аэропорт нас попросили предъявить паспорта и билеты и взвесить багаж. 3. Выбежав на улицу, дети тут же начали играть в футбол. 4. Приехав в чужой город, они взяли такси и попросили отвезти их в недорогую гостиницу. 5. Открыв дверь, она увидела, что перед ней стоят ее родители. 6. Придя на рынок, хозяйка с удивлением обнаружила, что цены на овощи резко поднялись. 7. Закончив ужинать, они сразу пошли в сад, чтобы подышать свежим воздухом. 8. Быстро купив все необходимое, мы отправились в путь. 9. Я очень устал и, закрыв глаза, тотчас же уснул.


4. Замените предложения с союзными словами kwa sababu, kwa vile, kwa kuwa, kwani, maana синонимичными с союзным словом kwa jinsi:

1. Hakufika masomoni kwa vile alivyokuwa mgonjwa. 2. Hatukununua viazi sokoni kwa sababu vilikuwa vibovu sana. 3. Umwambie mtoto wako asicheze na mbwa yule maana ni mkali. 4. Hamwezi kujiunga na mchezo huu sasa kwa vile mmechelewa kuja. 5. Tawi la mti limeanguka chini kwa sababu limekauka. 6. Alishindwa kuuvuka mto ule kwani hajui kuogelea. 7. Wamakonde huchonga sanamu za kupendeza sana kwa vile ni mabingwa hodari. 8. Wamasai hawapendi kulima kwa kuwa wamezoea kuhamahama. 9. Waarabu walifika pwani ya Afrika ya Mashariki kwa sababu walitaka kugundua sehemu mpya za kufanya biashara. 9. Mlima Kilimanjaro huitwa mnara wa Afrika maana ni mrefu sana.


5. Переведите, употребив союзное слово kwa jinsi:

1. Он не смог перевести текст, поскольку у него не было словаря, а текст был очень трудный. 2. Дерево упало от сильного ветра, так как было очень старым. 3. Гости не могли общаться с танзанийцами, потому что не знали языка суахили. 4. Работорговлю запретили, потому что она была очень жестокой и несправедливой. 5. Люди народности чагга получают высокие урожаи, поскольку они являются хорошими земледельцами. 6. Европейцы предпочитают жить в Кении, потому что климат в этой стране холоднее, чем в Танзании. 7. Отец пришел сегодня рано, потому что у него не было много работы. 8. Они прошли полпути и остановились, так как не знали, куда идти дальше.


HISTORIA FUPI

Tanganyika ikiwa ni sehemu ya Afrika ya Mashariki ilitembelewa na wageni hata hapo kale; sehemu zilizotembelewa hasa ni zile zilizo pwani. Wagiriki walitembelea pwani ya nchi yetu na wafanya biashara wakitoka Arabia, Uajemi na Bara Hindi walitembelea pwani za nchi yetu hata kabla ya kuzaliwa Kristo. Utawala wa kikoloni ulianzishwa na Waarabu toka Oman katika karne ya nane katika sehemu ya pwani; pwani hizo ni sehemu zenye bandari za biashara nzuri.

Safari ya Vasco da Gama ya kuizunguka Rasi ya Tumaini Jema mwaka 1498 ilifuatiwa na kuanzishwa kwa makazi au miji mipya ya Wareno na muda wa miaka mia mbili iliyofuata Wareno na Waarabu walipigana pigana sana – kila mmoja alitaka kuitwaa nchi yetu na sehemu nyingine za Afrika ya Mashariki.

Mnamo mwaka 1725 Wareno walishindwa na Waarabu ambao walikuwa wamekwishaiteka ngome yao ya Mombasa katika mwaka 1698. Hatimaye pwani yote ya Afrika ya Mashariki ilitwaliwa na Waarabu na ikawa sehemu ya himaya ya Oman.

Ijapokuwa Wazungu walikuwa wamekwisha fika katika nchi za pwani ya Afrika ya Mashariki mamia ya miaka nyuma, lakini hawakujua kabisa habari za nchi za bara. Walikuwa wamekwisha sikia hadithi za maziwa makubwa na milima mirefu tangu zamani, lakini habari zote walizozisikia zilikuwa kama hadithi tu, wala hapana mmoja aliyekwenda* kushuhudia kwa macho yake, mpaka kati kati ya karne ya 19.

Kati kati ya mwaka 1800 na 1850 mambo mawili yalitokea yaliyovuta sana habari za nchi za Afrika mbele ya watu wa Ulaya. Kwanza safari za Wazungu waliotaka kuvumbua mahali panapoanzia mto unaoitwa ‘Nile’, na la pili, kupigia marufuku ile biashara ya watumwa. Katika habari hizo, Waingereza ndio walioongoza mambo.

Jambo jingine lililokuwa na nguvu katika kufunua nchi za bara na kuwaanzisha Wazungu waingie katika nchi za bara na kuvumbua habari zake, ni watu wa misheni waliotaka kueneza habari za dini ya Kikristo, maana mpaka wakati huo walikuwa hawajatuma watu katika Afrika ya Mashariki.

Katika mwaka 1857 Waingereza wawili mmoja jina lake Richard Burton na wa pili Speke, walifika Bagamoyo. Kisha wakasafiri mpaka Unyamwezi, na kutoka huko waliendelea mpaka kufika Ziwa Tanganyika. Hapo Speke alimwacha Burton akashika safari yake** kwenda kaskazini akavumbua ziwa lile ambalo sasa linaitwa Ziwa Victoria, lakini Burton hakukubali kuendelea katika safari hiyo ya kuvumbua nchi hizo, wakarudi tena pwani. Katika mwaka 1860 mpaka 1861, Speke alirudi tena Afrika akasafiri akavumbua nchi zilizo karibu na Ziwa Victoria.

Huku nyuma*** Mwingereza mmoja jina lake David Livingstone alikuwa akisafiri katika nchi zilizo kati kati ya kusini mwa Afrika ya kati kati. Alifanya safari yake ya kwanza katika mwaka 1851, na katika mwaka 1859 alivumbua ziwa ambalo sasa laitwa Ziwa Nyasa. Hapo alishuhudia biashara ile ya watu waliokuwa wakinunua watumwa, akaona jinsi ilivyo mbaya kabisa, na moyo wake ulijaa huzuni. Basi alirudi Ulaya akawapasha habari watu wa misheni za Ulaya akawaomba wapeleke watu wao katika nchi hizi kwa ajili ya kuwasaidia wenyeji wa nchi na kuwalinda. Kisha yeye mwenyewe alirudi Afrika.

Watu wa Uingereza hawakupata habari zake kwa muda mrefu, wakafikiri kuwa amepotea au amekufa. Basi watu walipelekwa ili waje kumtafuta, na Stanley ndiye aliyekuwa mkubwa wa safari hiyo. Basi kufika Ujiji katika mwezi wa Novemba 1871 Stanley na watu wake walimkuta Livingstone mgonjwa sana. Stanley alijaribu kumshawishi Livingstone arudi pamoja naye, na ijapokuwa alikuwa mgonjwa sana, lakini kwa vile alivyokaza nia yake kumaliza kazi yake ya kuvumbua nchi, hakukubali kurudi. Katika safari zake za siku hizo aliugua sana, akafariki dunia katika mwezi wa Mei 1873. Watumishi wake wa Kiafrika walimpenda sana, wakajua namna alivyopenda nchi hii, basi walipasua maiti yake wakatoa moyo wake wakauzika huko huko, maana walifikiri, ingawa amekufa na maiti yake itachukuliwa Ulaya, lakini moyo wake utakuwa daima katika nchi hii aliyoipenda mno.

Katika mwaka 1885 Wadachi waliitwaa nchi yetu, eti**** kama wadhamini wa wananchi. Pwani yenye upana wa maili kumi ilikuwa bado iko chini ya himaya ya mtawala wa Unguja na ilitambuliwa hivyo na serikali ya Wadachi.

Katika mwaka 1889 palikuwa na mapigano baina ya Waarabu na Wadachi. Waarabu walianza kutia mashaka kwamba kuingiliwa na utawala wa Kidachi kungelikomesha biashara yao ya utumwa. Lakini Waarabu walipigwa na kushikishwa adabu zao. Mwaka 1890, ile pwani yenye upana wa maili kumi ilinunuliwa na Wadachi kutoka kwa mtawala wa Unguja. Baadaye, mwaka 1905 wananchi walianza fujo zao pia kwa jinsi utawala wa Kidachi ulivyokuwa wa kikatili mno. Wananchi pia walishindwa mwaka 1906 katika vita ijulikanayo kwa jina la ‘Vita ya Maji Maji’.

Baada ya vita kuu ya kwanza, Uingereza iliitwaa nchi yetu kwa idhini ya mkataba wa Umoja wa Mataifa wa siku hizo.

Baada ya vita kuu ya pili, Waingereza walipewa mamlaka ya kuitawala Tanganyika kwa mkataba wa udhamini wa Umoja wa Mataifa mpya.

Uchaguzi uliofanywa mwaka 1960 uliwapa wananchi idadi kubwa zaidi ya wajumbe wa Baraza la kutunga sheria, ambalo baadaye lilianza kuitwa Baraza la Taifa. Mwezi Machi, 1961, mkutano wa katiba ya Tanganyika ulifanywa mjini Dar es Salaam. Mkutano huo ulikubali nchi yetu ipate serikali ya madaraka kamili kwa mambo ya ndani tarehe 1 Mei, 1961 na uhuru wake kamili tarehe 28 Desemba, 1961. Baadaye tarehe ya kupata uhuru kamili ilibadilishwa na ilikubaliwa kuwa nchi yetu iwe huru tarehe 9 Desemba, 1961. Waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika huru alikuwa ni mheshimiwa Julius K. Nyerere.
Maelezo

*Локативная форма hapana, hakuna, hamna соответствует настоящему времени, но в контексте события в прошлом на русский язык переводится глаголом в прошедшем времени: “не было никого, кто поехал…”. Это помогает избежать сложных грамматических конструкций, особенно в разговорной речи, поскольку достаточно того, что указание на прошедшее время содержится в основном глаголе (aliyekwenda). Другие примеры:

Hapana aliyecheka “Не было никого, кто бы смеялся”;

Hamna ye yote kati yenu aliyetafsiri barabara sentensi hii “Никто из вас не перевел правильно это предложение”.
**akashika safari… имеет контекстуальное значение “отправился…”. Сравните выражение akafunga safari.
***huku nyuma имеет значение “раньше”, “ранее”, “прежде”. Сравните синонимичное выражение huko nyuma, имеющее дополнительные значения – “сзади”, “позади”.
****Eti/ati - слово, передающее сомнение по поводу какого-либо утверждения. Оно переводится как “якобы”, “будто бы”, “как будто”. Часто это слово стоит перед изложением чьих-либо слов или цитатой, когда автор хочет подчеркнуть сомнение по отношению к сказанному:

Wanasema kuwa yeye ati ni mwizi “Они говорят, будто он вор”.


Mazoezi

6. Дайте русские эквиваленты:

wafanya biashara wa Bara Hindi; kabla ya kuzaliwa Kristo; -anzisha utawala wa kikoloni; safari ya kuizunguka rasi; -teka ngome ya kiadui; sehemu ya himaya; -shuhudia mambo kwa macho yako mwenyewe; mjumbe wa baraza la kutunga sheria; -chaguliwa kuwa balozi wa Umoja wa Mataifa; -vumbua mahali panapoanzia mto; -piga marufuku biashara ya watumwa; watu wa misheni; -eneza habari za dini; -ongoza mambo; moyo ulijaa huzuni; -pasha habari; walimkuta mgonjwa sana; -kaza nia; -fariki dunia; wadhamini wa wananchi; -tia mashaka; -shikisha adabu; utawala wa kikatili; -anza fujo; kwa idhini ya mkataba; -pewa mamlaka ya kuitawala nchi; mkataba wa udhamini; -jitawala kwa mambo ya ndani; lugha ya Kiajemi.


7. Переведите:

1. Эти события происходили до нашей эры. 2. Европейцы основали новые поселения. 3. Они хотели прибрать к рукам чужие земли. 4. Страна стала подмандатной территорией. 5. Мы все увидели своими собственными глазами. 6. Они требовали запретить работорговлю. 7. Исследователям удалось обнаружить новое озеро. 8. Европейские миссионеры пришли туда в конце 19-го века. 9. Вы не должны распространять ложную информацию. 10. Собрав все необходимое, они смело отправились в путь. 11. Еще раньше он сообщил нам важные новости. 12. Вы были свидетелями того, как они дрались? 13. Мы настойчиво уговаривали своих друзей вернуться. 14. Отважный путешественник неуклонно шел к своей цели. 15. Главари преступников организовали беспорядки. 16. Англичане получили права на владение этой территорией с согласия ООН. 17. Он не хотел терять свои полномочия.


8. Ответьте на вопросы к тексту:

1. Tanganyika ilikuwa inatembelewa na wageni gani hapo kabla ya kuzaliwa Kristo? 2. Kwa nini Waarabu toka Oman walianzisha utawala wao pwani ya Afrika ya Mashariki? 3. Ni sababu gani iliyowafanya Wareno na Waarabu kupigana sana kwa muda mrefu? 4. Wazungu walifika lini katika Afrika ya Mashariki? 5. Ni nani miongoni mwa Waingereza waliokuwa wavumbuzi wa kwanza wa Afrika ya Mashariki? 6. Ni nani hasa kati ya wavumbuzi wa Ulaya aliyependwa sana na Waafrika na kwa nini? 7. Wadachi walifika lini katika Tanganyika? 8. Waarabu walikuwa wakiwaogopa Wadachi kwa sababu gani? 9. Historia ya Tanganyika iliendeleaje baada ya vita kuu ya kwanza na ya pili ya dunia? 10. Tanganyika ilipata lini uhuru wake kamili? 11. Nani alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika huru?


9. Расскажите на суахили об основных этапах истории Восточной Африки.
10. Переведите:

1. Не было никого, кто согласился бы выполнить эту сложную работу. 2. Никто не ответил на мой звонок. 3. Ни один закон не позволял использовать наемный труд детей. 4. Бывали дни, когда мы брали лодку и плавали на дальний остров. 5. Не было ничего, что напоминало мне о том страшном случае. 6. Ничто не угрожало его жизни в то время. 7. Были времена, когда наш народ мужественно сражался за независимость. 8. Была серьезная причина, которая заставила их изменить маршрут. 9. Я помню, были радостные дни, когда мы все вместе собирались в доме у дедушки.


11. Переведите следующий текст:

Mkwawa shujaa

Hapo zamani palikuwa na mzee akiitwa Muyugumba. Mzee huyo alikuwa mtemi wa Wahehe. Alikuwa akipendwa sana na watu wake.

Mtemi Muyugumba alikuwa na watoto wengi. Wawili kati yao walikuwa Mkwawa na Muhenga. Siku moja aliwaita watoto hao wawili ili kuzungumza nao. Walipofika aliwaambia, “Wanangu, nimewaiteni usiku huu wa leo niwaeleze habari muhimu sana. Kwanza, mnajua kwamba mimi nimekuwa mtemi wa nchi hii kwa muda mrefu. Nimeweza kuwaunganisha watu wangu mpaka tumekuwa na kauli moja. Kwa ajili ya umoja wetu, tumeweza kuwashinda maadui wetu. Tumeweza kuhifadhi uhuru wetu. Sasa mimi ni mzee. Nguvu zinaanza kumalizika taratibu. Nimetazama katika watoto wangu wote sikumwona ambaye ataweza kuendesha kazi yangu ila nyinyi. Hivyo leo nimewaita kuwapeni usia wangu. Mimi karibuni nitakufa. Nitakapokufa nyinyi mtaitawala nchi hii. Kwa hiyo, wewe Mkwawa utakuwa mtemi wa Kaskazini; nawe Muhenga utakuwa mtemi wa Kusini ya Iringa. Ninaigawa nchi sehemu mbili ili kazi yenu iwe rahisi. Jambo kubwa ninalotaka mlikumbuke wakati wote ni kudumisha uhuru, heshima na umoja katika nchi ya Uhehe. Msiposhirikiana hamtaweza kufanikiwa; na kazi yenu itakuwa ngumu sana.” Mkwawa na Muhenga wakajibu wote kwa pamoja, “Ahsante baba. Tutafanya kama ulivyotuagiza”.

Haukupita muda mrefu, mtemi Muyugumba akashikwa na ugonjwa, akafa. Wahehe wakawa na huzuni sana kwani walimpenda sana kiongozi wao. Matanga yalipokwisha Mkwawa aliwekwa kuwa mtemi wa kaskazini ya Iringa na Muhenga kusini kama walivyousiwa na baba yao. Kwa bahati mbaya Muhenga alikuwa na choyo. Hakuridhika na sehemu yake ya utawala. Hivyo aliyaamrisha majeshi yake yamvamie Mkwawa; nayo yakamvamia. Lakini Mkwawa hakukubali. Alipigana kiume, mwisho akamshinda nduguye akawa mtemi wa nchi yote ya Iringa kama ilivyokuwa wakati wa marehemu baba yake.

Wakati wa utawala wa Mkwawa, kulitokea wageni weupe kutoka Ulaya. Wageni hao walikuwa ni Wajerumani. Walifika katika nchi yetu ili kuondoa utawala wetu wa jadi na kuweka utawala wao wa kigeni. Kwa kweli wageni hao walikuwa katili sana. Waliwaua babu zetu bila kosa lolote. Waliwapiga bakora kama wanyama. Walitumia mashamba yao, wakatengeneza mabarabara na kujenga majumba yao makubwa makubwa. Yote haya yalikuwa kwa ajili ya manufaa yao. Jambo lililokuwa baya zaidi ni kuwa waliwafanya babu zetu kuwa si binadamu kamili kama wao.

Mkwawa hakuweza kuvumilia ukatili wa Wajerumani. Hakupenda watu wake watawaliwe na wageni. Kwa hiyo, hakuwa na njia nyingine ya kufanya ila kuyakabili majeshi ya Wajerumani. Jambo la kwanza alilofanya ni kuimarisha majeshi yake. Vijana wa Kihehe walijiandikisha kuwa askari kwa wingi sana. Ili Mkwawa awape askari wake mafunzo bora ya kivita, alijenga kambi kubwa mahali pamoja panapoitwa Kalenga. Kambi hii ilizungukwa na ngome kubwa sana. Katikati ya ngome hiyo palijengwa nyumba kubwa. Hiyo ndiyo iliyokuwa makao makuu ya Mkwawa. Pia mlikuwemo nyumba za askari, mifugo na mashamba ya vyakula. Ngome hiyo ililindwa barabara na askari wa zamu usiku na mchana. Kila kijiji kilikuwa na ngome za aina hii ili kuwalinda wananchi.

Baada ya kupigana kwa muda mrefu, na Wajerumani wengi kuuawa, Mtemi Mkwawa aliweza kuwashinda Wajerumani. Lakini majeshi yake yalianza kudhoofika kwa sababu askari wake wengi waliuawa. Wajerumani walipowashika viongozi wa Wahehe waliwanyonga hadharani.

Mkwawa alipoona kwamba Wajerumani wanazidi kuimarisha majeshi yao, na kwamba walikuwa wanamtafuta ili wamwue, alitoroka na kwenda msituni. Alitoroka na askari wake wawili ambao walikuwa wamekula kiapo cha uaminifu cha kufa pamoja naye. Mara siku moja Mkwawa akajiona amezungukwa na majeshi ya Wajerumani. Alikuwa mtu shujaa ambaye hakupenda kukamatwa mateka wala kuacha mwili wake uguswe na Mzungu. Hivyo alijiua mwenyewe kwa bunduki kabla Wajerumani hawajawahi kumgusa.

Kweli Mkwawa alikuwa shujaa. Anatukumbusha kuwa babu zetu hawakupenda kutawaliwa na wageni. Hivyo walikuwa tayari kufa kuliko kutawaliwa.

1   ...   8   9   10   11   12   13   14   15   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət