Ana səhifə

Taarifa ya tume ya taifa ya uchaguzi kuhusu uchaguzi wa rais, wabunge na


Yüklə 4.81 Mb.
səhifə26/33
tarix26.06.2016
ölçüsü4.81 Mb.
1   ...   22   23   24   25   26   27   28   29   ...   33

MAPENDEKEZO

Baada ya kukamilika kwa Uchaguzi wa mwaka 2005, Tume iliandaa Taarifa yake na kuiwasilisha Serikalini. Katika Taarifa hiyo Tume ilitoa mapendekezo kadhaa ya jinsi ya kuboresha chaguzi zitakazofuata. Tume inaishukuru Serikali kwa kutekeleza baadhi ya mapendekezo, hata hivyo kutokana na mapendekezo mengine kutotekelezwa Tume inapenda kuikumbusha Serikali mapendekezo yake ya awali na kuongeza mapendekezo mapya kama ifuatavyo:-


A. MAPENDEKEZO YA MWAKA 2005 AMBAYO HAYAJATEKELEZWA

(i) Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi

Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliyoanza kufanyiwa kazi na Serikali ikamilishwe mapema.
(ii) Bajeti ya Uchaguzi Kila Mwaka

Kwa kuwa Uchaguzi Mkuu unafanyika kila baada ya miaka mitano na Sheria inaitaka Tume kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mara mbili kati ya Chaguzi Kuu mbili, ni vema kuwepo na mfuko wa Kudumu wa Uchaguzi ambao utakuwa unatengewa fedha kutoka Bajeti ya Serikali ya kila mwaka. Hii itaepusha kuathiri utendaji wa Wizara na Taasisi za Serikali inapofikia mwaka wa Uchaguzi. Aidha, itaiwezesha Serikali kuzidi kujitegemea kifedha katika kuendesha chaguzi nchini.


(iii) Ukomo wa Mgombea Kujitoa

Kutokana na Wagombea wengi kuendelea kujitoa baada ya Uteuzi, Tume ilipendekeza Sheria irekebishwe ili kuweka ukomo wa Mgombea kujitoa na kuwepo na ada ya kulipa endapo Mgombea atajitoa baada ya ukomo uliowekwa kupita. Jambo hili litasaidia Wapiga Kura kutopoteza Kura zao kwa kumpigia Mgombea aliyejitoa ambaye jina lake linaendelea kuwepo kwenye Karatasi ya Kura.


(iv) Sheria Kuhusu Kampeni

Sheria ya Uchaguzi kuhusiana na Kampeni za Uchaguzi iangaliwe upya na kuhakikisha haikinzani na sheria zingine, kwa mfano Police Force Ordinance Act, Sura ya 322 na Sheria ya Nembo ya Taifa ya mwaka 1971 Sura ya 10.

(v) Tume Kuwa na Ofisi ya Uchaguzi Katika Halmashauri

Ili uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura uweze kufanikiwa na shughuli nyingine za Uchaguzi kuendeshwa kwa ufanisi zaidi ilipendekezwa kuwa na Ofisi za Uchaguzi katika kila Halmashauri.


(vi) Jengo la Kudumu la Ofisi ya Tume

Tume hadi sasa haina Jengo la Kudumu la Ofisi linalokidhi mahitaji yakiwemo ya utunzaji wa vifaa na Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Tume ilipendekeza ipatiwe fedha za kujenga Jengo la Kudumu la Ofisi litakalokidhi mahitaji yake.


(vii) Tume Kuwa na Ofisi Ndogo Tanzania Zanzibar

Ilipendekezwa kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi iwe na Ofisi ndogo Tanzania Zanzibar ili kuboresha uendeshaji wa chaguzi za Muungano.


(viii) Elimu ya Mpiga Kura

Tume ilipendekeza kuwa ili Elimu ya Mpiga Kura iweze kutolewa kwa ukamilifu kwa kipindi chote, Tume itengewe fedha za kutosha kwa ajili ya kutoa Elimu ya Mpiga Kura kila mwaka.


(ix) Elimu ya Uraia

Tume ilipendekeza Serikali iangalie uwezekano wa kuunda Chombo cha kutoa, kusimamia na kuratibu Elimu ya Uraia.


B. MAPENDEKEZO MAPYA
(i) Chombo cha Kugawa Majimbo na Kata Kiwe Kimoja

Kwa sasa Tume ina mamlaka ya kugawa majimbo ya Uchaguzi na kuyatangaza. OWM- TAMISEMI ina mamlaka ya kugawa Kata na Kuzitangaza. Tume inatangaza Maeneo ya Uchaguzi baada ya kuletewa orodha ya Kata na OWM – TAMISEMI. Majimbo ya Uchaguzi yanajumuisha maeneo ya Uchaguzi ambayo katika Halmashauri husika ni Kata. Inapotokea OWM – TAMISEMI kutangaza Kata baada ya Tume kutangaza Majimbo ya Uchaguzi inajitokeza haja ya kurekebisha mipaka ya Majimbo na hivyo kuathiri Ratiba Rasmi ya Uchaguzi. Hivyo, Tume inapendekeza chombo cha kugawa Majimbo na kata kiwe kimoja.


(ii) Serikali Kutoa Miadi ya Kiasi cha Fedha za Kugharamia Chaguzi Mapema

Shughuli za Uchaguzi zinagharamiwa na Serikali na Washirika wa Maendeleo. Mara nyingi Washirika wa Maendeleo wanapenda kufahamu mapema kiasi ambacho kitatolewa na Serikali kabla wao kuahidi kiasi watakachotoa. Hivyo, Tume inapendekeza Serikali itoe miadi yake mapema baada ya kupokea makadirio ya gharama za Uchaguzi kutoka Tume.


(iii) Tume Kuwa na Maghala Katika Halmashauri

Shughuli za Uchaguzi zinahusisha matumizi ya vifaa vingi, ambavyo vinatakiwa kutunzwa kwenye Halmashauri husika vikisubiri Uchaguzi mwingine. Kwa kuwa Halmashauri zina vifaa vingine vingi inakuwa vigumu kupata maghala ya kutosha kutunza vifaa vyote vya Uchaguzi.


Tume inapendekeza iwezeshwe kujenga maghala katika kila Halmashauri kwa ajili ya kutunza vifaa vya Uchaguzi.
(iv) Sheria ya Gharama za Uchaguzi Iangaliwe Upya

Tume inapendekeza Sheria ya Gharama ya Uchaguzi, ya mwaka 2010 iangaliwe upya ili kuviainisha na kuvirekebisha vifungu vinavyokinzana na Sheria za Uchaguzi.


(v) Tume Kuandikisha Wapiga Kura Wote Tanzania Zanzibar

Ili kuwa na Daftari la Kudumu la Wapiga Kura moja Tanzania, Tume inapendekeza ipewe mamlaka ya kuandikisha nchi nzima. Hivyo, Tume inapendekeza kifungu cha 12A kifutwe katika Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 ili kuiwezesha Tume kuandikisha Wapiga Kura wote Tanzania Zanzibar – kwa Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano.


(vi) Serikali Kutangaza Maeneo ya Kiutawala Mapema

Tume inapendekeza ugawaji wa Mikoa, Wilaya, Kata, Vijiji , Mitaa na Vitongoji ufanyike mapema ili kuiwezesha Tume kujiandaa kwa Uchaguzi.


(vii) Tume Iwe na Ofisi Katika Kanda, Mikoa na Majimbo

Tume ina Watendaji wa Kudumu Makao Makuu tu. Lakini shughuli za Uchaguzi ni endelevu. Ili kutekeleza shughuli za Uchaguzi kwa ufanisi Tume inapendekeza iwe na Ofisi za Kanda, Mikoa na Majimbo.



VIAMBATISHO



Kiambatanisho A: Orodha ya Kata Zilizofanya Uchaguzi Mdogo wa Madiwani Kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010


Na.

Halmashauri ya

Kata

Sababu

1

Wilaya ya Ludewa

1

Lupingu

Kifo

2

Wilaya ya Rufiji

2

Ngorongoro

Kifo

3

Wilaya ya Mkuranga

3

Shungubweni

Kifo

4

Wilaya ya Bukoba

4

Kasharu

Kifo

5

Wilaya ya Hai

5

Masama Kusini

Kifo




Wilaya ya Serengeti

6

Busawe

Kifo







7

Kisangura

Kifo

7

Mji wa Korogwe

8

Old Korogwe

Kifo

8

Manispaa ya Sumbawanga

9

Kizitwe

Kifo







10

Matanga

Kifo

9

Wilaya ya Kasulu

11

Nyamidaho

Kifo

10

Wilaya ya Nkasi

12

Kabwe

Kifo







13

Namanyere

Kifo

11

Wilaya ya Sumbawanga

14

Katazi

Kifo

12

Wilaya ya Maswa

15

Nguliguli

Kifo







16

Ipililo

Kifo

13

Manispaa ya Songea

17

Majengo

Kifo

14

Wilaya ya Muheza

18

Masuguru

Kifo

15

Wilaya ya Tunduru

19

Marumba

Kifo







20

Muhuwesi

Kifo

16

Manispaa ya Arusha

21

Sombetini*3

Kufukuzwa na Kuhama Chama







22

Kati

Kifo

17

Wilaya ya Moshi

23

Kilema-Kaskazini

Kifo

18

Jiji la Tanga

24

Ngamiani Kati

Kifo







25

Chongoleani

Kifo

19

Wilaya ya Ukerewe

26

Bukindo

Kifo

20

Wilaya ya Sengerema

27

Bupandwa

Kifo







28

Nyamazugo

Kifo







29

Busisi

Kifo

21

Wilaya ya Muleba

30

Kibanga

Kifo

22

Wilaya ya Ngara

31

Kabanga

Kifo

23

Wilaya ya Mpanda

32

Katuma

Kifo

24

Wilaya ya Nachingwea

33

Nditi

Kifo







34

Naipanga

Kifo

25

Manispaa ya Tabora

35

Ng’ambo

Kifo







36

Malolo

Kifo

26

Wilaya ya Urambo

37

Ushokola

Kifo

27

Wilaya ya Songea

38

Wino

Kifo

28

Wilaya ya Kigoma

39

Nguruka

Kifo

29

Wilaya ya Moshi

40

Uru-Mashariki

Kuhama Chama

30

Wilaya ya Tarime

41

Tarime Mjini

Kifo

31

Wilaya ya Korogwe

42

Mnyuzi

Kifo

32

Wilaya ya Ludewa

43

Lupingu

Kifo

33

Wilaya ya Magu

44

Sukuma

Kifo

34

Wilaya ya Mbarali

45

Rujewa

Kifo

35

Wilaya ya Morogoro

46

Mtombozi

Kifo

36

Wilaya ya Misenyi

47

Kitobo

Kifo

37

Wilaya ya Tandahimba

48

Mnyawa

Kifo







49

Mkundi

Kifo







50

Mahuta

Kifo

38

Manispaa ya Kigoma/Ujiji

51

Machinjioni

Kifo

39

Wilaya ya Mbinga

52

Utiri

Kifo

40

Manispaa ya Ilala

53

Upanga-Mashariki

Kifo

41

Wilaya ya Makete

54

Matamba

Kifo

42

Jiji la Mbeya

55

Forest

Kifo

43

Wilaya ya Iramba

56

Shelui

Kifo

44

Wilaya ya Ileje

57

Ngulugulu

Kifo

45

Wilaya ya Kahama

58

Mwalugulu

Kifo

46

Wilaya ya Masasi

59

Lipumburu

Kifo

47

Wilaya ya Chunya

60

Namkukwe

Kifo

48

Wilaya ya Iringa

61

Ulanda

Kifo







62

Ifunda

Kifo

49

Wilaya ya Kwimba

63

Mwandu

Kifo

50

Wilaya ya Magu

64

Mkula

Kifo

51

Wilaya ya Geita

65

Kagu

Kifo

52

Wilaya ya Mvomero

66

Langari

Kifo

53

Wilaya ya Bahi

67

Mundemu

Kifo

54

Manispaa ya Singida

68

Utemini

Kujiuzulu

55

Wilaya ya Monduli

69

Monduli Juu

Kufukuzwa kwenye Chama







70

Esilalei

Kifo

56

Wilaya ya Igunga

71

Bukoko

Kifo

57

Wilaya ya Mpwapwa

72

Lumuma

Kujiuzulu

58

Wilaya ya Mufindi

73

Ihowanza

Kifo

59

Wilaya ya Mbeya

74

Ulenje

Kifo
1   ...   22   23   24   25   26   27   28   29   ...   33


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət