Ana səhifə

Taarifa ya tume ya taifa ya uchaguzi kuhusu uchaguzi wa rais, wabunge na


Yüklə 4.81 Mb.
səhifə16/33
tarix26.06.2016
ölçüsü4.81 Mb.
1   ...   12   13   14   15   16   17   18   19   ...   33

Taratibu za Uteuzi wa Wagombea Udiwani


Utaratibu wa Uteuzi ulianzia kwa Mgombea mwenye sifa kujaza Fomu Na 8C na Fomu Na. 10 kukamilisha masharti mengine yaliyoainishwa na Tume kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi na Kanuni za Uchaguzi wa Madiwani za mwaka 2010.
      1. Mamlaka ya Uteuzi


Uteuzi wa Wagombea Udiwani ulifanywa na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wa ngazi ya Kata chini ya usimamizi wa Wasimamizi wa Uchaguzi.
      1. Sifa na Masharti ya Uteuzi


    1. Sifa za Mgombea Udiwani

Kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292 ili mtu aweze kuteuliwa kugombea Udiwani hana budi kuwa na sifa zifuatazo; Awe:

  1. Raia wa Tanzania;

  2. Ametimiza umri wa miaka ishirini na moja (21) au zaidi;

  3. Mkazi wa eneo la Halmashauri anayogombea;

  4. Anaweza kusoma na kuandika kwa lugha ya Kiswahili au

Kiingereza;

  1. Mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na Chama cha

Siasa;

  1. Na kipato halali kinachomwezesha kuishi; na

  2. Hajatiwa hatiani na Mahakama yoyote kwa kosa la kukwepa

kulipa Kodi ya Serikali katika kipindi cha miaka mitano kabla ya

tarehe ya Uchaguzi.




    1. Masharti ya Uteuzi kwa Mgombea Udiwani

Kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292 na Maelekezo ya Tume, ili mtu aweze kuteuliwa kuwa mgombea hana budi awe ametimiza masharti yafuatayo; Awe:

  1. Amedhaminiwa na Wapiga Kura wasiopungua kumi (10) walioandikishwa Kupiga Kura katika Kata anayogombea;

  2. Ametoa Tamko la kisheria mbele ya Hakimu kuthibitisha kuwa anazo sifa za kugombea;

  3. Ameweka dhamana ya shilingi 5,000/= kwa Msimamizi wa Uchaguzi;

  4. Hajatenda vitendo vilivyokatazwa kwa mujibu wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi, 2010;

  5. Amejaza Fomu zinazohitajika za Uteuzi ambazo ni Fomu Na. 8C na Fomu Na. 10 ya kukubali kutekeleza Maadili ya Uchaguzi; na

  6. Amewasilisha picha nne (4) za rangi zenye ukubwa wa pasi ya kusafiria (Passport size photo).
      1. Uchukuaji na Urejeshaji wa Fomu za Uteuzi na Fomu za Maadili


Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilianza kutoa Fomu za Uteuzi (Fomu Na.8C) na Fomu za Maadili ya Uchaguzi (Fomu Na. 10) tarehe 6 Agosti, 2010 hadi tarehe 19 Agosti, 2010.
Tume ilitoa nafasi kwa Wagombea kuwasilisha Fomu za Uteuzi (Fomu Na. 8C) mapema kuanzia siku tatu kabla ya uteuzi kwa ajili ya kufanyiwa ukaguzi na kurejeshewa. Upokeaji rasmi ulifanyika Siku ya Uteuzi.
      1. Wagombea Udiwani Walioteuliwa


Kwa ujumla idadi ya Wagombea 7,934 waliteuliwa kugombea kupitia Vyama vya Siasa mbalimbali katika jumla ya Kata 3,335. Aidha, katika Kata 600 Wagombea wa CCM walipita bila kupingwa.
Jedwali Na. 19: Idadi ya Wagombea Udiwani Walioteuliwa



Na.

Chama

Idadi ya Wagombea Udiwani

Jinsia

ME

KE

1.

AFP

11

9

2

2.

APPT-MAENDELEO

27

19

8

3.

CCM

3,335

3,112

223

4.

CHADEMA

1,864

1,786

78

5.

CHAUSTA

23

17

6

6.

CUF

1,575

1,510

65

7.

DP

41

33

8

8.

JAHAZI ASILIA

26

14

12

9.

MAKINI

13

8

5

10.

NCCR-MAGEUZI

280

251

29

11.

NLD

37

26

11

12.

NRA

43

26

17

13.

SAU

97

81

16

14.

TADEA

15

11

4

15.

TLP

285

258

27

16.

UDP

188

167

21

17.

UMD

42

25

17

18.

UPDP

32

22

10

Jumla

7,934

7,375

559

Mchoro Na. 6: Walioteuliwa Kugombea Udiwani

Wagombea Udiwani mia sita (600) walipita bila kupingwa kutokana na baada ya Wagombea wengine kuenguliwa na Msimamizi wa Uchaguzi/ Tume kwa sababu ya kukosa sifa au kutokana na kujitokeza kwa mgombea mmoja pekee katika Kata husika. Wagombea wote waliopita bila kupingwa ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kama inavyooneshwa kwenye Kiambatisho H.




      1. Pingamizi Dhidi ya Uteuzi


Pingamizi dhidi ya Uteuzi wa Madiwani ziliwasilishwa na kufanyiwa Uamuzi kwa Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wa Kata. Msimamizi wa Uchaguzi alikuwa na mamlaka ya kupitia Uamuzi wa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata. Wagombea ambao hawakuridhika na Uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi walikata Rufaa kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
      1. Rufaa kutokana na Uteuzi


Jumla ya Rufaa 122 ziliwasilishwa Tume baada ya uamuzi uliotolewa na Wasimamizi wa Uchaguzi kupingwa na Wagombea husika. Rufaa ishirini na mbili (22) zilikubaliwa na Rufaa 100 zilikataliwa. Miongoni mwa sababu za rufaa hizo ni:-

  1. Mgombea si mkazi wa Halmashauri husika;

  2. Mgombea ni mtumishi wa Serikali;

  3. Mgombea ana Uraia wa nchi mbili; na

  4. Mgombea ana mkataba wenye maslahi na Halmashauri husika.


Jedwali Na. 20: Uamuzi wa Tume juu ya Rufaa za Wagombea Udiwani



Na.

Chama

Idadi ya Rufaa

Rufaa Zilizokubaliwa

Rufaa Zilizokataliwa

1

CCM

45

2

43

2

CHADEMA

35

13

22

3

CUF

34

5

29

4

NCCR-MAGEUZI

2

0

2

5

TLP

5

2

3

6

UDP

1

0

1




Jumla

122

22

100
1   ...   12   13   14   15   16   17   18   19   ...   33


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət