Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə6/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   2   3   4   5   6   7   8   9   ...   25

11. Переведите текст и переделайте его в диалог с профессором:

Kinyonga

Wanafunzi wa chuo kikuu walipokutana na profesa Mohamed Haidari walimwuliza maswali mengi juu ya mnyama aitwaye kinyonga, na hasa walitaka kujua kama ni kweli kwamba kinyonga hubadili rangi yake kutokana na mazingira ambayo yamemzunguka.

Profesa alieleza kwamba kwa hakika ni kweli kuwa kinyonga rangi yake inabadilika na kufanana na rangi iliyopo kwenye mazingira ya wakati huo katika sehemu ambayo yupo.

Lengo la kubadilika huko kwa rangi ni kujipatia ulinzi kutoka kwa adui, hasa wale vinyonga ambao wanakwenda kwa mwendo wa taratibu sana, wale vinyonga ambao wana uwezo wa kwenda haraka hukimbia na kwenda kujificha. Maadui zao wakubwa hasa ni nyoka na wakati mwingine pia bundi na tai. Inapotokea hali kama hiyo ya hatari, basi atabadili rangi haraka ili aweze kujificha. Kubadilika kwake kwa rangi hutokana na mishipa yake ya mwilini.

Jicho ndilo ambalo anatumia kuona na kupeleka habari kwenye ubongo, nao hupeleka taarifa katika ngozi ambayo ina seli maalumu zenye rangi mbalimbali. Taarifa hiyo ndiyo ambayo humweleza ipo hatari katika mazingira hayo na huweza kubadilika rangi mara moja. Kama haoni au hana macho ni dhahiri hataweza kubadilika rangi yake. Hii rangi iliyobadilika katika mwili wake inaweza kukaa kwa muda wa nusu saa kufuatana na hali hiyo iliyomfanya abadilike.
Msamiati

-onya предупреждать, -chokoza 1) задевать,

предостерегать дразнить 2) провоцировать



onyo (ma-) предупреждение, -kunja складывать, сгибать;

предостережение сворачивать



-pambana 1) сталкиваться -kunjua разгибать,

2) бороться, сражаться расправлять



halali законный, легальный silaha (-) 1) оружие 2) орудие

kisingizio (vi-) предлог, отговорка bundi (-) филин, сова

-pinga 1) препятствовать 2) быть ubavu (mbavu) 1) ребро

против; возражать 2) бок; боковая сторона



mimba (-) зародыш, плод dhahiri ясно, отчетливо

-haribifu вредный; mzoga (mi-) труп, падаль

разрушительный -funua открывать,



mabadiliko (мн.) изменения; раскрывать

преобразования boma (ma-) забор,



-chimbuko (ma-) 1) источник, ключ ограждение

2) начало, происхождение mshipa (mi-) 1) мускул



kasoro (-) 1) недостаток 2) ошибка 2) нерв

kinyonga (vi-) хамелеон -ingilia вмешиваться

bata (ma-) утка seli (-) клетка (организма)

duma (-) гепард ubongo (bongo) мозг

pofu (-) вид антилопы

* * *

Урок 7. Somo la saba
Грамматика

Союзные слова tangu, toka/ tokea, mpaka в придаточных предложениях с временным значением.


Если придаточное предложение с глаголом в желательно-побудительном наклонении присоединяется к главному посредством таких слов как tangu, toka/tokea, mpaka, то оно может переводиться на русский язык как придаточное времени с помощью союзных слов типа “с тех пор, как...” или “до тех пор, пока...”. Например:

Miaka kumi imepita tangu aondoke hapa “Прошло десять лет с тех пор, как он покинул эти места”;

Hatutaweza kuwasiliana na wenyeji mpaka tujifunze lugha yao “Мы не сможем общаться с местными жителями до тех пор, пока не выучим их язык”;

Toka/ tokea mwanangu ahamie kaskazini sijapata habari zo zote kutoka kwake “С того времени, как мой сын переехал на север, я не получал от него никаких известий ”.

Здесь правильнее было бы говорить о двух омонимах в языке суахили – суффиксе -e, показателе перфектности, исчезнувшего в языке, и суффиксе -e, показателе желательно-побудительного наклонения. Обратите внимание, что четкое значение перфектности/результативности действия проявляется в придаточных предложениях с союзными словами tangu, toka/tokea.

Такие придаточные предложения времени синонимичны по смыслу конструкциям, образованным с помощью временного релятива -po- или видового показателя -me- (в случаях с mpaka). Но придаточные предложения с глаголом в желательно-побудительном наклонении часто добавляют значение обязательности выполнения действия. Сравните:

Hafungui duka mpaka mkubwa wake afike - (буквально) “Он не открывает лавку до того времени, как придти хозяину”;

Hafungui duka mpaka mkubwa wake atakapofika - (буквально) “Он не открывает лавку до тех пор, когда его хозяин придет”;

Hafungui duka mpaka mkubwa wake amefika - (буквально) “Он не открывает лавку до тех пор, когда его хозяин уже пришел”.


Mazoezi

1. Раскройте скобки и переведите:

1. Hutapata ruhusa ya kwenda likizoni mpaka (-maliza) kazi zote. 2. Katiba mpya ya nchi ilikubaliwa baada ya kupita miezi michache tu tokea wananchi (-pata) uhuru. 3. Mgonjwa hakuona nafuu yo yote tangu (-lazwa) hospitalini. 4. Wenyeji hawajafika mashambani toka mvua ya masika (-anza). 5. Tulishughulika na maandalizi ya sherehe usiku kucha mpaka (-ishiwa na nguvu) kabisa. 6. Wageni walikaribishwa chakula kitamu mpaka (kutoweza) kumeza hata kipande kimoja zaidi. 7. Tokea mto huo (-kauka) wakulima wameachwa bila ya chimbuko la maji wakaamua wachimbe kisima.


2. Переведите, используя в придаточных предложениях глагол в форме архаичного перфекта -e или в желательно-побудительном наклонении:

1. Ты не можешь водить машину, пока не выучишь правила уличного движения. 2. С тех пор, как мы вернулись в город, я часто вспоминаю своих деревенских друзей. 3. Вы не узнаете расписания поездов, пока не позвоните на станцию. 4. С того момента, когда я увидел океан, я не могу забыть, как он красив. 5. Она не видела своих родителей с тех пор, как ей исполнилось пять лет. 6. Я не буду помогать тебе до тех пор, пока ты не скажешь мне всю правду. 7. Как же ты узнаешь вкус манго, пока сам не попробуешь его? 8. С тех пор, как моя сестра уехала заграницу, я не получил от нее ни одного письма. 8. Я ни разу не был в музее с тех пор, как поступил в институт. 9. Иностранцы больше не приезжают в эту страну с тех пор, как там началась война.


PAA LA AFRIKA

Kwa muda wa miaka mingi nilikuwa nikililia kuona mlima huu mrefu ambao watu wengi walikuwa wakiimba sifa zake* kama kwamba hakuna mlima mwingine duniani. Nakumbuka wazi jinsi mwalimu wetu alivyokuwa akitusimulia habari za mlima huu. Alisema kuwa ndio mlima mrefu kupita yote katika Afrika nzima. Ni siku nyingi sasa tangu mwalimu anifundishe, kumbe leo ndoto yangu inatimilika.

Katika jua la magharibi niliona mbele yangu kitu mfano wa wingu kubwa. Sikuweza kuamini kwamba yawezekana huo ukawa mlima**, kwani jinsi ulivyotanda toka chini hadi mawinguni ilishangaza macho. Kwa ujumla nilianza kushangaa na kuduwaa. Nilifikiri kuwa zimwi kubwa jeusi lililovaa kofia nyeupe lilikuwa limesimama mbele yangu. Hivyo ndivyo mlima Kilimanjaro ulivyoonekana nilipofuata barabara ile itokayo Arusha. Tulipokaribia kama kilomita kumi na tano hivi kutoka Moshi ndipo kilele cha mlima kilionekana.

Maisha, dada yangu ambaye alilala kwa uchovu na taabu ya safari aliamka wakati huo huo. Nilinyosha mkono mbele na kumwonyesha wingu lile jeusi. Kwanza hakuelewa, baadaye nilipomnong’oneza, “Kilimanjaro” aliruka kwenye kiti chake hata watu wengine garini walishtuka. Wote wawili tukawa tunautazama ule mlima, mwisho tukakaribia Moshi. Hapo ndipo utukufu wa mlima huu ulipodhihirika. Kwanza wingu hili kubwa la mlima lilienea toka mashariki hadi magharibi. Jua lilipoangaza mara ya mwisho likitoa nuru yake ya dhahabu, mlima huu ulionekana kama malkia aliyevikwa taji.

Jioni ile tulilala kwenye hoteli ya Moshi, tukiwa na dukuduku la kuuona vyema mlima kesho yake. Alfajiri na mapema, tulisimama ukumbini mwa hoteli. Meneja wa hoteli ile alitueleza kuwa asubuhi sana mlima wote waweza kuonekana pamoja na vilele vyake. Mtu huyo hakutuhadaa, kwani tulipotazama mbele yetu tuliona wazi wazi, vilele vyote vya mlima vikikaribia kugusa mawinguni. Vilele vilikuwa kama vile watoto pacha, mmoja akiwa mrefu kidogo kuliko wa pili. Meneja alitueleza kuwa ni rahisi kwa wapandaji kukwea kilele cha Kibo bali kilele cha Mawenzi kimeinuka mno ghafla juu, hivyo si kazi rahisi kukwea mlima huo kwani hata mafundi huweza kuporomoka na kutumbukia katika mashimo. Wasafiri huchukua kamba ya kufungana viunoni wakweapo ili kuepuka hatari ya kutengana na kuporomoka. Haikupita nusu saa tuliona wingu jeupe likitanda juu ya mlima toka mashariki hadi magharibi. Wingu lilifunika mlima kabisa sehemu ya juu mpaka tusiweze kuuona tena.

Baada ya kifungua kinywa, tuliongozwa hadi kituo cha magari madogo yachukuayo watu na kuwapeleka huku na huko. Sisi tuliingia gari la Marangu. Tulipofika Himo tuliona kuwa gari lilikuwa likianza kupanda. Huku na huko kulikuwa na mashamba ya mahindi na migomba inayostahimili jua, bali jinsi tulivyoendelea kupanda ndivyo mashamba ya mahindi yalivyopungua, badala yake mashamba mazuri ya mibuni na migomba ya aina nyingine yalionekana. Kule uwandani hatukuzoea kuona mibuni, hivyo tulikodoa macho dirishani mpaka tulipofika Marangu.

Tukachukua barabara ndogo ipitayo chuo cha elimu ya taifa ya Marangu na kuanza kazi ngumu ya kuupanda mlima kwa miguu.

Hali ya hewa ilibadilika na ilitubidi kuvaa masweta yetu tuliyofunga katika vifurushi. Miti pia ilibadilika. Badala ya kuona miti ile yenye majani mapana tuliyoizoea, tuliona miti mingi yenye majani kama sindano na ile iliyokuwa na majani manene ili kuistahimili baridi.

Vijito vingi vilitiririka huku na huko kwa kasi sana. Ilipofika adhuhuri tulifikia kibanda cha Mandara, na hapo tukashindwa kuendelea mbele. Tulikuwa tumechoka, na pumzi yetu ilikuwa haitoshi. Hili tatizo la pumzi haba huwapata wengi wapandao milima.

Walinzi na viongozi wa kambi hii walitushauri kuwa jambo la busara lingekuwa kulala kwenye kambi hiyo ambapo paliwashwa moto*** na vitanda vilikuwa na mablanketi ya sufu kwa matandiko. Kwa vile tulivyochoka, tulikula chakula na kujipumzisha. Jioni kulikuwa na upepo mkali*** hivyo tulilala tu. Usingizi ulitutopea**** mpaka asubuhi tulipoamshwa na ndege waliokuwa wakiimba.

Kwa kuwa Maisha alichoka sana alinijulisha kuwa hangeweza kupanda zaidi ya kambi hii, hivyo niliamua kumwacha pale na walinzi wa kambi ya Mandara kwani nilijua nitamkuta tu salama salimini. Nikiwa na kikundi cha wasafiri wengine wapanda mlima, tulikwea hatua kwa hatua, tukipanua mapafu kwa nguvu ili kupata hewa ya kutosha.

Tuliendelea hivi mpaka jioni tukafika kambi ya Kibo. Hapo baridi ilizidi sana, na ardhi ilizidi kuwa wazi. Ni miti mifupimifupi tu iliyomea huku na huko pamoja na majani mafupimafupi ya mlimani. Usiku ilitubidi kuvaa masweta mawili ya sufu na kuvaa chupi ndefu ya sufu, kwani baridi ilikuwa haivumiliki.

Kulipopambazuka*** tulianza safari tena kumaliza hatua yetu ya mwisho ya kulipanda paa hili la Afrika. Tulifika kileleni Kibo nyakati za alasiri. Jua lililokuwa likiangaza magharibi halikutoa ukali wake. Furaha yetu ilikuwa kubwa kiasi kisichonenekana. Kweli tulifika juu ya mlima Kilimanjaro.

Tuliinamia nchi yote. Kwa kaskazini kabisa milima na nyanda za Kenya zikionekana kama ukungu wakati wa asubuhi. Kwa mashariki nyanda za majani za Taveta, hali kadhalika kusini na magharibi uzuri wa Tanzania ulidhihirika. Mito mingi ilionekana pamoja na maziwa. Hapo nilikumbuka kuwa nilisimama juu ya kilele cha mlima mtakatifu, ambao baba zetu wa Kichaga huusalimu kila asubuhi wanapoamka. Kwa Wachaga mlima huu ni mtakatifu kama vile mlima Kenya ulivyo kwa Wakikuyu.

Safari ya kurudi haikuwa ngumu, ila miguu sasa ilikuwa ikiuma. Kama nisingezoea mambo ya gwaride kwenye jeshi nisingeweza kamwe kumudu kupanda hadi kileleni. Maisha alikuwa akitungoja kwa hamu sana, naye alifurahi mno alipotuona. Aliahidi kuwa atakapokuwa mkubwa atapanda mlima ule hadi kileleni.

Siku ya pili tulirudi Moshi kuanza safari yetu ya kurudi nyumbani. Tulikuwa tumefanya makubwa, na hapo ndoto za utoto wangu zikatimia.


Maelezo

* …walikuwa wakiimba sifa zake переводится как “они воспевали ее” (букв.: “они пели ее достоинства”).
** Sikuweza kuamini kwamba yawezekana huo ukawa mlima “Я не мог поверить, что это может быть горой”. После вспомогательных глаголов, выражающих возможность, вероятность, предположительность действия в будущем, таких, как -weza “мочь”, yawezekana “возможно”, huenda “вероятно”, основной глагол оформляется показателем -ka-. Сравните: anaweza akaja “он, возможно, придет” и anaweza kuja “он может придти”; “ему можно придти”. После слова huenda инфинитивная форма недопустима вообще.
***Существительное локативного класса mahali может не присутствовать в предложении, но о нем свидетельствует согласование по одному из локативных классов: Paliwashwa moto “(в том месте) развели костер”. Kulikuwa na upepo mkali “(там) был сильный ветер”. Kulipopambazuka “Когда (там) наступил рассвет”.
**** …usingizi ulitutopea “мы крепко уснули” (букв.: “сон погрузился в нас”).
Mazoezi

3. Дайте эквиваленты на суахили:

что-то похожее на облако; гора похожая на гиганта; они совсем не похожи друг на друга как близнецы; следовать по дороге; следовать совету; волноваться; быть в смятении; сомневаться; взбираться на вершину; подниматься в гору; влезать на дерево; упасть в яму; свалиться вниз; упасть со стула; облако закрыло гору; закрыть дверь; закрыть глаза; выдерживать жару; переносить жизненные трудности; избегать трудности; терпеть боль; мой сон сбылся; мне исполнилось 20 лет; моя мечта стала явью; настало время; шаг за шагом; один за другим; по одному; после завтрака; шептаться; разговаривать громко; оказывается, уже рассвело.


4. Исходя из содержания текста, подтвердите или опровергните следующие высказывания:

1. Kwa muda mrefu sana mwandishi wa hadithi hii alikuwa na ndoto ya kuona mlima Kilimanjaro kwa vile alivyopata kusikia habari zake kutoka kwa babu yake. 2. Alipoifuata barabara iendayo kutoka Arusha msafiri huyu hakuweza kuona kilele cha mlima huo mpaka wamefika Moshi tu. 3. Wakati wa safari yake dada yake alikuwa amelala kwa sababu yeye aliwahi kuuona mlima Kilimanjaro mara nyingi hapo kabla. 4. Asubuhi na mapema walipoamka kwenye hoteli ya Arusha msafiri na dada yake waliweza kuona wazi wazi kilele kimoja tu kwa sababu ya mawingu mengi. 5. Vilele vya mlima Kilimanjaro ni kama watoto pacha, ni sawasawa kabisa, na ni rahisi kwa wapandaji kuvikwea vilele vyote viwili. 6. Wasafiri wanaokusudia kuukwea mlima huo huchukua kamba ya kufungana viunoni ili kuepuka hatari ya kutengana na kuporomoka. 7. Walipoanza kupanda juu na gari lao waliona mashamba mengi ya mibuni huku na huko. 8. Wasafiri walipozidi kupanda juu waliona joto sana hata iliwabidi kuvua masweta yao. 9. Walipofika kibanda cha Mandara hawakupenda kupumzika hata dakika moja wakaendelea na safari ili kuwahi kufikia vilele vya Kilimanjaro haraka iwezekanavyo. 10. Kwenye kambi ya Kibo baridi ilipungua kidogo. 11. Safari ya kurudi ilikuwa si ngumu, wasafiri hawakuchoka hata kidogo na walijiona wana raha.



5. Замените подчеркнутые слова в словосочетаниях синонимами из текста:

-panda mlima; -anguka chini; -kimbia hatari; chakula cha asubuhi; wingu limeufunika mlima; nilikuwa na hamu kubwa kuuona mlima; nakumbuka vizuri; mwalimu alituhadithia juu ya mlima; nilianza kustaajabu; ugumu wa safari; nilimwambia kwa sauti ya chini; umaarufu wa mlima; wasiwasi wa kuona mlima; mtu wa hoteli hakutudanganya; vilele vilifanana sana; -anguka shimoni; tulichungulia dirishani; vijito vilipita kwa kasi; tuliweza kuvumilia baridi kali; kiasi kisichosemekana.
6. Раскройте скобки и переведите:

1. Usiache kisu mezani, mwanangu anaweza (-chukua). 2. Wakati umetimia wa kurudi nyumbani, huenda mvua (-nyesha). 3. Inawezekana kaka yangu (-chelewa) kufanya mitihani ya koleji mwaka huu. 4. Vita huenda (-tokea) kwa sababu ya ugomvi mkali. 5. Usichukue pesa nyingi safarini, unaweza (-ibiwa) zote. 6. Hebu tuukate mti huo ambao unaweza (-anguka). 7. Inawezekana majirani zangu (-hamia) kuishi pembeni mwa mji.


7. Переведите:

1. В саду росло много красивых деревьев. Красивые цветы растут в моем доме. 2. В пещере слышались странные голоса. Странные звуки раздавались на улице. 3. На собрание пришло совсем немного людей. Много людей пришло на выставку. 4. На стадионе проходили соревнования студентов. Соревнования детей проходили в парке. 5. На площади играли праздничную музыку. Веселую музыку исполняли на концерте. 6. В этих озерах водится много рыбы. Крокодилы живут в той реке. 7. Здесь сидит мой товарищ. Мой брат сидит там.




8. Сделайте письменный перевод текста:

Katani

Katani ni namna moja ya mavuno inayohitaji fedha nyingi, mtu aweze kuipanda; maana kwa muda wa miaka minne au mitano yule aliyeipanda hapati kitu. Tena licha ya kupata kitu, lazima alipe mshahara wa watu wengi wanaopanda miche na kulisafisha shamba. Katani haipandwi kwa kutia mbegu, ila hupandwa kwa kupandikiza miche michanga, nayo hushika na kuota kwa upesi sana.

Mkitazama shamba la katani, mtaona mambo mengine yaliyo ya lazima sana. Kwanza, shamba ni kubwa mno, kwa sababu mikonge, yaani miche ya katani, ni mikubwa sana, nayo inataka nafasi nyingi, tena katani kidogo tu inapatikana katika mkonge mmoja. Ya pili, mtaona ya kuwa mikonge imepandwa katika safu zilizonyooka zenye nafasi kubwa katikati ya safu na ya mikonge pia, hii ni kwa sababu watu wanaokata katani lazima wawe na nafasi ya kuingia katikati bila ya kuchomwa na miiba. Mikonge ina miiba mikali sana nchani, na tena ina miiba inayozunguka pande zote za majani yake. Ya tatu, mtaona ya kuwa shamba ni karibu na mto au ziwa, maana lazima maji yawepo karibu kwa sababu katani lazima zisafishwe kabla ya kupelekwa mahali pengine. Ya nne, lazima kuwepo kinu, maana majani ya katani yanapondwa na kuondolewa nyama yake. Ya tano, lazima ziwe njia za magari madogo au za motokaa, kwa sababu majani ya mikonge ni mazito sana, na tena, kwa kuwa yana miiba mikali, hayawezi kuchukuliwa na watu, ila kwa magari. Ya sita, lazima mashamba yawe karibu na barabara au stesheni ya gari la moshi, au pwani panapoweza kufikiwa na tishali, ili wenye shamba waweze kuipeleka katani bandarini panapofikiwa na meli.

Wakati mikonge inapoota haina haja ya maji mengi, inasitawi katika nchi kavu sana. Mikonge inapokuwa tayari, watu huenda wakayakata majani yake na kuyapakia katika magari, nayo hupelekwa kinuni. Hapo majani yanatiwa katika mashine inayoyaponda na kuiondoa nyama ya majani, na kuzibakiza nyuzi zake tu. Nyama ya majani haina kazi, inatupwa tu. Nyuzi husafishwa sana katika maji, kisha, huanikwa juani ili zikauke. Nyuzi zikaukapo huwa nyeupe nzuri sana. Hapo nyuzi hupelekwa katika mashine inayozisafisha zaidi na kuzitia burashi mpaka zing’ae vizuri.

Nyuzi, yaani katani, zikiwa tayari, hufungwa katika marobota makubwa sana, na kupelekwa pwani kupakiwa ndani ya meli. Hupelekwa katika nchi nyingine kutengenezwa.

Katani zinatumiwa kwa kufanyia kamba za namna nyingi, na kamba yake ni nzuri yenye nguvu nyingi. Tena katani nyingi sana zinatumiwa kwa kufanyia karatasi au vitambaa.


9. Перескажите текст “Katani”, используя выражения:

zao linalohitaji fedha nyingi; haja ya kusafisha shamba; mshahara wa watu wengi; -pandikiza miche michanga; miche inataka nafasi nyingi; safu zilizonyooka; miche yenye miiba; maji yawepo karibu; lazima kuwepo kinu; panapoweza kufikiwa na tishali; panapofikiwa na meli; haina haja ya maji mengi; majani yanakatwa; mashine yenye kuponda majani; nyuzi zabakizwa; inatupwa tu; -anika juani; nyuzi zikaukapo; hufungwa katika marobota; yenye nguvu nyingi.


10. Переведите:

  • Килиманджаро – это не одна, а сразу три вершины, которые образуют необычную плоскую форму горы. Миллион лет назад на этом месте на высоте нескольких сот метров над уровнем моря располагалось ровное плато. Но затем в результате вулканической деятельности возникло три пика – Шира, Кибо и Мавензи. Сначала потухла и разрушилась Шира, затем Мавензи. А Кибо “заснул” и “спит” до сих пор.

  • Самой высокой точкой черного континента является вершина Кибо. Она находится на высоте 5895 метров. Она уникальна по своим огромным размерам – ее длина достигает 97 километров, а ширина 64 километра.

  • На вершине Килиманджаро формируется свой собственный микроклимат. Влажные ветры, дующие со стороны Индийского океана, буквально натыкаются на гору и отдают ей всю свою влагу в виде дождя или снега. Из-за большого количества осадков здесь необычно пышная для Африки растительность – и не только внизу, но и на склонах.

  • Равнина, окружающая гору на многие километры, не отличается богатой флорой, и эта пустынность еще больше подчеркивает величественность Килиманджаро. Если бы человек обладал способностью видеть на большие расстояния, с этой горы его восхищенному взору открылась бы практически вся Африка.

  • Эрнест Хемингуэй так описывал Килиманджаро: “…ее снега широки как мир, необъятны, высоки и невероятно чисты”. Одно из подлинных чудес природы, эта гора производит одинаково сильное впечатление на любого, кто однажды увидит ее перед собой – будь то знаменитый писатель или обычный путешественник.


Msamiati

robota (ma-) тюк, кипа -tumbukia падать;

malkia (-) королева проваливаться

busara (-) разум; мудрость zimwi (ma-) дух

-timia 1) исполняться (о возрасте, -tanda 1) расстилаться

мечте и т.п.) 2) наступать, 2) покрывать

приходить (о времени) pacha (ma-;-) близнец



-duwaa удивляться, быть -tandiko (-) покрывало

ошеломленным pumzi (-) вдох; дыхание



-nongona, -nongoneza шептать -kodoa macho смотреть

-tukufu великий, величественный пристально; таращиться

utukufu (ед.) величие pafu (ma-) легкое (анат.)

-takatifu священный, святой sufu, sufi (-) шерсть

-angaza светить, освещать nuru (-) свет; свечение

-stahimili выдерживать, терпеть adhuhuri (-) полдень

-vumilia терпеть, переносить kambi (-) лагерь

-vika надевать (на кого-л.) taji (ma-;-) корона

chupi (-) трусы, штаны; шорты -pambazuka рассветать

dukuduku (ma-) волнение, gwaride (ma-) 1) парад

смятение 2) строевые учения



ukumbi (kumbi) 1) зал; холл jeshi (ma-) армия

2) коридор volkeno (-) вулкан



-hadaa обманывать -zimika тухнуть, гаснуть

kinu (vi-) 1) мельница 2) фабрика -kumbana сталкиваться,

-kwea подниматься, взбираться наталкиваться, натыкаться

mkwezi (wa-) сборщик -pandikiza высаживать в

кокосовых орехов грунт (рассаду, саженцы)



-changa 1) молодой 2) недозрелый safu (-) ряд; строй

-anika сушить, высушивать nyama (-) 1) мясо

(на солце, воздухе, у огня) 2) мякоть



kifungua kinywa завтрак tishali (ma-) баржа

* * *

Урок 8. Somo la nane

(marudio)
1. Переведите текст и перескажите его на суахили:

Mnazi

Minazi hupenda sana kuota karibu na pwani, na hewa inayotoka baharini inaisitawisha sana. Ni mti mwembamba na mrefu sana. Una majani marefu ambayo yaitwa makuti. Mnazi ni mti wa kupendeza sana, hasa wakati upepo unavuma na kuutikisa huku na huku. Mtu akiwa anautazama wakati unapepea hivyo huwa hataki kuyaondoa macho yake jinsi anavyopendezwa.

Lakini uzuri wa mnazi si wa kutazamwa tu. Mnazi una faida nyingi sana. Watu wamesema ya kuwa mtu akiwa na minazi hana haja ya kitu kingine. Anaweza kujijengea nyumba yake kwa sehemu ya minazi; anaweza kujipatia nguo kwa sehemu ya minazi; anaweza kujilisha kwa sehemu nyingine. Kwa kweli tunapata vitu vingi sana katika minazi. Makuti yanatumiwa kwa kuezekea nyumba, na pengine yanatumiwa kwa kuzungushia ua. Vijiti vya makuti hufungwa pamoja na kuwa ufagio. Gogo la mnazi hufaa kwa kujenga nyumba, kufanya makasia, mipini ya visu, vizingiti vya nyumba na vitu vinginevyo.

Mnazi huzaa nazi. Makumbi yaliyoko juu ya nazi hayatupwi bali yanatumiwa kufanyia burashi za namna nyingi, nguo, nyavu, karatasi, kofia, matanga, mienge na kamba. Kamba ya mnazi ni bora sana. Ina nguvu na inaweza kutanuka sana, kwa hivi inafaa kufunga vitu kama mashua zinazovutwa na maji, maana kamba haikatiki, hutanuka tu. Tena kamba ya nazi ikitiwa baharini haiozi bali huzidi kupata nguvu.

Nazi yenyewe inakunwa na tui linatumiwa kwa kupikia, tena madafu yanaburudisha sana mtu akichoka au akiwa na kiu. Tena nazi iliyokunwa au kusagwa inatumiwa sana katika vitu vitamu kama maandazi. Kweli, matumizi ya nazi hayana mwisho.

Minazi inaota katika nchi za joto, kama ilivyo nchi yetu. Watu hupanda minazi na kuziangua nazi. Kwetu wanaitwa wakwezi, nao hupanda juu na kukata nazi na kuziangua.

Minazi mingine inayoonekana katika pwani za nchi nyingine haikupandwa na watu, bali nazi zilianguka katika nchi moja zikachukuliwa na bahari na kutupwa pwani katika nchi nyingine, zikaota pale. Nazi haziharibiki kwa maji ya bahari kwa vile zimefunikwa kabisa na makumbi na maganda magumu.

Kwa kawaida mnazi huanza kuzaa unapopata umri wa miaka mitano, nao huendelea kuzaa mpaka kupata miaka themanini au zaidi. Kila mwaka hutoa nazi zipatazo mia moja au zaidi.

Minazi inasitawi si pwani ya Afrika ya Mashariki tu, bali pia sehemu nyingine za Asia na Amerika.

Minazi lazima ilimwe na kutunzwa sana, maana wadudu wengine ni adui zake.


2. Переведите, используя аналитические глагольные конструкции:

1. Когда мой младший брат приедет в Москву на каникулы, я буду водить его по городу и знакомить с достопримечательностями. 2. Когда туристы спустились с горы, они были очень довольны, что смогли на нее подняться, несмотря на все сложности пути. 3. Учась на первом курсе, мы регулярно занимались не только дома, но и в библиотеке. 4. Менеджер не смог улететь в командировку, потому что билеты на самолет были распроданы еще на прошлой неделе. 5. Дети не научатся плавать, пока родители не отвезут их на море.


3. Раскройте скобки:

1. Wanakijiji hawawezi kujenga nyumba za aina bora mpaka (-pata) mbao na saruji. 2. Alianza kuishi kwa raha tangu (-rithi) pesa nyingi. 3. Amewahi kujifunza mengi tangu (-anza kutembelea) maktaba kila siku. 4. Biashara ya utalii haitaanza kusitawi mpaka wakuu wa mji (-jenga) hoteli zenye raha. 5. Hatuna budi kuchukua hatua kali mpaka misitu yetu (-linda) vizuri zaidi. 6. Mafundi walianza kufanya kazi kwa bidii tangu mishahara yao (-ongezwa). 7. Hawezi kuacha ulevi mpaka (-fahamu) kwamba afya yake imeharibika sana.


4. Перескажите текст:

Fisi

Ingawa kuna watu fulani ambao mpaka sasa bado hawajamwona fisi kwa macho, lakini haikosi wamemsikia akilia wakati wa usiku. Mpaka hivi sasa kuna miji mingine ambayo waweza kumsikia fisi akipiga kelele wakati wa jioni au usiku, kama vile Mwanza au Dodoma. Kuna msemo mwingine, usemao kuwa palipo na simba hapakosi fisi, kwa sababu fisi hana uwezo mkubwa wa kumkamata mnyama anayemtaka, yeye hungojea tu mabaki ya mnyama aliyekamatwa na mwingine kama vile simba au chui au aliyekufa.

Fisi si mnyama mkubwa, urefu wake ni karibu santimita 150. Hupenda kuishi katika mashimo na mapango. Chakula chao kikubwa ni nyama na mifupa ya wanyama waliokufa.

Kwa kawaida fisi ni mnyama mwoga lakini wakati mwingine huweza kuwa mkali hata akamshambulia binadamu na hasa kama mtu huyo amelewa huweza hata kumwua na kumla. Meno ya fisi huwa ni yenye nguvu nyingi hata huweza kuvunjavunja na kutafuna mifupa ya mnyama aliyekufa.

Fisi mwenye madoadoa ni mbaya zaidi na amewekwa katika kundi la wanyama waharibifu kwa mujibu wa sheria ya Tanzania.
5. Определите, о каком животном идет речь в следующем тексте. Расскажите о нем на суахили:

Mnyama huyu ni jamaa yake kobe na nyoka, maana damu yake haina moto, ila ni baridi. Watu waliozichungua habari za mnyama huyu, husema kuwa kuna aina zake ishirini katika dunia.

Mnyama huyu ni adui sana wa wanadamu, na watu wengi katika Afrika ya Mashariki wanachukuliwa na kuuawa au kuumizwa vibaya naye kila mwaka. Anaweza kuishi majini, na pia anatoka mara kwa mara kutafuta mawindo yake nchi kavu. Hula samaki na takataka zinazoonekana katika mito, lakini apenda sana kula wanyama, na wanadamu. Akimtazama, mtu angefikiri ya kuwa hana mbio; lakini anaweza kwenda mbio sana. Hawezi kuwakamata watu nchi kavu, maana hawezi kujigeuza kichwa, na kwa hivi watu wanaweza kutoka katika njia yake. Lakini akipata nafasi ya kuwapiga kwa mkia wake, ole wao! Wataangushwa mara ile, na kukamatwa.

Lakini katika maji, ndipo anapoweza kuwakamata kwa upesi. Anapoogelea majini anaweza kushika mtu kwa kinywa chake, huku pua yake ni juu ya maji, lakini kinywa ni chini. Basi yule mtu huuawa kwa maji, lakini mnyama huyu huvuta pumzi kwa pua yake iliyo juu ya maji. Tena anaweza kuyaziba masikio yake maji yasipite humo, na tena anaweza kufumba macho kwa ngozi iliyo mfano wa kioo, na ingawa amefumba macho, lakini anaweza kuona hata kama anakwenda chini ya maji.

Mwili wake haukuumbwa kama mwili wa mnyama wa kawaida. Ukimtazama ng’ombe, kwa mfano, utaona kuwa mwili wake huwa juu ya miguu yake, lakini mwili wa mnyama huyu huwa katikati ya miguu. Ana maisha marefu sana, anaweza kuishi kwa miaka mia tatu. Hazai watoto wazima, ila hutaga mayai.

Anapenda sana kukaa karibu na mahali watu wanapochota maji, na kuwavizia. Imedhaniwa ya kuwa mnyama huyu huwaua watu wengi kuliko mnyama ye yote katika nchi za Afrika ya Mashariki.


6. Замените синонимами подчеркнутые слова:

maji ya chemchemi; maanguko ya mto; -tilia mkazo; umati wa watu; mtaalamu wa uchumi; -epukana na shida; -kwea kileleni; -gundua kasoro; chimbuko la elimu; -pambana na adui; -winda pofu; -funua kinywa; -fumba macho; hewa ya kuburudisha; -fanya jitihada; uzembe usionenekana; tabia ya kuhadaa.



7. Назовите правильный вариант ответа:

1. Nyumba za aina bora lazima ziezekwe kwa (nyasi, mabati, makuti). 2. Kamba zilizo bora hutengenezwa kwa (katani, makumbi ya nazi, nyasi). 3. Minazi huota katika sehemu za (msitu mnene, pwani, karibu na maziwa). 4. Maji ya madafu ni maji kutokana na (machungwa, ndimu, nazi). 5. Mkwezi ni mtu anayefanya kazi ya (kujenga nyumba, kuangua nazi, kusafisha katani). 6. Mnazi ni mti unaoweza kuzaa matunda mpaka umri wa miaka (80, 50, miaka mitano). 7. Ziwa Tanganyika kwa kina chake kirefu ni sawa na ziwa (Victoria, Manyara, Baikal). 8. Katani ni zao la (mkonge, mbuni, mgomba). 9. Kilimo cha katani kinahitaji maji mengi wakati (miche inapoota, wakati wa kupanda, majani yake yanaposafishwa).


8. Дайте русские эквиваленты:

-dumisha mali asili; -chuma uyoga; hatari ya kutoweka; -chonga sanamu; safu ya milima; -funga kwa marobota; watoto pacha; -wa na ubongo; -chemsha bongo; -mudu kujitoa pangoni; duka la jumla; ustaarabu wa asili; -shika utawala; -kanusha uwongo; -ondoa imani potofu; kiongozi mwenye hadhi ya juu; kamba ya kufungana kiunoni; mimea ya jangwani; -kodoa macho; kiasi kisichonenekana; jambo la busara; -vuta pumzi; -epukana na shida; baridi isiyovumilika; maofisa wa serikali; -wa kivutio; -vunja mbavu; harufu ya kupendeza; tabia haribifu; maonyo makali; -pinga mabadiliko; silaha ya kupambana na makatili; utukufu wa mlima; -chokoza adui mkali; lori lenye bodi ya kukunja na kukunjua; msingi wa maisha bora; ukumbi wa mikutano; kwa mujibu wa katiba; -safisha vioo vya madirisha; -kanusha shauri la busara; maisha ya upotovu.


9. Переведите:

  1. Правительство Танзании принимает активные меры для сохранения природных богатств страны; лесных территорий, животного и растительного мира.

  2. Нехватка воды – это серьезная проблема, которую предстоит решить всем жителям этой деревни. Они договорились построить у себя запруду на реке, а также прокопать канал.

  3. Раньше в этих местах были одни болота, и земледельцам приходилось постоянно проделывать огромную работу по их осушению.

  4. Руководство города будет ежегодно выделять крупные суммы на строительство водопровода и проведение электричества во все новые кварталы.

  5. Нелицензированная охота на диких зверей наносит огромный ущерб природе, сокращает численность редких животных, и необходимо уделять этой проблеме больше внимания.

  6. Восточную Африку еще издавна называли страной Великих озер, поскольку три крупнейших озера не только Африки, но и мира находятся на ее территории.

  7. Между озерами Ньяса и Танганьика лежит озеро Руква, которое постоянно меняет свою площадь, так как в очень жаркие сезоны оно высыхает почти полностью. Погибает много рыбы и бегемотов.

  8. Специалисты предпочитают заниматься изучением флоры и фауны Восточной Африки в заповедниках, где уже давно запрещена охота на диких животных и птиц.

  9. Главная сельскохозяйственная культура Танзании – сизаль, растение, из которого получают прочные волокна и делают ткани и веревки. Сизаль был завезен в зту страну из Мексики более 100 лет назад.

  10. Толстые листья сизаля обрубают длинными ножами. Затем их промывают водой, высушивают на солнце, собирают в кипы и отправляют на фабрики.

  11. Листья у сизаля очень колючие, поэтому растения сажают рядами с большими промежутками с тем, чтобы крестьяне могли свободно проходить между ними не поранившись.

  12. Кофе также очень важная экспортная культура Танзании. Например, на севере страны выращивание кофе является одним из основных занятий народности чага.

  13. Кофейные поля обычно окружаются банановыми растениями, которые дают тень кофейным деревцам.

  14. У подножья горы Килиманджаро лежит город Моши, который является важным центром торговли и туризма.

  15. На пути к вершинам Килиманджаро можно встретить растения с толстыми листьями, которые привыкли к местным условиям и легко переносят холод.

  16. Величие горы Килиманджаро издавна привлекает массы туристов со всех уголков света, которые мечтают взобраться на ее снежные вершины.

  17. Поднимаясь вверх на “крышу Африки”, вы увидите, как меняется окружающий ландшафт, как прекрасна остающаяся внизу земля.

  18. Современные люди, которые любят проводить время в лесу, оставляют после себя огромное количество мусора, жгут костры, срывают редкие растения. Их действия наносят большой вред окружающей среде, и нам следует бороться с такими привычками.


10. Переведите текст письменно:

Waziri wa mali asili na utalii wa Tanzania alisema kwamba maofisa wa serikali watatembea duniani kutangaza kwamba mlima Kilimanjaro na visiwa vya Zanzibar viko nchini Tanzania ili kuondoa imani potofu iliyokuwepo kwamba mlima huo ulio mrefu Afrika kote na visiwa vya karafuu viko nchi jirani.

Waziri alisema kuwa serikali iliamua kutembea nje kwa kufanya jitihada ili kuuzima uvumi huo na kutangaza waziwazi kwamba mlima Kilimanjaro uko Tanzania. Moja ya jitihada hizo ni kutumia matangazo mbali mbali ambayo yangekuwa kama ni kivutio kikubwa kwa watalii kutoka nchi nyingi.

Waziri alitaja mfano wa vivutio vya kusini nchini Tanzania ambavyo ni muhimu kwa utalii. Ni pori la akiba la Selous, hifadhi za taifa za Mikumi, Ruaha na Udzungwa, maziwa Nyasa na Rukwa, milima kama vile ya David Livingston, Bonde la Ufa, mito, maeneo ya kihistoria na mambo ya kale na mandhari nzuri za kuvutia. Alisema serikali ina mipango mingi ya kuendeleza vivutio hivyo vya kusini mwa Tanzania ili kuongeza kasi ya utalii nchini.


11. Дайте эквиваленты на суахили:

средства к существованию; выделять деньги на строительство; незаконная охота; под предлогом болезни; толпа людей; плодородная почва; человеческие недостатки; вмешиваться в дела друг друга; подыскивать себе жилище; получать наследство; принимать жесткие меры; выслеживать врага; сбывшаяся мечта; шерстяное одеяло; участвовать в параде; раскрывать истину; горько сожалеть; постыдная работорговля; принять важное решение; искоренять недостатки; крыть крышу пальмовыми ветками; ряды домов; опровергать слухи; обманным путем; искаженные факты; пещерые люди; согласно принятому решению.


12. Переведите суахилийские пословицы. Какие из них имеют точные эквиваленты в русском языке?
Milima haikutani lakini binadamu hukutana.

Mchimba kisima huingia mwenyewe.

Vita havina macho.

Simba hamli mwanawe.

Samaki mmoja akioza, huoza wote.

Penye moto hapakosi moshi.

Njia mbili zilimshinda fisi.

Ndovu wawili wakipambana ziumiazo ni nyasi.

Kamba hukatika pembamba.

Akiba haiozi.
Msamiati

kuti (ma-) пальмовый лист, ветка kobe (ma-) черепаха

kumbi (ma-) волокнистая -vizia выслеживать,

оболочка растения высматривать



tui (ma-) напиток из кокосового -fumba закрывать,

молока смыкать (глаза)



dafu (ma-) кокосовый орех в -ondoa удалять,

стадии созревания молока устранять



-taga mayai откладывать яйца ufagio (fagio) метла, веник

kwa mujibu wa в соответствии kioo (vi-) 1) стекло 2) зеркало

-vuma дуть, бушевать (о ветре) imani (-) 1) вера, верование

uvumi (ед.) молва, слух, сплетня 2) убеждение, убежденность

kizingiti (vi-) порог; подоконник kijiti (vi-) 1) палочка; лучина

-potofu, -potovu 1) искаженный, 2) стебель (растения)

2) извращенный, развращенный -kanusha 1) отвергать,



mandhari (-) пейзаж; ландшафт отклонять 2) опровергать

-burudisha освежать, бодрить mwenge (mi-) факел

-angua сбрасывать; снимать -kunjamana сморщиваться

(то, что висит) kivutio (vi-) 1) стимул 2)



jitihada (-) усилие; старание достопримечательность

haikosi несомненно, непременно ole wangu (wako, wake n.k.) о

pango (ma-) 1) пещера 2) нора горе мне (тебе, ему и т.п.)
* * *

III. WABANTU NA DESTURI ZAO

Банту и их традиции
Урок 9. Somo la tisa

Грамматика

Вспомогательная функция личных форм некоторых глаголов в пассивной форме.


Некоторые глаголы в пассивной форме могут выполнять вспомогательную функцию в предложении. Это ряд глаголов, выражающих предположение (-dhaniwa, -tazamiwa, -fikiriwa -kisiwa), ожидание (-tarajiwa, -tegemewa, -ngojewa), утверждение (-tangazwa, -daiwa, -arifiwa), опасение (-hofiwa) и т.п. Подобные глаголы могут иметь субъектное согласование по любому из именных классов и оформляться практически всеми показателями времени или вида: -na-, -li-, -me-, hu-, -a-, -ka-. В русском переводе обычно используются безличные или неопределенно-личные формы глаголов: “предполагают”, “ожидается”, “как было объявлено”, “опасаются” и т.п.

Смысловой глагол следует за таким модификатором в форме инфинитива:

Wageni walitazamiwa kupokelewa kwenye uwanja wa ndege “Предполагалось, что гостей встретят в аэропорту”;

Rais ametangazwa kuondoka kwa safari kesho asubuhi “Объявлено, что президент отправится в поездку завтра утром”;

Anahofiwa kujihusisha na wizi kiwandani “Есть опасения, что он замешан в краже на предприятии”;

Mlima Kilimanjaro hudaiwa kupatikana nchini Kenya “Утверждается, что гора Килиманджаро находится в Кении.”

Негативные конструкции могут иметь два варианта – либо отрицание помещается во вспомогательный глагол, либо в смысловой, в зависимости от нюансов контекста. Сравните:

Fisi hawadhaniwi kuishi mahali hapa “Не предполагается, что гиены обитают в этих краях”;

Fisi wanadhaniwa kutoishi mahali hapa “Предполагают, что гиены здесь не водятся”.

Обратите внимание, что данные конструкции с личными формами глаголов семантически близки к предложениям с глаголами в неопределенно-личной форме. Сравните:

Ujenzi wa nyumba unatarajiwa kumalizika mwakani;

Inatarajiwa kwamba ujenzi wa nyumba utamalizika mwakani “Рассчитывают, что строительство дома будет завершено в следующем году”;

Mvua zinategemewa kuanza kesho;



Inategemewa kwamba mvua zitaanza kesho “Надеются, что дожди начнутся завтра”.

Mazoezi

1. Переведите, используя личные формы глаголов, -tarajia, -kisia, -tazamia и т.п.:

1. Ожидается, что новая железная дорога вскоре соединит наш город с крупным портом на берегу озера. 2. Считают, что экономическая программа правительства будет зачитана на завтрашнем заседании парламента. 3. Есть надежда, что срочные меры по предотвращению наводнения будут приняты незамедлительно. 4. Полагают, что штаб-квартиру нашей организации скоро переведут в другое здание. 5. Ожидается, что зарплата будет выплачиваться послезавтра. 6. Не предполагалось, что эта река пригодна для судоходства. 7. Было объявлено, что гости из Уганды прибудут к нам в страну сегодня вечером. 8. Есть надежда, что новый американский фильм будет показан по телевидению на этой неделе. 9. Как утверждалось, детская больница в нашем районе будет построена до конца года. 10. Есть опасения, что некоторые студенты первого курса не будут допущены до экзаменов. 11. Нет надежды на то, что дожди прекратятся скоро.



2. Замените подчеркнутые глаголы неопределенно-личными конструкциями и переведите их:

1. Wataalamu wanahofia kwamba wanyama wa porini wanaweza kutoweka kabisa. 2. Wanadhani kwamba vitu hivi vinaweza kuleta faida kubwa. 3. Hatutaweza kuwinda katika mbuga hizi. 4. Mnajua kwamba uvutaji wa sigara umepigwa marufuku hapa. 5. Anafikiri kuwa mitihani itaanza mapema mwaka huu. 6. Wanahistoria walidai kwamba Wabantu wa kwanza walihamia nchi hii zamani ya miaka elfu mbili. 7. Wanasema kwamba mahali hapo palikuwa na msitu mnene. 8. Tunaamini kwamba watu wa taifa la Wabantu walikuwa wa kiamani. 9. Mkuu ametangaza kwamba safari yetu itaendelea kwa wiki moja tu. 10. Mababu walieleza kwamba zamani sana hapa palikuwa na ziwa lenye kina kirefu sana. 11. Tukajua kwamba mwandishi huyu maarufu atakamilisha kitabu chake kipya mwezi ujao. 12. Wasitarajie kuweza kukiona kilele cha Kilimanjaro asubuhi ya leo, mawingu yako mengi mbinguni. 13. Mahali hapa panafikiriwa kugeuzwa kuwa eneo la hifadhi.


ASILI YA WATU WA NCHI ZETU

Wako watu wa namna nyingi wanaokaa duniani, wako watu weupe, watu wekundu, watu wenye rangi ya kimanjano, na watu wenye rangi nyinginezo*. Tena watu wa dunia hutumia lugha nyingi. Watu wa nchi fulani hawawezi kusikilizana na watu wa nchi nyingine mpaka wajifunze lugha yao. Hata katika nchi yetu ya Tanzania wako watu wa namna nyingi wanaotumia lugha nyingi sana. Wako Wazungu, na kumbe, wote si wa namna moja. Wako Waingereza, Wafaransa, Waitaliano, Wagiriki, Wadachi na wengineo*, na kila taifa lina desturi na lugha yake. Wako Wahindi, nao si wa namna moja wala hawasemi lugha moja tu. Wako Waarabu na desturi zao na lugha yao zimeachana kabisa na desturi na lugha za wale wengine tuliowataja.

Tena wako watu weusi wenyeji wa nchi hizi, na hata sisi watu wa Afrika si wa taifa moja. Basi kwanza afadhali tueleze habari kidogo juu ya kila taifa namna linavyohusu habari za nchi hii na wenyeji wanaokaa humu.

“Wabushmen” maana yake ni “watu wakaao mwituni”. Zamani sana kabla babu zetu hawajafika katika nchi hizi, wenyeji walikuwa watu wakaao mwituni tu wala hawakujenga nyumba wala miji. Waliwinda wanyama wa porini wakala nyama zao, na vitu walivyopata mwituni kama matunda, na majani ya namna nyingine, na mizizi.

Jambo linaloelekea kuthibitisha** kuwa Wabushmen walikaa katika nchi yetu ni picha nyingine zinazoonekana juu ya miamba na mawe na ndani ya mapango katika nchi ya Mkalama na Kondoa Irangi. Picha hizo zimeandikwa juu ya miamba na mawe kwa rangi nyekundu. Watu wengine wa huko hata sasa wanaweza kuandika picha za namna hizo, lakini hapana anayejua nani aliyeziandika picha hizo. Picha hizo za wanyama, yaani nyati, mbuni, twiga, pofu na wengine, na wanadamu, nazo zimefanana kabisa na picha zinazoonekana katika nchi za Afrika ya Kusini zilizo kazi za Wabushmen, na rangi inayotumiwa ni namna ile ile.

Wabushmen hao, yaani wenyeji wa asili, walifukuzwa au kuuawa au waliingizwa katika kabila la Wabantu walipokuja kutoka nchi za kaskazini, na waliobaki hukaa sasa katika Afrika ya Kusini.

Taifa jingine linalohusu wenyeji wa nchi hii huitwa mbilikimo. Watu hao ni wafupi sana, nao walikaa katika sehemu nyingine za nchi yetu kabla hawajafika babu zetu na kufanya makwao huku***. Watu hao hawakujenga nyumba wala kufuga wanyama kama wenyeji wanaokaa huku sasa. Wazao wengine wa watu hao wanakaa hata sasa katika nchi hizi, maana watu wanaokaa katika misitu ya nchi ya Kongo hudhaniwa kuwa ni wazao wao.

Watu wanaoitwa “Wahamitic” sasa ni wale waliokuwa wakikaa katika nchi za kaskazini mwa Afrika, yaani kupita Uganda na Kenya. Watu wengine wa taifa hilo waliingia nchi yetu wakasimamisha falme zao mahali pengine. Makabila mengine ya taifa hilo la “Wahamitic” ni Wamasai, Wambugu, Watatoga na wengine.

Kuna kabila moja tu la watu waitwao “Wasemitic” linaloingia sana katika habari za nchi yetu, ndilo Waarabu. Waarabu wa kwanza wanaodhaniwa kufika na kufanya makwao*** katika nchi hizi za Afrika ya Mashariki ni wale waliofika Pate katika mwaka 689.

“Wabantu” maana yake “watu”. Watu wa taifa hilo linaloitwa Wabantu wameenea katika Afrika kutoka Uganda na Kenya mpaka Afrika ya Kusini, na tena kwa upande wa Afrika ya Magharibi vile vile, yaani katika sehemu ile ya moja kwa tatu iliyo katika kusini ya Afrika nzima. Kweli wapo watu wa mataifa mengine wanaokaa humo, lakini ni wachache tu, tena wametengwa mpaka wamekuwa mfano wa visiwa vidogo katika bahari ya Wabantu.

Taifa hili kubwa la Wabantu lilipewa jina la Bantu na Mwingereza mmoja jina lake Bleek. Huyu Bleek alichungua sana habari za watu wa Afrika na lugha zao, akaona ya kuwa wako wengi sana ambao lugha zao zimefanana mno. Akazidi kutafuta habari na katika mwaka 1862, aliandika kitabu ili kuonyesha namna lugha nyingi za Afrika zilivyofanana, na kwa sababu katika lugha hizo nyingi hutumia neno kama “Bantu” au “Watu” au “Wandu” au “Atu” kwa wanadamu, basi alianza kutaja taifa hilo kubwa, yaani jumla ya watu wanaotumia lugha hizo zilizofanana, kwa jina la Bantu.

Wabantu wote walikuwa wakikaa katika nchi yao ya asili katika kaskazini zamani ya miaka 2,500 au 3,000. Wakati ule labda walikuwa kama kabila moja au sehemu ya taifa jingine, wakawa na lugha yao moja wakasikilizana pamoja.

Kwa pole pole Wabantu walianza kuhama kwenda mashariki na kusini, na watu wote hawakuhama pamoja kwa wakati mmoja. Wengine walihama kwanza wakakuta wenyeji wa asili, labda waliwafukuza au labda waliwaua, au labda walichukua wanawake wao wakakaa nao, au labda wakapatana nao wakakaa pamoja. Baadaye wengine walienea kwenda mahali pengine, au kwenda mbele zaidi, na vivi hivi**** ikawa kila walipofanya makao walichanganyika pamoja na wenyeji wa asili. Basi watoto waliozaliwa walifundishwa maneno mengine kwa kusikia lugha za mama zao, na maneno mengine kwa kusikia lugha za baba zao, ikawa baadaye lugha zikachanganyika vile vile. Halafu ikatokea ya kuwa maneno mengine ya lugha ya asili yalisahauliwa na watu wengine, yakatumika yale ya wenyeji wa asili.

Basi watu wa taifa la Wabantu walienea wakatengana na sehemu nyingine za taifa, lugha ikabadilika na baada ya kupita miaka mingi ikawa si lugha moja tu ila nyingi, yaani kila kabila lina lugha yake. Lakini asili ya lugha ni moja, na maneno mengine ya asili yanatumiwa na makabila mengi hata sasa, na hiyo ndiyo sababu si vigumu kwa Myao kujifunza Kinyamwezi, wala Mnyamwezi kujifunza Kiyao, wala Mswahili kujifunza lugha nyingine ya Wabantu. Watu wa taifa hilo la Wabantu wana lugha nyingi, lakini zote zimefanana sana, ingawa nyingine zimeachana sana kwa namna nyingine.


Maelezo

*.…rangi nyinginezo “и других цветов”, …Wadachi na wengineo “…немцы и другие”. Релятив в суффиксальной позиции местоимения -ingine “другой”, согласованный по классу определяемого существительного во множественном числе, подчеркивает большое количество или разнообразие предметов, о которых идет речь: watu wengineo “многие другие люди”; matunda mengineyo “многие другие фрукты”; kwingineko “в других местах”. Иногда само слово -ingi “много” может присутствовать в таком словосочетании, занимая позицию перед местоимением -ingine: vitu vingi vinginevyo “множество других вещей”.
** Jambo linaloelekea kuthibitisha…“то, что, возможно, подтверждает…” Глагол -elekea “направляться” имеет переносное значение, и его можно перевести словами “возможно”, “представляется”, “похоже”.
***…fanya makwao huku “заселить эти места” (буквально: “сделать своими эти места”). Притяжательные местоимения, согласованные по локативному классу при помощи префикса ku- (kwangu, kwako, kwake, kwetu, kwenu, kwao), субстантивируются, переходя в разряд имени существительного, тем самым, выполняя в предложении функции подлежащего, дополнения или обстоятельства места:
1   2   3   4   5   6   7   8   9   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət