Ana səhifə

Taarifa ya tume ya taifa ya uchaguzi kuhusu uchaguzi wa rais, wabunge na


Yüklə 4.81 Mb.
səhifə15/33
tarix26.06.2016
ölçüsü4.81 Mb.
1   ...   11   12   13   14   15   16   17   18   ...   33

Taratibu za Uteuzi wa Wagombea Ubunge


Mgombea Ubunge alipaswa kujaza Fomu Na. 8B ambayo ndiyo Fomu ya Uteuzi na Fomu Na. 10 ya kukubali kuzingatia Maadili ya Uchaguzi.

  1. Wasimamizi wa Uchaguzi wa Majimbo ndio waliohusika na uteuzi kwa mujibu wa Sheria.

  2. Mgombea hana budi kuwa na Sifa na atimize Masharti kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Maelekezo ya Tume.
      1. Mamlaka ya Uteuzi wa Wagombea Ubunge


Kwa mujibu wa Sheria za Uchaguzi Wasimamizi wa Uchaguzi ndio wenye jukumu la kuteua Wagombea Ubunge walio na sifa na waliotimiza masharti.
      1. Sifa na Masharti ya Uteuzi


  1. Sifa za Kuteuliwa kuwa Mgombea Ubunge

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977 ili mtu aweze kuteuliwa kuwa Mgombea Ubunge hana budi kuwa na sifa zifuatazo; Awe:-



  1. Raia wa Tanzania.

  2. Ametimiza umri wa miaka ishirini na moja .

  3. Anajua kusoma na kuandika kwa Kiswahili au

Kiingereza.

  1. Ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa

na Chama cha Siasa.

  1. Hajatiwa hatiani na Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kodi yoyote ya Serikali katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi.




  1. Masharti ya Kuteuliwa kuwa Mgombea Ubunge

Kwa mujibu wa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343 na Maelekezo ya Tume ili mtu aweze kuteuliwa kuwa mgombea Ubunge, pamoja na sifa zilizotajwa hapo juu, hana budi kutimiza masharti yafuatayo; Awe:

    1. Amejaza kikamilifu Fomu ya Uteuzi yaani Fomu Na.8B.

    2. Amedhaminiwa na Wapiga Kura wasiopungua ishirini na tano ambao wamejiandikisha kuwa Wapiga Kura katika Jimbo hilo.

    3. Ameweka dhamana ya shilingi elfu hamsini (50,000/=) kwa Msimamizi wa Uchaguzi.

    4. Ametoa Tamko mbele ya Hakimu kuwa anazo sifa zinazotakiwa ili kugombea Ubunge.

    5. Hajatenda vitendo vilivyokatazwa chini ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi, 2010.

    6. Amewasilisha picha nne za rangi zenye ukubwa sawa na Pasi ya Kusafiria (Passport size photo).

    7. Amejaza Fomu zote zinazohitajika zikiwemo Fomu za kukubali kutekeleza Maadili ya Uchaguzi (Fomu Na. 10).
      1. Uchukuaji na Urejeshaji wa Fomu za Uteuzi na Fomu za Maadili


Tume ilianza kutoa Fomu za Uteuzi (Fomu Na. 8B) na Fomu ya Kuthibitisha kutekeleza Maadili ya Uchaguzi (Fomu Na.10) tarehe 06 Agosti, 2010 hadi tarehe 19 Agosti, 2010.
Tume ilitoa nafasi kwa Wagombea kuwasilisha Fomu za Uteuzi (Fomu Na. 8B) mapema kuanzia siku tatu kabla ya Siku ya Uteuzi kwa ajili ya kufanyiwa ukaguzi na kurejeshewa. Upokeaji rasmi ulifanyika Siku ya Uteuzi.
      1. Wagombea Ubunge Walioteuliwa Majimboni


Jumla ya Wagombea 1,036 waliteuliwa kugombea Ubunge katika majimbo 239 ya Uchaguzi. Kati ya Wagombea hao, jumla ya Wagombea 845 (asilimia 81.5) walikuwa ni wanaume na 191 (asilimia 18.4) ni wanawake. Vyama vyote vya Siasa kumi na nane (18) vilivyopata usajili kamili viliweka Wagombea katika majimbo mbalimbali.
Jedwali Na. 16: Idadi ya Wagombea Ubunge Walioteuliwa



Na.

Chama

Idadi ya Wagombea Ubunge

Jinsia

Me

Ke

1.

AFP

15

11

4

2.

APPT – Maendeleo

16

9

7

3.

CCM

239

215

24

4.

CHADEMA

179

154

25

5.

CHAUSTA

13

8

5

6.

CUF

182

168

14

7.

DP

35

24

11

8.

JAHAZI ASILIA

21

15

6

9

MAKINI

17

12

5

1010.

NCCR-Mageuzi

67

52

15

1111.

NLD

23

15

8

12

NRA

19

13

6

13

SAU

32

26

6

14

TADEA

32

20

12

15

TLP

42

36

6

16

UDP

45

31

14

17

UMD

23

13

10

18

UPDP

36

23

13




JUMLA

1036

845

191

Mchoro Na. 5: Walioteuliwa Kugombea Ubunge


Wagombea Ubunge kumi na saba (17) walipita bila kupingwa kutokana na baada ya Wagombea wengine kuenguliwa na Msimamizi wa Uchaguzi au Tume kwa sababu ya kukosa sifa au kutokana na kujitokeza kwa mgombea mmoja pekee katika Jimbo husika.
Katika Majimbo yote kumi na saba (17) ni Wagombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ndiyo waliopita bila kupingwa, kama inavyooneshwa kwenye Jedwali Na. 17.

Jedwali Na. 17: Orodha ya Majimbo Ambayo Wabunge Walipita bila Kupingwa


Na.

Halmashauri

Jimbo

Sababu

1

Mji wa Njombe

Njombe Kusini

Hakupata mpinzani

2

Wilaya ya Chunya

Songwe

Hakupata mpinzani

3

Wilaya ya Iringa

Ismani

Hakupata mpinzani

4

Wilaya ya Kongwa

Kongwa

Hakupata mpinzani

5

Wilaya ya Ludewa

Ludewa

Hakupata mpinzani

6

Wilaya ya Mpanda

Katavi

Hakupata mpinzani

7

Wilaya ya Mpwapwa

Mpwapwa

Hakupata mpinzani

8

Wilaya ya Mufindi

Mufindi Kaskazini

Mpinzani kuenguliwa

9

Wilaya ya Mufindi

Mufindi Kusini

Mpinzani kuenguliwa

10

Wilaya ya Muleba

Muleba Kusini

Hakupata mpinzani

11

Wilaya ya Musoma

Musoma Vijijini

Mpinzani alijitoa

12

Wilaya ya Rungwe

Rungwe Mashariki

Hakupata mpinzani

13

Wilaya ya Rungwe

Rungwe Magharibi

Mpinzani kuenguliwa

14

Wilaya ya Sengerema

Sengerema

Mpinzani kuenguliwa

15

Wilaya ya Simanjiro

Simanjiro

Hakupata mpinzani

16

Wilaya ya Ulanga

Ulanga Mashariki

Hakupata mpinzani

17

Wilaya ya Lushoto

Bumbuli

Hakupata mpinzani
      1. Pingamizi Dhidi ya Wagombea


Kwa mujibu wa taratibu za Uteuzi baada ya Tume kufanya Uteuzi, inapaswa kubandika Fomu za Uteuzi wa Wagombea wote mahali pa wazi kwa muda wa saa ishirini na nne (24) ili kutoa nafasi kuzikagua kwa wanaoruhusiwa Kisheria kuweka pingamizi. Baada ya Fomu hizo kubandikwa mahali pa wazi kuanzia saa kumi alasiri Siku ya Uteuzi hadi saa kumi alasiri ya siku iliyofuata.


        1. Pingamizi za Msajili wa Vyama vya Siasa

Kwa mujibu wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi, 2010 Msajili wa Vyama vya Siasa anaruhusiwa kuweka pingamizi dhidi ya Mgombea yeyote ambaye hakutimiza au amekiuka masharti ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi, 2010.
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, Msajili wa Vyama vya Siasa aliwasilisha pingamizi kwa Msimamizi wa Uchaguzi dhidi ya uteuzi wa Mgombea Ubunge wa TLP katika Jimbo la Mtama kwa kutokutoa taarifa za gharama atakazotumia katika Uchaguzi. Pingamizi hiyo ilikubaliwa na Msimamizi wa Uchaguzi. Hata hivyo, Mgombea alikata Rufaa Tume na Rufaa hiyo ilikubaliwa.


        1. Pingamizi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Kwa mujibu wa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 Kifungu cha 40(3), Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaruhusiwa kutoa pingamizi dhidi ya uteuzi wa Mgombea. Katika Uchaguzi uliopita hakukuwa na pingamizi yoyote iliyowasilishwa kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
      1. Rufaa Dhidi ya Maamuzi ya Pingamizi


Baada ya Siku ya Uteuzi, Wasimamizi wa Uchaguzi walipokea pingamizi mbalimbali na kuzitolea maamuzi. Wagombea ambao hawakukubaliana na maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi walikata Rufaa kwa Tume.
Jumla ya Rufaa hamsini na moja (51) ziliwasilishwa Tume na Wagombea mbalimbali wa Ubunge. Katika Rufaa zilizowasilisha na kuamuliwa na Tume, Rufaa kumi na nne (14) zilikubaliwa na thelathini na saba (37) zilikataliwa. Kwa muhtasari sababu za Rufaa hizo ni pamoja na:-

  1. Kutokujaza Fomu Na. 10.

  2. Kutodhaminiwa na Chama chake cha Siasa.

  3. Hakusaini Tamko la Kisheria.

  4. Namba za kadi za Wapiga Kura waliomdhamini zilikuwa na kasoro.

  5. Kutoa maelezo ya uongo katika Fomu ya uteuzi.

  6. Tuhuma za rushwa.

Rufani zilizowasilishwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na matokeo ya Rufaa yanaoneshwa katika Jedwali Na. 18.


Jedwali Na. 18: Uamuzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika Rufaa za Wagombea Ubunge



Na.

Chama

Idadi ya Rufaa

Rufaa Zilizokubaliwa

Rufaa

Zilizokataliwa

1

AFP

1

1

0

2

CCM

11

0

11

3

CHADEMA

15

7

8

4

CUF

12

4

8

5

MAKINI

1

0

1

6

JAHAZI ASILIA

1

0

1

7

NCCR-MAGEUZI

4

0

4

8

SAU

2

1

1

9

TLP

3

1

2

10

UDP

1

0

1




Jumla

51

14

37
1   ...   11   12   13   14   15   16   17   18   ...   33


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət