Ana səhifə

Bismillah Ar-Rahman Ar-Rahiim Harakati za Uislamu dhidi ya Ahmadiya Chungu Mosi, Rabiul Awwal 1430 Februari 24, 2009


Yüklə 0.51 Mb.
səhifə5/5
tarix26.06.2016
ölçüsü0.51 Mb.
1   2   3   4   5

Maelezo ya Mirza katika Mahakama ya Kodi ya Mapato-Vito vya Mkewe
...Mimi ninamiliki vijiji vitatu kama Ta’aluqadari, mapato yake ya mwaka yanakaribia Rupia 82......mbali na hivyo, namiliki shamba ambalo linakaribia Ghumao 80 (Ghumao moja ni kipande cha ardhi kinachoweza kulimwa na ng’ombe wawili kwa siku moja). Si la urithi (yaani kalilinunua-Rashid) na namiliki ardhi fulani ya kurithi ambayo pato lake la jumla kwa mwaka ni Rupia 300. Pia ninayo bustani ambayo pato lake hutofautiana, mwaka fulani huwa Rupia 300, wakati mwingine 400 na hasahasa huwa 500 kwa mwaka. Sina chanzo kingine cha mapato.....mke wangu ana vito vya thamani vinavyokaribia Rupia 4000 lakini hivyo si mali yangu. Nimeweka rehani bustani yangu kwa mke wangu (nafuu iliyoje hiyo!)...badala yake mimi nikapata vito vya thamani vya Rupia 4000 na Rupia 1000 kwa fedha taslimu....karibu Rupia 2000 za thamani ya vito hivyo vya mke wangu alipewa na mamaake na Rupia 2000 zilizobaki za thamani ya vito hivyo, nimenunua mimi kutokana na miaka 14 ya mapato, lakini vito hivi vya Rupia 2000 nilishampa vyote-vyote (mke wangu)....” (Stetimenti ya Mirza Ghulam katika Kesi ya Kodi ya Mapato katika Maakama ya Bw. F.T Doxon, Naibu Kamishina, mbele ya Munshi Tajuddin Sahib, Mkusanyaji wa Kodi ya Mapato wa Kanda, Batala, District Gurdaspur tarehe 20 Juni 1898 Kesi Na.46/55 ya Kodi ya Mapato. Imechukuliwa kutoka Tazyana-e-Ebrat mwandishi Karamuddin Dabeer uk. 70-73)
Sihitaji kutumia fedha za wafuasi wangu kwa ajili yangu binafsi. Matumizi yangu yako chini ya kipato changu, ambacho kinatokana na kilimo tu na hakuna chanzo cha mapato....chochote kinachosalia katika kipato changu binafsi baada ya matumizi, nakitumia kwa kazi ya dini.” (Stetimenti ya Mirza Ghulam Ahmad katika Shauri la Kodi ya Mapato kwenye Maakama ya Bw. F Dixon, Naibu Kamishina, mbele ya Munshi Tajuddin Sahib, Mkusanyaji Kodi ya Mapato wa Kanda, Batala, Wilaya ya Gurdaspur tarehe 20 uni 1898 Shauri Na. 46/55 la Kodi ya Mapato. Imechukuliwa kutoka Tazyana-e-Ebrat, mwandishi Karamuddin Dabeer uk 72-73)
Maelezo ya Hakiim Nuruddin katika mahakama ya Kodi ya Mapato yapingana na alichokisema Mirza
Watu humpa Mirza Sahib pesa kama hidaya kwa aili ya matumizi yake binafsi, wakiwa kama ni Muriidi wa dhati, lakini nashindwa kusema ni kiasi gani hicho kwa mwaka.” (Stetimenti ya Hakim Nuruddin katika Kesi ya Kodi ya Mapato dhidi ya Mirza Ghulam Ahmad katika Mahakama ya Mr.F. T Dixon, Naibu Kamishina, mbele ya Munshi Tajuddin Sahib, Mkusanyaji Kodi ya Mapato wa Kanda, Batala, District Gurdaspur tarehe 20 uni 1898 Kesi Na 46?55 ya Kodi ya Mapato. Imechukuliwa kutoka kitabu Tazyna-e-Ebrat, mwandishi Karamuddin Dabeer uk.74)

Maelezo ya Mkusanya Kodi, Munshi Tajuddin:
Kwa muibu wa stetimenti ya Mirza Sahib mwenyewe, hivi karibuni aliweka rehani bustani yake kwa mkewe badala yake akapata vito vya thamani vya Rupia 4000 na Rupia 1000 kwa feda taslimu. Mtu ambaye mkewe anaweza kumpa kiasi kikubwa kama hicho, inaweza kukisiwa kuwa ni tajiri.” (Stetimenti ya Munshi Tajuddin Sahib, Mkusanyaji Kodi ya Mapato wa Kanda, Batala, District Gurdaspur tarehe 31 Agosti 1898, iliyonakiliwa katika shauri la kodi ya mapato Na. 46/55 la mwaka 1898; lililotajwa katika Roohani Khazain juz.13uk.517)
Je hiki si kioja jamani kwamba, kwa upande mmoja MGAQ alikuwa akiwanasihi wafuasi wake kujitolea na kuishi maisha ya kawaida, watu wakawa wanauza vito vya tamani vya wake zao ili kutoa ‘Sadaka ya Fedha’, kutoa CHANDA, na kwa upande mwingine Mirza Ghulam akaweza kununua shamba na kupata vito vya thamani vya Rupia 2000, ambayo ni sawa na 15,000 x 2000 = Rupia.30,000,000!!!
Mnamo mwaka 1907, akielekea mwishoni mwa maisha yake, Mirza akatazama miaka yake yote ya utumishi wa dini na kwa hilo alifaulu:
Hakuna hata mmoja aliyenijua mimi wala njia za kipato changu kwamba eti niliishi maisha ya raha na starehe. Kile chote nilichomiliki kilikuwa ni kijiurithi kidogo mno kutoka kwa baba yangu. Kisha Mungu akaiweka dunia mikononi mwangu wakati ambao sikuwa nikitarajia kupata hata rupia 10 kwa mwezi. Hata hivyo, Mungu akaibadili hali yangu na akanishika mkono. Sasa, nina zaidi ya rupia laki tatu.” (kwa maelezo ya mkusanyaji: leo hii kiasi hicho ni sawa na mamilioni ya dola) (Roohani Khazain, Juz. 22, uk. 220-221, Haqiiqat-ul-Wahi, uk. 211-212, 1907)
Hebu hiki kiwe kifumbua macho kwa wafuasi wake

ATHARI ZA MAISHA YA MGAQ KWA WAFUASI
“Mti mchungu hawezi Kuzaa Matunda Matamu” (Kauli ya Mirza, Barakaat-rd-Dua, RK juz.6 uk.36)
Ulichopanda ndicho unachovuna. Hebu soma mifano ifuatayo:
Khalifa wa Kwanza-Hakiim Nuruddin
Yawezekana huyu ndiye aliyekuwa mtu pekee tofauti katika msonge wa uongozi wa Jumuiya ya Ahmadiya ambaye alitoa mcango mkubwa kwa ajili ya miradi mbalimbali wakati wa uhai wa MGAQ na baada ya apo akawa Khalifa. Hakuna kumbukumbu kama wanajumuiya wa Familia ya Qadiani wakiwemio Makhalifa wa 2, wa 3, wa 4 na wa tano na wengine waliopata kutoa michango ya CHANDA katika Tehrik au miradi yoyote. Kama ilivyoelezwa hapo juu, MGAQ aliweza hata kuiepusha familia yake isitoe chochote kwa ajili ya kuzikwa katika makaburi ya Peponi.
Mungu kanitoa mimi na familia yangu ambapo kila mwanaume na kila mwanamke lazima afuate masharti haya na yeyote anayenung’unika, atakuwa ni mnafiki.” (Al-Wasiiyat la tarehe 20 Desemba 1905, Roohani Khazain ju.20 uk.327)
Hakiim Nuruddin, lica ya kutoa michango ya hisani katika miradi mbalimbali, katika hali ya kushangaza, akutoa Wasia, jambo ambalo lina maana kuwa yeye akuwa MUSI. Wasia wake ukasomwa siku moja baada ya kifo chake, na Nawab Moammad Ali Khan:

Vitabu vyangu na mali yangu ujumuishwe katika taasisi kwa manufaa ya watoto wangu.” (Life of Hadhrat Khalifatul Masih 1, The Review of Religions, Jan 2008, juz.103 Issue 01, uk.52)


Khalifa wa 2-Mirza Bashiiruddin Mahmud na Shaghalabagala ya Fedha
Mnamo mwaka 1934 “Hadhrat Khulifatul Masih II akatangaza mpango wa Tashrik Jadid. Mwanzoni mpango uu ulikuwa kwa kipindi cha miaka lakini baadae ukafanywa wa kudumu. Mpango huo ukahamasisha kuishi maisha ya kawaida, kutoa sadaka ya fedha (yaani CHANDA) na kujitengea muda kwa ajili ya utumishi na tabligh ya Uislamu.” (The Life and Achievements of Hadhrat Khalifatul Masih II, The Review of Religions, Feb 2008, Juz.103, Issue 02, uk.53)
Mnamo mwaka 1924 Mirza Mahamud aliamua kufanya Ziara ULAYA. Gazeti la Ahmadia wa Lahore likaandika hivi:
tunashindwa kuamini kuwa Mian Sahib (Mirza Mahmud) hakuweza kudhibiti matamanio yake kwenda safarini Ulaya kiasi kwamba maelfu ya Rupia za mfuko wa Umma yanatapanywa kwa namna hiyo na hawakuwa na huruma na wanawake waliotoa vito vyao vya thamani na kumpa Mian Sahib ili msikiti ujengwe mjini Berlin; kumbe msikiti wenyewe bado ulikuwa haujakamilika kiasi kwamba agizo likatolewa (na Mirza Mahmud) kuuza msikiti huo; jina msikiti limebadilika na kuwa nyumba ya kawaida. Sasa basi pesa zitakapokuja baada ya kuuza nyumba hiyo iliyokuwa msikiti wakati huo basi zile pesa zilizoazimwa zingerejeshwa kwa wale watu ambao amana yao ndio hiyo Mian Sahib anaondoka nayo kwenda Uingereza akiandamana na kundi lake la wafanyakazi.” (Akhbar Paigham-i-Sulh, Lahore, tarehe 16 Julai 1924)
Leo hii Fazl Umar (Mirza Mahmud) anaondoka kwenda Ulaya na Damascus. Kundi la wafanyakazi lina watu chungu mzima....hakuna cha kujali gharama za safiri wala malazi. Kinachofikiriwa ni starehe na propaganda tu, yeye si mtu wa kubaki nyuma ya yeyote yule., mahitaji yote ya kumpatia starehe yawepo hata kama ni kufuja fedha za umma, na iwe hivyo. Mian Sahib anadai kuwa yeye ni William, Mbabe.....je panaweza kuwepo na mlingano kati ya maisha ya starehe ya Fazl Umar (Mirza Mahmud) na maisha ya unyenyekevu na heshima ya Sayidina Umar radhiAllahu anhu? Katu.” (Akbar Paigham-i-Sulh, Lahore, tarehe 20 Julai 1924)
Khalifa wa 3 na Tehriki Mpya za CHANDA
Moja kati ya itihada za awali za Hadhrat Khalifatul Masih III ilikuwa ni ombi la Desemba 21, 1965 la Kuanzisha Taasisi ya FADL-I-UMAR FOUNDATION kwa ajili ya kumbukumbu ya Khalifa wa Pili......Ombi hilo likatolewa kwa Jamii kutoa rupia milioni mbili na nusu (sawa na GBP 125,000 kiwango cha kihistoria katika ubadilishaji fedha, 1=20PKR).....kwa kipindi kifupi tu cha muda, wajumbe walichangia Rupia milioni 3.4.....” (Significant Appeals, The Review of Religions, Machi 2008, Juz. 103, Toleo 03, uk.11)
MPANGO WA NUSRAT JAHAN: Mnamo Aprili 4 1970, Hadhrat Khalifatul Masih wa Tatu (Khalifa III) akawa Khalifa wa kwanza kusafiri kwenda Afrika...ilipokwisha ziara yake katika nchi za Afrika Magharibi, akawasili London.....huko akatangaza mpango mmoja aliokuwa ameutia fikirani kwa mwongozo wa Mungu....mpango huo ungehitaji msingi wa malaki ya Pauni (Pounds), baadae Khalifatul Masihi huyo akaandika hivi:
Wakati nilipokuwa Gambia MwenyeziMungu Mtukufu, alinifunulia kwa mkazo wazo moja.....Kwa mnasaba wa wazo hili, nikahitaji haraka watu mia mbili wa kujitolea kutoka Jumuiya ya Ahmadiya ya Uingereza waliokuwa tayari kuchangia 200 kila mmoja na nikahitaji watu wengine mia mbili wa kujitolea waliokuwa tayari kuchangia 100 kila mmoja na waliosalia ambao wangekuwa tayari kuchangia 36 kila mmoja.....Nikaandaa chini ya usimamizi wangu mwenyewe akaunti ya benki na nikaiita ‘Nusrat Jahan Reserve Fund.
Ukafanikiwa kweli Mpango huu wa Nusrat Jahan, kwamba ulitanuka kutoka mpango wa awali wa programu ya miaka mitatu na kuwa wakfu wa kudumu” (Significant Appeals, The Review of Religions, Machi 2008, Juz. 103, Issue 03, uk.14-15)
MFUKO WA MAADHIMISHO YA AHMADIYA: Hadhrat Khalifatul Masih III aliwaomba wanajumuiya kuchanga Rupia milioni 2.5 katika mradi huu. Ahadi zilizopokelewa kwa ajili hii zilikuwa ni mara nne ya kiasi kilichoombwa.” (Significant Appeals, The Review of Religions, Machi 2008, Juz.103, Toleo 03, uk. 16-17)
Tehrik Mpya ya Khalifa wa 4-Kuwabadili wengi wawe Ahmadia
Kila Khalifa mpya amekuja na wazo la ujanja la kuwachomoa fedha kutoka kwa wafuasi wao wepesi kuamini. Mirza Bshiiruddin ndiye aliyeanzisha Tehreek Jadid ambayo sasa imekuwa wajibu kwa kila Ahmadia. Mirza Tahir, Khalifa wa 4 akaja na wazo baya la kuifunika CHANDA kwa dai la kuongeza mara dufu idadi ya watu wanaoingia Ahmadiya. Hivyo, akaanza mbio za panya. Murabi, Mubaligha na Ahmadia wa kawaida wote wakahaha kupata fomu zilizosainiwa kiujanja-ujanja ili kufikia lengo lililowekwa na Jumuiya na kumfurahisha Khalifa. Kuanzia mwaka 1993 hadi 2002 kulikuwa na watu wapya milioni 159 walioripotiwa kuingia Ahmadiya:
“Katika Mkutano wa Mwaka wa Uingereza, Ahmadia 200,000 wapya ambao walikuwa wamejiunga na Ahmadia kuanzia Agosti 1992 hadi Julai 1993, hadi kufikia mwaka 2002, idadi hii ilituna na kufura haraka haraka:
.400,000 mwaka 1994

800,000 // 1995

1,600,000 // 1996

3,000,000 // 1997

5,000,000 // 1998

10,000,000 // 1999

40,000,000 // 2000

80,000,000 // 2001 na



20,000,000 // 2002
(Milestones in the Life lived to the Full, Review of Religion, April 2003, Juz.98, Issue 04, uk.26).
Wazo lililofichikana nyuma ya zoezi hili zima lilikuwa hili kwamba kuongezeka kwa Ahmadia maana yake ni MICHANGO (CHANDA) nyingi zaidi kwani MGAQ alishasema waziwazi kuwa:
“.....kama mtu hachangii hata pesa 1 kwa nini basi anaendelea kukaa katika Jumuiya.” (Malfuuzaat juz.6 uk.38 tarehe 5 Julai 1903)
Utajiri wa Mirza Tahir Ahmad Qadiani-Khalifa wa Nne

Yeye alikuwa ni Waqif Zindagi. Kwa istilahi ya Ahadiya, huyu ni mtu ambaye kajitolea maisha yake katika mpango wa Tehrik-i-Jadid kwa ajili ya Jumuiya na haruhusiwi kufanya shughuli nyingine ya kumnufaisha na aishi kwa mafao madogo yanayolipwa na Anjuman Tehrik-e-Jadid). Kwa mujibu wa tafsiri yake mwenyewe ( yeye ni mtu wa Mungu), angali akiwa mtoto, wakati mwingine, hakuwa na shati zuri la kuvaa, hivyo, akaenda shule, akiwa amevaa Sherwani (koti kubwa) juu ya mwili usio na nguo ndani na alipooa mke akiwa anafanya kazi Rabwah hakuweza kupanda gari hivyo akawa anatembea kwa baiskeli.
Bado akiwa hajawa hata Khalifa akawa mmiliki wa nyumba tatu za mtindo wa Kimagharibi (vifaa vyote vya nyumba hizo vikiwa vimeagizwa kutoka nje ya nchi; zikakamilishwa kwa bustani na bwawa la kuogelea) mjini Ahmad Nagar, akawa mmiliki wa Kiwanda cha Nguo (Mataulo, vitani na na tepe) mjini Korangi, Karachi, mmiliki wa Tahirabad Housing Colony jirani na Rabwah, bwawa la kuogelea la biashara mjini Rabbwa na kadhalika. Vyote hivi alivipata KABLA hajawa Khalifa. Akiwa Khalifa vipi kuhusu maghorofa aliyonunua kwa kisingizio cha watumishi wa nyumba yake mjini London, maghorofa ambayo yalitumika kuwapa makaziAhmadia waliokuwa wakitafuta pa kujihifadhi, sio bure bali kwa kuwatoza kodi katika Baraza la Mtaa. Vyote hivi ndivyo vilivyounda sehemu ya dhamana aliyoweka kabla ya kufa kwake, kipato kilichotokana na dhamana hiyo kikigawanywa kwa mabinti zake.
Kwamujibu wa vyanzo vya kuaminika kutoka London, urithi ulioachwa na Mirza Tahir Ahmadi kwa ajili ya binti zake kilizidi thamani ya paundi milioni nane.
(Source: http//ahmedi.org/article/articles.php?art id=25&start=1)
Ndoa ya Bintiye Mirza Tahir: Ndoa iliyosherehekewa mno ambayo cha kusikitisha ilifeli:
“.....Ndoa ya binti mdogo kabisa wa Amirul Muuminiin, Khalifatul Masiih alRabia (Mirza Tahir), Atiya-tul-Mujiib (Tooba), Mungu amlinde, ilifanyika katika hadhara ya watu iliyojaa furaha na kheri majira ya saa moja usiku katika viwanja vya Msikiti wa Alfazl...takribani wageni 600 walihudhuria....kabla ya hilo, baada ya Sala za Ijumaa na Al-asr Huzuur alitangaza Nikah (ndoa) ambayo ilifanyika ikimuhusu Mukarram Malik Sultan Mohammed Khan Sahib, mtoto wa Mukarram Malik Sultan Haruun Khan Sahib kwa kulipa mahari ya Rupia milioni 1. (AlFazl International 19 Novemba 1999 hadi 25 Novemba 1999).
Tehrik Mpya ya Khalifa wa 5, Mirza Masruur-Kuongeza Musis wengi zaidi
.. tangu tlipopata makamo makubwa tumekuwa tukisikia tu Tahriik za Jumuiya (maombi ya Michango), kila Khalifa kaleta Tahrik mpya. Unapohudhuria hadhara ya ndoa au msiba wa mtu, wajumbe (wa Jumuiya) huwepo hapo na hurudiarudia kuzungumzia WASIA. (Ahmadia kutoka Ujerumani http//www.ahmedi.org/article/urdu/wassiyyat.php)
Baada ya Mirza Masruur kuwa Khalifa wa 5, naye akaja na wazo jingine la ujanja wa kuwachomolea fedha wafuasi wake wanyenyekevu. Mnamo mwaka 2004, alilenga shabaha kwa Mubaligha na Murabi wake kuwa hadi kufikia mwaka 2008, ikiwa ni miaka 100 baada ya kifo cha Mirza Ghulam Ahmad Qadiani, takriban asilimia 50 ya wafuasi wa Jumuiya wangepaswa kuwa MUSI,ili mwaka huo 2008atangaze kwa fahari kuwa miaka 100 baada ya kifo cha MGAQ nusu ya Jumuiya ni MUSI (zingatia mamilioni ya fedha yanakuja kwenye makasha ya familia ya Kiongozi). Mwanamke mmoja wa Ahmadia kutoka Uholanzi kaandika hivi:
“Utaratibu wa Jumuiya yetu, kwa kiasi fulani, unatofautiana na nyingine....tunaambiwa kuwa ili kumfurahisha Kiongozi wetu wa Zama hizi yaani Khalifa wa Zama hizi, tushindane katika kutoa sadaka za fedha (CHANDA); Mungu pia hupendezwa na jambo hili na kadhalika. Sasa Huzuur (Mirza Masruur, Khalifa wa 5) katangaza juu ya Wasia kuwa hadi kufikia mwaka 2008 asilimia 50 ya Jumuiya iwe MUSI. Utaratibu mbali na na pato la uhakika la Jumuiya, anapokufa Musi, kasma ya mali nayo pia itapokelewa. Sasa Huzuur kaufanya Wasia uwe nafuu sana kiasi kwamba unaweza kuwa mwema na mchaMungu hapo baadae, lakini utoe Wasia hivi sasa, Mungu atakupeleka Mwenyewe katika uchaMungu.” (http://www.ahmed.org/gazat/200410?page=3)
MUSI wa Umri wa Miaka 15
Bw. Malik Mustaq Ahmed ni Ahmadia wa kuzaliwa. Yeye ametengeneza video nyingi kufichua udanganyifu wa Jumuiya ya sasa. Katika moja ya video hizo anasema:
Nimezaliwa Ahmadia. Tumefanywa kama vile
Mfumo wa chandajaat, kuna CHANDA 35, tumetwishwa mzigo kwa Chanda hizo. Wakitumia vitisho na nguvu, Mamurabi hupokea chanda hizo kutoka kwetu, na iwapo panatokea dosari katika malipo wanayotutishia kwa vikwazo na hatua za kutengwa mbali na Jumuiya; na tunaambiwa kuwa imani yetu imedhoofika.
Bwana huyo anasema kuwa alipokea barua pepe kutoka kwa mvulana wa miaka 15 wa Ahmadia akijitangaza kwa fahari kuwa yeye ametoa Wasia. Kwa haki kabisa Bwana huyo anauliza, inawezekanaje kwa mtoto ambaye, kisheria, hastahili hata kutoa ushahidi, awe MUSI. Inakuwaje wakati yeye hana chochote anachochuma awe MUSI? Kutoka chanzo gani ataweza kutoa CHANDA ya lazima kila mwezi. Je atachukua kutoka kwa wazazi wake kutoa CHANDA ya kila mwezi kwa Jumuiya? Hii ni kinyume na masharti yaliyowekwa na MGAQ. Na ataendelea kutoa kiasi kinachozidi kuongezeka kwa miaka 40 au hamsini ijayo!!! Lakini nani anayejali, Murabi na Mubaligh wao yawabidi wamfurahishe Khalifa!! (http://nx--mgb4dcqb.net/video/mvmlfyOU/--ahmadiyya.html)
Tunamuomba MwenyeziMungu amlipe ndugu yetu Mushtaq kwa jitihada zake, Tunamuomba MwenyeziMungu ampambanulie yeye, awapambanulie Ahmadia wote na atupambanulie sote haki kama ilivyo na atupe Taufiiq ya kuifuata, na atupambanulie batili kama ilivyo na atupe uwongofu wa kuepukana nayo. Amiin.
Abul Akhaz-Babaake Taker
Molvi Hayat Abul Ata alikuwa Mubaligha wa Ahmadiyya ambaye alitumwa katika nchi za Arabuni kwenda kushajiisha uhamadiya. Mkakati ukawa uleule, kukusanya CHANDA kila inapotokea nafasi. Yeye anasimulia mkasa wa mwaka 1934 wakati alipokuwa mjini Cairo na akataka kukusanya CHANDA kununua mtambo wa kuchapishia. Kaandika hivi:
Ndugu yangu Ustadh Muniir Afendi Al-Husni tayari alishakuwa Ahmadia. Kakaake mkubwa As-Syed Mohuddin Al-Husni Al-Marhuum ambaye alikuwa ni mfanyabishara mkubwa mjini Cairo aliingia katika dini ya Ahmadiyya katika kipindi changu, pia alikuwepo katika mkutano huu. Nikaomba CHANDA na jamaa nao wakatangaza CHANDA na ndio walioanza kutoa. Naye akatoa kiasi kikubwa cha CHANDA lakini kwa nia nzuri akasema! “Ya ustaz innaka abul ataa wa laakinaaka daaimun tahriznaa ‘ala taburruaat, fa limaa laa tismaa ismukaa abal akhaz’-O Ustadh! Wewe ni Abul Ata (mtoaji) lakini mara kwa mara unatukarahisha na CHANDA. Kwa nini basi usibadili jina lako liwe Abul Akhaz (mchukuaji)?” (Al-Furqan, Rabwah, Juni 1971 uk.25-26; AlFazl In ternational juz.15 Na. 46 tarehe 14 Novemba 2008).
Mirza Mubarak-Mkuu wa Harakati za Nje
Mirza Mubarak (mwanajumuiya mwingine wa Familia Kiongozi ya Ahmadiyya ndiye aliyekuwa Mkuu wa Harakati za Nje pamoja na Tehrik-i-Jadid na alikuwa akisafiri (daraja la kwanza) huku na kule duniani (Katika miezi ya majira ya kiangazi) kwenda “KUKAGUA” Harakati za Ahmadiyya nchi za nje. Wakati mmoja( huenda ni kawaida yake lakini mimi ni shuhuda wa wakati huu mmoja tu) alipeleka maagizo yake kwa Imamu wa Msikiti wa London aombe itengwe NAFASI kwa ajili yake na mkewe katika Hoteli ya Nyota 5 mjini Brighton NA NAFASI HII LAZIMA ITAZAMIE BAHARINI. Kilichotokea ni hadithi nyingine lakini jambo muhimu la kueleza ni kwamba Hakuutembelea Msikiti wa London hata siku moja. Aliwaalika tu hapo (hotelini) Imam na Naibu Imam kwa nyakati tofauti kwa ajili ya huo UKAGUZI wake.
Ahmadia! Msiingiwe na kihoro. Kuna maelfu ya mikasa hiyo ya Khidmati Islam kwa fedha za chanda kuanzia miaka ya awali ya Mirza Mahmud kuponda starehe za safari ambapo yeye na “ujumbea’ wake waliburudika na majira ya Kiangazi katika Vituo vya Milima huku Jumuiya ikiendesha shughuli zake kwa kukopa fedha. Waajiriwa wa Jumuiya (akiwemo baba yangu) mjini Qadian hawakupata vijishahara vyao kwa miezi na miezi huku Mirza Mahmud na familia yake wakiwa kwenye matembezi ya starehe kule Dalhousie na Simla. (Wauza maduka wote mjini Qadian walikataa kuendeleza vifaa vya mkopo kwa ajili ya manunuzi katika duka letu kwa sababu hawakuwa na salio la mtaji ili kununua bidhaa kwa ajili ya kuwasambazia wakopaji kama sisi.)
(Chanzo: http://ahmedi.org/article/articles.php_id=25&start=1)
Chanda ya Jumuiya Katika Nyakati za Karibuni
Baadhi ya mifano ya UTARATIBU WA CHANDA inatolewa hapa ambayo sasa imekuwa na mtandao zaidi.
1   2   3   4   5


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət