Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə22/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   ...   17   18   19   20   21   22   23   24   25

-tapatapa барахтаться nargisi (-) нарцисс

-pachika прикреплять waridi (ma-) роза

* * *


VIII. LUGHA, FASIHI NA SANAA

Язык, литература, искусство
Урок 29. Somo la ishirini na tisa

Грамматика

  1. Префиксный способ образования отглагольных существительных.

  2. Аналитическая конструкция с глаголом -wa в желательно-побудительном наклонении.

Одним из продуктивных способов словообразования существительных в суахили является оформление глагольной основы префиксом класса одушевленных лиц. Эта модель словообразования используется для обозначения имен деятеля. Причем, исходной формой может служить любая глагольная основа, как простая, так и оформленная суффиксами производных форм – чаще всего пассивной, направительно-пассивной, реже стативной. Например: mhutubu “оратор” (тот, кто выступает); mpewa “получатель” (тот, кому дают); mpelekewa “адресат” (тот, кому посылают); mwathirika “пострадавший” (испытывающий влияние негативных факторов).


Из числа наиболее распространенных аналитических глагольных форм в языке суахили можно выделить конструкции, имеющие в своем составе глагол -wa в форме желательно-побудительногого наклонения и смысловой глагол, оформленный показателем перфектности -me- или показателем настоящего времени -na-. Конструкция с перфектом передает обязательность или желательность завершения действия при наличии его результата к определенному моменту. Показатель -na- подчеркивает необходимость регулярного, постоянного действия. На русский язык подобные глагольные формы можно переводить с помощью модальных слов, таких как “должен, надо, следует” или глаголов типа “требовать, настаивать, приказывать” и т.п. Например:

Watalii waliambiwa kuwa wawe wamerudi kituoni kabla ya giza kuingia “Туристам сказали, что им следует вернуться на базу до наступления темноты”;

Vyumba vyote hotelini viwe vimeandaliwa vizuri ifikapo siku ya Jumatatu “Все номера в гостинице должны быть приготовлены к понедельнику”;

Waziri anasisitiza mbuga za wanyama ziwe zinalindwa ipasavyo kutokana na majangili “Министр настаивает на том, чтобы заповедники охранялись должным образом от браконьеров”.

В отличие от простых глагольных форм с модальным значением, данные аналитические конструкции акцентируют результативность действия, ожидаемого в обозначенные временные рамки (с показателем -me-), либо его постоянство (с показателем -na-). Хотя семантически, безусловно, обе модели конструкций очень близки. Сравните: …watalii hawana budi kurudi; … vyumba lazima viandaliwe; …mbuga zinapaswa kulindwa.

Mazoezi

1. Объясните на суахили значение следующих слов:

mpewa; mwenziwa; mtendwa; mtendewa; mshiriki; mtibiwa; mtunukiwa; mpelekewa; mpendwa; mfungwa; mshtakiwa; mlengwa; mtafsiri; mhudumu; mhudumiwa; mhusika; mhukumiwa; msaidiwa; mwathirika; mdaiwa; mhutubu; mtawaliwa; mtumwa; mzaliwa.


2. Переведите, используя аналитические глагольные формы с показателем -me-:

1. Преподаватель сказал, что книги должны быть возвращены в библиотеку до 1-го июля. 2. Инженер потребовал, чтобы строители закончили крыть крышу нового дома до начала сезона дождей. 3. Нас информировали о том, что все игрушки должны быть привезены в детский сад за неделю до его открытия. 4. Опытные земледельцы знают, что для получения хороших урожаев поля необходимо пропалывать регулярно, а удобрения вносить ежегодно. 5. Рабочие этого предприятия должны проработать не менее 35-ти лет, чтобы получить право на высокую пенсию. 6. По законодательству этой страны молодые люди должны достичь 18-летнего возраста прежде, чем им разрешат заключить брак. 7. Хорошо бы вам приехать на торжества часа за два до их официального открытия, чтобы все как следует подготовить. 8. Министр здравоохранения дал указания проводить вакцинацию населения, особенно детей, на регулярной основе. 9. Цветы в моем саду должны быть надежно укрыты до наступления морозов. 10. Президент потребовал, чтобы местные законы были приведены в соответствие с Конституцией страны.


SIKU YA KISWAHILI

Mahojiano kati ya Katibu Mtendaji wa BAKITA

na mwandishi wa habari

SWALI: Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) linatarajia kuadhimisha Siku ya Kiswahili kitaifa. Kwa ufupi nini historia ya sherehe hizo na hadhira inayolengwa ni ipi?

JIBU: Kwa mara ya kwanza Siku ya Kiswahili ilizinduliwa rasmi nchini Tanzania na rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Januari 7, 1995.

Uzinduzi huo ni matokeo ya utekelezaji wa wazo lililotolewa Julai 31, 1992 katika kijiji cha Kwembe, mkoa wa Dar es Salaam na aliyekuwa wakati huo katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), hayati Horace Kolimba.

Siku hiyo kulifanyika hafla fupi ya kumpongeza Mzee Saadan Abdul Kandoro kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili hapa nchini, hasa kwa fani ya ushairi.

Katika hafla hiyo kulitolewa wito wa kuwa na siku maalum, angalau mara moja kwa mwaka ya kuwakutanisha wapenzi mbalimbali wa kila rika na kiwango ili wapate kupeana mawazo kuhusu maendeleo ya lugha ya Kiswahili ikiwa ni pamoja na kuwatambua au kuwakumbuka watu mbalimbali waliochangia kwa namna moja au nyingine katika maendeleo ya Kiswahili.

Baada ya hafla hiyo Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) zilifuatilia suala hilo na kuandaa utekelezaji wa wito huo. Miongoni mwa mambo muhimu ni kuweka bayana madhumuni ya kuwa na Siku ya Kiswahili kitaifa na utaratibu wa msingi wa kuadhimisha Siku hiyo, ikiwa ni pamoja na kutaja baadhi ya madhumuni yake.

Kimsingi kuadhimisha Siku ya Kiswahili kila mwaka ni njia mojawapo ya kufikia lengo hili ili:



  • Kuirejesha hadhi kamili ya Kiswahili kama lugha ya Taifa ya Tanzania na kitambulisho* cha Waafrika kwa jumla.

  • Kuwahamasisha na kuwaelemisha wananchi kuhusu masuala ya lugha na utamaduni ili wawe wanashiriki kwa hali na mali katika ukuzaji wa Kiswahili.

  • Kuzipa msukumo juhudi za kukuza Kiswahili na fasihi yake kwa kuwatambua na kuwaenzi wale wote waliotoa au wanaotoa mchango mkubwa katika juhudi hizo.

  • Kuihamasisha serikali na chama kinachotawala kuhusu wajibu wake wa kuikuza na kuithamini lugha ya Kiswahili ambayo pia ndiyo lugha ya Taifa.

  • Kuwakutanisha, kuwatambua na kuwatunuku wapenzi wa Kiswahili wa nchini na popote Kiswahili kinapotumika.

SWALI: Je, kuna tunzo zozote zinazotolewa kwa watu na taasisi ambazo zina mchango mkubwa katika kukuza lugha ya Kiswahili?

JIBU: Kwa kawaida huwa tunatoa tunzo mbalimbali hasa kutegemea uwezo wa fedha wa mwaka husika. Tunzo hugharimu kiasi fulani cha fedha hata kama ni ndogo namna gani. Wachina wanao usemi kwamba “Tunzo hata iwe na uzito kama wa unyoya ina thamani kubwa”. Sizungumzii thamani kwa mpewa tu, hata maandalizi ya kujua nani apewe na kwa sababu gani.

Kimsingi, huwa tunatoa Nishani ya Shaaban Robert ya Kiswahili, hii ni nishani ya dhahabu halisi na si ya kughushi ya wastani wa gramu 20 na fedha taslimu, pia huwa na Tunzo ya Mtetezi wa Kiswahili, Tunzo ya Mwanataaluma Bora wa Fasihi ya Kiswahili, Tunzo ya Kitabu Bora cha Watoto, Tunzo ya Vyombo vya Habari, Tunzo ya Mwandishi Bora wa Makala za Kiswahili na Tunzo ya Mwanafunzi Bora wa Kiswahili.



SWALI: Ni vigezo gani mlivyovitumia katika kuwateua waenziwa?

JIBU: Kuna vigezo vingi. Kwa mfano Mwanataaluma Bora wa Kiswahili hana budi awe amefanya utafiti wa kina kwa Kiswahili na kuhusu Kiswahili, awe na machapisho ya kiwango cha juu cha taaluma kwa Kiswahili au kuhusu Kiswahili.

Kitabu Bora cha Fasihi ya Kiswahili hakina budi kiwe kimechapishwa miaka miwili ya nyuma, na kwamba kiwe kwenye soko na kiwe kazi halisi ya mwandishi. Watoto nao hawakusahauliwa vitabu vyao, kitabu cha kundi hilo sifa zake zinalingana na Kitabu cha Fasihi isipokuwa hiki ni cha watoto.



SWALI: Inaelekea** kuwa juhudi za kufufua Kiswahili sasa zina mwamko katika Afrika Mashariki yote (Kenya, Uganda). Je, kuna mwaliko wowote wa kutaka kuungana na majirani hao katika kukienzi au kukithamini Kiswahili?

JIBU: Ni kweli kuwa mwamko ni mkubwa sasa kuliko hata wakati mwingine. Tumeipeleka mialiko Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Baadhi ya mialiko imekwenda moja kwa moja kupitia vyama na taasisi mbalimbali na mingine tumepitishia kwenye balozi zao. Na hata wananchi binafsi nao wamealikwa kupitia vyombo vya habari.

SWALI: Je, unaweza kuthibitisha hoja mnayodai kwamba Kiswahili kikichukua nafasi ya Kiingereza hakitakuwa na madhara katika kukuza elimu hapa nchini?

JIBU: Ni swali zuri. Kila lugha ina uwezo ule ule katika kuelezea hisia, fikra, taaluma n.k. kwa sababu ni zao la jamii yenye watu wa utamaduni unaofanana. Nina hakika na hasa kupitia tafiti mbalimbali kuwa mawasiliano bora ni yale yanayotumia lugha inayofahamika na wengi na kwa urahisi.

Leo hii, kwa mfano, ukiingia darasani katika vyuo au taasisi za elimu ya juu, utaona kuwa wanafunzi wanashindwa kujadiliana sana kwa lugha ya kigeni kuliko kwa Kiswahili. Ushiriki mzuri na bora katika somo ni ule wenye uwezo wa kuzishirikisha kwa ukamilifu pande mbili.

Kiswahili kina uwezo huo dhidi ya Kiingereza. Kiswahili kinafahamika na wengi. Hatuhitaji gharama kubwa kama tunayotumia kwa lugha ya kigeni.

Kwa hakika Kiswahili ni lugha ya taifa na ya kimataifa kwa sababu imevuka mipaka ya matumizi Afrika Mashariki. Aidha, Kiswahili kina thamani kubwa kwenye vyuo, idhaa na nchi mbalimbali duniani. Watanzania wakionee fahari Kiswahili kama vile alivyosisitiza Shaaban Robert kuwa “Titi la mama li tamu, jingine halishi hamu”***.


Maelezo

* В данном контексте слово kitambulisho можно перевести как “визитная карточка”.
** Безличная форма глагола -elekea “направляться” – inaelekea – имеет переносное значение и может переводиться на русский язык такими оборотами как “представляется, кажется, по всей вероятности” и т.п.. Возможны также варианты yaelekea, huelekea.
*** “Молоко матери вкуснее чужого”. (Буквально: “Грудь матери сладкая, другая не утолит жажды”).
Mazoezi

3. Найдите русские эквиваленты для следующих выражений из текста:

mahojiano na mwandishi wa habari; hadhira inayolengwa; siku ya Kiswahili ilizinduliwa rasmi na rais mstaafu; aliyekuwa wakati huo katibu mkuu wa CCM; kulifanyika hafla fupi; kutokana na mchango mkubwa uliotolewa; fani ya ushairi; kulitolewa wito wa kuwa na siku maalum; wapenzi wa lugha wa kila rika na kiwango; kwa namna moja au nyingine; kuwatambua au kuwakumbuka watu mbali mbali; -weka bayana madhumuni ya kuwa na Siku ya Kiswahili; -andaa utekelezaji wa wito; utaratibu wa msingi; -rejesha hadhi kamili ya Kiswahili; -shiriki kwa hali na mali; kuzipa msukumo juhudi za kukuza lugha; kuihamasisha serikali kuhusu wajibu wake; kuwatunuku wapenzi wa Kiswahili; tunzo zinazotolewa kwa taasisi; kutegemea uwezo wa fedha wa mwaka husika; -gharimu kiasi fulani cha fedha; nishani ya dhahabu halisi na si ya kughushi; vigezo vilivyotumiwa; -fanya utafiti wa kina; awe na machapisho ya kiwango cha juu; juhudi zina mwamko mkubwa; -thibitisha hoja; zao la jamii.


4. Переведите:

1. Страна отметила день независимости. 2. На какую аудиторию рассчитана эта радиопередача? 3. Официальная церемония открытия музея состоялась вчера. 4. Этот писатель внес огромный вклад в развитие литературы. 5. В области современной поэзии он большой специалист. 6. Сотрудники последовали указаниям начальника. 7. Они получили прекрасную возможность обменяться мыслями. 8. По существу, подготовка к празднику прошла успешно. 9. Задача на сегодня – восстановить полностью статус суахили. 10. Они должны участвовать в этом и словом и делом. 11. Процедура чествования и награждения победителей намечена на завтра. 12. Им вручат специальные награды. 13. Это стоит определенных денег. 14. Эта медаль не подделка, она из чистого золота. 15. С нас потребовали заплатить наличными. 16. Какие используются критерии при отборе лучших актеров? 17. Этот ученый проводил глубокие исследования. 18. Он имеет много публикаций в прессе. 19. Его призыв имеет широкий отклик. 20. Можете ли вы подтвердить ваш аргумент? 21. Язык – это продукт общества. 22. Нам следует гордиться своим языком.


5. Перескажите текст от имени корреспондента.
6. Замените притяжательный формант в подчеркнутых выражениях притяжательным местоимением, изменив конструкцию предложения.

1. Thamani ya vitabu vingi vilivyoko katika maktaba ya chuo kikuu chetu ni kwamba havina mfanowe ko kote kwengineko. 2. Ubora wa chakula cha aina ya mboga au majani na kisicho na mafuta mengi ni kwamba kinasaidia kujenga afya. 3. Umuhimu wa shughuli za kurutubisha ardhi katika maeneo yenye joto na mvua haba ni mkubwa mno. 4. Ukweli wa maneno yake juu ya hatari ya kufanya safari hiyo tuliufahamu wazi baadaye tu. 5. Ubaya wa hatua za kukata ovyo miti ya misituni unatiliwa mkazo na wataalamu kwani hiyo ni athari mbaya kwa mazingira. 6. Umaarufu wa mwandishi wa hadithi hiyo ya kusisimua umeenea kwa haraka duniani kote.


7. Переведите предложения на суахили по следующему образцу:

Значение языка суахили как языка общения народов Восточной Африки очевидно для всех.

Lugha ya Kiswahili umuhimu wake kama lugha ya kuwasiliana kwa mataifa ya Afrika ya Mashariki ni dhahiri kwa wote.
1. Охрана лесных ресурсов, нещадно эксплуатируемых на территории этих стран, активно обсуждалась на совещании экологов. 2. Строительство первых водных сооружений, представлявших собой каменные траншеи, началось в Дар эс Салааме и Багамойо усилиями арабов. 3. Территория заповедника Серенгети, расположенного на северо-западе и являющегося крупнейшим в Танзании, занимает огромную площадь в 12 тысяч кв.км. 4. Развитию туристического бизнеса, приносящего большие доходы развивающимся странам, уделялось особое внимание на международной выставке. 5. Важность защиты окружающей среды в интересах нынешнего и будущих поколений, должна быть осознана всем населением нашей страны.
8. Сделайте письменный перевод текста:

Namna lugha ya Kiswahili ilivyojengwa na kuenea

Watu wengine, na hasa wale wanaojiita Waswahili, hufikiri kuwa zamani kulikuwa na kabila moja la Waswahili kama yalivyo makabila mengine. Lakini hatuna habari zake katika habari za dunia, na huelekea kuwa halikuwako kabisa. Huelekea kuwa Waswahili ni mchanganyiko wa watu wa makabila ya Afrika na wageni wa nchi nyingine waliokuja pwani.

Tunajua kuwa Waarabu wengine walikuja wakafanya makao Lamu katika mwaka 689, na hata kabla ya wakati huo Waarabu na wageni wengine walizoea kuja huko kufanya biashara.

Waarabu wale walipokuja walikaa Lamu na nchi nyingine za pwani wakaoa wanawake wa wenyeji, yaani Wabantu, na watoto wao vile vile walioa wanawake wa Wabantu na hivyo Waarabu na Wabantu walichanganyika pamoja. Tena, baadaye Waarabu na Waajemi na wageni wengine wakaja wakafanya makwao katika nchi za pwani, na wao vile vile walichanganyika pamoja na Wabantu mpaka asili yao iliwapotea wakawa mchanganyiko tu. Basi Waarabu walikuwa na lugha yao na Wabantu walikuwa na lugha yao, ikawa watoto wao walichanganya lugha au kusema kweli waliingiza maneno mengi ya kigeni katika lugha za Wabantu waliokuwa wakikaa pwani. Ni dhahiri kuwa waliingiza maneno tu kwa sababu taratibu za lugha, yaani sarufi haikubadilika, ilidumu kuwa na taratibu au sarufi za kibantu. Waarabu walikuja kufanya biashara, ikawabidi kujifunza maneno mengine ya wenyeji, yaani Wabantu, na vile vile wenyeji walikuwa hawana budi kujifunza maneno ya Kiarabu wasiwe wajinga wanapofanya biashara nao.

Basi, hii ndiyo asili ya Kiswahili, na labda mwanzo wa kukua kwake ni mwaka 689 walipokuja Waarabu wale wakakaa Lamu. Kiswahili ni lugha ya Wabantu wa pwani wa zamani waliokaa kutoka Lamu mpaka mto Ruvuma zilizochukua maneno mengi ya Kiarabu, na Kiajemi, na Kireno na Kihindi, na siku hizi zinachukua maneno ya Kizungu.

Kwa kawaida maneno mengi yaliyochukuliwa na kuingizwa katika lugha hizo za Kibantu yalibadilishwa kidogo na yote yalifuata taratibu za sarufi ya lugha za Kibantu. Lugha za Kibantu hazikubadilika hata kidogo ila zilisitawishwa na kutukuka na kuongezeka kwa ajili ya kupata faida ya maneno yaliyotoka katika lugha za watu waliostaarabika zaidi kuliko Wabantu.

Lugha ya Kiswahili imeenea pote katika nchi hizi kwa sababu watu wa nchi hizi hutumia lugha nyingi sana na kila lugha inatumiwa na watu wachache tu. Kama watu wakitaka kukaa peke yao katika kabila lao na kuishi maisha ya kishenzi, lugha yao inawatosha, lakini wakitaka kuongea na wenzao wa makabila mengine na kustaarabika, lazima wajifunze lugha nyingine. Wakijifunza lugha ya wenzao wa kabila lililo jirani nao, basi wataweza kuongea nao kweli, lakini je, wataweza kuongea na watu wa makabila mengine? La, na hii ndiyo sababu inafaa wajifunze lugha inayojulikana na watu wengi, ndipo watakapoweza kuongea na watu wa makabila mengi. Basi, kama tulivyosema, Kiswahili ni lugha inayojulikana na watu wengi katika nchi yetu na hivyo inawapasa watu wa makabila yote wajifunze Kiswahili.

Wageni waliokuja kwa njia za pwani ndio walioleta ustaarabu na biashara na elimu katika nchi hizi, wakajifunza lugha inayotumiwa pwani, yaani Kiswahili, na kila walipokwenda kufanya biashara au kufanya makao walieneza lugha hiyo na hivi ikaenea nchi nzima.

Basi hivyo ndivyo lugha ya Kiswahili ilivyoenea na kutukuka, na kwa ajili ya maneno mengi yaliyochukuliwa katika lugha za mataifa yaliyostaarabika, basi sasa imekuwa ndiyo lugha inayotumiwa katika Tanzania kwa kazi za biashara, tena ni lugha inayotumiwa na serikali na katika skuli za nchi hizi, na kwa hiyo ni lugha ya kuelemisha watu, isipokuwa siku hizi watoto na watu wazima pia hujifunza Kiingereza pia maana lugha hiyo inatusaidia katika elimu za juu na kufahamiana na mataifa mengine.

Vitabu vingi na magazeti yanapigwa chapa kwa Kiswahili na kila mwaka vinazidi.


9. Перескажите на суахили следующие заметки:

A. Kamusi ya Kiingereza-Kiswahili ilitolewa na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Rais wa nchi, akiwa mpenzi mkubwa wa Kiswahili wakati akipokea zawadi ya kamusi hiyo kwenye sherehe ameisifu TUKI kwa kukamilisha kamusi hiyo kwa mtindo wa kujitegemea katika hatua zote za maandalizi hadi uchapishaji. Alisema kwamba kamusi hiyo ni chombo na silaha muhimu kwa shule na wataalam wa fani mbali mbali.

Kuhusu uwezo wa Kiswahili kama lugha ya kufundishia, rais alisema kwamba hana hofu na lugha hiyo, ingawa hayati mwalimu Nyerere aliyekuwa mkuzaji, mwendelezaji na msambazaji mkubwa wa Kiswahili aliagiza Kiingereza kifundishwe kwa nguvu zaidi na kwa makini kama somo.



B. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimeendelea kufanya mabadiliko katika uendeshaji wa vyombo vyake mbalimbali kwa lengo la kuongeza ufanisi wa kiutendaji.

Iliyokuwa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) imekufa na iliyokuwa Idara ya Lugha ya Kiswahili nayo imefutwa. Kwa pamoja vyombo hivi sasa vinaunda taasisi mpya ijulikanayo kama Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI)

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa taasisi hiyo iliyofanyika mwishoni mwa Juni mwaka huu, Waziri Mkuu wa Tanzania alisifu uanzishwaji wa chombo hicho akiamini kuwa ni sehemu ya jitihada za kukuza Kiswahili kama chombo muhimu kinachowaunganisha Watanzania tangu enzi za kudai uhuru.

“Lugha ya Kiswahili imeimarisha mahusiano ya makabila na kuifanya nchi ionekane kama ina kabila moja badala ya makabila takriban 120. Kiswahili kimekuwa nguzo imara ya mshikamano, amani, utulivu na upendo miongoni mwa Watanzania,” Waziri Mkuu alisema.



C. Kamati ya Utendaji ya Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) imeiagiza ofisi yake ifanye juhudi za haraka kukamilisha taarifa ya tathmini ya maoni ya wananchi kuhusu mjadala wa matumizi ya Kiswahili kama lugha ya kufundishia elimu ya juu.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Mwenyekiti wa BAKITA imesema agizo hilo lilifikiwa katika kikao cha 44 cha kamati hiyo kilichofanyika jijini hivi karibuni.

Taarifa hiyo imeitaka ofisi ya BAKITA kuimarisha ushirikiano zaidi na idara, mashirika na vyombo vingine vinavyokuza Kiswahili na fasihi ndani na nje ya nchi ili kuinua uwanja wa ukuzaji Kiswahili.
10. Дайте синонимы подчеркнутым словам:

-adhimisha ushindi; wa rika moja; -andaa mkutano; -weka bayana; kwa madhumuni ya; -toa tunzo; -fanya utafiti; -ona fahari; mtindo mpya; -tathmini mchango; agizo la kimsingi; -endesha mjadala; kuwa mjinga; fani za elimu; -saidia kwa hali na mali.


11. Переведите:

  1. В интервью нашему корреспонденту исполнительный директор Национального совета языка суахили сообщил, что в этом году планируется отпраздновать день суахили на общенациональном уровне.

  2. Идея отмечать день языка суахили принадлежит одному из бывших руководителей Революционной партии Танзании, а Али Хассан Мвиньи, являвшийся президентом страны, воплотил ее в жизнь 7-го января 1995 года.

  3. На официальной церемонии прозвучал призыв выбрать хотя бы один день в году, когда все любители и профессионалы в области изучения суахили получили бы возможность обмениваться мнениями по актуальным вопросам совершенствования языка и отметить тех, кто внес особый вклад в развитие литературы и поэзии.

  4. Главный приз, учрежденный Советом БАКИТА, это медаль в честь Шаабана Роберта, сделанная из чистого золота, а также определенная сумма наличных денег.

  5. Существует множество критериев, на основе которых выбираются лучшие из литераторов или ученых. Например, звание лучшего специалиста получает тот, у кого уже есть серьезные публикации.

  6. Усилия по возрождению статуса суахили нашли широкий отклик и в других странах Восточной Африки, где также высоко оценивают возможности этого языка и признают его международное значение.

  7. В танзанийском обществе в эти дни ведется горячая дискуссия об использовании суахили в качестве языка преподавания в высших учебных заведениях.

  8. Словарный состав суахили изменялся на протяжении многих веков за счет включения новых слов из арабского и персидского, а позднее из португальского, немецкого и английского языков. Но при этом грамматический строй суахили оставался чисто бантуским.


Msamiati

hoja (-) довод; аргумент wajibu (ед.) долг, обязанность

-hoji расспрашивать, задавать -enzi прославлять,

вопросы чествовать



mahojiano (мн.) интервью sarufi (-) грамматика

dhahiri 1) ясный, очевидный fasihi (-) литература

2) ясно, очевидно -tukuka 1) быть великим,



hafla (-) торжество; церемония возвышенным 2) славиться,

kwa hali na mali словом и быть известным

делом; морально и материально mjadala (mi-) обсуждение,



hadhira (-) аудитория; публика дискуссия

-staafu уходить на пенсию, ufanisi (ед.) 1) процветание

увольняться 2) продуктивность


1   ...   17   18   19   20   21   22   23   24   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət