Ana səhifə

Bismillah Ar-Rahman Ar-Rahiim Harakati za Uislamu dhidi ya Ahmadiya Chungu Mosi, Rabiul Awwal 1430 Februari 24, 2009


Yüklə 0.51 Mb.
səhifə4/5
tarix26.06.2016
ölçüsü0.51 Mb.
1   2   3   4   5

....hivyo, mimi nilifikiri kuwa nitawaalika matajiri na wenyenacho kusaidia harakati zangu...

....lakini kwa vile wanadamu hawakosi kudhaniana vibaya na kutoaminiana na kufikiriana na bila kutambua kuwa imani pia haijengeki, ambayo ndiyo ya kujenga moyo wa kufanya mambo makubwa, hivyo natoa tangazo la jumla kwa Wakubwa wote kuwa kama wanasita kusaidia bila kuutahini (uwezo wangu), wanitumie kwa maandishi baadhi ya matakwa yao, matatizo yao na shida zao, ili nami niwaombee kuwatimizia wayatakayo, lakini waandike wazi kuwa pindi malengo yao yatakapofikiwa, ni kwa kiasi gani na wao watatoa msaada na kwamba waandike kuwa wameweka dhamira ya dhati kabisa na ya mwisho kabisa kuwa hapana shaka yoyote watatoa msaada huo wa fedha....” (Matangazo ya Aprili 1893, Majmuu-e-Ishtihaarat, Mkusanyo wa Matangazo, juz.1 uk.387-389).
Mkakati wa Kupata Mfuasi wa dhati
Haji Seth Abdur Rahman amekuwa mfuasi mkereketwa wa Mirza Ghulam ambaye alikuwa akituma michango mikubwa mara kwa mara. Fungua Mkhtuubaat-e-Ahmadiyya juz. 5, sehemu 1 na utakuta lundo la barua kutoka kwa Mirza Ghulam akikiri kupokea michango aliyoipokea:
...jana nilipokea posta Rupia 100 kutoka kwako...” (Makhtuubaat-i-Ahmadiyya juz. 5 sehemu ya 1 uk.3).
“...jana nilipokea wahayi....maana yake ni kwamba mtu mmoja hivi atatoa sehemu kubwa ya mali yake kwangu kama hidaya...Niliomba kuwa kwa kipindi fulani wewe ndiye utakayeshabihiana na wahayi huu, na namuomba Mungu ajaalie hivyo, kiasi cha Rupia 100,000 au 200,000 si fungu kubwa kwa ajili ya Mungu...” (Makhtuubaat-i-Ahmadiyya juz.5 sehemu ya 1 uk.20)
..“leo nilipokea Rupia 100 kwa njia ya posta.....Napata msaada huo mkubwa katika kazi yangu kwa pesa zako kiasi kwamba sipata hata kusema.....Sina uchungu mkubwa sana kwamba kwa sababu ya kukosa fedha nashindwa kuchapisha vitabu vya dini. Kwa ajili hii, nafikiria mkakati huu kwako kwamba ujipangie kiasi fulani moyoni mwako ambapo kama ukipata mafanikio mazuri katika biashara yako basi utume utume fungu kwa ajili ya kazi hii...” (Makhtuubaat-i-Ahmadiyya juz.5 sehemu ya 1 uk.21).
Kuna barua nyingi kama hizo kutoka kwa MGAQ kwenda kwa Seth Abdur Rahman, katika kila barua kakiri kupokea fedha taslimu, akimbashiria habari njema za Mungu kumkubalia CHANDA yake (mchango wake) hata kabla haijamfikia yeye MGAQ, akimtakia baraka tele na kumuombea dua azidishiwe katika biashara zake na mwishowe akimuomba atoe CHANDA (mchango) zaidi. Kuna wafuasi wengine wengi watiifu ambao walitapeliwa kwa njia kama hiyo.
Njia nyingi za kujipatia pesa!
MGAQ alitumia njia kadhaa kuvuna mapesa kutoka kwa wafuasi wake. Moja kati ya njia hizo ilikuwa ni kumshawishi mfuasi wake mwaminifu kuamini kuwa Munge ameiridhia ‘NAZAR’ au CHANDA yake kwa kutangulia kubashiri kuja kwake:
Kipenzi changu, mpendwa wangu, ndugu yangu Dkt. Khalifa Rashiiduddin Sahed....Leo nilipokea Rupia 50 kutoka kwako kwa njia ya posta. Allah akulipe. Inashangaza kuwa siku hizi nakuwa katika shida kubwa. Leo Novemba 1898 nimeoteshwa ndotoni kuwa mtu mtu ananitumia pesa. Nilifurahi sana na nikaamini kuwa leo pesa itakuja. Hivyo, leo Novemba 4, 1898 nilipokea pesa. Hivyo, Alhamdulillah, na namuomba Mungu akulipe. Yaelekea kuwa kutuma pesa kunaridhiwa mbele ya Mungu. Hivyo, leo ambayo ni Ijumaa nilikuombea dua kwa Mungu katika Sala ya Ijumaa. Natumai kuwa nitafanya hivyo mara nyingi. (we endelea tu kutuma pesa! Rashid). Nakupenda kwa dhati kabisa na moyo wangu unatamani kwa hamu kubwa uje karibu nami.” (Barua ya Mirza Qadian, iliyochapishwa katika Akhbar Al-Fazl Qadian Na. 1-2, Juz. 34 28 August 1942)

Kwako Haji Seth Abdur Rahman” “...jana nilipokea wahayi....wenye maana kuwa mtu fulani atatoa sehemu kubwa ya mali yake kama hidaya...Niliomba kuwa kwa kipindi fulani wewe ndio ushabihiane na wahayi huu na Mungu akujaalie, kwani kiasi cha 100,000 au 200,000 si fungu kubwa kwa ajili ya Mungu...” (Makhtuubaat-i-Ahmadiyya juz.5 sehemu ya 1 uk.. 20)
Kwako Haji Seth Abdur Rahman: “Nilipokea kwa njia ya posta Rupia 100 kutoka kwako....moyoni mwangu naitakidi kuwa ni nia ya MwenyeziMungu kukupa wewe malipo makubwa.....Nakupenda kwa dhati kabisa na huwa nakuombea dua bila wewe mwenyewe kuwepo...” (Makhtuubaat-i-Ahmadiyya juz.5 sehemu 1 uk.2-3, tarehe 9 Desemba 1894).
Kwako Haji Seth Abdur Rahman: “..siku chache zilizopita niliota ndoto kuwa niko mahali fulani, tahamaki nikaona kitu cha kutatanisha, fedha zikawa mbele yangu na nikashangaa zimetokea wapi; basi nikaona kuwa Malaika wa Mungu ndiye aliyeiweka hapa kwa ajili ya mahitaji yetu. Nikapata wahayi kuwa ‘ninakutumia zawadi’ na ikaelezwa moyoni mwangu kwamba swahibu wetu wa dhati Haji Seth Abdur Rahman Sahib anafananishwa na malaika na inavyoelekea atatuma pesa, na nikaandika ndoto hii kwa Kiarabu katika kitabu. Basi jana ikatimizwa. Alhamdulillah hii ni ishara ya kukubalika, kwamba Mungu kathibitisha ndoto hii kwa njia na whyi.” (Makhtuubaat-i-Ahmadiyya juz. 5 sehemu ya 1 uk.3, letter No.5, Machi 1895)
Kwako Seth Abdur Rahman: “Jana nilipokea Rupia 100 kwa telegramu....Hii ni Rehema ya Mwingi wa Rehema na ishara ya kukubalika kwa utumishi ambao wote huwa nafahamishwa kabla ya wewe hujatoa msaada wa kifedha, hiivyo ndivyo jambo hilo lilivyotokea ambapo kwa wengine jambo kama hutokea kwa nadra....” (Makhtuubaat-i-Ahmadiyya juz.5 sehemu ya 3. Barua Na.6, June 1896).
******************
Pesa- Ndiyo Kigezo cha Mafanikio
Katika Kitabu chake Haqiiqatul-ul-Wahi, MGAQ kaelezea ishara 140 za ukweli wake, nyingi kati ya hizo zinahusiana na masuala ya fedha:
...basi Molvi Abdul Haq Ghaznavi akaamka na kufanya Mubahila na mimi.....Mungu akaninyanyua na kunionyesha ishara kubwa kubwa kutoka mbinguni na kutoka ardhini pia na akawageuze watu wengi waelekee kwangu. Pale mubahila ulipofanyika, karibu watu 40 wakawa wafuasi wangu na sasa idadi yao inakaribia 70,000 ambapo FUTUUHAAT ni zaidi ya 200,000 na ulimwengu wa watu uko kama watumwa wafuasi wangu...na nendeni mkamuone Abdul Haq Ghaznavi dukani au sokoni kule Amritser jinsi anavyokwenda...” (Nuzuul-i-Masiih, Roohani Khazain juz. 18 uk. 410) (herufi za saizi kubwa kwa kitabu chenyewe).
Riziki na starehe zetu zote zilitegemea kipato kidogo cha babaangu na hakuna mtu baki aliyenijua mimi na nilikuwa mtu nisiyefahamika nikiishi kwenye kijiji cha jangwani cha Qadian....ndipo Mungu, kwa mujibu wa bishara yake, akageuza ulimwengu wa wanadamu unielekee mimi na akanisaidia kwa namna ambayo naweza kusema kweli kuwa hadi sasa karibu Rupia 300,000 zimeingia au pengine ni zaidi ya hizo...” ((Haqeeqat-ul-Wahi, Roohani Khazain juz.22 uk.220-221)
“Kama hamuamini maneno yangu, basi nendeni wenywe mkaone kwenye daftari la Ofisi ya Posta ili mjue mlango wa mapato umefunga kiasi gani katika kipindi hiki. Mapato hayo hayaishii katika njia ya posta, badala yake maelfu ya rupia huja katika namna ambayo watu huja wenyewe hapa Qadian kutoa, isitoshe kuna mapato yanayokuwa (kwa sarafu) na noti ndani ya bahasha.” (Haqiiqat-u-u-Wahi, Roohani Khazain juz.221).
Ingawaje maelfu ya Rupia yameingia kwa njia ya hawara ya fedha, lakini zaidi ya hivyo, ni kwamba kiasi ambacho watu wenye nyoyo za dhati wametoa kibinafsi na pesa iliyokuja katika barua na baadhi ya watu wenye moyo wa dhati wametuma pesa au dhahabu kwa namna ambayo hawakutaka kutaja majina yao na mpaka hivi sasa, mimi siyajui majina yao.” (Haqiiqat-ul-Wahi, Roohani Khazain juz. 221, tanbihi)
Dau la Pesa- Kipimo cha Ukweli cha Mirza
Mirza Ghulam Ahmad Qadian alikuwa mtu mashuhuri kwa kujitangaza magazetini. Mwanzoni wakati alipojifanya kuwa yeye ni mtumishi wa Uislamu, alikuwa akiwachagiza wapinzani wa Uislamu kwa njia ya uchokozi. Baadae akatumia mbinu hiyo hiyo kuwakabili wapinzani wake. Methodolojia yake ilikuwa ya kivyake-vyake. Simjui ni mtume yeyote wa Mungu wala simjui mwanazuoni wa tabaka lolote lile aliyeweka malipo kwa maandiko au madai au matamshi yake. Jambo hili lilibainisha kasumba yake binafsi kwamba pesa ndiyo iliyokuwa juu ya akili yake. Hata hivyo, alikuwa mjanja kwelikweli wa kuweka masharti hayo ili asipoteze pesa.
Matangazo Rupia 500: Iwapo mtu fulani kutoka Arya Samaj anaweza kuzikataa aya zangu....nitampa malipo ya fedha taslimu.” (Tangazo la tarehe 2 Machi 1878, Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.1 uk.1-2)
Yeyote atakayekataa aya zangu zilizomo katika kitabu hiki.....nitatoa mali zangu zenye thamani ya Rupia 10,000 na kumkabidhi yeye kila kitu.” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz. 1 uk. 11-12, tangazo la Mwezi Mei 1879)
Mimi, ambaye ni mtunzi wa kitabu hiki, Brahiin-i-Ahmadiyya, kwa ahadi ya kutoa Rupia 10,000 (Rupia 150,000,000 = dola za Marekani 3,000,000 kwa thamani ya fedha ya sasa), natangaza dhidi ya viongozi wa dini zote na Mataifa yote....yeyote atakayekataa aya na ishara kuhusiana na ukweli wa Qur’an Tukufu na Ukweli wa Unabii wa Khatimul Anbiya SAAW.....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.1 uk.72, Matangazo la Mei 1880).
Hivyo, alihusika kuwafungulia mlango watu wa imani nyingine kuandika dhidi ya Qur’an na Mtume Mtukufu SAW!!!
Kwa Mheshimiwa Padri Sahebaan wa Punjab na Hindustan na Uingereza na Mheshimiwa Brahmin Sahebaan, na Arya Sahebaan na Naturasti Sahebaan na Hazraat Molvi Sahebaan....ambao wanakanusha kuwepo kwa miujiza na matukio yasiyo ya kawaida na kwa sababu hiyo, waanampinga mtu huyu mnyenyekevu....waje Qadian kama ni mujitahidi wa kweli na wakae nami kwa MWAKA MMOJA na wajionee kwa macho yao ishara hizi za mbinguni. Kama mkija na msione ishara yoyote ya mbinguni kwa MWAKA MMOJA, basi mimi nitalipa fidia kwa kiasi cha Rupia 200 kwa mwezi...” (Majmuu-i-Ishtihaarrat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz. 20-21, hakuna tarehe)
Kwa kuwa ninyi hamsisitizi kupokea pesa kama sharti la mwanzo, bali kwa moyo safi mnataka kuona ishara, kwa upande wangu pia hakuna sharti la kuukubali Uislamu.....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz. 1. uk.96 hakuna tarehe)
Ishtihaarat Mufiid-ul-Akhyaar-Akihutubia waariya wa Kihundi na Wamisheni wa Kikristo: “.....Kama wana hoja za kupinga Qur’an Tukufu....nikishindwa kutoa jibu la kuridhisha na kutosheleza....kisha kwa hali hiyo, kwa kule kushindwa kwangu, nitalipa fidia ya Rupia 50 kwa kila hoja...” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.1.uk.121, Sept 1886).
Ishtihaar Ina’ami Rupia 500 kuhusiana na kitabu kisicho na mfano ‘Kuhul al-Jawahir Surma Chasma-i-Arya’.....hiki kinafutilia mbali kabisa imani potofu ya Vedas. Kimeandikwa kwa dai na imani hii kuwa hakuna arya anayeweza kukosoa kitabu hiki.....Namtaka Arya Sahib yeyote yule kwa jina la Aishwer yuleyule kuandika tahakiki ya kupinga kitabu hiki achukue zawafi ya Rupia 500....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.1. uk.133-134, Sept 1886).
Arya mmoja wa Kihindu alikuwa akipinga madai ya MGAQ na akaifanyia dhihaka mialiko yake na akajificha bila utambulisho wake kujulikana kabisa. Kutokana na maandiko yake, ni wazi hii ilimuuma MGAQ: “...ni lazima sana kwamba nikomeshe vitendo vyake huyu ambaye amekuwa akificha uso wake mafichoni, wakati mwingine akituapia katika matangazo yake, wakati mwingine anatushutumu na kutunasibisha na matapeli na wakati mwingine anatutangaza sisi ni mafukara tusio na pesa na anasema twende kwa nani sijui tukapambane naye, yeye hana mali yoyote ya kutupa.....sasa namtaka rasmi ajitokeze kwa ushindani, toa uso wako mafichoni na njoo mbele yetu, na nitajieni jina lake....ukae pamoja nami kwa siku arobaini...Kama hakuna bishara ya ilihamu inayodhihiri katika kipindi hiki, basi kwa kukufidia siku hizo arobaini, Rupia 100 au mshahara wowote ambao kaupata katika serikali ya Mwingereza kwetu utakuwa mara dufu....ifahamike kuwa kwa ajili ya kumridhisha yeye, hela hili zitawekwa kwa Brahmin Sahib.....namuagiza tena huyu jamaa wa arya ambaye katwita sisi waongo, kauita ufunuo wa Mungu uongo mtupu, kama walivyokuwa maarya washenzi wa zamani na yeye huyu katumiminia matusi mabaya, katishia kutuua, katukaripia kuwa kwa kututukana kwa tusi lolote ndio alikuwa anatimiza utashi wake , alitoa matusi yote, lakini kama kweli yeye ni mtoto wa halali (halaalzada), basi ajitokeze mbele yetu kwa jaribio hili, ili na sisi tumuone yukoje huyu mtu mwenye ulimi wa kiungwana wenye asili ya Malaika. Lakini asipojitokeza hadi mwishoni mwa Mei, 1887, na asipoacha tabia yake ya urathi, basi kwa kumtanguliza Mungu nawaahidi watazamaji wa tangazo hili kuwa nampa Mwongo na Mgomvi huyu zawadi ifuatayo ambayo anastahili kwani yeye ni mtu mkali na katili ambapo ili nione kama atatoka shimoni kwake au ameze na zawadi hii pia. Na zawadi hiyo kama hajitokezi na kukimbia ni hii:
Laana 1 Laana 2 Laana 3 Laana 4 Laana 4 Laana 5 Laana 6 Laana 7 Laana 8 Laana 9 Laana 10”
(Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.1, uk.137-140, Sept 1887)
Wow!! Hasira gani gani hizi! Je kweli huu ndio mwenendo wa mtu aliyechaguliwa na Mungu! Nadhani kitu ambacho kimemuuma zaidi nafsini mwake na kumkera ni lile dai kuwa Mirza hana pesa wala mali!
Kama bishara yangu iliyotolewa ni upuuzi na uzushi mbele ya macho ya hadhira, haiko juu ya uwezo wa binadamu au hatimaye ikionekana kuwa ni uwongo, basi mimi nitamlipa Rupia 200 Padri Sahib.....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz. 1, uk.151, tareh 19 Juni 1888).

...hivyo Padri Brachet akifanya mhadhara mjini Batala basi atoe ahadi kwa kula kiapo kuwa kama nitamtajia vitu vilivyomo ndani ya bahasha iliyofungwa ambayo kaileta yeye, basi yeye papo hapo ataukana Ukristo na kuwa Muislamu. Na asipofanya hivyo, basi atatoa Rupia 1000 kwa jumuiya ya Anjuman Hemayat-i-Islam, Lahore......iwapo ndani ya siku kumi nitashindwa kutaja vilivyomo ndani ya bahasha iliyofungwa...basi nitaachana na dai langu la kudai la kupokea Wahyi...” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.1. uk.152,tarehe 9 Juni 1888).


Iwapo Molvi Syed Nazir Hussein Saheb anaweza kutoa Aya na Hadith kuthibitisha imani yake kuwa Hazarat Masiih Ibn Maryam kapaishwa mbinguni na damu yake.....basi mimi naapa kwa Mungu kuwa nitampa Rupia 25 kwa kila Aya na Hadith.” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz. Uk.249, tarehe 17 Oktoba 1891).
Kuandika mada ya kifo cha Hazarat Issa Ibn Maryam: “Iwapo mtu yeyote anaweza kuonesha dalili kutoka katika Qur’an na Hadith au Mashairi ya Kiarabu....kwamba neno “Tawwafanii’, maana yake ni kitu kingine na si kutolewa roho na kufa.....basi mimi nitampa mtu huyo Rupia 1000....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz. 1. uk.286, hamna tarehe, ilichapishwa katika Izala-i-Auham sehemu 2 uk.917)
Kumpa changamoto ya Mubahila Dkt. Clark, Mmeshenari wa Kikristo
“...yapasa kuwe na dua ya mubahila baina ya pande mbili....kumuomba Mungu aonyeshe ishara fulani ya mbinguni ndani ya mwaka mmoja...kisha kwa fadhila ya upande wowote ule ishara fulani ya mbinguni ionyeshwe...yule anayeshindwa aingie katika dini ya upande mwingine ambayo ndiyo iliyoshinda...na akikataa kubadili dini, basi hapana budi akabidhi nusu ya mali yake kwa upande ulioshinda....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.1, uk.411, tarehe 8 Mei 1893).
Rupia 2 kwa kila kosa moja: “...Waandike kitabu kulinganisha na kitabu changu ‘Sirrul Khilafat’, na kisha iwapo kitabu chao kisipokuwa na makosa na kikilingana na kitabu changu kwa ufasaha, basi mbali ya zawadi ya kuandika kitabu kinachofanana nacho, pia nitalipa Rupia 2 kwa kila kosa moja.” (majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2.uk.14, hakuna tarehe)
...Fanyeni tafsiri inayofanana na tafsiri yangu mpate donge nono la Rupia 1000.” (Majmuu-i-Ishtiharaat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2, uk.16, tarehe 16, Muharram 1312)
..andikeni kitabu kinachofanana (na kitabu changu) ‘Nur ul Haq’, mchukue Paundi 5000...”
Nilikusanya ‘Karamatus Sadiqiin kwa Kiarabu...mtu yeyote akiweza kuandika kitabu kinachofanana na kitabu changu, nitatoa donge nono la Rupia 1000....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2, uk.16 ya Muharram 1312)
..sasa nimeandika ‘Sirrul Khilafah’ ambayo ni fupi tu....tunawapa (wapinzani akina Molvi) siku 27 (kuandika kitabu cha mfano wa kitabu changu). Tutachapisha kitabu hiki kwa bei ya Rupia 1 kwa siku, hii ni zawadi ya Rupia 27.....msiiachie Rupia 27 (msisitizo ni kwa kila matini halisi). Tumesikia kuwa Sheikh Sahib anakabiliwa na dhiki kwa sababu ya ufukara, kwa hiyo, siku hizi, Rupia moja ni kama sarafu ya dhahabu, Rupia 27 ni sarafu 27 za dhahabu....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2, uk.18, Muharram 1312)
..dua hii isipojibiwa ndani ya mwaka mmoja na isiposhuka adhabu ya kumpatiliza mwongo, basi mimi nitamlipa Bw. Abdullah Atham Rupia 1000 kama faini.....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2 uk.30 tarehe 5 Sept.1894)
...pale Bw. Atham atakapokiri....jumuiya yangu itasema Amiin, kisha wakati huo huo hati ya ahadi ya Rupia 1000 itatolewa kwake.....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2. uk.51 tarehe 9 Sept 1894)
Tangazo la Donge nono la Rupia 2000 kwa mara ya pili. Hizi zitatolewa bila kukawia iwapo atakula kiapo kuwa yeye hakuvutiwa na Uislamu na hivyo akabaki kuwa adui wa Uislamu)....(Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2 uk.56, tarehe 20 Sept 1894)
Donge nono la Rupia 3000 litatolewa bila kukawia kama Bw. Atham akila kiapo hakuvutiwa na Uislamu na akabaki kuwa adui wa Uislamu)...” (Majmuu-i-Ishtihaarat Mkusanyiko wa Matangazo, juz. 2, uk..64 tarehe 5 Oktoba 1894)
Donge nono la Rupia 4000 zitatolewa bila kukawia kama Bw. Atham atakula kiapo (kwamba hakuvutiwa na Uislamu na akabaki kuwa adui wa Uislamu)...” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2, uk.69,tarehe 27 Oktoba.1894)
Kwa nini MGAQ alijaribu kiasi kikubwa namna hiyo kwamba Bw. Abdullah Atham ale kiapo? Ni muhimu kusoma kisa kizima ama katika kitabu chake au katika: Death of Deputy Abdullah Atham (http://alhafeez.org/rashid/atham.htm)
Donge nono la Rupia 5000 kwa arya au yeyote atakayeandika kitabu......kuthibitisha tofauti ya Sanskrit au lugha nyingine yoyote kukipiku Kiarabu...kitabu changu Manan-ur-Rehman....” (Majmuu-i-Ishtihaarat. Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2.uk.136, 1895)
Tangazo la Pili la donge nono Rupia 1000: Mimi nadai kuwa kwa kulinganisha na bishara za Yesu, bishara na ishara zangu zinaonekana kuwa zaidi. Padri yeyote yule akiweza kuonesha uthibitisho kuwa bishara na ishara za Yesu ndiyo zenye nguvu zaidi basi mimi nitampa Rupia 1000 taslimu.” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2, uk.314, hakuna tarehe)
Donge nono la Rupia 1000 kwa Mkristo yeyote yule anayeweza kuthibitisha kuwa ishara za Yesu ambazo ni ishara za uungu wake ndizo nyingi na zenye sifa ya kiungu basi mimi nitampa zawadi ya Rupia 1000.” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.2, uk.69, tarehe 317 Januari 1897)

Donge nono la Rupia 20,000.....Hazarat Issa amekwenda mbinguni kwa kiwiliwili na hapo baadae atarudi tena duniani, kama kuna mtu anayeweza kutoa Hadith hiyo basi mimi nitampa zawadi ya Rupia 20,000 kama faini kwa mtu huyo, na kuomba toba na kukichoma moto kitabu changu kutakuwa sehemu ya hatua hii...” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.3, uk.84, pia taz. Kitabul Bairiyah uk. 189-193)


Mzozo wa mwisho na Molvi Muhammad Hussein Batalvi....Mwaliko wa Mubahila bila masharti yoyote na Zawadi ya Rupia.2525.50.....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.3, uk.90)
Kumchagiza Hazarat Pir Mehr Ali Shah kuandika sherehe ya Kiarabu na MGAQ naye ataandika sherehe ya Surat Fatiha kuthibitisha dai lake na “...Kama Maulamaa watatu wasio upande wowote wakitanhgaza kuwa kitabu cha Pir Sahib ni bora zaidi kwa ufasaha na hekima ya Qur’an basi mimi natoa ahadi ya kweli kuwa nitampa Pir Sahib Rupia 500 taslimu papo kwa hapo...” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.3, uk.371 tarehe 15 Desemba 1900)
Kama Pir Sahib anaweza kuandika kitabu cha mfano wa kitabu changu, na kubatilisha dalili zilizotolewa humo...basi mimi nitampa zawadi ya Rupia 50 papo hapo....” (Majmuu-i-Ishtihaarat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.3, uk.476 tarehe 1 Sept 1902)
Tangazo kwa Rupia 10,000: tangazo hili ni kwa ajili ya kutangaza ile ishara ishara ya Mungu ambayo kama zilivyo nyinginezo, nayo pia itatimiza bishara....Nimeandika utenzi ambao ni ishara isiyokuwa ya kawaida na ni njia rahisi ya kutatua mambo.....Zawadi ya Rupia 10,000 kwa mtu atakayeandika utenzi unaofanana na huu....lakini kama bado wapinzani wangu watakwepa kwa makusudi basi sio tu watakosa zawadi hii ya Rupia 10,000 bali LAANA 10 zitakuwa kasma yao ya milele......” (Majmuu-i-Ishtiharaat, Mkusanyiko wa Matangazo, juz.3, uk.478-479 hakuna tarehe)
********************
Ndoto ya Mirza kuhusiana na Qadian
Tuliota ndoto kuwa Qadian imekuwa jiji kubwa na soko limepanuka nje ya upeo wa macho. Maghorofa ya Roshani mbili na nne au yapo maduka yenye ngazi ndefu zaidi yaliyotengenezwa katika majumba mazuri, na vibonge vya watu matajiri waliofutuka matumbo, ambao wanachangamsha masoko, wanakaa ambapo mbele yao, kuna malundo ya vito vya thamani, almasi, lulu, pesa na sarafu za dhahabu.” (Matamshi ya Mirza katika gazeti la AlHakm Newspaper Qadian la tarehe 3 Aprili 1902).
Falsafa ya Utume wa MGAQ
Wateule wa Mungu, ambao hutokea Mbinguni, huwa na dhamana ya kufanya biashara na Jumii yao. Hujichumia utajiri wao wa muda na huwafanya kuwa warithi wa utajiri wa milele...” (Makhtuubaat-e-Ahmadiyyah juz.5 sehemu ya 1 uk.31, tarehe 26 Sept 1899) (SubHanAllah! Ujanja gani huu!!)
Funuo 50,000 kuhusu Pesa
Ni dhahiri kuwa kutokana na hayo yaliyoandikwa juu pesa ndiyo inayochukua nafasi muhimu katika maisha ya MGAQ. Hii inadhihirika katika funuo ambazo Mirza alikuwa akidai kuzipokea. Kwafahari, yeye mwenyewe alitangaza jambo hili kuwa ni moja ya ishara:
Ikumbukwe kuwa Mungu huwa na kawaida moja na mimi kwamba rupia hasahasa taslimu ziwapo mbioni kuja au vitu vingine vijavyo kama zawadi, Yeye hunitaarifu ama kwa wahyi au kwa ndoto ambapo aya za namna hiyo ni nyingi zaidi ya 50,000.” (Haqeeqat-ul-Wahi, Roohani Khazain juz.22 uk.346)

Mifano Michache ya Funuo za Pesa
Katika ndoto yangu mtu mmoja kasema: Noti za fedha hizo. Basi hapo nikapewa kitabu kana kwamba ndani yake kilikuwa na noti za fedha na wahyi ukatiririka kutoka kwenye ulimi wangu (lugha ya ki-Urdu): Zingatieni rafiki zangu, habari hiyo imechapishwa.” (Al-Hakam, Juz.10. Na.6, Februari 17, 1906, uk.1;Tadhkirah toleo la 2 uk. 589).
Niliona karatasi ndotoni, mistari michache ya mwanzo katika kiratasi hiyo iliandikwa kwa herufi za Kiajemi na zilizosalia zote kwa Kiingereza. Mimi nikaelewa kama vile mtu kanitaja jina na kusema: (Kwa Kiurdu): Huyu apewe rupia 25. (Review of Religions, juz. IV, Na.2, Feb.1905)

Niliona katika ndoto yangu kuwa mke wa Qudratullah kanizawadia rundo la rupia” (Al-Hakam, Juz. 9, Na.36, Okt.171905,uk.10)


Niliona katika ndoto yangu karibia na asubuhi kuwa mtu mmoja kanipa mfuko wa karatasi uliojaa rupia ambazo nilizipokea na nikaanza kuzifunga kwenye kitambaa cheupe.” (Diary of the Promised Messiah, uk.23)
Punde nilipopata wahyi kuwa rupia 21 ziko mbioni kuja. Basi wahyi huu pia wakaelezwa Waarya (Wahindu wanaoishi Qadian)....zaidi ya hivyo ili kuwafanya waarya hao wawe mashahidi, pipi zenye thamani ya Rupia 1 zikagawanywa miongoni mwao...Kama si vinginevyo, basi wangekumbuka ishara hii baada ya kula pipi hizi.” (Roohani Khazain juz.22 uk.318).
TEECHEE TEECHEE-Malaika wa Pesa
Wakati fulani mwezi Machi 1905, kwa sababu ya uhaba wa kipato (yeye michango aliona ndio kama kipato-Rashid), kulikuwa na shida kubwa katika gharama za Langerkhana (jiko la hadhara) kwa sababu wageni walikuwa wanakuja kwa wingi na kwa kulinganisha na wingi huo, vipato vya fedha vilikuwa vidogo, kwa hali hiyo dua zikaombwa. Nikaota ndoto tarehe 5 Machi 1905 kuwa mtu mmoja aliyeonekana kama malaika akaja mbele yangu na kuweka pesa nyingi kwenye paja langu. Nikamuuliza jina lake, akasema hana jina. Nikasema lazima kuwe na jina fulani. Akasema jina langu ni Teechee Teechee.....” (Haqeeqat-ul-Wahi Roohani Khazain juz.22 uk.346)

KITENDAWILI CHA MAISHA YA KAWAIDA
MGAQ ashutumiwa kwa Kufuja Fedha za Umma
Unaweza kuwadanganya baadhi ya watu kwa mudafulani lakini huwezi kuwadanganya watu kwa wakati wote. Kwa hakika, si watu wote katika Jumuiya yake walipofuka kwa utii wa kijahili, wakaanza kung’amua mambo na kupaza sauti na huku wakielezea wasiwasi wao juu ya ung’ang’anizi wa fedha wa Mirza. Hili ni jambo baya mno linaloweza kutokea kwa mzushi yeyote anayedai hadhi ya kutumwa na Mungu. Hata wafuasi wake wa kufa na kupona nao wakaanza kuutilia shaka uadilifu wake. Yeye kawahubiria wafuasi wake waishi maisha ya kawaida, wajitoe muhanga na wawe na imani juu ya MwenyeziMungu lakini yeye katika maisha yake hakuwa anatekeleza yale aliyoyahubiri jambo ambalo ;i;iwaudhi baadhi ya wafuasi wake wasomi kama inavyobainisha mifano hii.
Fedha zilizokusanywa Zatumika kwa Maisha Binafsi ya MGAQ:
Sasa tuone kama Mahdi aliyeahidiwa alikuwa akiipa familia yake au kuwapa ndugu zake fedha zilizotokana na makusanyo ya michango au kutoka katika chanzo kingine chochote kile. Kila mmoja anajua jambo hili kuwa Huzoor (Mirza) alikuwa akitoa kutokana na makusanyo hayo hayo. Hivyo baada ya (kufa) kwake ikawa wajibu kwa Jumuiya (ya Ahmadiya, Qadian) kuwa itoe kama vilevile katika michango hiyo kama alivyokuwa akifanya Hazrat Masiih Muwuud, kwa kuwa jumuiya haiwezi kuwa na uaminifu zaidi ya Masiih Muwuud.” (Izhzaar—Haqeeqat uk.13 tarehe 28 Novemba 1913, iliyochapishwa na Anjuman Ansarullah Qadian).
Pesa Zatumika Katika Maisha ya Nyumbani.
Mwanzoni tulikuwa tukiwaambia wanawake wake kuwa wafuate maisha ya mitume na maswahaba., wale vitu kidogo na vikavu, na wavae nguo duni, na kingine (wake wa Mitume na maswahaba) walikuwa wakiweka akiba na kutumia katika njia ya MwenyeziMungu. Na wao (wanawake wetu) wafanye hivyo. Hivyo, kwa kutoa hotuba hizi, tukawa tunaweka akiba kiasi fulani cha fedha na kukipeleka Qadiani. Lakini pale wake zetu walipokwenda Qadian (kwa ajili ya Jalsa Salana) na kukaa hapo, wakaona kila kitu kwa undani, kisha baada ya kurejea wakatushambulia kuwa sisi ni waongo wakubwa, kwamba wao wameshuhudia wenyewe maisha ya huyo Nabii (Mirza) na maswahaba wake baada ya kuzuru Qadiani. Aina ya starehe na anasa ambazo wanawake wanafaidi huko, haipatikani hata kwa asilimia 0.1 mahali pengine nje ya huko, licha ya ukweli kwamba sisi tunahangaika wenyewe kutafuta pesa zetu na licha ya ukweli kuwa chochote kiandacho huko kinakwenda kwa manufaa ya umma, ni pesa ya umma. Kwa hiyo, ninyi ni waongo ambao mmekuwa mkitulaghai kwa muda mrefu namna hiyo kwa maneno ya uwongo, sasa hatutadanganywa nanyi tena. Hivyo, hivi sasa hawatupi pesa kupeleka Qadian...” (Kashf-ul-Ikhtilaf uk.13 imeandikwa na Sarwar Shah Qadiani).

Mtu mmoja kutoka Ludhiana aliwahi kusema Msikitini mbele ya Molvi Mohammed Ali, Kwaja Kamaluddin, Sheikh Rehmat Ali kwamba Jumuiya huchukua mkopo, na watu huwanyima watoto cha kutia mdomoni ili kupeleka mchango (CHANDA) katika Jumuiya, lakini vito vya thamani na nguo hununuliwa kwa ajili ya Biwi Saheba (Mke wa Mirza Qadiani)! Kuna nini tena kingine hapo?” (Hotuba ya Mirza Mahmud, Khalifa wa 2, AlFazl Qadian tarehe 31 Agosti 1938).


“Upinzani mkubwa kabisa ambao (Dkt. Abdul Hakiim) aliibuka nao dhidi ya Masihi aliyeahidiwa, ulihusiana na masuala ya fedha, kwamba Mirza huchukua pesa kwa watu nma kisha huzitumia atakavyo....yeye (Mirza) hukusanya michango kwa kisingizio cha kuchapisha vitabu, na kwa namna yoyote ile hukusanya pesa kutoka kwa watu kwa kuwaghilibu, na kisha huzitumia kulia na kushoto, kwa namna atakavyo, hakuna hesabu zinazowekwa.” (AlFazl Qadian ya tarehe 20 Januari 1921)
Dkt. Abdul Hakiim alikuwa mfuasi mtiifu wa MGAQ lakini hatimaye akamkana MGAQ kuwa ni mzushi.
Mitapanyo ya Mahesabu
“Molvi (Mohammed Hussein Batalvi) Saheb alisema kuwa nenda kule Qadian, mpe ujumbe Mirza Saheb kwamba atoe hesabu ya kipato chake kunipa mimi...fedha za umma zinatumika vibaya, wap fedha hizi zinatumika....Nilifika Qadian, na kufikisha ujumbe huo wa Molvi Saheb. Hazrat Masiih Muwuud akaniambia kuwa nimemjibu Molvi Sahib kuwa pesa huja kwangu kwa ajili ya Mungu na tunaitumia kwa ajili ya Mungu, hatujaweka hesabu zozote...” (Qadiani narration iliyotajwa katika AlFazl Qadian Na. 201 juz.23 ya tarehe 28 Agosti 1946).
Maoni ya Wafuasi kuhusu Mirza
Mtu akidhani kuwa wafuasi wa Mirza Ghulam walikuwa wakifurahia mitapanyo hiyo ya fedha ya Mirza Ghulam Ahmad Qadian, basi hebu asome yafuatayo:
Hazrat Masiih Muwuud...alielezea masikitiko makubwa ndani ya nyumba kuwa licha ya kauli yangu kuwa ni matakwa ya Mungu kuwa katika kipindi cha uhai wangu usimamizi wa Jiko la Umma uwe mikononi mwangu, na kama ikitokea kinyume chake basi jiko la umma litafungwa, bado hawa akina Khawaja (Kamaluddin) na wengine, wanaendelea tu kunitaka eti niwakabidhi wao usimamizi wa Jiko la Umma na hawana imani na mimi.” (Kashf-ul-Ikhtilaaf uk.14 iliyoandikwa na Sarwar Shah Qadian)
Shaghalabaghala katika Masuala ya Fedha, usimamizi mbaya wa Jiko la umma, na matumizi ya isirafu nyumbani kwa Mirza Sahib:
Khawaja Kamaluddin na Molvi Mohammed walikuwa wafuasi wa karibu na waaminifu sana wa MGAQ. Aliposhindwa kuivumilia tena hali hiyo, Khawaja Kamaluddin siku moja alimwambia kwa hasira Molvi Mohammed Ali:
Dhuluma gani hii jamani we mtu unajua kuwa pesa kwa ajili ya umma zinakusanywa kwa tabu na uma unahoji kwa kitu gani watoe CHANDA, watu wanajinyima mahitaji yao, halafu kumbe pesa haitumikis katika miradi hiyo, badala yake inatumika kwa maslahi binafsi (ya Mirza na Familia yake) na halafu kiasi kinachotumika ni kikubwa mno kiasi kwamba miradi yoyote ambayo tumeianzisha imeshindikana kukamilika kwa sababu ya ukosefu wa fedha na imebaki tu hivi hivi, kama jiko la umma likitumika vizuri, basi kwa fedha hizo tu zitakazohifadhiwa, miradi hiyo inaweza kukamilika.” (Kashf-ul-Ikhtilaaf uk.15 mwandishi Sarwar Shah Qadian)
“Wakati fulani pale ujumbe ulipokwenda kukusanya CHANDA kwa ajili ya ujenzi wa shule, Khawaj Sahid akamwambia Molvi Mohammed Ali kuwa Hazrat Sahib (Mirza Qadian) binafsi anaishi maishi ya starehe lakini sisi anatuhubiria kuwa tupunguze matumizi. Katika jibu lake, Molvi Sahib akasema kuwa ndio hilo haliwezi kukanushwa lakini ni ubinadamu tu.” (Barua ya Mian Mahmud kwenda kwa Hakiim Nuruddin, Haqiiqat-i-Ikhtilaaf uk. 53 mwandishi Molvi Mohammed Ali)
Mirza awakasirikia Muriidi wake
Yule anayenipa na kisha akanisimanga kuwa ni mbadhirifu, huyo ananipiga vita, shambulio hilo haliwezi kuvumilika... Nashindwa hata kuwafikiria watu hao wanaokuwa kama mizoga ya wadudu ambao nyoyo zao zina mashaka...Mimi si mfanyabiashara eti niweke hati ya salio. Na pia mimi si mweka hazima eti nimpatie mtu fulani mahesabu.” (Maelezo ya MGAQ katika Gazeti la AlHakm tarehe 31 Machi 1905. Malfuuzaat juz.7 uk.325)
Alisema (Mirza Sahib) kuwa leo Khawaja Sahib alileta barua ya Molvi Mohammed Ali na kusema kuwa Molvi Sahib ameandika kuwa matumizi ya Jiko la Uma ni kidogo mno, kiasi kisaliacho cha maelfu ya rupia ambacho hukusanywa, kinakwenda wapi? Na hapo ndipo Mirza alipoingia ndani na kuhamaki kwa hasira kuwa ‘hivi hawa watu wanatufikiria sisi ni HARAM KHOR (wabadhirifu)? Wao wanahusika nini na pesa? Leo hii mimi nikiacha, kipato chote hiki kitakomelea mbali.” (Barua ya Mian Mahmud kwenda kwa Molvi Nuruddin, Haqiiqat-i-lkhtilaaf uk.52 mwandishi Molvi Mohammed Ali)

MGAQ ashitakiwa kwa Udanganyifu wa Kodi ya Mapato
Mwaka huu pato la mwaka la Mirza Ghulam lilifikia Rupia 7200 na kodi iliyotozwa ilikuwa ni Rupia 187.50....Mirza Ghulam Ahmad alibainisha katika tamko lake la kiapo kwamba yeye hupata kipato chake kutokana na rasilimaliardhi yake, shamba lake na bustani yake; pato litokanalo na rasilimali ardhi ni Rupia 82 annas 10. Makisio ya pato la mwaka litokanalo na shamba lake ni Rupia 300, na makisio ya pato la mwaka litokanalo na bustani yake ni Rupia 200/300, au 400 au makisio ya juu kabisa ni 500. Ukiondoa hayo hapati pato jingine lolote. Aidha Mirza Ghulam Ahmad alisema kuwa mwaka huu amepokea Rupia zinazokisiwa kufika 5200 kutoka kwa wafuasi wake.....ambapo hii haitumiki kwa ajili yake binafsi. Hakuna kumbukumbu ya mapato na matumizi, amekariri tu haya kutokana na kumbukumbu za kichwani mwake. Vilevile, Mirza amesema kuwa pato lake binafsi hutokana na rasilimali ardhi yake, shamba lake na bustani yake vinatosha kwa mahitaji yake, na hahitaji kutumia fedha za wafuasi wake kwa matumizi yake binafsi.” (Stetimenti ya Munshi Tajuddin Sahib, Sub.Divisional Income Tax Collector, Batala, District Guardaspur tarehe 31 Agosti 1898, imenakiliwa katika Shauri la Kodi ya Mapato Na. 46/55 la 1898; imetajwa katika Roohani Khazain juz.13 uk.516)
1   2   3   4   5


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət