Ana səhifə

П р е д и с л о в и е данный учебно-методический комплекс


Yüklə 2.19 Mb.
səhifə4/25
tarix26.06.2016
ölçüsü2.19 Mb.
1   2   3   4   5   6   7   8   9   ...   25

Ukuni mbaya haufichiki. Ukuni ulio mbaya hata ukiwekwa kwenye kuni nyingi nzuri hujitokeza, kwa sababu moshi wake haufichiki. Kwa mfano mtu mbaya hata ikiwa anakaa na kuishi na watu wema, ubaya wake haufichiki, unajitokeza tu.

Tone na tone huwa mchirizi. Tone la maji, moja baada ya moja, huweza kuwa maji mengi, yakafanya hata mchirizi. Maana yake, tusidharau kitu kidogo, kwani hiyo hiyo kidogo kidogo mwishowe hukusanyika ikawa kubwa au nyingi.

Moja ya mkononi yashinda mia za mbali. Maana yake ni kuwa kidogo kilicho karibu na wewe chashinda kingi cha mbali. Mtu bora akubali kidogo alichokipata kuliko kikubwa au kingi anachokitarajia tu kuwa labda atakipata baadaye.

Mchungulia bahari si msafiri. Ukiazimia kusafiri na ukihofia bahari jinsi ilivyo huwezi kusafiri. Methali hii yamfundisha mtu kuwa akiamua kufanya jambo aache uwoga wake na alifanye.
8. Переведите стихотворение и выучите его наизусть:

Kesho ama leo?

1. Kesho! Kesho nitafanya. 4. Fanya leo, fanya leo,

Maneno gani haya? Ndipo utakapojua,

Fanya leo, fanya leo, Mambo yametendekana,

Mara upatapo njia. Mambo yameendelea.

2. Kesho! Kesho ni uvivu, 5. Fanya leo, fanya leo,

Ni desturi ya ovyo, Tena fanya kwa bidii,

Ni desturi ya mzembe, Usiwe mtepetevu,

Hana nia ya kufanya. Bali uwe mwenye nguvu.

3. Kesho! Kesho atajuta, 6. Fanya leo, fanya leo,

Atafanya nini je, Hakika utasitawi,

Akingoja mpaka kesho, Utakuwa mtu kweli,

Kumbe, kesho haifiki? Mwaminifu na imara.
9. Напишите сочинение о том, какие города в Танзании вам хотелось бы посетить и почему. Опишите их.
Msamiati

kanisa (ma-) церковь kichochoro (vi-) переулок

hekalu (ma-; -) храм; mhamiaji (wa-) переселенец;

молитвенный дом; церковь иммигрант



msikiti (mi-) мечеть shimo (ma-) шахта; рудник

mkarafuu (mi-) гвоздичное дерево wavu (nyavu) сетка; сеть

riziki (-) средства к существованию mchirizi (mi-) ручей

-kua 1) развиваться -juta раскаиваться, сожалеть

2) возрастать, увеличиваться majuto (мн.) сожаления



tamasha (-;ma-) 1) зрелище methali, mithali (-) пословица

представление 2) праздник -tepetevu ленивый;



nidhamu (-) 1) порядок праздный

2) дисциплина, организованность mzembe (wa-) разгильдяй,



-gandana gandana стоять нерадивый человек

вплотную друг к другу kitovu (vi-) пуп[ок]; перен. центр


* * *

II. MAZINGIRA YETU

Окружающая среда
Урок 5. Somo la tano

Грамматика

  1. 1. Заставительная форма глагола.

  2. 2. Определительные конструкции с инфинитивом


Заставительная, или каузативная, форма является одной из наиболее продуктивных словообразовательных форм суахилийского глагола. Эта форма передает значение побуждения к действию, а иногда просто усиливает качество действия. Глагол при этом становится переходным. Заставительная форма образуется с помощью суффикса -isha/-esha или -iza/-eza, который присоединяется к основе глагола, вытесняя конечную гласную -a бантуских глаголов:

-pitisha (от -pita) “проводить” (букв. ”заставить пройти”);

-somesha (от -soma) “обучать”;

-pendeza (от -penda) “нравиться” (букв. ”заставить любить”);

-lipiza (от -lipa) “заставить платить”.

Если на конце глагола две гласные, то каузативная форма образуется с помощью суффикса -sha или -za, который, как правило, вытесняет конечную гласную -a:

-punguza (от -pungua) “снижать”, “сокращать”;

-ondosha (от -ondoa) “убирать”, “устранять”.

Глаголы, оканчивающиеся на -ka, в большинстве своем при образовании каузатива меняют этот суффикс на суффикс -sha:

-kausha (от -kauka) “сушить”, “высушивать”;

-pumzisha (от -pumzika) “давать передышку”, “отдых”.

Однако в некоторых случаях каузативная форма у таких глаголов образуется с помощью суффикса -isha/-esha, который вытесняет окончание -a:

-fikisha (от -fika) “доставлять”, “привозить”;

-chekesha (от -cheka) “веселить”, “забавлять”.

В глаголах, заимствованных из арабского языка, употребляется суффикс -sha. При этом последняя гласная -e или -i не меняется, а гласная -u меняется на -i:

-starehesha (от -starehe) “давать отдых”, “развлекать”;

-rudisha (от -rudi) “возвращать”;

-ruhusisha (от -ruhusu) “разрешать”, “позволять”.

Заставительная форма может быть образована через другие производные формы глагола – направительную, взаимную и т.д. Суффикс пассивного залога исключается (кроме как при образовании каузатива от глаголов с застывшим пассивом: -nywesha “поить” от -nywa; -elewesha “разъяснять” от -elewa):

-kalisha (от -kalia) “поселять”, “заселять”;

-unganisha (от -ungana) “объединять”.

В свою очередь заставительная форма может быть промежуточной при образовании других форм глагола – взаимной, направительной, стативной и т.д.:

-sikilizana (от -sikiliza) “прислушиваться друг к другу”;

-safirishia (от -safirisha) “перевозить кому-л., для кого-л.”;

-safishika (от -safisha) “быть возможным для очистки”.

Особенностью заставительной формы глагола является то, что она может быть образована не только от глагола, но и от других частей речи – прилагательного (-refusha “удлинять” от -refu “длинный”), существительного (-sainisha “подписывать” от saini “подпись”), наречия (-boresha “улучшать” от bora “лучше”).

Кроме того, некоторые глаголы могут иметь несколько вариантов словообразования с помощью суффикса каузатива. При этом значения новых слов могут быть одинаковыми или различаться:

От глагола -pita “проходить” > -pitisha “проводить” и -pisha ”пропускать”; от -choka “уставать” > -chosha и -chokesha “утомлять”; от -lala “спать” > -laza и -lalisha “укладывать спать”.

Каузативные формы от односложных глаголов образуются следующим образом:

-lisha (от -la) “кормить”;

-nywesha (от -nywa) “поить”;

-fisha (от -fa) “умерщвлять”.


Определительные конструкции с инфинитивом. Среди таких конструкций можно выделить целую группу терминологических словосочетаний. Они образуются путем присоединения инфинитивной формы глагола к определяемому существительному с помощью притяжательного форманта. При этом чаще всего глагол оформляется суффиксом направительной формы. Самым распространенным значением таких конструкций является значение инструмента действия или функции предмета:

miti ya kujengea nyumba “строительная древесина” (букв. “деревья для строительства домов”);

silaha za kuwindia wanyama “охотничье оружие” (букв.“оружие для охоты на зверей”);

vifaa vya kulimia ardhi “земледельческие орудия” (букв. “принадлежности для обработки земли”);

maji ya kusitawishia kilimo “вода для сельско-хозяйственных нужд” (букв. “вода для развития сельского хозяйства”).

Объект действия может опускаться, если позволяет контекст, но при этом направительная форма сохраняется. Можно сказать: miti ya kujengea, silaha za kuwindia, vifaa vya kulimia.

Среди определительных конструкций с инфинитивом часто встречаются словосочетания с глаголом в заставительной, пассивной или стативной форме:

kitu cha kushangaza “удивительная вещь” (букв. “вещь, которая заставляет удивляться”);

hadithi ya kuchekesha “смешной рассказ” (букв. “рассказ, который смешит”);

kitabu cha kusomwa ”книга, которую надлежит прочитать”.

ndizi za kupikika “бананы для приготовления пищи” (букв. “бананы, из которых возможно готовить еду”).

Инфинитивные словосочетания, в которых инфинитив выполняет определительную функцию, не являются замкнутыми конструкциями, в них можно вставить дополнительные слова между существительным и притяжательным формантом. Это могут быть прилагательные, числительные или местоимения: miti mingi mizuri ya kujengea nyumba “много хорошей строительной древесины”; vifaa vile vya kulimia ardhi “те сельско-хозяйственные орудия”; hadithi moja ya kuchekesha “один смешной рассказ”.


Mazoezi

1. Переведите глаголы в каузативной форме на русский язык, определите их исходную форму:

-refusha, -sahihisha, -patanisha, -tosheleza, -tenganisha, -shibisha, -tofautisha, -kataza, -kuza, -samehesha, -hamisha, -taabisha, -zungusha, -chosha, -chekesha, -safisha, -andikisha, -ainisha, -fananisha, -kondesha, -jaza, -kausha, -furahisha, -jiumiza, -sahaulisha, -pasha, -komesha, -lisha, -laza, -otesha, -liza, -kosesha, -dogesha, -ondosha, -katiza, -tokeza, -ogesha.


2. Образуйте каузативную форму глаголов и переведите их на русский язык:

-shona, -kimbia, -fupi, tofauti, starehe, -kumbuka, -ona, -tembea, bora, -toa, -ota, -nywa, -dharau, -karibia, -gombana, -chungua, -piga, -kalia, hakika, -poa, -teremka, maana, -inama, -anguka, -pungua, -geuka, ajabu, -elekea, -beba, -zidi, -kutana, -tapika, -panda, -ingia, -fahamu, -lipa.


3. Образуйте определительные словосочетания и дайте им русские эквиваленты:

shamba, -fuga, kuku; chombo, -vuta, vumbi; kiwanja, -cheza, mpira; vitu, -cheza, watoto; kiwanda, -safisha, petroli; gari, -chukua, mizigo; mafuta, -pika; chumba, -la; meli, -pakia, ndege; wavu, -vua, samaki; mashine, -fua, nguo; ghala, -weka, bidhaa; saa, -amsha; kisu, -kata, nyama; kitanda, -lala, watoto; askari, -linda, zamu; matini, -tafsiri.


4. Переведите словосочетания с помощью определительной конструкции с инфинитивом:

книга для перевода; гости, которых нужно встретить; мысль, которую стоит обдумать; решение, от которого стоит отказаться; слова, вызывающие горечь; новости, подтверждающие это; деньги на проезд; правила для заучивания; зал для просмотра фильмов; багаж, который надо разгрузить; радостный праздник; день отдыха; животные, которых надлежит охранять; письмо для отправки; города для посещения; деревья, которые следует посадить; крепость, которую придется построить; проблемы, которые предстоит решить.


MALI ASILI

Misitu ni eneo la nchi ambapo miti huota. Sehemu ambazo miti ni mifupi na imeota karibu karibu huitwa vichaka na sehemu ambayo miti hiyo ni mifupi na imeota mbali mbali huitwa makoko au vichaka vidogo. Kwa kawaida msitu ni mchanganyiko wa yote hayo. Sehemu zenye manyasi tu pia hupatikana ndani ya misitu. Misitu pia ni maskani ya wanyama wa mwituni.

Wananchi wa kale walipata sehemu kubwa ya riziki zao toka msituni. Msitu uliwalisha, kwani msituni mlikuwa matunda, majani na mizizi ambayo ilitumiwa kwa chakula. Mawindo yao yalikuwa msituni na miti shamba kadha wa kadha misituni ilitoa dawa mbali mbali, rangi na hata nguo pengine. Mbao na mazao mengine ya miti yalitumika kutengeneza vifaa mbali mbali, silaha za kuwindia wanyama mwitu au vitu vya kuvulia samaki au viti na vifaa vya kulimia. Misitu pia ilikuwa ndio ghala ya miti ya kujengea nyumba na ya kuni. Siku hizo za kale watu waliishi msituni katika vikundi vidogo vidogo.

Baadaye, vijiji na miji ilipositawi, binadamu walianza kuiaga misitu na kuanza kuishi na wenzao mahali pamoja. Idadi ya wananchi ilianza kuongezeka katika miji na vijiji. Ardhi ilianza kupungua na kutumiwa sana bila kupumzishwa kwa muda mrefu. Kwa hivyo misitu ilitoweka. Baada ya muda kidogo sehemu ambazo hazina misitu zilianza kuongezeka na idadi ya wananchi ilianza kuwa kubwa zaidi. Kwa hiyo watu walianza kuishambulia misitu kwa ukali sana kwa vile wakati huo walikuwa wamefikia hatua ya kutoyapenda tena maisha ya misituni. Katika wilaya nyingine katika nchi yetu misitu ilibaki kidogo sana.

Wadachi walipofika nchini kwetu walikata shauri kuwa Tanganyika ilikuwa na haja ya misitu na kwa hiyo walitenga sehemu nyingi nchini ambazo walitaka ziwe ni sehemu za misitu daima. Sehemu nyingi zilizoteuliwa kwa jambo hili zilikuwa porini ingawa sehemu chache nyingine zilikuwa karibu ya miji na vijiji. Sehemu hizi zilifaa sana kwa kutoa kuni na miti ya kujengea.

Misitu mingi ambayo ilikubaliwa idumishwe hivyo ilikuwa ni ile yenye miti ya mbao, kama vile msitu wa Rondo huko Lindi, na misitu iliyoonekana kuwa inasaidia kuzuia maji yasikauke kama vile misitu ya mlima Kilimanjaro na mlima Meru.

Idara ya misitu katika enzi ya Waingereza iliendelea na kazi ya idara ya misitu ya Wadachi ila kazi ya kuongezwa misitu ilipanuliwa. Sehemu nyingi zaidi zilitengwa kwa ajili ya misitu katika kila mkoa na hasa katika mikoa ya nyanda za juu Kusini. Upelelezi zaidi ulifanywa kutafuta misitu yenye miti ya mbao.

Miti mingine migeni ilipandwa katika mikoa ya Kaskazini, Tanga, Mashariki na nyanda za juu Kusini. Tawala za wananchi pia zilianza kutenga sehemu za maeneo yao fulani kwa ajili ya misitu. Juhudi kubwa ilifanywa kuzuia mioto inayoangamiza misitu na mwaka 1936 shule ya waangalizi wa misitu ilifunguliwa huko Arusha.

Kazi ya kutunza misitu ni ya maana sana. Mahitaji ya taifa ya mbao, miti ya kujengea na kuni ni makubwa mno na yatazidi kuongezeka. Tukijua kuwa mahitaji haya lazima yatazidi baada ya idadi yetu kuongezeka na ujengaji wa nyumba za kisasa kuongezeka, hatuna budi tuanze kuitilia mkazo kazi ya kupanda miti zaidi na kudumisha misitu yetu.

Kadhalika mahitaji ya taifa juu ya maji ni makubwa sana. Maisha ya wananchi wengi yanategemea kilimo na ufugaji. Na juhudi za kusitawisha kilimo na ufugaji hutegemea kupatikana kwa maji.

Makabila ya wananchi wa kale kwa kawaida yalikuwa yakikaa katika sehemu zilizokuwa na maji kila wakati, kama vile karibu na mito na maziwa. Kwa sababu hizo, usitawishaji wa kazi za maji uliendeshwa zaidi katika sehemu hizo hizo, na sehemu hizo zilipata watu wengi sana. Sehemu za namna hii ni kama zile zinazolizunguka ziwa Victoria, ziwa Tanganyika na ziwa Nyasa na katika mitelemko ya mlima Kilimanjaro, mlima Meru na mlima Rungwe. Umati wa watu katika sehemu hizo ni mkubwa mno na ardhi ni haba. Njia ya kulishinda tatizo hili kubwa la taifa ni kuzisitawisha sehemu zile ambazo ni kavu na kuzipatia maji ili nafasi ya kukalika nchini iongezeke.

Hapo zamani makabila manyonge katika mambo ya vita yalifukuzwa toka sehemu nzuri zenye maji na yalianza kuzunguka zunguka wakitafuta visima vya maji au chemchemi kwa ajili yao wenyewe, jamaa zao na mifugo yao. Makabila hayo hayakujenga visima vyo vyote vya daima, lakini, wakati wa mvua walijaribu kuweka akiba ya maji kwa matumizi ya wakati usiokuwa na mvua. Hata hivyo, kwa jumla, baadhi ya babu zetu wa kale walikuwa hawana masikani sawa sawa; walizunguka zunguka wakitafuta maji kila mara.

Mpaka sasa inajulikana kuwa usitawishaji wa maji ulifanywa kwa mara ya kwanza na Waarabu ambao walianza kujenga mifereji ya maji kwa mawe mjini Dar es Salaam na Bagamoyo. Na baadhi ya mifereji hiyo bado inatumiwa huko Bagamoyo mpaka sasa.

Ni baada ya Wadachi kufika nchini mwetu kazi ya kujenga mabwawa ilipoanza. Wadachi walijenga mabomba ya maji Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Tabora, Lindi, Mikindani na Kilwa. Katika miji mingine maji yaliyokuwa yakitumiwa yalitoka mitoni, kwenye maziwa au visimani. Mkonge ambao mpaka sasa ni zao kubwa la nchi yetu, ulianzishwa kupandwa katika enzi za Wadachi na kwa sababu maji mengi sana yalihitajiwa kuzisafisha katani toka mashamba hayo, ilibidi kuanzisha mashamba ya mikonge karibu na mito ya daima katika mikoa ya Tanga na pwani. Maji zaidi kwa kazi hiyo yalipatikana kwa kuchimba visima au kutengeneza mabwawa katika mashamba hayo.

Waingereza walipoingia nchini mwetu mabomba mengine ya maji yalijengwa Iringa, Mbeya, Mwanza, Bukoba, Tanga, Moshi, Arusha, Mafia na sehemu nyingine. Miaka ya 1947-1960 ilikuwa miaka ya kupanua kazi ya kuongeza maji nchini. Miji mingi mikubwa na midogo ilikuwa imepata mabomba ya maji.

Yafaa pia isisahauliwe kwamba maji yana matumizi mengine bora vile vile. Katika nchi kama yetu maji, na hasa maporomoko ya maji, yanaweza kutumiwa kwa kutoa nguvu ya umeme. Sehemu kubwa ya nguvu ya umeme itumiwayo huko Uganda hutokana na maanguko ya mto Naili. Mto Pangani hutoa nguvu ya umeme pia. Mto Kiwira pia unaweza kutumiwa na ukatoa nguvu ya umeme kwa vile mto wenyewe una maporomoko mengi sana. Maji ya mto Rufiji na ya mito mingine ni akiba ya nguvu ya umeme kwa taifa na pia ni akiba ya maji ya kusitawishia kilimo nchini.

Maji yataendelea kuwa shida ya taifa letu kwa muda mrefu mpaka wakati ule tutakapopata fedha za kutosha na wataalamu wa kutosha juu ya upimaji na usitawishaji wa maji nchini.
Mazoezi

5. Дайте русские эквиваленты:

-ota karibu karibu; -pata riziki; mawindo ya watu wa kale; mitishamba kadha wa kadha; -aga misitu; kushambuliwa na kutoweka kwa misitu; makabila manyonge; -tenga sehemu za nchi; -dumisha mali ya taifa; matumizi ya maji; -panua kazi ya kuongeza misitu; -fanya upelelezi; -fikia hatua; -angamia kwa wanyama; -angamiza maeneo ya misitu; -tilia mkazo maswali muhimu; -weka akiba ya maji; -jenga mabwawa na mifereji; -tumia bomba la maji; maanguko ya mto.


6. Дайте эквиваленты на суахили:

среда обитания диких животных, пристанище для бездомных людей, жилище для гостей, жилье для людей; добывать средства к существованию, не иметь средств к существованию; некоторые растения, некоторые слова, некоторые решения, кое-какие мысли, кое-какие поступки; хранилище сельскохозяйственной продукции, продовольственный склад, товарный склад, амбар; покидать леса, покидать родной дом, оставлять родителей, оставлять надежду; нападать на диких животных, нападать на поля, атаковать врага; принимать решение, принимать документ, принимать гостя, принимать лекарство; потребность в еде, потребность в получении помощи, необходимость охранять леса; выделять деньги на строительство, выделять средства на образование, отделять землю; отбирать подходящие территории, отбирать вопросы для обсуждения, выбирать слова, выбирать руководителей, выбирать дорогу; сохранять национальные богатства, сохранять здоровье, продлевать срок оплаты, сохранять жизнь редких животных; расширять деятельность, расширять права, расширять территории заселения; заботиться о родителях, охранять водные ресурсы, ухаживать за больным, смотреть за домом; уничтожать лесные угодья, уничтожать врага, уничтожать вредных насекомых; подчеркивать важность решения, уделять особое внимание охране лесов, уделять внимание сложной проблеме; это зависит от количества денег, урожаи зависят от дождей, мы надеемся на чудо; вести работу, вести машину, проводить собрание, проводить время.


7. Ответьте на вопросы по содержанию текста:

1. Kuna misitu ya aina gani katika Afrika ya Mashariki? 2. Misitu iliwasaidia binadamu wa kale namna gani? 3. Kwa nini watu wa zamani walianza kuiaga misitu? 4. Binadamu walileta hasara gani kwa misitu? 5. Kazi ya kutunza misitu ina maana gani? 6. Kwa nini maji ni kitu kinachohitajika sana kwa maisha ya watu? 7. Kuna njia gani ya kumaliza tatizo la uhaba wa maji nchini? 8. Watu wa zamani walipata maji jinsi gani? 9. Mabomba ya maji yalianza kujengwa kwa wingi mnamo wakati gani? 10. Mito husaidia vipi kusitawisha maisha ya binadamu?


8. Закончите предложения, опираясь на содержание текста:

1. Wananchi wa kale walipata faida kubwa kutoka misitu kwa sababu ... 2. Miti ilitumiwa sana na wananchi hapo zamani kwa ajili ya kutengeneza ... 3. Baada ya watu wa kale kuhamia katika miji na vijiji, misitu ilianza kutoweka na ardhi kupungua kwa sababu ... 4. Sehemu nyingi za eneo la Tanganyika ziliamuliwa ziwe misitu baada ya ... 5. Upelelezi zaidi ulifanywa na Waingereza waliojitahidi kutafuta misitu mipya ili ... 6. Shule ya waangalizi wa misitu ilifunguliwa Arusha mnamo mwaka ... ili ... 7. Wananchi hawana budi kuipanda miti mipya zaidi kwa sababu ... 8. Sehemu zilizokuwa zimepata watu wengi zaidi nchini Tanganyika ni zile ... kwa sababu ... 9. Hapo zamani watu hawakuwa na maskani ya kudumu kwa sababu ... 10. Mifereji ya kwanza ilijengwa na ... katika miji ya ... 11. Kazi ya kujenga mabwawa ilianza baada ya ... 12. Mito ya nchi inaweza kutumika kwa ajili ya ...


9. Переведите и перескажите коротко на суахили содержание следующего текста:

Faida ya misitu

Masanje alikuwa mkulima stadi katika kijiji chao. Alilima pamba, mahindi na mtama. Pia alifuga ng’ombe wengi. Kwa hiyo alikuwa anajipatia fedha nyingi kwa kuuza mazao yake. Lakini nyumba yake ilikuwa ndogo sana. Haikuwa na madirisha wala sakafu imara. Paa lake lilikuwa limeezekwa kwa nyasi na wakati wa mvua lilikuwa linavuja sana.

Karibu na kijiji hicho kulikuwa na msitu mnene. Msitu huo uliwaletea wananchi wa kijiji hicho faida kubwa. Watu wote walikuwa wakiokota kuni katika msitu huo. Walizitumia kuni hizo kwa kupikia, kuchomea matofali na kutengenezea mkaa. Wanaume walichonga mizinga ya nyuki kwa kutumia magogo au magome ya miti. Pia walichonga vitu mbali mbali kama fimbo, mipini, vitana na vinginevyo. Wengine walichonga sanamu za watu, wanyama na ndege. Waliuza vitu hivyo na kujipatia fedha nyingi. Mzee Masanje alikuwa fundi sana wa kuchonga vinyago.

Siku moja bwana Musa alifika kufanya mkutano katika kijiji cha akina mzee Masanje. Aliwaeleza wananchi faida ya kuwa na nyumba bora, akasema, “Nyumba imara na safi ni mmoja kati ya misingi ya maisha bora. Nyumba chafu ni makao ya wadudu wanaotuletea magonjwa. Tukitaka kuepukana na wadudu hao lazima tujenge nyumba bora kwa matofali na kuziezeka kwa bati. Serikali yetu inataka kila miongoni mwetu awe na nyumba bora.” Alipomaliza kusema hayo, watu wote waliondoka na kwenda nyumbani kwao.

Mzee Masanje alifikiri sana maneno ya bwana Musa. Mwisho wakapatana kushirikiana kujenga nyumba mpya. Wakajenga nyumba nzuri sana. Nyumba hizo zilijengwa kwa matofali na kuezekwa kwa mabati. Zilikuwa na sakafu imara za saruji. Tena zilikuwa na madirisha na milango iliyotengenezwa kwa mbao. Ndani mlikuwa na vifaa vya kupendeza kama vile meza, kabati, viti na vitanda. Hivi vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa mbao zilizotoka katika msitu wao.

Katika msitu huo ilikuwamo pia miti iliyozaa matunda matamu, na watu wa kijiji hicho walikwenda kuyachuma. Wakati wa masika wanawake walikwenda msituni kuchuma uyoga. Wanyama mbalimbali waliishi katika msitu huo kama vile nyati, ndovu, twiga na swala. Walikuwemo pia ndege wa namna mbalimbali.

Siku moja Bwana Hamisi alikuja kuwaeleza wananchi wa kijiji hicho jinsi ya kutunza msitu wao maana alisikia walikuwa wanakata miti ovyo. Akasema, “Misitu ndiyo urithi wetu. Huzuia udongo wenye rutuba usichukuliwe na maji ya mvua au upepo. Tena ni makao ya wanyama na ndege wetu wa porini. Tukikata miti na kuchoma moto ovyo nchi yetu itakuwa kame na mwisho itageuka kuwa jangwa. Mtu akitaka kukata miti lazima apate leseni. Watu wa kijiji hiki mna bahati ya kuwa na msitu, kwa hiyo utunzeni. Tena inafaa sana mwanzishe msitu mwingine wa miti ya mbao. Idara ya Miti itawaleta wataalamu kuwaeleza jinsi ya kuanzisha msitu huo. Inatupasa kupanda miti kwa sababu matumizi yake yameongezeka sana siku hizi. Tusipoanzisha misitu mipya tutaishiwa na miti. Tena tutafanana na mtu anayekula chakula chake chote bila kulima kingine.”

Mkutano ulipokwisha watu wote walirudi nyumbani kwao. Mzee Masanje na wananchi wenzake walianzisha mara moja msitu mwingine. Sasa wanapata mahitaji yao mengi kutoka msitu huo.
10. Объясните на суахили значение следующих слов:

-kata miti ovyo; -ezeka nyumba; sakafu; kitana; kabati; uyoga; -chonga vinyago; -pata urithi; mtaalamu; -ishiwa na pesa.
11. Поменяйте конструкцию предложений, употребив форманты -po, -ko, -mo и поставив на место субъекта подчеркнутые словосочетания:

1. Karibu na kijiji kulikuwa na msitu mnene. 2. Katika msitu mlikuwa na miti iliyozaa matunda. 3. Vichakani hakukuwa na manyasi marefu. 4. Katika wilaya nyingine palikuwa na misitu kidogo sana. 5. Sehemu za nyanda za juu kulikuwa na miti ya mbao. 6. Mji wa Arusha ulikuwa na shule ya waangalizi wa misitu. 7. Karibu na mito na maziwa kulikuwa na wakaazi wengi. 8. Nyumba ya mkulima haikuwa na madirisha wala sakafu imara. 9. Kwenye mitelemko ya mlima kuna ardhi haba. 10. Porini kulikuwa na sehemu nyingi zilizofaa ziwe misitu daima. 11. Katika nyumba chafu mna wadudu waletao magonjwa. 12. Chumba chake hakitakuwa na kabati lo lote. 13. Katika nchi nzima kulikuwa na wataalamu wachache tu. 14. Ndani ya nyumba mpya patakuwa na vifaa vya kupendeza.

1   2   3   4   5   6   7   8   9   ...   25


Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©atelim.com 2016
rəhbərliyinə müraciət